Kufuatia upungufu wa dola, BoT yatoa maelekezo ya kudhibiti Viwango Vya Miamala

Kufuatia upungufu wa dola, BoT yatoa maelekezo ya kudhibiti Viwango Vya Miamala

ChoiceVariable

JF-Expert Member
Joined
May 23, 2017
Posts
66,537
Reaction score
75,687
Kufuatia Hali ya upungufu wa Fedha za Kigeni hasa Dol ya Marekani,BoT yaja na maelekezo ya kudhibiti Viwango Vya Miamala Kwa mtu mmja mmja, taasisi na kampuni ikiwemo kupiga Marufuku madalali Ili kulinda Afya ya Uchumi.

Awali Waziri wa Fedha amenukuliwa akisema Kupungua Kwa mzunguko wa Dola kumetokana na Sera Mpya za Fedha za Marekani kubana Matumizi na kupunguza dollar kwenye mzunguko hivyo kuleta athari hasi kwenye Nchi zinazoendelea.

Tanzania Current Account (𝐐𝟏 - 𝟐𝟎𝟐𝟑)
Q1 2023: TZS 2.3trn/-
Q2 2022: TZS 2trn/-

The deficit is driven by import bills;
Q1 2022: TZS 6.5trn/-
Q1 2023: TZS 7.5bn/-

Resulting to foreign reserve drop to TZS 11.7trn/- Q1 2023, from 12.9trn/- of Q1 2O22.

bot.jpg

My Take: Tupunguze utegemezi wa dollar kwenye miamala yetu na pia tuzaloshe bidhaa nyingi ndani ya Nchi.

===

WhatsApp Image 2023-05-31 at 8.18.02 PM.jpeg

Kwa mujibu wa maelekezo hayo mapya, miamala yote ya fedha za kigeni inayozidi thamani ya Dola za Kimarekani milioni 1 kwa muamala mmoja katika soko la rejareja, lazima ifanyike kwa bei ya soko la fedha za kigeni baina ya benki. Aidha, miamala yote ya mteja mmoja kwa siku itajumlishwa ili kujua jumla ya kiasi husika.

Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania, Bwana Emmanuel Tutuba, ametoa wito kwa taasisi zinazojihusisha na biashara ya fedha za kigeni kufuata maelekezo hayo. Amesisitiza kuwa ni marufuku kufanya biashara ya fedha za kigeni na madalali wa kimataifa wa fedha za kigeni ambao hawajasajiliwa ndani ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Pia, madalali na wafanyabiashara wa fedha za kigeni wanatakiwa kuzingatia utaratibu wa kumtambua mteja (KYC) kabla ya kufanya biashara na mteja yeyote.

Kwa mujibu wa maelekezo hayo, kiwango cha juu cha mizania kati ya mali na amana katika fedha za kigeni (Foreign Exchange Net Open Position - NOP) kitakuwa asilimia 10 ya mtaji wa msingi (core capital), na kinapaswa kuzingatiwa kila wakati.

Gavana Tutuba ameagiza pia kuwa barua za udhamini (Letters of Credit - LCs) za shehena zinazopitia Tanzania (transit cargoes) zitapaswa kutokana na fedha za kigeni kutoka nchi ambako shehena hizo zinakwenda.

Gavana Tutuba amesisitiza kwamba kuzingatia matakwa yaliyoainishwa katika maelekezo hayo ni jambo la muhimu na kukiuka maelekezo hayo kutasababisha adhabu kwa mujibu wa Sheria ya Fedha za Kigeni ya mwaka 1992.

Utekelezaji wa maelekezo haya ya uendeshaji wa huduma za fedha za kigeni, kulingana na mahitaji ya soko la sasa, utaanza rasmi tarehe 1 Juni 2023. Maelekezo haya mapya, yaliyotolewa tarehe 31 Mei 2023, yanafuta maagizo yaliyotolewa na Benki Kuu ya Tanzania tarehe 6 Aprili 2020. Gavana amewakumbusha wahusika wote wa huduma za fedha za kigeni kuzingatia matakwa ya mpango wa fedha za kigeni nchini wakati wote.
 
Luhaga Mpina copy?.
BENKI Kuu ya Tanzania (BoT), imepiga marufuku biashara ya fedha za kigeni na madalali wa kimataifa wa fedha za kigeni ambao hawajasajiliwa ndani ya Tanzania.

Aidha, imetoa maelekezo mapya kuhusu miamala yote ya fedha za kigeni inayozidi thamani ya Dola za Kimarekani milioni 1.0 kwa muamala mmoja katika soko la rejareja, lazima ifanyike kwa bei ya soko la fedha za kigeni baina ya benki.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa kwa umma leo (Mei 31,2023), BoT imesema miamala yote ya mteja mmoja kwa siku itajumlishwa, ili kujua jumla ya kiasi husika lengo likiwa ni kulinda utulivu wa uchumi mpana na uthabiti wa mfumo wa kifedha nchini.

Gavana wa BoT, Emmanuel Tutuba, amesema: “Madalali/wafanyabiashara wa fedha za kigeni hapa nchini wanatakiwa wakati wote kuzingatia utaratibu wa kumtambua mteja (KYC) kabla ya kufanya naye biashara hiyo.”
 
Our economy is heading for a cliff. Bila shaka vihela vyote vya kigeni vinaishia kulipa riba za mikopo mingi mingi iliyokopwa kwa pupa na kificho.

Historia inaweza kujirudia,
Mkapa alikuwa na kazi ngumu ya kurejesha uchumi kwenye reli baada ya mtangulizi wake kuharibu kwelikweli.

Magufuli akalazimika kufanya hivyo hivyo baada ya mtangulizi wake naye kuharibu.
 
31 May 2023

Mwigulu Lameck Nchemba waziri wa fedha afafanua sababu za uhaba dola za Kimarekani nchini Tanzania



DKT. NCHEMBA AWAAGIZA WATAALAM WA UCHUMI WA KITAIFA NA KIMATAIFA KUTAFUTA SULUHU YA UPUNGUFU WA DOLA ZA MAREKANI KATIKA SOKO LA FEDHA​


31 May, 2023
Dodoma, Tanzania

DKT. NCHEMBA AWAAGIZA WATAALAM WA UCHUMI WA KITAIFA NA KIMATAIFA KUTAFUTA SULUHU YA UPUNGUFU WA DOLA ZA MAREKANI KATIKA SOKO LA FEDHA

Na Farida Ramadhani-Dodoma

Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb), amewaagiza wataalamu wa Wizara ya Fedha na Mipango na ujumbe kutoka Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF), kujadili namna ya kushughulikia athari za upungufu wa dola za Kimarekani katika mzunguko wa fedha ili kunusuru uchumi wa nchi zinazoendelea.

Mhe. Dkt. Nchemba (Mb) ametoa maagizo hayo wakati wa kufungua kikao kilichowashirikisha wataalam kutoka Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) unaoongozwa na Bw. Harris Tsangaride waliowasili nchini kwa ajili ya kufanya tathimini ya Program ya Huduma za Mikopo - Extended Credit Facility (ECF) (EFC), kwa kushirikiana na wataalam wa ndani wa Serikali.

Alisema mabadiliko ya Sera za Fedha nchini Marekani ya kubana matumzi na kupunguza dola kwenye mzunguko wa fedha, yameleta athari zinazoonekana mpaka kwenye nchi zinazoendelea, ikiwemo Tanzania.

"Tumekuwa tukirejea Covid-19 / Uviko na vita baina ya Urusi na Ukraine kama moja ya vitu vinavyoathiri uchumi wa nchi zinazoendelea ikiwemo Tanzania lakini upungufu wa dola unaathiri uchumi kwa kiwango kikubwa ikiwemo uagizaji wa mafuta na uagizwaji wa bidhaa mbalimbali zinazotumika katika shughuli za Sekta Binafsi", alisema Dkt. Nchemba.

Alisema ni vema kutafuta namna ya kushughulikia jambo hilo kisera ili kunusuru nchi zinazoendelea kwa kuwa sekta ya nje ni muhimu katika kuchochea ukuaji wa uchumi wa ndani.

Kwa upande wake Kiongozi wa ujumbe kutoka Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF), Bw. Harris Tsangaride, alisema Shirika hilo litaendelea kushirikiana na Tanzania ili kuhakikisha nchi inaendelea kupiga hatua kiuchumi na kijamii.


Bw. Harris Tsangaride amepongeza Serikali kwa Sera zake nzuri ambazo zinaendelea kutekelezwa katika kukabiliana na athari za vita ya Ukraine na kuongeza kuwa ni matarajio yao kuwa zitaendelea kuchokea ukuaji wa uchumi na maisha ya wananchi.

Bw. Tsangaride alisema Tanzania ni miongoni mwa nchi chache katika kanda ambazo zinafanya vizuri katika kutekeleza programu mbalimbali kwa kushirikiana na Shirika hilo na hivyo katika kikao hicho watajadiliana namna bora ya kuendelea kuiona nchi ikifanya vizuri zaidi.
Mwisho.

Source :
Tovuti ya wizara ya fedha tanzania

More info :

Country Report No. 2023/153

United Republic of Tanzania: 2023

Article IV Consultation and First Review Under the Extended Credit Facility (ECF) Arrangement -Press Release; Staff Report; and Statement by the Executive Director for the United Republic of Tanzania

Spillovers from the war in Ukraine and shortfalls in rainfall stalled Tanzania’s recovery from the COVID-19 pandemic. Despite fuel and fertilizer subsidies, inflation has picked up in recent months, approaching the Bank of Tanzania’s target. External balances deteriorated significantly last year due in large part to spillovers from the war in Ukraine.

Series:

Country Report No. 2023/153

Subject:

International organization Monetary policy

Source : United Republic of Tanzania: 2023 Article IV Consultation and First Review Under the Extended Credit Facility Arrangement-Press Release; Staff Report; and Statement by the Executive Director for the United Republic of Tanzania
 
Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania, Emanuel Tutuba amepiga marufuku taasisi zinazofanya biashara ya fedha za kigeni na madalali wa kimataifa wa fedha hizo ambao hawajasajiliwa ndani ya nchi.

Katika taarifa ya BOT kwa vyombo vya habari, imesema madalali/wafanyabiashara wa fedha za kigeni nchini wanapaswa wakati wote kuzingatia utaratibu wa kumtambua mteja kabla ya kufanya naye biashara hiyo.

Katika maelekezo hayo, kiwango cha juu cha mizania kati ya mali na amana katika fedha za kigeni (foreign exchange Net Open Position (NOP) kitakuwa asilimia 10 ya mtaji wa msingi (core capital) na kinatakiwa kuzingatiwa wakati wake.

Aidha, ameelekeza kuwa Barua za Udhamini (Letters of Credit (LCs) za shehena zinazopitia hapa nchini (transit cargoes) zitatokana na fedha za kigeni kutoka katika nchi ambako shehena hizo zinakwenda.

“Inasisitizwa kwamba uzingatiaji wa matakwa yaliyoainishwa hapa ni wa lazima na kutakuwa na usimamizi na ukaguzi kutoka Benki Kuu ya Tanzania. Kukiuka maelezo haya kutasababisha adhabu kama zinavyoelezwa katika Sheria ya Fedha za Kigeni ya mwaka 1992,” ameeleza Tutuba.
 
Kufuatia Hali ya upungufu wa Fedha za Kigeni hasa Dol ya Marekani,BoT yaja na maelekezo ya kudhibiti Viwango Vya Miamala Kwa mtu mmja mmja, taasisi na kampuni ikiwemo kupiga Marufuku madalali Ili kulinda Afya ya Uchumi...
Chawa si walisema hilo ni tatizo la kidunia na kuwa serikali hairprint dolla imekuwaje tena
 
Benki Kuu ya Tanzania imetoa maelekezo muhimu kwa taasisi za fedha zinazojihusisha na biashara ya fedha za kigeni. Hatua hii imechukuliwa kwa lengo la kulinda utulivu wa uchumi mpana na uthabiti wa mfumo wa kifedha nchini.

Kwa mujibu wa maelekezo hayo mapya, miamala yote ya fedha za kigeni inayozidi thamani ya Dola za Kimarekani milioni 1 kwa muamala mmoja katika soko la rejareja, lazima ifanyike kwa bei ya soko la fedha za kigeni baina ya benki. Aidha, miamala yote ya mteja mmoja kwa siku itajumlishwa ili kujua jumla ya kiasi husika.

Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania, Bwana Emmanuel Tutuba, ametoa wito kwa taasisi zinazojihusisha na biashara ya fedha za kigeni kufuata maelekezo hayo. Amesisitiza kuwa ni marufuku kufanya biashara ya fedha za kigeni na madalali wa kimataifa wa fedha za kigeni ambao hawajasajiliwa ndani ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Pia, madalali na wafanyabiashara wa fedha za kigeni wanatakiwa kuzingatia utaratibu wa kumtambua mteja (KYC) kabla ya kufanya biashara na mteja yeyote.

Kwa mujibu wa maelekezo hayo, kiwango cha juu cha mizania kati ya mali na amana katika fedha za kigeni (Foreign Exchange Net Open Position - NOP) kitakuwa asilimia 10 ya mtaji wa msingi (core capital), na kinapaswa kuzingatiwa kila wakati.

Gavana Tutuba ameagiza pia kuwa barua za udhamini (Letters of Credit - LCs) za shehena zinazopitia Tanzania (transit cargoes) zitapaswa kutokana na fedha za kigeni kutoka nchi ambako shehena hizo zinakwenda.

Gavana Tutuba amesisitiza kwamba kuzingatia matakwa yaliyoainishwa katika maelekezo hayo ni jambo la muhimu na kukiuka maelekezo hayo kutasababisha adhabu kwa mujibu wa Sheria ya Fedha za Kigeni ya mwaka 1992.

Utekelezaji wa maelekezo haya ya uendeshaji wa huduma za fedha za kigeni, kulingana na mahitaji ya soko la sasa, utaanza rasmi tarehe 1 Juni 2023. Maelekezo haya mapya, yaliyotolewa tarehe 31 Mei 2023, yanafuta maagizo yaliyotolewa na Benki Kuu ya Tanzania tarehe 6 Aprili 2020. Gavana amewakumbusha wahusika wote wa huduma za fedha za kigeni kuzingatia matakwa ya mpango wa fedha za kigeni nchini wakati wote.

WhatsApp Image 2023-05-31 at 8.18.02 PM.jpeg
 
Sheria zipo tangu 1992, ila kama kawaida, WaTz wanajifanyia mambo wanavyojisikia, kiwizi na rushwa.
 
Kufuatia Hali ya upungufu wa Fedha za Kigeni hasa Dol ya Marekani,BoT yaja na maelekezo ya kudhibiti Viwango Vya Miamala Kwa mtu mmja mmja, taasisi na kampuni ikiwemo kupiga Marufuku madalali Ili kulinda Afya ya Uchumi..


Awali Waziri wa Fedha amenukuliwa akisema Kupungua Kwa mzunguko wa Dola kumetokana na Sera Mpya za Fedha za Marekani kubana Matumizi na kupunguza dollar kwenye mzunguko hivyo kuleta athari hasi kwenye Nchi zinazoendelea..


My Take
Tupunguze utegemezi wa dollar kwenye miamala yetu na pia tuzaloshe bidhaa nyingi ndani ya Nchi..

 
Back
Top Bottom