Kuendelea kumtaja Hayati Magufuli kwa mabaya ni upuuzi wa ajabu

Kuendelea kumtaja Hayati Magufuli kwa mabaya ni upuuzi wa ajabu

Tunajifunza kwa kina mambo yaliyopita (yaliyotendwa na wafu), kwa lengo la kutatua changamoto za wakati huu na hata ujao.
Ni wapumbavu pekee wanaojenga hoja kwamba wafu wasitajwe.
Ni muhimu kuweka kumbukumbu za mema na mabaya ya vizazi vilivyopita kwa lengo la kubotesha kizazi hiki na vile vijavyo.
Ni bahati mbaya sana, siasa zetu zimejaa wapumbavu huku watu wenye akili nzuri na busara wakikaa pembeni.

MTU akiamua kuwa mwenye Haki na awe mwenye HAKI.
MTU akiamua kuwa Mbaya na awe Mbaya.

Huyo Magufuli anayomabaya mazito aliyoyafanya, lakini pia anayomema makubwa aliyoyafanya, hapo ndipo MTU atakayekumzungumzia MTU huyo ambaye ni Mfu utagundua anahaki endapo atataka mabaya yake na mazuri yake pia. Lakini kutaja mazuri bila kutaja mabaya yake au kutaja mabaya yake bila kutaja mazuri yake huyo MTU atakuwa kundi la Watu waovu
 
Sasa Kwa taarifa yako kama unapenda Magufuli asisemwe kama kimya, ukianzisha thread ya Magufuli unatutowa pangoni ambao hata hatukuwa na mpango wa kucomment humu leo zaidi ya kusoma tu.

Uelewa wako unapoishia wengine ndio unapoanzia hapo, kwahiyo kuwa makini usicheze na hisia za watu kwenye vitu sensitive kama vya huyu muuwaji.
Ukitoka pangoni ukisema alafu inakua nn?? Wewe ni mjinga mkubwa
 
basi kaa huko unyamaze kimya kuna watu bado wana vidonda wakivitizama tu wanamkumbuka huyo muuaji na kuongea kwao inawapa faraja

Kama ilivyo sina mamlaka ya kumwambia yeyote akae kimya, ndivyo ilivyo kuwa hakuna wakuniambia nikae kimya ikiwa tuu ninachokisema sio dhambi wala kosa
 
Tunamtaje jpm kama sehemu ya mktaba wa maridhiano na mama,japo hata sisi hatupendi kumtaja,lkn maelekezo ni lazima tumnange na kumkashifi na kimxushua mambo mabaya,lengo ni kupunguza nguvu kubwa ya ushawishi alionao kwa watanzania na dunia nzima,Na nikili kuwa tunao wakati mgumu sana mbele ta watanzania,kwani tunaxomewa na kutukanwa,
 
Anaandika, Robert Heriel

Sikuwa mshabiki wa Magufuli Kutokana na namna alivyokuwa anaongoza, sisemi Kuwa Magufuli hakuwa na mambo Mema aliyoyafanya, yapo mengi mazuri Sana hasa ya miundombinu, lakini pia yapo Mabaya ambayo aidha aliyafanya au kuyafumbia macho, ambayo ndio yalinifanya nimuone kama kiongozi asiyefaa.

Ninashangazwa na kile kinachoendelea hasa Kwa upande wa Upinzani kuendelea kumtaja taja MTU ambaye tayari anasiku nyingi ameshafariki.
Kuna vitu huwa unafeli big times!Umuumize mtu halafu umchagulie namna ya kulia?Upo sawa kichwani kweli?Kwani wakimtaja weye unaumia nini?Una ubia na jina lake kwamba herufi zitapungua?Umemjadili na Hitler au Vladimir?
 
Tunamtaje jpm kama sehemu ya mktaba wa maridhiano na mama,japo hata sisi hatupendi kumtaja,lkn maelekezo ni lazima tumnange na kumkashifi na kimxushua mambo mabaya,lengo ni kupunguza nguvu kubwa ya ushawishi alionao kwa watanzania na dunia nzima,Na nikili kuwa tunao wakati mgumu sana mbele ta watanzania,kwani tunaxomewa na kutukanwa,
Marehemu anakuwaje na ushawishi Mkuu au wewe anakushawishi nini
 
Mimi huyu mzee nalia nae kwenye ajira tu., just imagine anaingia madarakani tu ndio namaliza chuo na kuingia mtani then for 6 consecutive years serikali ikaacha kuajiri na sasa hivi tuliokaa mtaani kitambo kirefu tunawekwa kando wanapewa kipaumele zaidi fresh graduates. Roho yake ihifadhiwe panapomstahili.
 
Mleta mada amesahau msemo maarufu wa "Historia itanihukumu"

Na amesahau kuwa Maisha ni kama hadithi, ukiandika hadithi nzuri itasomwa kwa uzuri wake na ukiandika hadithi mbaya itasomwa kwa ubaya wake!.

Rais siyo sawa na muuza kahawa, Matendo yake yanaacha athari chanya na hasi zinazoathiri maisha ya watu wengi sana, huwezi kukwepa kuyazungumzia mambo yake pindi akiwa hai au kafa!.

Kwa hiyo mleta mada tuliza ball. Mabaya ya Magufuli yatasemwa tu, ili watawala wa sasa wajifunze kuwa heshima na rekodi zao ziko at stake kama watafanya udhalimu
 
Siasa ni kugusa hisia. Ukiwa huna hoja na unatumika lazima ubaki kwenye kucheza na hisia za watu. Tanzania haina upinzani,ina wasanii tu wanaocheza ngoma ya chama tawala. Kwa kumsema sana Hayati Rais Magufuli ambaye hakuwa mtakatifu kama ambavyo watawala wote sio,yupo ambaye wanamkwepesha na mijadala na hawamsemi sana. Fungua macho ujue wanavyotumika. Halafu tulia,ucheke.
 
Anaandika, Robert Heriel

Sikuwa mshabiki wa Magufuli Kutokana na namna alivyokuwa anaongoza, sisemi Kuwa Magufuli hakuwa na mambo Mema aliyoyafanya, yapo mengi mazuri Sana hasa ya miundombinu, lakini pia yapo Mabaya ambayo aidha aliyafanya au kuyafumbia macho, ambayo ndio yalinifanya nimuone kama kiongozi asiyefaa.
Usikose kufika Same upate nyama pale bar ya kimweri
 
Kuna kitu kinaitwa "closure". Kwa kiswahili cha mtaani tunaweza kuita "kufunga mafaili" ya jambo au suala. Katika utawala wa Magufuli kuna mambo mengi mabaya sana yaliyofanyika ambayo hadi leo hayajapatiwa majibu au tuseme bado yako gizani. Kwa mfano, mauaji ya Akwilina, Lwajabe, miili iliyookotwa kwenye viroba, kupotea kwa Azori, Ben Saanane, risasi za Lissu, kutekwa kwa Mo, Roma, Magoti, wizi wa uchaguzi 2019, 2020. kuzima vyombo vya habari, vyama vya upinzani, ukwapuaji wa fedha za watu benki, bureau de change, n.k. Na majuzi Rais wa sasa kaongezea ufisadi kwenye pesa za "plea bargain" zisizojulikana zilipo.

Yote hayo bado yako gizani. Serikali ya CCM bado haionyeshi utashi wa kuleta CLOSURE kwenye kadhia hizi.

Lazima mkondo wa sheria ufanye kazi, ukweli ujulikane, hukumu sahihi itolewe (hata posthumously ikibidi) na hatua zichukuliwe kwa wahusika waliopo. MUHIMU ZAIDI kwa amani na utulivu wa nchi ni vyema kuwa na mchakato wa maridhiano ya kitaifa (truth and reconcilliation process). Hiyo ndiyo namna bora ya kupata CLOSURE. Maridhiano yanayoendelea ni hatua nzuri lakini haitoshi. Kinachosikitisha sana ni kwamba miaka ya karibuni serikali ya CCM imezidi kuendesha propaganda hatarishi za kuwagawa wananchi.

Kwa wale watakaodai hata awamu zilizopita zina matatizo ya aina hiyo wako sawa ingawa ni wazi kuwa Rais wa awamu ya tano aliyafikisha kwenye kiwango cha kutisha. Yaliyotokea kwa Mwangosi, Zona, Ulimboka na Kibanda awamu ya nne nayo bado "yananing'inia". Hayajapata CLOSURE. Ni doa kubwa kwa serikali ya CCM. Wahenga hawakukosea waliposema "damu ya mtu haipotei bure". Yote haya yataendelea kulitesa taifa kwa miaka mingi ijayo.

Walio na shauku kubwa kutaka Magufuli asisemwe au asitajwe basi waiombe serikali yao ya CCM ichukue hatua kuleta CLOSURE na UTANGAMANO kwa wananchi wote nchini. NA pia wajue wakianzisha mada za kumsifu Magufuli katika mazingira haya ambapo kadhia nyingi za utawla wake hajipata CLOSURE basi wasishangae kujibiwa na wenye kero zao. Waingereza wanaita kujibiwa "in kind".
 
Ujerumani Hitler ni kiongozi shujaa.
Ni kama Ghadafi tuu
Vp sasa kwenye upande wa mabaya yake Hitler je wajerumani hawazunguzii mabaya yake muda wote hadi leo hii? Maana wenye kuzungumzia hayo mabaya Magufuli wanadai kwamba hata Hitler anazungumziwa mabaya yake muda wote hadi sasa.
 
Back
Top Bottom