Kuhusu kununua gesi na mafuta kwa Rouble: Putin awafanya mabeberu Kama watoto wadogo

Kuhusu kununua gesi na mafuta kwa Rouble: Putin awafanya mabeberu Kama watoto wadogo

mbingunikwetu

JF-Expert Member
Joined
Feb 17, 2015
Posts
13,897
Reaction score
18,477
Kulikuwa na kisa kimoja kuwa mama mmoja alikuwa na watoto watatu. Kati ya hao wawili ni watoto wa kambo na mmoja ni WA kwake. Huyu mama alinunua machungwa mawili huku akitaka mtoto wake apate chungwa Zima lakini wale wa kambo wagawane chungwa moja nusu kwa nusu!!

Ili kuwadanganya Hawa watoto wa kambo aliwagawia Kila mmoja chungwa moja na yule wa kwake akakosa!! Halafu akawaambia Hawa wa kambo kuwa Kila mmoja amgawie "kidogo' huyu aliyekosa!! Hawa watoto wakafurahi kuwa wao wamepata chungwa Zima halafu wanamgawia huyu mwenzao "kidogo" tu kwa hiyo wakakubali!!

Yule mama akawaambia niwasaidie kumkatia huyu mwenzenu kidogo na wakakubali. Mama akakata nusu ya Kila chungwa na kumgawia mtoto wake!!

Mwisho wa siku mtoto wake alipata chungwa Zima na hawa watoto wa kambo wakafurahi kuwa wao walipewa chungwa Zima na wakamgawia mwenzao "kidogo" tu maana hawajui kuwa nusu Mara mbili ni chungwa Zima!!

Hicho ndicho alichokifanya Putin, iko hivi:

Urusi aliwekewa vikwazo na mabeberu, moja ya kikwazo ni kwamba haruhusiwi kufanya miamala yoyote kwa kutumia Dola au Euro!!

Kwa maneno mengine ni kuwa Dola na Euro alizokuwa nazo zilikosa kabisa thamani maana Hana jinsi ya kuzitumia. Ndio maana Putin alisema kuuza gesi yake kwa Dola ni sawa na kuuza bure maana hiyo Dola Haina faida kwake.

Putin akasema kuanzia tarehe 31/03/2022 atauza gesi na mafuta kwa Rouble!! Na akasema hakuna gesi na mafuta ya bure! Ukitaka mafuta na gesi ya Urusi tafuta Rouble! Mabeberu wakagoma kabisa kununua kwa Rouble!!

Ilipofika tarehe 30/03/2022 yaani siku moja kabla ya utekelezaji kansela wa Ujerumani akaamua kuongea moja kwa moja na Putin kuhusu jambo Hilo. Hapo ndipo Putin alipomchezea mchezo wa kitoto!! Akamwambia hivi, kwa Sasa hatukubali kuuza mafuta na gesi kwa Dola au Euro!

Nenda ukanunue Rouble halafu Uje ulipie!! Ukiona kwako ni shida kwenda kununua Rouble, tupe sisi hiyo Dola halafu TUTAITUMIA HIYO DOLA KUNUNUA ROUBLE, KWA HIYO WEWE UTAONA UMENUNUA KWA DOLA! KWA MANENO MENGINE MTURUHUSU SISI KUTUMIA HIYO DOLA KUNUNULIA ROUBLE!! (Kumbuka kwa mujibu wa vikwazo Urusi hairuhusiwi kufanya miamala kwa Dola au Euro, kwa hiyo ukikubali pendekezo la Putin ni kwamba unafuta kikwazo Cha awali Ili upate gesi na mafuta). Kwa maneno mengine Kuna vitu viwili Putin amevipataa kwa pamoja:

1. Amewalazimisha mabeberu wakubali Urusi kufanya miamala kwa kutumia Dola kununua Rouble! Kwa hiyo kikwazo Cha kufanya miamala kwa Dola kinakuwa kimekufa kifo Cha Mende asubuhi na mapema

2. Urusi imetimiza lengo lake la kuuza gesi na mafuta kwa Rouble maana Mara beberu anaponunua kwa Dola au Euro, Urusi inaibalilisha hiyo Dola kuwa Rouble!!

Hivyo Urusi kufanikiwa kuhifadhi utajiri wake kwa fedha ya ndani ambayo hakuna mwingine mwenye mamlaka nayo!!
Mwisho wa siku ni kwamba Mabeberu wamenunua kwa Rouble kwa njia ya mzunguko Kama ambavyo yule mama alivyompa mtoto wake chungwa Zima kwa njia ya mzunguko!

Vinginevyo wangesema hatukubali kununua kwa Rouble, tutaendelea kununua kwa Dola, na wewe huruhusiwi kufanya miamala kwa Dola!!

Kwa hiyo hizo Dola tunazokulipa huwezi kuzitumia kwenye miamala yoyote! Lakini mjerumani alinywea akasema SAWA!!
 
Kwani gesi na mafuta urussi anawapa bure ulaya anawauzia kwa hiyo ulaya kugoma kunamfanya urussi naye ku-loose sababu mapato asilimia 30 ya Russia yanatokana na kuuza gesi na mafuta, kwa hiyo ni hasara kwa pande zote
Kwa hoja yako unadhn nan ataipatapata zaid? Hakunaga usawa kat ua muuzaj na mnunuaji endapo mnununuaj hana muuzaj wa ziada na muuzaj ana mnunuaji wa ziada
 
Kwa hoja yako unadhn nan ataipatapata zaid? Hakunaga usawa kat ua muuzaj na mnunuaji endapo mnununuaj hana muuzaj wa ziada na muuzaj ana mnunuaji wa ziada
Wote wataipata, urussi mapato yake makubwa yanatokana na gesi na mafuta na mteja wake Mkubwa ni ulaya

Na ulaya atapata shida lakin huwezi mtuhumu ulaya ata loose huku ukimsifia urussi huo ni ushabiki na sio uhalisia

We kua na duka alafu wateja wasije alafu jidandanye unawakomoa wateja baada ya mda hata wewe utakuja gundua unapata hasara
 
Kwani gesi na mafuta urussi anawapa bure ulaya anawauzia kwa hiyo ulaya kugoma kunamfanya urussi naye ku-loose sababu mapato asilimia 30 ya Russia yanatokana na kuuza gesi na mafuta, kwa hiyo ni hasara kwa pande zote

Iko hivi: Kwa mujibu wa vikwazo alivyowekewa Urusi, kimojawapo ni kuwa Urusi HAIRUHUSIWI KUFANYA MIAMALA KWA KUTUMIA DOLA AU EURO!! Kwa kikwazo hicho Urusi ikiuza gesi na mafuta kwa kupokea Dola au Euro ni Kama imeuza BURE maana Dola ilizopata haiwezi kuzitumia kwenye miamala yoyote!!! Ndiyo maana Urusi ilisema haiwezi kutoa gesi yake bure!! Hiyo ndiyo maana yake!

Lakini Kama ukiikubalia kuzibadilisha hizo Dola ulizonunulia gesi na mafuta kuwa Rouble, hapo ni sawa maana kwa kuwa inaweza kutumia Rouble yake kwenye miamala na huwezi kuingilia mamalaka ya fedha ya Nchi nyingine.
 
Iko hivi: Kwa mujibu wa vikwazo alivyowekewa Urusi, kimojawapo ni kuwa Urusi HAIRUHUSIWI KUFANYA MIAMALA KWA KUTUMIA DOLA AU EURO!! Kwa kikwazo hicho Urusi ikiuza gesi na mafuta kwa kupokea...
Mikataba inasema ulaya atamlipa urussi kwa dollar au euro ikinunua gesi na mafuta hizo narrative Zako unazitolea wapi
 
Wote wataipata, urussi mapato yake makubwa yanatokana na gesi na mafuta na mteja wake Mkubwa ni ulaya

Na ulaya atapata shida lakin huwezi mtuhumu ulaya ata loose huku ukimsifia urussi huo ni ushabiki na sio uhalisia

We kua na duka alafu wateja wasije alafu jidandanye unawakomoa wateja baada ya mda hata wewe utakuja gundua unapata hasara

Sina uhakika Kama unajua undani wa sakata hili. Ni kweli ukiwa na duka unahitaji wateja wake, lakini Hawa wateja wake na fedha unayoweza kuzitumia kwenye miamala! Kama wateja wanakuja na kukupatia fedha ambayo huruhusiwi kuzitumia kwenye miamala ni kwamba unauza bure. Ni Mara mia wateja wasije taratibu nitapata wateja wengine kuliko wale ambao wananioa pesa ambayo wamenizuia kuzitumia!

Urusi alizuiwa kutumia Dola na Euro kwenye miamala, angekuwa ni punguani Sana Kama anger delea kupokea Dola bila kiruhusiwa kuzitumia!

Lakini kwa Sasa wamekubsli aitumie Dola kwa kuzibadilisha kuwa Rouble!! Hapo kingingi Cha mabeberu kwishney!! Mrusi atatunza utajiri wake unaotokana na mafuta na gesi kwa fedha ya ndani Rouble!!
 
Sina uhakika Kama unajua undani wa sakata hili. Ni kweli ukiwa na duka unahitaji wateja wake, lakini Hawa wateja wake na fedha unayoweza kuzitumia kwenye miamala! Kama wateja wanakuja na kukupatia fedha ambayo huruhusiwi kuzitumia kwenye miamala ni kwamba unauza bure. Ni Mara mia wateja wasije taratibu nitapata wateja wengine kuliko wale ambao wananioa pesa ambayo wamenizuia kuzitumia!!
Urusi alizuiwa kutumia Dola na Euro kwenye miamala, angekuwa ni punguani Sana Kama anger delea kupokea Dola bila kiruhusiwa kuzitumia!!
Lakini kwa Sasa wamekubsli aitumie Dola kwa kuzibadilisha kuwa Rouble!! Hapo kingingi Cha mabeberu kwishney!! Mrusi atatunza utajiri wake unaotokana na mafuta na gesi kwa fedha ya ndani Rouble!!
Gesi na mafuta inafaida gani kama huiuzi kwa hiyo unakaa nayo kama mapambo hivi ni vibweka
 
Mikataba inasema ulaya atamlipa urussi kwa dollar au euro ikinunua gesi na mafuta hizo narrative Zako unazitolea wapi

Mkataba lazima uheshimiwe na pande zote mbili!! Mkataba ulipokuwa unawekwa halikuwepo suala la Urusi kutokuruhusiwa kutumia Dola kwenye miamala yake! Upande mmoja umebadilisha mazingira yaliyokuwepo wakati mkataba unawekwa, hivyo kuulazimisha upande mwingine na wenyewe kubadilisha makubaliano!
Nikuulize swali, hivi unadhani Kama wakati wa kujadiliana mkataba kulikuwa na kikwazo Cha Urusi kutokuruhusiwa kutumia Dola kwenye miamala unadhani Urusi ingekubali wanunuaji wa gesi watumie Dola?? Mabeberu ndio wakiukaji wakubwa wa mikataba!! Halafu nikuulize, mkataba waliingia wa kununua mafuta miaka kadhaa mbona ghafla Marekani imesema inasitisha kununua mafuta ya Urusi? Je hapo haijakiuka mkataba? Iko hivi: Mazingira yaliyokuwepo wakati mkataba unaingiwa lazima yasibadilike!! Yakibadilika lazima mkataba urejewe upya!! Huwezi kuendelea na mkataba usiokuletea faida kinyume na makubaliano ya awali!!
 
Gesi na mafuta inafaida gani kama huiuzi kwa hiyo unakaa nayo kama mapambo hivi ni vibweka

Hujafuatilia!! Waswahili wanasema "ukisusa wenzio Wala". Juzi tu hapa India yenye watu wengi kuliko ulaya magharibi yote wameingia makubaliano na Urusi ya kununua gesi na mafuta!!
Hata Kama isingekuwa hivyo ndiyo uuze gesi yako kwa kupokea mawe badala ya pesa? Kwa Sasa Dola ni Kama mawe kwa Urusi maana imewekewa vikwazo vya kutumia Dola na Euro kwenye miamala yake (sijui Kama Hilo unalijua). Hata Kama unataka wateja, ndio uwaruhusu kununua kwa kutumia nawe? Ni afadhali nibaki na gesi yangu nitakuja kupatawateja wengine mbele ya safari!
Halafu Urusi Wana uhakika Kuna Nchi hazina kabisa ubavu wa kususia gesi ya Urusi kwa Sasa. Nchi hizo ni Ujerumani, Hungary nk. Piga ya lazima wakubali masharti ya Urusi angalau kwa Sasa!!
 
Unaelewa unachoelezwa lakini? Hakuna sehemu urusi amekataa kuuza gesi. Ameweka masharti ya jinsi ya kununua gesi yake kua ni rouble, Ulaya wamekataa kununua kwa rouble wamesema mkataba hausemi hivyo, na wala hawajui sehemu ya kuipata hizo roubles.
Sasa urusi kawaambia sawa, nunueni kwa euro au dollar kisha mimi nitazibadilisha kua rubles. Yaani anaenda benki kulipia gesi kwa euro pale benk wanazigeuza kwa Russian ruble. Ni sawa na kufanya kitu kile kile.

Na ulaya wameanza kukubali hilo jambo na jana chancellor wa Germany ameongea na Putin.
 
Mabeberu kuruhusiwa kununua gesi kwa Dola halafu wakubali hiyo Dola ibadilishwe na Urusi iwe Rouble hapo hapo ni sawa na watoto wawili waliopewa chungwa Zima Kila mmoja amkatie nusu yule aliyekosa!! Kama ambavyo yule mama alifanikisha kumpatia mtoto wake chungwa Zima kwa kuwahadaa watoto wa kambo kwa njia ya mzunguko, Hali kadhalika imefanikiwa kuuza gesi yake kwa Rouble kwa njia yamzunguko!! Chezea Putin wewe! Kumbuka kuwa mchakato wa kupokea fedha za mauzo ya gesi utakuwa umekamilika tu pale ambapo hiyo Dola itakuwa imebadilishwa na kuwa Rouble na ndipo mteja atakapopewa gesi au mafuta! Hapo patamu!!
 
Unaelewa unachoelezwa lakini? Hakuna sehemu urusi amekataa kuuza gesi. Ameweka masharti ya jinsi ya kununua gesi yake kua ni rouble, Ulaya wamekataa kununua kwa rouble wamesema mkataba hausemi hivyo, na wala hawajui sehemu ya kuipata hizo roubles.
Sasa urusi kawaambia sawa, nunueni kwa euro au dollar kisha mimi nitazibadilisha kua rubles. Yaani anaenda benki kulipia gesi kwa euro pale benk wanazigeuza kwa Russian ruble. Ni sawa na kufanya kitu kile kile.

Na ulaya wameanza kukubali hilo jambo na jana chancellor wa Germany ameongea na Putin.

Nakushukuru Sana kwa kulifafanua jambo hili kwa maelezo ya kueleweka Sana!! Mwisho wa siku mauzo ya gesi na mafuta yataingiza Rouble kwenye akiba ya Urusi na Siyo Dola!
 
Naisifu Nchi Kama Hungary ambayo imekataa kuwaumiza watu wake kwa ajili tu ya kuwafurshisha mabeberu wenzake! Imegoma kuiwekea vikwazo Urusi!! Imeamua kuzingatia maslahi yake binafsi!
Nchi ya Poland ndiyo inayotia huruma Sana, iko tayari watu wake wanunue gesi Toka Marekani kwa Bei karibuni Mara mbili ya Ile ya Urusi Ili kumfurahisha tu baba wa mabeberu Marekani!
 
Hili saga likiendelea EU itagawanyika, au kuna baadhi ya nchi serikali zitaanguka. Nchi kama italy imepita kipindi kigumu cha Korona, then waje wapate matatizo mengine kwenye gesi na mafuta, kisa kuifurahisha jumuiya nadhani watakataa tu.
Ikiwa russia ata strengthen biashara ya gesi na mafuta na india pamoja na China, basi soko la ulaya hawatakua na uhitaji nao sana kama ilivyo sasa. China na india zina watu karibu bilion 4.

Mpaka leo USA bado anachukua mafuta urusi, wanasema watasitisha by end of April. Lakini wataalamu wa mambo wanaona ni geresha. Sasa nchi za ulaya zitakua makini mno na mienendo ya US.
 
Kwani gesi na mafuta urussi anawapa bure ulaya anawauzia kwa hiyo ulaya kugoma kunamfanya urussi naye ku-loose sababu mapato asilimia 30 ya Russia yanatokana na kuuza gesi na mafuta, kwa hiyo ni hasara kwa pande zote
tofauti urusi atabaki na mafuta na gesi yake huku wengine wakifunga viwanda, kupunguza wafanyakazi na kuongeza mfumuko wa bei
 
Back
Top Bottom