jd41
JF-Expert Member
- Aug 23, 2015
- 3,756
- 4,847
Wanabodi Salaam.
Ikiwa taarifa za kufukuzwa uanachama wa Chama Cha Mapinduzi Ndugu. Bernard Camilius Membe zikiwa bado zinatikisa mimbari ya siasa Tanzania, nimejikuta ninakumbuka matukio machache kabla ya uchaguzi mkuu uliopita mwaka 2015.
Ikumbukwe wakati ule mgombea aliekuwa anapewa nafasi ya kupeperusha bendera ya CCM kwenye uchaguzi mkuu alikuwa ni Ndg. Edward Lowassa, japo baadae aliikosa ile nafasi ikaangukia kwa Rais John Magufuli.
Hata hivyo wachambuzi wa mambo walibainisha kwamba Ndg. Membe ndie alikuwa chaguo la Rais mstaafu Kikwete, lakini kutokana na joto lililokuwepo ndani ya mkutano mkuu wakati ule baada ya jina la Lowassa kukatwa ikabidi ampitishe Rais Magufuli kuwa mgombea wa CCM ili kutuliza hali ya mambo.
Hii ilisababisha Ndg. Lowassa aondoke CCM (sio kwa kufukuzwa) na kuelekea upinzani CHADEMA ambapo aligombea urais japo hakushinda. Membe kwa upande wake aliendelea kuwa mwanachama wa CCM, mpaka leo alivyofukuzwa uanachama.
Tukikumbuka matukio machache yaliyotokea miezi michache iliyopita ambapo kwanza Ndg. Lowassa alirejea CCM, akiongozana na rafiki yake Ndg. Rostam Aziz, ambao kwa nyakati tofauti wote waliondoka CCM chini ya uenyekiti wa Rais Mstaafu Kikwete, sasa hao wote wamerejea CCM na kuongeza nguvu upande wa Rais Magufuli, halafu yule aliekuwa kipenzi cha Mwenyekiti aliepita (Kikwete) amefukuzwa uanachama wake, hivyo kumuondoa kabisa kwenye system kwasababu alionekana threat kwa Rais Magufuli.
Hii inaonesha siasa ni mchezo kama ilivyo michezo mingine karata (last card), na draft, siku zote wachezaji wa hiyo michezo huficha karata zao au kete kumvizia mpinzani wao wampe pigo la kushtukiza waumalize mchezo.
Hili linaweza kuthibitishwa kutokana na kelele zilizozuka siku za karibuni kwamba Ndg. Membe anaweza kuomba nafasi ndani ya CCM aweze kupitishwa kugombea nafasi ya urais ambayo imezoeleka Rais aliepo madarakani hupewa nafasi ya kumalizia muhula wa pili wa utawala wake, hii inaweza kuwa ndio sababu ya Membe leo kufukuzwa uanachama wake ndani ya CCM, na sio sababu za kinidhamu kama zilivyoainishwa na Pole Pole ambazo hazionekani kuwa na direct impact kwa Magufuli ku-seek his second term.
Sent using Jamii Forums mobile app
Ikiwa taarifa za kufukuzwa uanachama wa Chama Cha Mapinduzi Ndugu. Bernard Camilius Membe zikiwa bado zinatikisa mimbari ya siasa Tanzania, nimejikuta ninakumbuka matukio machache kabla ya uchaguzi mkuu uliopita mwaka 2015.
Ikumbukwe wakati ule mgombea aliekuwa anapewa nafasi ya kupeperusha bendera ya CCM kwenye uchaguzi mkuu alikuwa ni Ndg. Edward Lowassa, japo baadae aliikosa ile nafasi ikaangukia kwa Rais John Magufuli.
Hata hivyo wachambuzi wa mambo walibainisha kwamba Ndg. Membe ndie alikuwa chaguo la Rais mstaafu Kikwete, lakini kutokana na joto lililokuwepo ndani ya mkutano mkuu wakati ule baada ya jina la Lowassa kukatwa ikabidi ampitishe Rais Magufuli kuwa mgombea wa CCM ili kutuliza hali ya mambo.
Hii ilisababisha Ndg. Lowassa aondoke CCM (sio kwa kufukuzwa) na kuelekea upinzani CHADEMA ambapo aligombea urais japo hakushinda. Membe kwa upande wake aliendelea kuwa mwanachama wa CCM, mpaka leo alivyofukuzwa uanachama.
Tukikumbuka matukio machache yaliyotokea miezi michache iliyopita ambapo kwanza Ndg. Lowassa alirejea CCM, akiongozana na rafiki yake Ndg. Rostam Aziz, ambao kwa nyakati tofauti wote waliondoka CCM chini ya uenyekiti wa Rais Mstaafu Kikwete, sasa hao wote wamerejea CCM na kuongeza nguvu upande wa Rais Magufuli, halafu yule aliekuwa kipenzi cha Mwenyekiti aliepita (Kikwete) amefukuzwa uanachama wake, hivyo kumuondoa kabisa kwenye system kwasababu alionekana threat kwa Rais Magufuli.
Hii inaonesha siasa ni mchezo kama ilivyo michezo mingine karata (last card), na draft, siku zote wachezaji wa hiyo michezo huficha karata zao au kete kumvizia mpinzani wao wampe pigo la kushtukiza waumalize mchezo.
Hili linaweza kuthibitishwa kutokana na kelele zilizozuka siku za karibuni kwamba Ndg. Membe anaweza kuomba nafasi ndani ya CCM aweze kupitishwa kugombea nafasi ya urais ambayo imezoeleka Rais aliepo madarakani hupewa nafasi ya kumalizia muhula wa pili wa utawala wake, hii inaweza kuwa ndio sababu ya Membe leo kufukuzwa uanachama wake ndani ya CCM, na sio sababu za kinidhamu kama zilivyoainishwa na Pole Pole ambazo hazionekani kuwa na direct impact kwa Magufuli ku-seek his second term.
Sent using Jamii Forums mobile app