Kufundisha Watu Kura ya Ndiyo (Serikali), Hapana (Maaskofu,UKAWA) ni Sahihi?

Kufundisha Watu Kura ya Ndiyo (Serikali), Hapana (Maaskofu,UKAWA) ni Sahihi?

troll-slap-rage-smiley-emoticon.gif
Wewe ni mpuuzi namba moja humu cjawah kuona, akili zako hazina tofauti na hizo katuni unazoweka, kwa maana kama ungekuwa na akili timamu ungeweka hoja, sasa wewe unaweka katuni ambazo hazina mashiko na hazina connection zaidi ya kutueleza jinsi akili yako ilivyo.
 
mbona hao wanasiasa walisusa vikao vya kuiandaa
Ache ujinga katiba ni ya wote hivyo mchungaji, kafil, shahe pamoja mwenasiasa wanatakiwa kuwa na nguvu sawa wakati wa kuiandaa.
 
..maajabu haya...wao wanasema wakati ikifika pigia kura ya ndiyo mimi nikisema piga kura ya hapana kosa unalo..WANAFIKI

Ni wakati wako kusema hivyo la matokeo ndio yatawaeleza tukwani tatizo liko wapi?
 
Wadau wa JF Great Thinkers,

Kwa wale wanaotaka kuutambua ukweli ili ukweli uwaweke huru na wadumu ktk nuru hiyo daima wataafikiana na uwazi na wataukubali ukweli hata kama unawaumiza saana, watajua ndio mwelekeo wa haki.

Tangu mwaka jana, mara baada ya kumalizika kwa bunge maalumu la katiba, serikali ya ccm ilifanya matamasha, kuhamasisha na kusherehekea 'katiba pendekezwa' kuwa 'ccm wameshinda' dhidi ya 'wapinga rasimu ya 2 ya katiba' kama ilivyowasilishwa na jaji joseph sinde warioba. Hii ikimaanisha kuwa ccm walianza kusherehekea [hadi kucheza taarabu bungeni waziwazi] hata kabla ya kuanza kunadi kwa wananchi ili waelewe kilichoandikwa ndani ya chapisho hilo waliloliita 'katiba pendekezwa' na pia mikakati iliwekwa kuhakikisha kuwa chapisho hili halisambazi mapema sana, halichapishwi nakala nyingi sana, na haliwafikii wengi saana [tofauti na walengwa wa ccm], hii yote ni kuhakikisha kuwa mikakati ya watawala kuelekeza watu waipigie kura ya ndio inafanikiwa siku na wakati utakapofika. Siyo hivyo tu:

* Kikwete mwenyewe na makamu wake kupitia serikali yake yote iliandaa bajeti ya mabilioni ili kuhakikisha vyombo vya habari [hasa vinavyomilikiwa na serikali, na hasa tbc1, magazeti, radio na vile vingi vya binafsi ila vinavyoendeshwa 'kinjaa njaa' kuwa upande wa kuwaelekeza na kuwafundisha wananchi la kufanya] vinaandaa programu kabambe kuhamasisha na kuwaelekeza wananchi popote waipigie katiba pendekezwa kura ya ndiyo!!! Toka mwaka jana hadi leo hii 'mafundisho' hayo na 'maelekezo' hayo ya kupiga kura ya ndiyo yanaendelea!! Ukweli ni uhuru na hatuwezi kufumbia macho unafiki au woga utokanao na watawala, au wapambe wao wanaohemea ktk meza zao ili kushibishwa na kusahau utu wao.

Je, hayo yote yaliyofanyika kwa aidi ya miezi 7, hayakuwa mafundisho, maelekezo na kuingilia uhuru wa mwananchi kusema ndiyo au hapana?? Kwa nini serikali haikuwaelekeza kuwa wasome machapisho hayo ili siku ya kura 'waamue watakavyo'?? Bali inasema wazi wazi kuwa waipigie kura ya ndiyo?? Unafiki! Mhashamu kardinali pengo hakupata ufahamu wa 'matenddo haya maovu' ya serikali na ccm kuingilia 'akili au dhamira' za wananchi [ambao ndio waumini wake pia] kuwaelekeza wapige kura ya ndiyo badala ya kujiamulia wenyewe? Upofu huo!

* Baraza la maaskofu na jumuiya za makanisa ya kikristo yaliyotoa tamko rasmi hivi karibuni la kuwaelimisha waumini na watanzania wote waiosome katiba pendekezwa [ambayo hata hivyo imefichwa-fichwa, tena wasioielewa, na imevurugwa mambo muhimu] na kuipigia kura ya hapana ili 'kuikataa' ni tamko na fundisho sahihi kabisha ni la haki, elimu sahihi, na iliyojaa ukweli na unayoutenga unafiki pembeni na kueneza nuru itawale ili taifa lipate chombo sahihi, na kamilifu kinachoitwa katiba ya wote. Maaskofu na viongozi hawa wa dini walichelewa sana kutoa tamko au mafundisho yao maana serikali ilianza toka mwaka jana, ndipo ukawa nao wakaikabili serikali na ccm kwa kuwaelekeza wafuasi wa wasiipigie kura! Lakini ukweli ni kuwa baraza la maaskofu na jumuiya za makanisa ya kikristo tanzania, wapo sahihi, wapo ktk haki na tunawaomba wasimamie waliyoyasema na kuyaelekeza makanisa yote tanzania nzima, waumini wao wasimame imara kupiga kuwa ya 'hapana'!

Haki inajibiwa kwa haki, na sio dhuluma! Kama serikali imetumia miezi zaidi ya 7 kuwafundisha wananchi wapige kuwa ya 'ndiyo' basi viongozi wetu wa dini wapo sahihi kuwafundisha waumini wao wapige kura ya 'hapana' angalau kwa hizi wiki chache zilizobakia, ili haki ikamilike! Kuwakemea maaskofu kwa tamko lao ni unafiki, upofu na woga wa kuukwepa ukweli, au 'kujipendekeza kwa kaisari'. Mh askofu mkuu kardinali pengo angetambua kuwa kushirikiana na 'kaisari' [serikali] kuwapokonya watauwa haki, 'kuwanyima kauli' au kuwaingiza wtu ktk giza nene kama la kuipa nchi katiba mbovu...hii dhambi haitafutika usoni pako daima!! Hii ni kwaresma...tutende haki-kwa-haki.

Nawasilisha kwa mjadala!
hawa viongzi wahache wanaotaka kutupeleka njia isiyofaa kwa maslahi yao zaidi,chonde viongozi wa dini siuingilie kwenye mambo ya msingi kma hilo a kitiba inayopendekezw!katik kupiga kura wakati ukifika
 
not_yet_uhuru tambua kwamba serikali ni kaizari na maaskofu ni watumishi wa bwana.

Serikali kufundisha wananchi wapige kura ya ndio wako sahihi kabisa kwa kuwa katiba ni mtoto wao waliyemuasisi na wanataka kumhalalisha lakini ikitokea watumishi wa bwana wanaingilia serikali na kuwadanganya waumini kwamba ati watapata dhambi wakipiga kura ya ndio hapo unapaswa kutia shaka uadilifu wa hao watumishi wa bwana kwani wameenda kinyume na usemi wa "ya kaizari mpe kaizari na ya mungu mpe mungu".

Watuache tuisome kwani dunia yetu chaguo letu sisi ndio tutaamua tupige kura ya ndiyo au hapana

pointless
 
..maajabu haya...wao wanasema wakati ikifika pigia kura ya ndiyo mimi nikisema piga kura ya hapana kosa unalo..WANAFIKI

Wewe hulioni kosa hapo ina maana huoni hilo neno uliloliandika kwa herufi kubwa hulioni wewe?lazime upingwe kwa mitusi yako afu wewe unfikiri nini hapa!
 
Wadau wa JF Great Thinkers,

Kwa wale wanaotaka kuutambua ukweli ili ukweli uwaweke huru na wadumu ktk nuru hiyo daima wataafikiana na uwazi na wataukubali ukweli hata kama unawaumiza saana, watajua ndio mwelekeo wa haki.

Tangu mwaka jana, mara baada ya kumalizika kwa bunge maalumu la katiba, serikali ya ccm ilifanya matamasha, kuhamasisha na kusherehekea 'katiba pendekezwa' kuwa 'ccm wameshinda' dhidi ya 'wapinga rasimu ya 2 ya katiba' kama ilivyowasilishwa na jaji joseph sinde warioba. Hii ikimaanisha kuwa ccm walianza kusherehekea [hadi kucheza taarabu bungeni waziwazi] hata kabla ya kuanza kunadi kwa wananchi ili waelewe kilichoandikwa ndani ya chapisho hilo waliloliita 'katiba pendekezwa' na pia mikakati iliwekwa kuhakikisha kuwa chapisho hili halisambazi mapema sana, halichapishwi nakala nyingi sana, na haliwafikii wengi saana [tofauti na walengwa wa ccm], hii yote ni kuhakikisha kuwa mikakati ya watawala kuelekeza watu waipigie kura ya ndio inafanikiwa siku na wakati utakapofika. Siyo hivyo tu:

* Kikwete mwenyewe na makamu wake kupitia serikali yake yote iliandaa bajeti ya mabilioni ili kuhakikisha vyombo vya habari [hasa vinavyomilikiwa na serikali, na hasa tbc1, magazeti, radio na vile vingi vya binafsi ila vinavyoendeshwa 'kinjaa njaa' kuwa upande wa kuwaelekeza na kuwafundisha wananchi la kufanya] vinaandaa programu kabambe kuhamasisha na kuwaelekeza wananchi popote waipigie katiba pendekezwa kura ya ndiyo!!! Toka mwaka jana hadi leo hii 'mafundisho' hayo na 'maelekezo' hayo ya kupiga kura ya ndiyo yanaendelea!! Ukweli ni uhuru na hatuwezi kufumbia macho unafiki au woga utokanao na watawala, au wapambe wao wanaohemea ktk meza zao ili kushibishwa na kusahau utu wao.

Je, hayo yote yaliyofanyika kwa aidi ya miezi 7, hayakuwa mafundisho, maelekezo na kuingilia uhuru wa mwananchi kusema ndiyo au hapana?? Kwa nini serikali haikuwaelekeza kuwa wasome machapisho hayo ili siku ya kura 'waamue watakavyo'?? Bali inasema wazi wazi kuwa waipigie kura ya ndiyo?? Unafiki! Mhashamu kardinali pengo hakupata ufahamu wa 'matenddo haya maovu' ya serikali na ccm kuingilia 'akili au dhamira' za wananchi [ambao ndio waumini wake pia] kuwaelekeza wapige kura ya ndiyo badala ya kujiamulia wenyewe? Upofu huo!

* Baraza la maaskofu na jumuiya za makanisa ya kikristo yaliyotoa tamko rasmi hivi karibuni la kuwaelimisha waumini na watanzania wote waiosome katiba pendekezwa [ambayo hata hivyo imefichwa-fichwa, tena wasioielewa, na imevurugwa mambo muhimu] na kuipigia kura ya hapana ili 'kuikataa' ni tamko na fundisho sahihi kabisha ni la haki, elimu sahihi, na iliyojaa ukweli na unayoutenga unafiki pembeni na kueneza nuru itawale ili taifa lipate chombo sahihi, na kamilifu kinachoitwa katiba ya wote. Maaskofu na viongozi hawa wa dini walichelewa sana kutoa tamko au mafundisho yao maana serikali ilianza toka mwaka jana, ndipo ukawa nao wakaikabili serikali na ccm kwa kuwaelekeza wafuasi wa wasiipigie kura! Lakini ukweli ni kuwa baraza la maaskofu na jumuiya za makanisa ya kikristo tanzania, wapo sahihi, wapo ktk haki na tunawaomba wasimamie waliyoyasema na kuyaelekeza makanisa yote tanzania nzima, waumini wao wasimame imara kupiga kuwa ya 'hapana'!

Haki inajibiwa kwa haki, na sio dhuluma! Kama serikali imetumia miezi zaidi ya 7 kuwafundisha wananchi wapige kuwa ya 'ndiyo' basi viongozi wetu wa dini wapo sahihi kuwafundisha waumini wao wapige kura ya 'hapana' angalau kwa hizi wiki chache zilizobakia, ili haki ikamilike! Kuwakemea maaskofu kwa tamko lao ni unafiki, upofu na woga wa kuukwepa ukweli, au 'kujipendekeza kwa kaisari'. Mh askofu mkuu kardinali pengo angetambua kuwa kushirikiana na 'kaisari' [serikali] kuwapokonya watauwa haki, 'kuwanyima kauli' au kuwaingiza wtu ktk giza nene kama la kuipa nchi katiba mbovu...hii dhambi haitafutika usoni pako daima!! Hii ni kwaresma...tutende haki-kwa-haki.

Nawasilisha kwa mjadala!

Wakristo wanajua sana kutokana na maandiko kwamba Pilato alimhukumu Yesu kufa msalabani si kwa sababu aliona kosa bali aliogopa macho ya Mayahudi na kubembeleza urafiki na Kaisari. Tuangalie kwa makini hapa, kati ya viongozi wa dini wanaowahamasisha waumini waipigie kura ya hapana katiba, na wale wanaopingana na hao, ni kundi lipi kati yao linaogopa macho ya Mayahudi. Lazima tuongozwe na ukweli, kura hupigwa tu pale ambapo kuna ndiyo na hapana. Kama serikali nzima pamoja na chama tawala wote hao kwa nguvu kabisa wanahamasisha wananchi kupiga kura ya ndiyo, taasisi nyingine ikija na wazo tofauti na hilo katika nchi inayoamini utawala wa sheria na demokrasia, kosa liko wapi. Hapa lazima tuulizane, kati ya wale wanaohamasisha watu waipigie kura ya hapana katiba na wale wanaoiunga mkono serikali inayohamasisha watu waipigie katiba kura ya ndiyo ni nani Pilato anayeogopa macho ya Mayahudi. Kiongozi anajitokeza na kusema kwa uhakika kwamba tusiwafanye waamini wetu wajinga na kuwachagulia cha kusema wakati kiongozi huyo huyo alinyamaza kimya serikali ilipowahamasisha watu wapige kura ya ndiyo kwa nini tusimfananishe na Pilato aliyeogopa macho ya Mayahudi na kubembeleza urafiki na Kaisari.
 
Viongozi wa dini jukumu lao ni kutulea kiroho,huku kwenye siasa naona mmeingia sehemu si yenu na hasa hii hatua mliyofikia ya kutushawishi tukapige kura ya hapana kwenye kura ya maoni kuhusu katiba mpya,nashangaa sana hasa viongozi wangu wa katoliki badala ya kupanga mipango ya kuwainua waumini kiroho na kuondoa mambo yasiyofaA ndani ya kanisa,sasa mmegeuka kuwa wanasiasa au mawakala wa siasa zisizofaa zenye chuki na mgawanyiko,hatutaki utaratibu huu wa kutuandikia waraka na kutulazimisha tuufuate,hatutaki ,tunao utashi na tutaamua wenyewe siku ikifika
 
viongozi wa dini jukumu lao ni kutulea kiroho,huku kwenye siasa naona mmeingia sehemu si yenu
haiwezekani kupata malezi mazuri ya kiroho tu wakati huohuo mwili unadhulumiwa au upo katika mateso.siasa haikwepeki kwa maisha ya sasa.
 
haiwezekani kupata malezi mazuri ya kiroho tu wakati huohuo mwili unadhulumiwa au upo katika mateso.siasa haikwepeki kwa maisha ya sasa.

Biblia imewashinda sahiv wanakimbilia siasa jambo ambalo ni hatari kwani linaleta mvurugano.
 
Viongozi wa dini wafuate wito wao waachane na siasa na wajikite kutusaidia waumini wao badala ya kuanza shughuli za siasa ndani ya makanisa yao na misikiti,tuacheni waamini wenu tuacheni tutaamua wenyewe
 
Back
Top Bottom