Kufungiwa kwa kanisa la “Kiboko ya Wachawi” pongezi kwa Serikali

Kufungiwa kwa kanisa la “Kiboko ya Wachawi” pongezi kwa Serikali

Baraka za Mungu hazinunuliwi Kwa pesa.

Watu hao washughulikiwe, ingawa pia Kwakuwa Serikali Haina dini, ni JUKUMU la viongozi wa Dini kuwatambua hao wahuni na kuwachoma serikalini Ili wachukuliwe hatua.
 
Alikuwa muuza kuku Buza ,anasema alinunua nguvu ya wachawi milioni 7

USSR
Watu wanaonywa Makanisani wawaepuke hao wapigaji lakini hawasikii ngoja wapigwe. Hosea 4: 6 inaonya kabisa "Watu wangu wanaangamizwa kwa kukosa maarifa".Makanisani wanafundishwa jinsi ya kuwatambua hao watu lakini wanaziba masikio wacha wapigwe.
 
Kweli lakini huduma yako ikiwa inadumaza fikra za watu lazima ufungiwe.
Njia sahihi kwa mujibu wa maandiko ni watu kuitafuta kweli wenyewe. Kimsingi huduma nyingi sana ziko kinyume na maandiko, sema nyingine zimekiwa extreme. Serikali haina mamlaka ya kiroho kuamua nani ana hubiri kweli na nani anasema uongo, hiyo ni standard ya neno pekee. Labda kama serikali yetu ina dini.
 
Ndio Mafuta ni ya Mzeituni au ya Manemane Ila haya ya Manemane ni ngumu kuyapata hata ukienda madukani huyapati, Waislamu wanayaita mafuta ya Maiti sababu hupakwa Maiti baada ya kufa Ila usichokijua Mafuta ya Manemane ndio Mafuta yenye nguvu kuliko hata mafuta ya Mzeituni na Watu hawajui na hio elimu hawapewi, Yesu alipozaliwa Wale Mama Jusi ee Bwana kwa sasa utawaita Wanajimu Wazee wa kubashiri walienda kumpeleka vitu vitatu vyenye nguvu ya kifalme na nguvu ya kimuungu ambavyo ni : Dhahabu, Ubani na Manemane, sio na Mzeituni bali na Manemane, ushaelewa? na Manemane sio na Mzeituni ni -na Manemane hawakupeleka Mzeituni wale

Hivyo vitu vitatu ndio vina nguvu ya kimungu nguvu ya kifalme sasa Mafuta ya Manemane kuyapata kwake ni mtiti hata huyo Mwoposa sijui km anayo nilisikia kuhani mmoja wa kuitwa Musa wa pale Kimara Temboni alikua anawauzia Waumini wake Ila sidhani km kweli yalikua Mafuta ya Manemane yale, ukisikia mfalme Daudi alipakwa Mafuta sio ya Mzeituni ni Mafuta ya Manemane

Mwoposa hata siku hasemi Mafuta yake ni Mafuta gani yaan yanatokana Mmea gani Ila ukicheck pale mbele utaona machupa ya Mafuta ya Mzeituni yamejaa sasa Mafuta ya Mzeituni hayana nguvu kuzidi Mafuta ya Manemane na Mafuta ya Mzeituni yanauzwa Madukani yaan yametapakaa vibaya sana ni mengi Mno supamaketi zote yapo unaweza kuyanywa km unavyokunywa juice au Maji, unaweza kupikia kwenye Mboga, unaweza kuyapakaa mwilini km Mafuta ya kawaida, unaweza kuingiziwa kwenye matundu yote ya Mwili bila shida yoyote hayadhuru Mwili hata kidogo

Na Mafuta ya Mzeituni huna haja ya kuyafuata kwa Mwoposa ni vile tu watu hawana akili hawana maarifa hawana uelewa na alivyo Mwehu yule Jamaa hawapi formula hawapi maelezo hawaambii kwamba haya ni Mafuta gani na yanatokana na Mmea gani na ukienda sehemu gani na sehemu gani unayapata huna haja ya kuja kununua kwangu labda upende mwenyewe ili waendelee kuja na kujaza uwanja na yeye aendelee kuwapiga vizuri

Sababu akiwaambia haya ni mafuta ya Mmea fulani haya mafuta ni ya Mzeituni ukienda supamaketi zote utayakuta yanauzwa bei nafuu kabisa si wataacha kununua wataenda kutafuta madukani kwingine na yeye biashara inakua imekufa na kuishia hapo

Ila Mafuta ya Manemane utazinguka sana madukani kote usiyapate mpaka uagize kutoka nje

Nimekutobolea Siri uliyokua hauijui
Tupe sasa siri mnofu kidogo jinsi mafauta ya manemane yanafanya kazi ...
 
Tupe sasa siri mnofu kidogo jinsi mafauta ya manemane yanafanya kazi ...
Hapo sasa ndio penyewe tena umenikumbusha inabidi niweke Bango lenye Namba ya Muamala hapa mchange change Sadaka kwanza kuna wale mafala mafala wa JF wachangie changie Sadaka maana JF kuna mafala na hawaishi na lazima watachangia sasa nikiona zimetosha ndio nawapa Siri ya Mafuta ya Manemane, au hapo unasemaje?
 
Mafala hawaishi hata humu JF wamejaa kibao Wewe jifanye una shida na wakati huna shida Tunga Tunga sentensi ya uongo uongo weka bandiko JF chini weka Namba nakwambia kuna mafala kweli watakurushia Hela za miamala km hauamini kesho fanya jaribio zingatia kuweka Namba ya miamala utawapiga mafala kibao
Hao sio mafala ila ni binadam walio na utu ndani yao.Fala ni ww sasa mwenye shida ukiyedanganya maana mtoaji Katoa kwa moyo wa upendo ww mpokeaji ndo unabeba mikosi.Msifanye watu tushindwe kusaidia watu wenye shida kisa kuna waongo.Pia kumbuka kumsaidia mtu sio ufala.
 
Hao sio mafala ila ni binadam walio na utu ndani yao.Fala ni ww sasa mwenye shida ukiyedanganya maana mtoaji Katoa kwa moyo wa upendo ww mpokeaji ndo unabeba mikosi.Msifanye watu tushindwe kusaidia watu wenye shida kisa kuna waongo.Pia kumbuka kumsaidia mtu sio ufala.
Kwa hio Mwoposa anakusaidia au unamsaidia?
 
Sijaelewa sababu zilizomfanya yeye huyo kiboko ya wachawi kufungiwa!


Wizi kwa njia ya ulaghai,
Wizi wa kuaniniwa.
A.k.a. Utapeli

Unaelewa maana yake?

Kazi ya msingi ya jeshi la polisi ni kulinda raia na mali zao.

Fedha wanazokwapuliwa watu kwa kigezo cha sadaka anayo kimsingi haikupaswa kupangiwa kiasi ni wizi kwa njia ya ulaghai?!
 
Back
Top Bottom