Uchaguzi 2020 Kufuatia kauli ya Polepole ya kuwa CHADEMA walichapisha kura bandia ili kuchafua uchaguzi, CCM tunawataka mfungue kesi kuwashtaki CHADEMA

Uchaguzi 2020 Kufuatia kauli ya Polepole ya kuwa CHADEMA walichapisha kura bandia ili kuchafua uchaguzi, CCM tunawataka mfungue kesi kuwashtaki CHADEMA

Natumai jambo hili litafanyiwa kazi haraka maana sio busara kuliacha jambo zito hivi lipite bila wahalifu hawa kuadhibiwa kulingana na tuhuma za Bwana Polepole.
HAKUNA kesi itafunguliwa hapo maana polepole ndo mhusika mkuu.

Hizo kura feki ziliagizwa na ccm, zilichapwa na JAMANA Printers, zikasambazwa nchi nzima na ccm kupitia vibaraka na mawakala wao
 
propaganda zingine huwa za hovyo sana,kama ana ushahidi wakashitaki tu umma ufahamu chama cha mbowe kama anavyokiita kana kwamba chama cha mtu binafsi hupewa usajili kufanya siasa ufahamu kosa hilo la kijinai
 
Kufuatia kauli aliyotoa bwana Polepole kuwa CHADEMA walichapisha kura fake ili kuchafua uchaguzi, ni vyema CCM ikawashtaki hawa CHADEMA kwa kutenda kosa hilo la jinai.

Kama ambavyo CCM imekuwa ikijinasibu kuwa ipo kwa ajili ya kupigania maslahi ya wananchi wanyonge ni vyema sasa ikaonesha kwa vitendo kuwapigania hao wananchi kwa kufungua kesi maana wananchi ndio wamehujumiwa na si CCM pekee.

Natumai jambo hili litafanyiwa kazi haraka maana sio busara kuliacha jambo zito hivi lipite bila wahalifu hawa kuadhibiwa kulingana na tuhuma za Bwana Polepole.

Asante.
Polepole!
Loose mouth of the year!
 
Back
Top Bottom