Kuhusu miundombinu Chato, Rais anawaagiza au viongozi wenyewe wanaamua tu kuipeleka huko?

Kuhusu miundombinu Chato, Rais anawaagiza au viongozi wenyewe wanaamua tu kuipeleka huko?


WanaJF,

Hongereni na usiku wa mapinduzi ya Zanzibar. Na naenda kwenye mada moja kwa moja.
Kumekuwepo na maoni mengi sana siku za karibuni kuhusu uwekezaji au miondombinu inayojengwa wilayani Chato(nyumbani kwa rais wetu).

Kila kundi wameongea yao; Wanasiasa, wanaharakati, wasomi wa kawaida, wanasheria, viongozi wa dini na makundi mengineyo.

Swali ambalo leo naliweka kama principal question kwa makundi hayo yanayotoa maoni ni hili;
Je, mheshimiwa rais anawatuma viongozi wapeleke au viongozi wanyewe wanaamua kwa utashi wao wapeleke Chato miondombinu hiyo?

Mimi kama Mtanzania nadhani huenda nadharia ya pili ya swali la msingi ina nguvu.

Tunajua wazi viongozi wa siku hizi walioko chini ya rais walivyo na tabia ya kujipendekeza na unafiki, ili tu waendelee kubaki kwenye nyadhifa zao, wakijua pia kuwa Kuna makosa yao fulanifulani mheshimiwa rais anayajua.

Nahitimisha kwa kuwakaribisha Watanzania wenzangu, na nyinyi muone ni nadharia ipi kati ya hizo mbili zilizopo kwenye "Principal question".

Wakati wa kampeni alisema yeye ndiye anaamua maendeleo yaende wapinakuwahawezi kupeleka maendeleo kwa wanaochagua wapinzani.Kwa hiyo ikowazi nani anayeamua
 
Hata Chato ni Tanzania Ila kwanini kila mradi ni huko Chato? Tanzania ni kubwa sana kuna Mtwara, Kigoma na Mikoa mingine ambayo nayo ilistahili kupata miradi ya mikakati ya maendeleo. Kinachotokea hivi kinaweza kuleta madhara uongozi utakapobadilika. Upo uwezekano kila Rais akafanya upendeleo Kwa kanda atakayotoka. Tuchukue tahadhari Kwa kumshauri Rais wetu.
 
Hata Chato ni Tanzania Ila kwanini kila mradi ni huko Chato? Tanzania ni kubwa sana kuna Mtwara, Kigoma na Mikoa mingine ambayo nayo ilistahili kupata miradi ya mikakati ya maendeleo. Kinachotokea hivi kinaweza kuleta madhara uongozi utakapobadilika. Upo uwezekano kila Rais akafanya upendeleo Kwa kanda atakayotoka. Tuchukue tahadhari Kwa kumshauri Rais wetu.
Na mbaya zaidi,miradi inaenda huko kwa mfululizo! Is it a simple probability or?
 
Rejea kauli zao youtube wakati wa kampeni,ikirudiwa na mtoto wa dada pia kwamba wao ndio uamua wapi maendeleo yaende wapi yasiende.
Rejea kauli ya Mwalimu ikulu ni sehemu takatifu sio KILA mtu ni lzm aende.
 
Kama ni viongozi wanajipendekeza kwa nini Rais akae kimya?Kwa nini Rais asikemee?
Rais alikwisha kemea pale Dodoma mbele ya TAKUKURU. Ila maendeleo haya ni kwa wote iwe chato, iwe Manyoni,iwe Manyara nk.
 
Hii miaka 4 iliyobaki tungependekeza miradi yote iende Chato Ili akastaafu salama na apewe nchi ya Chato atawale milele atuachie nchi yetu tumpe mwingine atakae tumia vizuri Kodi zetu.
 
Toeni ushauri na siyo kukata tamaa.Hakuna mwenye hii nchi,ni yetu sote.
Hii miaka 4 iliyobaki tungependekeza miradi yote iende Chato Ili akastaafu salama na apewe nchi ya Chato atawale milele atuachie nchi yetu tumpe mwingine atakae tumia vizuri Kodi zetu.
 
Anapenda mwenyewe....wangekuwa wamepeleka miundombinu miwili ningesema wanajipendekeza kwake sasa wanapeleka kila kitu unategemea nini?

Anawaambia mwenyewe nataka Chato muweke hiki na hiki.
 

WanaJF,

Hongereni na usiku wa mapinduzi ya Zanzibar. Na naenda kwenye mada moja kwa moja.
Kumekuwepo na maoni mengi sana siku za karibuni kuhusu uwekezaji au miondombinu inayojengwa wilayani Chato(nyumbani kwa rais wetu).

Kila kundi wameongea yao; Wanasiasa, wanaharakati, wasomi wa kawaida, wanasheria, viongozi wa dini na makundi mengineyo.

Swali ambalo leo naliweka kama principal question kwa makundi hayo yanayotoa maoni ni hili;
Je, mheshimiwa rais anawatuma viongozi wapeleke au viongozi wanyewe wanaamua kwa utashi wao wapeleke Chato miondombinu hiyo?

Mimi kama Mtanzania nadhani huenda nadharia ya pili ya swali la msingi ina nguvu.

Tunajua wazi viongozi wa siku hizi walioko chini ya rais walivyo na tabia ya kujipendekeza na unafiki, ili tu waendelee kubaki kwenye nyadhifa zao, wakijua pia kuwa Kuna makosa yao fulanifulani mheshimiwa rais anayajua.

Nahitimisha kwa kuwakaribisha Watanzania wenzangu, na nyinyi muone ni nadharia ipi kati ya hizo mbili zilizopo kwenye "Principal question".

Dr Chalz KIMEI alitatua ilo swali lako kipindi anazindua CRDB ,KIMEI alisema MAGUFULI ndio aliyefanya utafiti na ndio wakaamua wajenge CRDB CHATTLE.

Conclusion: JIWE ndio anatoa maelekezo ya mambo yanayofanyika CHATTLE.
 
Back
Top Bottom