Kuhusu miundombinu Chato, Rais anawaagiza au viongozi wenyewe wanaamua tu kuipeleka huko?

Kuhusu miundombinu Chato, Rais anawaagiza au viongozi wenyewe wanaamua tu kuipeleka huko?

Samiaagain2025

JF-Expert Member
Joined
Dec 2, 2020
Posts
3,626
Reaction score
3,869

WanaJF,

Hongereni na usiku wa mapinduzi ya Zanzibar. Na naenda kwenye mada moja kwa moja.
Kumekuwepo na maoni mengi sana siku za karibuni kuhusu uwekezaji au miondombinu inayojengwa wilayani Chato(nyumbani kwa rais wetu).

Kila kundi wameongea yao; Wanasiasa, wanaharakati, wasomi wa kawaida, wanasheria, viongozi wa dini na makundi mengineyo.

Swali ambalo leo naliweka kama principal question kwa makundi hayo yanayotoa maoni ni hili;
Je, mheshimiwa rais anawatuma viongozi wapeleke au viongozi wanyewe wanaamua kwa utashi wao wapeleke Chato miondombinu hiyo?

Mimi kama Mtanzania nadhani huenda nadharia ya pili ya swali la msingi ina nguvu.

Tunajua wazi viongozi wa siku hizi walioko chini ya rais walivyo na tabia ya kujipendekeza na unafiki, ili tu waendelee kubaki kwenye nyadhifa zao, wakijua pia kuwa Kuna makosa yao fulanifulani mheshimiwa rais anayajua.

Nahitimisha kwa kuwakaribisha Watanzania wenzangu, na nyinyi muone ni nadharia ipi kati ya hizo mbili zilizopo kwenye "Principal question".
 
Katika swali lako yote yanawezekana kwani hakuna anaejua kilichopo akilini kwa viongozi wakuu wa serikali.

Lakini kwa mimi naona nadharia ya pili ina nguvu sana kwa sababu ya ‘woga’
 
Usipoteze mda. Hajengi kwa ajili yake ni kwa ajili ya Watanzania.
 
Thibitisha mkuu!!
Swala la wageni wa kitaifa, hili ni wivu na Maumivu ya waliokosa wingi wa Kura!!
na wewe umetoka wapi ? hebu thibitisha Mirembe hawajakukosea kukufungulia File? katika watu wanaoaminika hapa jukwaani ulikuwa ww na tumeshajadili sana kuhusu Ikulu ni Chamwino na Magogoni
sasa thibitisha aliyeonekana wodini sio ww
 
na wewe umetoka wapi ? hebu thibitisha Mirembe hawajakukosea kukufungulia File? katika watu wanaoaminika hapa jukwaani ulikuwa ww na tumeshajadili sana kuhusu Ikulu ni Chamwino na Magogoni
sasa thibitisha aliyeonekana wodini sio ww
Hasira za kukosa kura za kutosha ndio hizi

Tunaposema haya mambo, tunauhakika
 
Back
Top Bottom