Kufungulia Nchi? Kurudi Kujivunia Umaskini?

Kufungulia Nchi? Kurudi Kujivunia Umaskini?

Umeandika uongo mtupu. Tuonyeshe evidence ya hiki ulichokisema. Wataalam wa kichina ni zao la mambo matatu mkuu.
1. Kundi la wasomi lililokimbia nchi kutokana na kukubaliana na sera mbovu za uchumi na kuwa Diaspora ambapo walirudi kwao baada ya kile kilichoitwa "it does matter whether a cat is black or white as long can catch a mice".
2. Sera za elimu nzuri walizokopi kutoka Ulaya na Marekani
3. Jitihada mahsusi za serikali kupeleka wachina nje kujifunza fani mbalimbali.
Haya mambo yote jiwe hakuyataka. Msiongee vitu msivyo na ujuzi navyo jiwe alikuwa anaitia hii nchi shimoni. Lazima ingeanzia 1986 tulipopata msaada wa "recovery program " kutoka taasisi/jumuiya za kimataifa baada ya kuwa desperate kutokana na kushindwa kwa sera za Mwalimu.
Pumba tupu!
 
1. Huogopi kuitwa MATAGA?

2. Wewe ni Sukuma Gang!

3. Utaambiwa unamchukia Mama 🤣.

4. Usisahau kuwa huyu Mama hakosolewi! Ukithubutu tu, utaambiwa unamtaka Magufuli ila bahati mbaya harudi tena!
Tulieni tu nyie waumini wa kutekana kwa mgongo wa kutuletea maendeleo
 
Chawa wanapata tabu Sana hawakuwa na plan B huku wakiamini mwendazake ataishi milele leo upambe aulipi na hawana plan B.Kubalini matokeo kusafisha mikojo sio dili tena,limeni hata mboga msife njaa.Aliyeondoka atorudi tena.
 
Pumba tupu!
Siyo pumba hizo wacha unazi ulokupofua. Kumbe exposure haijakusaidia ndiyo maana mnaitwa sukuma gang. Maana ukabila na udini haujalishi exposure uliyonayo. Vinapofusha. Ndo maana bado tuko masikini. Unathubutu kuuita ukweli pumba kwasababu hukubaliani nao?
 
Inasikitisha sana ukifuatilia page na post mbalimbali za Chadema wanavyotukanwa kwenye comments na wachangiaji.
Kuna group linaitwa Chadema in blood kule facebook yani kila wanachopost ni kutukanwa tu na watu, huko instagram ndiyo balaa kabisa, njoo Jamii forum hali ni hiyo hiyo!

Nimeangalia comments za kwenye hotuba ya Mbowe aliyoitoa akisema vibaya utawala wa hayati Magufuli, kwa kweli ni huzuni raia walivyomtukana Mbowe. Swali la kujiuliza Chadema imefikaje huku?

Enzi za Dr Slaa ulikuwa unavaa gwanda la Chadema kwa maringo yote ,leo tuvae kwa aibu ya kujifichaficha?
Je Tundu Lisu ameharibu image ya chama baada ya kuanza kutetea mabeberu?

Je ni Mbowe ameharibu image ya chama baada ya kuwa anaangushwa na konyagi anasingizia amepigwa na wasiojulikana?, au ule uongo wake wa kuibia familia inapompeleka mahakamani anasingizia amefungiwa akaunti zake na serikali??

Kiukweli inahitajika tathimini ya haraka sana kuikoa na kuirudisha Chadema kwa wananchi ili waiamini tena kama zamani.
Hahahahahaha leo hii kumbe mitandao ndio kipimo cha mtu kupendwa? Ila kipindi cha kampeni mlidai ni wahuni tu wasiozidi 10.

Messi na Ronaldo wametishia kufunga akaunti zao kisa tu matusi ya mitandaoni ndio sembuse hao MATAGA.

Issue ni field mzee, ndio kuna majibu yote nadhani wote mashahidi hapa kote alipopita Lissu alipokelewa na maelfu ya wananchi kwa bashasha kuliko chama chochote kingine cha upinzani.

Embu kunywa maji glass nzima ukifaidi mafuriko ya Lissu!! Ndio eti Facebook??

 
Acha ukabila kumbe unamchukia Magufuli kwa usukuma wake?

Unafananisha mtu aliyekaa miaka mitano na aliyekaa miaka 25?

Shule? shule gani ilijengwa na serikali au hujui shule za kata zimejengwa na wananchi kwa nguvu zao serikali ilikuwa inafanya hamasa tu.
imekuwa ni bahati mbaya sana kumbe nabishana na mkabila anaechukia wasukuma mimi siwezi wachukia sababu hawajanikosea lolote.
JPM kwangu ni shujaa na sababu nimekueleza.
Angalia ulivyo mjinga...

Unajua maana ya ukabila wewe?

Kusema Gwajima alikuwa anawahamasisha Wasukuma watetee urais wa Jiwe ni ukabila au kupinga ukabila mliokuwa mnahamasishana?!
 
Katika dunia hii ya globalization huwezi kuifungia nchi na wala huwezi kuifungulia nchi na kumeza kila kitu kama dodoki! Kwa hiyo unachofanya ni kuiunganisha nchi na dunia in away ya win win situation.

Sasa, naona kuna upotoshaji wa makusudi kuhusu notion ya Rais Samia kuhusu "Kufungua nchi!" Kwa makusudi kabisa wapotoshaji hawajadili mantiki bali ajenda ovu. Rais amekuwa wazi ana maanisha nini. Kwamba lengo ni kuweka mazingira mazuri ya kibiashara yanayotabirika. Ni pamoja na mfumo wa haki wa kodi, usimamizi na utekelezaji wa sheria na sera ya Uwekezaji na kuondoa urasimu. Kwa kifupi ni kuboresha Mpango wa Blue print.

Utekelezaji wa miradi mikubwa unahitaji pesa nyingi ambazo hazitaathiri shughuli nyingine za kiserikali, kama haki ya kuongeza mishahara watumishi wa umma, dawa hospitalini, elimu bure, mikopo elimu ya juu, ajira na operesheni nyingine. Sasa huwezi kufanya yote hayo bila kuwa na wigo mpana wa wawekezaji wa walipa kodi. Ukiendesha miradi kwa kukopa utaizamisha nchi katika dimbwi la deni lisilolipika! Sasa faida ya globalization ukifungua nchi ; ni kuruhusu mitaji ya uchumi na biashara kumiminika.

Utazalisha kwenye viwanda na ni rahisi pia kufanya Mapinduzi makubwa ya kilimo. Binafsi natamani tupate wawekezaji wakubwa katika sekta ya kilimo ili tufanye Mapinduzi ya Kilimo. Tuna tatizo kubwa la umasikini wa kurithi (Generational poverty), kwa sababu asilimia 70 ya wakulima ni sawa na 'toto lililodumaa!' Kwa hiyo hujikuta masikini wanazaa masikini.

SULUHU: Ni kufungua nchi waje wawekezaji wakubwa katika sekta mbalimbali hasa kilimo, ili tufanye Mapinduzi ya Kilimo, tukuze viwanda, kodi, ajira, uchumi, biashara, tuondoe umasikini wa KURITHI, tu export na kuongeza pato la mtu.

MSIMAMO: Naamini Serikali itafanya haya katika mazingira ya win win situation. Ndicho ninachojua katika focus ya Rais wetu Mama Samia. Tumuunge mkono na tumpe muda.

SISI NI TAIFA.
 
1. Huogopi kuitwa MATAGA?

2. Wewe ni Sukuma Gang!

3. Utaambiwa unamchukia Mama 🤣.

4. Usisahau kuwa huyu Mama hakosolewi! Ukithubutu tu, utaambiwa unamtaka Magufuli ila bahati mbaya harudi tena!
Utaambiwa unamchukia sababu
1. Ni mwanamke
2. Ni muislamu
3. Sababu wewe ni Mataga.

Mama ni Malaika. Amekuja toka mbinguni hakuwepo Duniani. Ni msafi na anawapa watanzania Furaha
 
Yaani haujatofautisha tu kile unataka tuamini?

Umetumia msamiati mzito mno kwenye ubongo wako hata usiuelewe licha ya wewe mwenyewe kuuandika?

Kwamba, wenzake Hadi wanatoka madarakani walijenga leri Hadi Zambia, lakini ukashindwa pia kutofautisha ni reli aina gani hiyo iliyojengwa kipindi hiko na Aina ya reli ambayo Hayati alikuwa ameianzisha

Lakini pia, ukashindwa tena kutofautisha Kati ya miaka 20 ya utawala wa kiongozi mmoja na utawala wa miaka 5 wa kiongozi mwingine!

Nachoweza kusema, ingawa siwexi kukulazimisha chochote, Ila ninaamini kuna mahali nafsi Yako inakusuta, tena inakusuta zaidi unapochanganya na matusi makalii yenye chuki za kipumbavu

Kwani uliambiwa TAZARA ilijengwa kwa miaka 23?

Kwani uliambiwa mashule yalijengwa kwa miaka 23?

Hapo tu unathibitisha ulivyo na ufinyu mdogo wa mawazo, no wonder badala ya kujadilia hoja umeingia na matusi!!

Check your records uone TAZARA ilijengwa kwa muda gani, UDSM ilijengwa kwa muda gani, n.k!
 
Duh....watu mna moyo kweli!

Hivi Askofu Gwajima si anaweza kufufua? Amrudishe tu JPM, kuna watu wanamiss kufokewa na kunyimwa uhuru ndani ya nchi yao!
Labda kama umekufa kichawi lkn kiamri ya Mungu huwezi fufuka.Anafufua waliokufa kichawi
 
Ukimaliza huko ulipo, uje utuambie kama reli ya Tanzania mpaka Zambia nayo ni SGR? Ilijengwa kwa muda gani? Kiasi gani na ubora upi? Je Rais wa wakati huo naye alifia ofisini kabla ya ujenzi kwisha? Baada ya hapo, twende kwenye hizo nukta zilizobaki, moja baada ya nyingine.
Ingawaje umeuliza swali la msingi lakini nimeshakudharau ulipoanza matusi eti kisa tu nimekuelimisha uandike kwa paragraph!
 
Inawezekana wakati mama anaenda kufungulia nchi anaweza kufungulia hizi hisia za kutukuza na kukumbushana juu ya kile kinachoitwa umaskini wetu?

Tunatakiwa kutokujaribu au kuthubutu kufanya makubwa kwa sababu sisi ni masikini? Ndio mwanzo wa kuanza kuombaomba tena...maskini wa fikra hatajiriki na hawezi kutoka kwenye umaskini ambao anaamini unamnufaisha. Inanikumbusha kile kisa cha"Mtumwa Mpendwa" aliyefurahia kupendelewa na bwana wake hadi siku ile yule bwana alipokufa.

Mama ana kazi na kibarua kigumu..maana hata kufoka hawezi na akiwabwatukia watalia hawa kama watoto waliodekezwa, wakadeka, na kudekeka..mtaa mzima utawasikia...na hawanyamazi hadi wapewe "fanta"
Kwn nchi ilikua imefungwa?
 
Angalia ulivyo mjinga...

Kwani uliambiwa TAZARA ilijengwa kwa miaka 23?

Kwani uliambiwa mashule yalijengwa kwa miaka 23?

Hapo tu unathibitisha ulivyo na ufinyu mdogo wa mawazo, no wonder badala ya kujadilia hoja umeingia na matusi!!

Check your records uone TAZARA ilijengwa kwa muda gani, UDSM ilijengwa kwa muda gani, n.k!
Wewe unafahamika, sifa no moja kwako ni ujinga, na ndivyo ulivyo

Nimekuuliza, Tazara na SGR unaanzaje kuzilinganisha?

Hivi unajua kwamba, Tazara inadaiwa mabilioni ya fedha na mchina hajalipwa fedha zake zote?

Jitahidi aghalau kidogo Tu kutofautisha mambo ingawa ni mjinga! Lkn Jitahidi hivyohivyo, mwisho wa siku utaelewa

Halafu tabia yako chafu ya ukabila Jitahidi Nayo uipotezee, vinginevyo, utambue kabisa hapa kwetu, Tunaweza kuwa washindani wa maendeleo Kati ya mtu na mtu na kuhamasishana kufanya maendeleo kama ilivyo Baadhi ya sehemu Kwa wachapa kazi

La hutaki, basi hamia Kenya mkashindane kuoneshana ubabe Kati ya kabila na kabila
 
Kwani bei yako ni kiasi gani usiku mzima?
Tatizo lenu lingine watu dizaini yako, ni ujuaji mwingi bila kujua, kumbe unatumika tu kama malaya muuza nyata barabarani.
Hahaha hamna elimu yeyote, wewe ndiyo hujui kuandika au pengine hujui kusoma. Au umeishiwa ‘nukta za kuongea’ ulizopewa na mabwana zako.
Dadangu vipi tena unaanza matusi? Ni frustration za kuletewa nyumba ndogo na mumeo au frustration za kuingiliwa kwa nguvu kinyume na maumbile na huyo mumeo?

Unaonaje basi ungeenda kumshitaki Dawati la Jinsia badala ya kuleta frustrations zako mitandaoni?!
 
Sikujua kumbe shida yako ni wasukuma. ok bye.
Shida yangu sio Wasukuma, nimekuambia wazi shida yangu ni Gwajima aliyekuwa anawahamiza Wasukuma wautetee urais wa JPM!! Na shida yangu nyingine ni kwa wale wote wanaotetea urais wa JPM sio kwa sababu ya kuongozwa na itikadi bali kwa sababu tu ni Msukuma mwenzao...

Ukweli mchungu ndo huo... mtajibaraguza sana hapa lakini kuna watu kibao hapa JF support yao kwa JPM haiongozwi na itikadi bali ukabila!

Ningekuwa wa maana kama ungekemea upuuzi wa Gwajima aliyekuwa anahamasisha Wasukuma wamtetee JPM, vinginevyo, nawe ni wale wale tu!
 
Inasikitisha sana ukifuatilia page na post mbalimbali za Chadema wanavyotukanwa kwenye comments na wachangiaji.
Kuna group linaitwa Chadema in blood kule facebook yani kila wanachopost ni kutukanwa tu na watu, huko instagram ndiyo balaa kabisa, njoo Jamii forum hali ni hiyo hiyo!

Nimeangalia comments za kwenye hotuba ya Mbowe aliyoitoa akisema vibaya utawala wa hayati Magufuli, kwa kweli ni huzuni raia walivyomtukana Mbowe. Swali la kujiuliza Chadema imefikaje huku?

Enzi za Dr Slaa ulikuwa unavaa gwanda la Chadema kwa maringo yote ,leo tuvae kwa aibu ya kujifichaficha?
Je Tundu Lisu ameharibu image ya chama baada ya kuanza kutetea mabeberu?

Je ni Mbowe ameharibu image ya chama baada ya kuwa anaangushwa na konyagi anasingizia amepigwa na wasiojulikana?, au ule uongo wake wa kuibia familia inapompeleka mahakamani anasingizia amefungiwa akaunti zake na serikali??

Kiukweli inahitajika tathimini ya haraka sana kuikoa na kuirudisha Chadema kwa wananchi ili waiamini tena kama zamani.
Mbona hii haina uhusiano na mada kuu!
 
Labda kama umekufa kichawi lkn kiamri ya Mungu huwezi fufuka.Anafufua waliokufa kichawi
Yap....that's the point. HE IS DEAD!

Tuendelee na tuliye naye sasa. Tuepuke kumpa masifa ya kijinga na asiyo stahili. Penye makosa tukosoe (hata mwenyewe Samia anapenda hivyo). Penye kushauri, tushauri kwa maslahi mapana ya nchi yetu.

Na so far anaonekana ni msikivu zaidi ya mtangulizi wake. Sio mtu wa kujifanya mjuaji wa kila kitu wakati hajui kitu. Si mtumiaji mbaya wa madaraka tuliyompa. Anaheshimu wananchi wake (sio kama yule mwingine anayethubutu kumwambia mwananchi wake ati "abaki na m.avi yake nyumbani"!).

Namuomba tu "akerwe" na umasikini wa watanzania walio wengi. Pesa za umma zielekezwe zaidi kuinua hali za maisha ya watu masikini hasa kwenye elimu na mazingira ya kutolea elimu kwa ujumla. Hizi zawadi za mabenzi (kama kweli ni zawadi na sio replacement) ni non starter!
 
Acha ukabila kumbe unamchukia Magufuli kwa usukuma wake?

Unafananisha mtu aliyekaa miaka mitano na aliyekaa miaka 25?

Shule? shule gani ilijengwa na serikali au hujui shule za kata zimejengwa na wananchi kwa nguvu zao serikali ilikuwa inafanya hamasa tu.
imekuwa ni bahati mbaya sana kumbe nabishana na mkabila anaechukia wasukuma mimi siwezi wachukia sababu hawajanikosea lolote.
JPM kwangu ni shujaa na sababu nimekueleza.
And this was my first post to you...
Kwa lipi?

Hivi una habari wakati yeye kajenga reli ambayo ukiunganishwa vipande vyake haiwezi kuvuka hata Dodoma, wenzake hadi wanatoka madarakani waliacha reli kutoka Tanzania hadi Zambia?

Hivi una habari wakati yeye kakarabati shule pale Ihungo wenzake walijenga mashule nchi mzima?

Hivi una habari wakati yeye kajenga mabweni pale UDSM wenzake wamejenga vyuo?

Hivi una habari wakati yeye amenunua ndege zinazolitia hasara taifa, wenzake walianzisha kampuni frpm the scratch na ikawa na ndege ambazo zilikuwa zinapiga route?

Hivi una habari wakati yeye hata kupandisha madaraja alikuwa hataki, wenzake walikuwa wanaajiri na kupandisha mishahara kila mwaka?

Ukweli upi uliosema wakati unaonesha wazi huna lolote unalojua?! Btw, wapi nimesema suala la Wasukuma kusema ukweli au uongo?! Au unajaribu kupinga suala la Gwajima kuwahamasisha Wasukuma watetee urais wa JPM?
Kuna popote hapo nimekutukana?

L:akini badala ya kujibu hoja, ukakimbilia kusema "Oh, nina chuki na JPM, na pia mkabila"

Ni kutokana na kauli yako hiyo ndo maana nikakuita mjinga, kwa sababu ni ujinga kweli kukimbilia kuwaita watu wana chuki na JPM eti kisa tu hawakubaliani nae? Na ni ujinga kuwaita watu Wakabila kisa tu hawakubaliana na JPM au kusema Gwajima alikuwa anahamasisha Wasukuma wamtetee JPM!

Na hilo ndo tatizo lenu... yaani mnataka WOOOOOOOTE wamuiimbe Jiwe kwa mapambio, na wakitokea wa kumpinga, "oh, mnamchukia"

Kama kueleza udhaifu wake na kumpinga ni kumchukia, LET IT BE.... it's enough mkimpenda nyie!!

Kwani Gwajima hakufanya hicho kitu?
 
Kwanza unalinganisha nchi tofauti kabisa China ya Xiaping na Tanzania ya Samia, hilo ni kosa lakwanza linaloonyesha hujui mlinganisho hata kabla ya kuzungumzia mengine.
China ya Xiaoping ilikuwa tayari. Hawakufungulia tu holela kila takataka zije kuondoa hicho walichokuwa tayari wamekiweka sawa kiwaletee manufa.

Tanzania ya Samia, hivi ni lini imefungwa, na imefungwa vipi? Wawekezaji walizuwiwa kuja kuwekeza; au nati zilikazwa ili wakija hapa wasitufanye kama shamba la bibi?
Nitaonekana kama shabiki wa Magufuli kwenye mambo haya; lakini sikuwahi kupenda yale maovu yake.

Mama asitupeleke tena kujinadi na kunadi mali za taifa hili kwa hasara ya wananchi wake. Ni wakati angalau ahimize, waTanzania wachangamkie fursa nyingi tu zilizopo hapa na aweke mifumo ya kuwawezesha kuliendeleza taifa hili, na siyo kuonyesha kana kwamba maendeleo ya nchi hii bila ya wawekezaji toka nje haiwezi kuendelea. Huku ni kujidharau kusikofaa kabisa.

Na usije ukanirukia na kusema sitaki wawekezaji wa nje. Waje kwa wingi, lakini kwa manufaa ya wananchi wa Tanzania na sio kuja kupora mali zao.
[emoji419][emoji375] ni bora kuwa na wawekezaji wachache wanaokubali win-win agreements....kuliko kuwa na masifa ya kuwa na wawekezaji babaishi

Mzee Kiujumla nimekuelewa na nakubaliana na hoja zako
 
Back
Top Bottom