UHURU JR
JF-Expert Member
- Jul 24, 2014
- 16,543
- 7,880
Iddi Amini na Mugabe nani anaongozwa kwa kutajwa huko Uganda?Mara kibao tu wanamtaja
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Iddi Amini na Mugabe nani anaongozwa kwa kutajwa huko Uganda?Mara kibao tu wanamtaja
Mimi siwezi kuwa chawa Mkuu.
Najua wapo ambao wanamakovu ya milele lakini lazima wasamehe kwani Mungu ndiye mjuzi WA yote, tena aliwasaidia kuwalipia kisasi.
Au walitakaje zaidi
Historia haifutiki. Maisha aliyoishi ni kitabu amekiandika hivyo lazima kisomwe kama alivyokiandika mwenyewe na ni ujinga kuwapangia wasomaji kurasa za kukisoma kitabu hicho.Anaandika, Robert Heriel
Sikuwa mshabiki wa Magufuli Kutokana na namna alivyokuwa anaongoza, sisemi Kuwa Magufuli hakuwa na mambo Mema aliyoyafanya, yapo mengi mazuri Sana hasa ya miundombinu, lakini pia yapo Mabaya ambayo aidha aliyafanya au kuyafumbia macho, ambayo ndio yalinifanya nimuone kama kiongozi asiyefaa.
Rafiki kwa maana watu wa karibu anayojuana nao?Hakuna gaidi wa watu wote ambaye hana rafiki
Shetani pia anatajwa tena anatajwa sana kwenye nyumba za ibada. Ni upuuzi kuzuia watu wasimtaje shetaniAnatajwa na Wajerumani? Au kina Nani?
Kutaja taja Wafu kila mara ni dalili ya kuchanganyikiwa.
Unataja Watu ambao hawana chochote chakufanya
Kwahiyo Iddy Amini hawampendi Waganda?Nenda kamsifie Iddy Amini huko Uganda kisha ulete mrejesho hapa.
Unataka kusema Duniani huko wanamtambua kwamba Tanzania iliwahi na kiongozi muovu na kwamba huyo kiongozi anaingia kwenye list ya vuongozi waovu duniani?Wewe endelea na makala za kuelimisha vijana na mahusiano upo vizuri, huku tuache wenyewe huna upako huo.
Magufuli tutaendelea kumsema Kwa maovu aliyowatendea Watanzania tangu kuumbwa Kwa ulimwengu huu, udikteta na utawala wa mkono wa chuma tulikuwa tunausikia tu Kwa wenzetu na kusoma kwenye historia, lakini yule Mrundi wa Chato akaja kutuonesha dhahiri.
Hadithi kama hii usithubutu kwenda kuiogea kwenye familia ya Ben Saanane utakimbizwa na mashoka.
Hebu tuache, huyu tunaye liwe fundisho Kwa waovu wote kwamba ukiishi Kwa Ubaya utasemwa daima Kwa Mabaya yako na mema yako tutayasahau.
Imagine Profesa mzima Kabudi leo anatuambia eti yeye na Magufuli walitudanganya kuhusu pesa za Makinikia halafu unataka tukae kimya?
Kama wewe humtaji kwa utashi wako basi usiwaite wapuuzi wanaomlaani huyu sheitwanMagufuli nilimlaani akiwa hai lakini sinaga Laana wala baraka Kwa Watu waliokwisha Kufa.
Kila MTU MTU mpenda Haki alichukizwa na Matendo hayo, ikiwemo Mimi.
Wanampenda sana, wanasema hawajawahi kupata rais mwenye roho nzuri na mzalendo kama yeye.Kwahiyo Iddy Amini hawampendi Waganda?
Kwa hiyo yeye ndio alie piga risasi,yeye ndio aliewateka hao ulio waoanisha hapo juu,kwani wangapi walitekwa na wakapatikana,haya ikatokea taarifa kwamba hao waliotekwa yaweza ikawa ni wao kwa wao waliofanyiana unyama huu,au huyo aliepigwa risasi kapigwa na watu wake wa karibu kutokana na maslahi baina yao wao kwa wao,jee familia ngapi zenyewe kwa zenyewe zinauana kwa njia mbali mbali sembuse kwenye vyama?Ingekuwa wewe ndiye uliyepigwa Risasi thealthini,Mtoto wako alipotezwa, Ndugu zako waliuawa(Baba au mama yako) ulibomolewa nyumba yako Morogoro Road bila kulipwa hata mia nazani ungekuwa unamlaani milele hata kama amekufa
Na nyie wa CCM wapumbavu sana kupita maelezoChadema watakuelewa?
Wapuuzi sana hawa vijana wa chadema
Mbona Lucifer hasamehewi?Mungu ndiye anayejua Zaidi.
Kila Jambo limekadiriwa,
Samehe nawe usamehewe.
Shetani yupo hai na anatajwa kwa sababu anashawishi watu maovu hivyo bado anatenda hazungumziwi kama habari ambayo imeshapita.Kama shetani anatajwa na dini zote kwanini Magufuli asitajwe kwa aliyo yatenda.? Mwinyi alisema maisha ya mwanadamu ni hadithi tu. Magufuli kosa lake alijiona Mungu mtu na ni yeye pekee ndiye mwadilifu na wengine wote ni wezi tu.
Basi kaa kimyaSina mamlaka, nguvu na uwezo wa kumlazimisha yeyote kwenye huu Ulimwengu.
Sasa kwa nini unasema wanaomsema Magufuli ni wapuuzi?Kama ilivyo sina mamlaka ya kumwambia yeyote akae kimya, ndivyo ilivyo kuwa hakuna wakuniambia nikae kimya ikiwa tuu ninachokisema sio dhambi wala kosa
Wanaomsema magufuli, na Kwa usahihi zaidi sio kumsema bali kuonyesha 'sura' yake halisi, sio upinzani. Ni watu wote ambao sio wanafiki, wanaopenda ukweli.Ninashangazwa na kile kinachoendelea hasa Kwa upande wa Upinzani kuendelea kumtaja taja MTU ambaye tayari anasiku nyingi ameshafari