Kuhusu Muungano, Makamo wa Kwanza wa Zanzibar, Adai ni Zanzibar Pekee iliyopoteza Sovereignty, Je Yuko Sahihi?

Kuhusu Muungano, Makamo wa Kwanza wa Zanzibar, Adai ni Zanzibar Pekee iliyopoteza Sovereignty, Je Yuko Sahihi?

Wanabodi,
Leo sikukuu ya Muungano, nafanya mapitio ya baadhi ya mabandiko ya muungano.

Japo waasisi wa muungano wetu huu adhimu ni Nyerere na Karume, muungano ni kama ndoa, kuna mtu ana proposes, mwingine anakubali, ndoa inafungwa. Kwenye muungano wetu huu adhimu, aliye proposes ni Nyerere, Karume akakubali. Nia ya Nyerere ni kwenda kwenye serikali moja. Wito kwa viongozi wetu, kama nia ya kweli ni kudumisha muungano, twende kwenye serikali moja. Tumuenzi Mwalimu Nyerere kwa kuyaishi maono yake!. Nawatakia Muungano Mwema.

Paskali
Mawazo yako hayana tofauti na haya ya Mswekwa, nadhani hamufahamu umuhimu wa utambulisho wa mtu. Kama wazanzibari watakubali ni sawa jaribu kupeleka mswada barazani wa serekali moja. Au ni bunge tuu litapitisha serekali kama lilivyopitisha muungano mawazo ya wazanzibari hayana umuhimu.

Mfano wako pia ni Nyerere alipropose (mwanaume) ukimaanisha Karume (Zanzibar) ndio unaolewa. Sema huu mfano ni wa ndoa za wanaume wawili gay mariage. Kwa sie waislamu ni haramu mifano ya namna hii, sijuwi huko Tanganyika pengine imezoeleka kidogo 🤷‍♂️
 
Mawazo yako hayana tofauti na haya ya Mswekwa, nadhani hamufahamu umuhimu wa utambulisho wa mtu. Kama wazanzibari watakubali ni sawa jaribu kupeleka mswada barazani wa serekali moja. Au ni bunge tuu litapitisha serekali kama lilivyopitisha muungano mawazo ya wazanzibari hayana umuhimu.

Mfano wako pia ni Nyerere alipropose (mwanaume) ukimaanisha Karume (Zanzibar) ndio unaolewa. Sema huu mfano ni wa ndoa za wanaume wawili gay mariage. Kwa sie waislamu ni haramu mifano ya namna hii, sijuwi huko Tanganyika pengine imezoeleka kidogo [emoji2369]
Wavaa kobazi bhna.

Chamsingi kuwe na serikali moja tu.

#MaendeleoHayanaChama
 
Wanabodi,

Wale wenye access na Plus TV, watch now kipindi cha Uso kwa Uso, Makamo wa Kwanza wa Zanzibar, Mhe. Othman Masoud Othman asema uongo wa wazi wa mchana kweupe kuhusu muungano wetu.

Mhe. Masoud anadanganya u kuwa Tanganyika na Zanzibar tulipoungana, ile 1964, ni nchi moja tuu ya Jamhuri ya Watu wa Zanzibar, ndio pekee iliyopoteza sovereignity yake na kuikabidhi kwa Jamhuri ya Tanganyika, lakini Tanganyika haikupoteza sovereignity yake, bali Tanganyika ilibadili tuu jina kutoka Tanganyika kugeuka Tanzania with its sovereignity, kitu ambacho sii kweli!.

Kiukweli kabisa Tanzania bado tunahitaji sana civic éducation kuhusu huu muungano wetu, hata kwa baadhi ya Viongozi wetu, hawaujui vizuri huu muungano wetu hivyo wanapotosha bure watu wao na umma kwa ujumla.

Msingi mkuu wa muungano wetu ni dhima, kuwa sisi Watanzania ni ndugu moja, sisi ni wamoja, hivyo muungano ni kurudisha tuu asili yetu iliyotenganishwa na wakoloni. Dhima hiyo ndio ikatumiwa na Nyerere na Karume kuasisi huu muungano uliopo hadi leo. Hivyo anapoibuka kiongozi yeyote kutaka kuipotosha hii Dhima, Wazalendo tuliopo tunaoujua ukweli huu hatuwezi kunyamaza !.

Ukweli ni kuwa, tulipoungana ile 1964, nchi zote mbili, Jamhuri ya Tanganyika na Jamhuri ya Watu wa Zanzibar, nchi zote mbili zilipoteza sovereignity zake, kwa Zanzibar kupoteza sovereignity yake na kuikabidhi kwa Tanzania, la Tanganyika pia sio tuu ikapoteza sovereignity yake, bali hadi jina lake la Tanganyika na kuikabidhi kwa Tanzania. Tukaunda taifa moja jipya la Tanzania lenye nchi mbili ndani yake na zote hazina sovereignity zake. Nchi iliyokuwa Jamhuri ya Watu wa Zanzibar ikawa haipo tena na nchi ya Jamhuri ya Tanganyika pia ikawa haipo, kilichopo ni nchi moja mpya ya JMT, ambayo ina sehemu mbili, Tanzania Bara iliyokuwa Tanganyika na Tanzania Visiwani, au Tanzania Zanzibar iliyokuwa Jamhuri ya Watu wa Zanzibar.

Mimi sitatizwi na uongo wowote wa kawaida ambao hauna madhara, lakini uongo mkubwa kama huu, kuhusu muungano wetu adhimu, na kutoka kwa mtu mwenye cheo kikubwa kama hiki, aliyekuwa mwanasheria Mkuu wa Zanzibar, huu ni uongo wenye madhara makubwa kwa mustakabali mwema wa muungano wetu. Uongo kama huu una kitu kinachoitwa "ill motives" kwenye "the reasons or motivés behind" Jee lengo la uongo huu ni nini?.

Wakati wa Bunge la Katiba, niliwahi kutoa angalizo hili kuhusu mtu huyu
na kweli Dr. Shein alimshughulikia.

Muungano wetu ni muungano wa nchi mbili zenye hadhi sawa sawa, hakuna mkubwa wala mdogo, ndani ya muungano Tanganyika na Zanzibar ziko sawa sawa na zote mbili zilipoteza sovereignity zake na kuikabidhi kwa serikali ya JMT.

Muungano wetu ni aina ya muungano very unique duniani, kimataifa muungano wetu ni union wa nchi mbili zimeungana na kuunda nchi moja ya Tanzania. Hivyo Tanzania kimataifa ni nchi moja ya JMT, ni taifa moja, ni dola moja yenye rais mmoja, rais wa JMT ambaye ni Samia. Pia tuna Amiri Jeshi Mkuu mmoja tuu. Kimataifa Zanzibar sio nchi, Zanzibar ni sehemu ya JMT yenye utawala wake wa ndani.

Muungano wetu ndani ya muungano, muungano wetu ni muungano wa nchi mbili, yaani federation, hivyo ndani ya muungano, Zanzibar ni nchi, yenye rais wake, serikali yake, ina katiba yake, ambayo mabadiliko yaliyofanywa 2010 kuunda SUK, hayatambuliwi na katiba ya JMT. Kwa vile ndani ya muungano Zanzibar ina mamlaka yake huru bila kuingiliwa na serikali ya JMT, la katiba hiyo ni kwa ajili ya mambo yake ya ndani, japo katiba hiyo iko kinyume cha katiba ya JMT, lakini kwa vile ni ya ndani ya Zanzibar,

Kwa upande wa GNU au SUK,
ni serikali ya coalition. Kwenye coalition zote kuna the majority na a minority. A minority ndani ya coalition anatekeleza sera za à majority. Hivyo Viongozi wa ACT ndani ya serikali ya SUK ya Zanzibar, wanatekeza sera CCM.

Hivyo Viongozi wote wa ACT Wazalendo waliomo ndani ya Serikali ya Umoja wa Kitaifa ya Zanzibar wanapaswa kuhubiri na kutekeleza sera za CCM, hivyo hata wanapoalikwa popote kwenye public, watatanguliza maslahi ya Zanzibar kwa mujibu wa sera za chama tawala.

Sasa mtu huyu ndio yuko ndani ya nyumba, yuko jikoni kabisa, asipothibitiwa, amini usiamini, amini nawaambieni akija tokea kufika kule juu kileleni, very soon, tutagawana fito!.

Paskali
Yaani huyo sijui ndiyo makamo au Makamu....Ukimwangalia utaona ni kama jitu fulani lisiloelewa, ni kulalama kutwa nzima, sijui yukoje?
 
Kwani aliyetakiwa kutangaza msiba ni makamu wa Rais au katibu mkuu kiongozi?
Tanganyika ndio tumepoteza kila kitu. Just imagine now tunaongozwa na huyu bibi mkojani?!!!!
Ndio maana ilimchukua muda sana Dr. Bashiru kutangaza msiba, maana alikuwa anajiuliza huyu bibi ataweza?!!!
 
Wavaa kobazi bhna.

Chamsingi kuwe na serikali moja tu.

#MaendeleoHayanaChama
Kama nilivyoanisha awali pelekeni mswada tuu wa serekali moja. Mtazame alipo Karume wakati wa kuchanganya, halafu utafsiri vizuri ni kwanini Nyerere ndio anachanganya mchanga ? Ukijua hilo utapata tafsiri kamili ya muungano huu na utashi wa Tanganyika kutaka kuimeza Zanzibar (serekali moja).
muunganopiic.jpeg
 
Niwapeni tuu maoni yangu binafsi juu muungano, I am being honest hapa. Sitaki muungano na Tanganyika wala Kenya, napendelea Zanzibar ilio huru na mamlaka yake kamili. Sisemi hivi kwamba namchukia mtu lakini siwezi kujua faida za muungano, faida yake kubwa ninayoifahamu ni kila uchaguzi viboko ili Tanganyika ipate kueka mtu inaemtaka aongoze Zanzibar.

Jengine ni vitunguu na viazi, I really can not tell anything positive at the moment and trust me I am trying hard to think! Lakini hasara za muungano na madhila yake mkiyataka naweza jaza chapisho zima hapa!

Kama muungano una faida basi nadhani ni wazi ukimuuliza mwananchi wa kawaida kule visiwani haswa Pemba, inatakiwa mzanzibari aweze kusema haraka faida. Hata Mswekwa mwenyewe hajaweza kuorodhesha faida za muungano badala ya Nyerere alikunywa mvinyo kwa furaha ya kutimiza ndoto yake.

Obviously Mapinduzi yalipangwa na Nyerere na kuyalinda makes lots of sense.
 
Wanabodi,
Leo sikukuu ya Muungano, nafanya mapitio ya baadhi ya mabandiko ya muungano.

Japo waasisi wa muungano wetu huu adhimu ni Nyerere na Karume, muungano ni kama ndoa, kuna mtu ana proposes, mwingine anakubali, ndoa inafungwa. Kwenye muungano wetu huu adhimu, aliye proposes ni Nyerere, Karume akakubali. Nia ya Nyerere ni kwenda kwenye serikali moja. Wito kwa viongozi wetu, kama nia ya kweli ni kudumisha muungano, twende kwenye serikali moja. Tumuenzi Mwalimu Nyerere kwa kuyaishi maono yake!. Nawatakia Muungano Mwema.

Paskali
Nyerere mwenyewe alikataa pendekezo hilo kwamba utaifa wa Zanzibar utapotea kwenye serikali moja, japokuwa Karume alikubali na hata kuwa tayari kuachia urais ili Nyerere aongoze. Ndiyo maana Wazanzibar wanakosea wanapomlaumu Mwl kwa muungano ambao muundo wake umebakisha utaifa wao na pia wanafaidi vingi ambavyo huenda wasingefaidi kama wangeendelea kubaki nje ya muungano. Bitter Truth.
 
Asante sana, anayezungumza ni Makamo wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Mhe
Othman Masoud Othman Sharrif sio Makamo wa Pili.

Naombeni sana mnisamehe kuwachanganya hawa Makamo wawili, hivyo vyeo vya Zanzibar ambayo havitambuliki ndani ya katiba ya JMT, vinatuchanganya sana sisi waumini wa supremacy ya Katiba. Kama katiba yetu ya JMT haiwatambui Makamo hawa, who M I nisiwachanganye ?

Mixing is highly regreted. Mode please do the needful.
P
Pascal Mayalla, unachanganya maneno haya mawili , makamo na makamu. Usahihi ni Makamu wa kwanza au wa pili wa Rais na siyo Makamo wa kwanza au wa pili wa Rais.
 
Wanabodi,

Wale wenye access na Plus TV, watch now kipindi cha Uso kwa Uso, Makamo wa Kwanza wa Zanzibar, Mhe. Othman Masoud Othman asema uongo wa wazi wa mchana kweupe kuhusu muungano wetu.

Mhe. Masoud anadanganya u kuwa Tanganyika na Zanzibar tulipoungana, ile 1964, ni nchi moja tuu ya Jamhuri ya Watu wa Zanzibar, ndio pekee iliyopoteza sovereignity yake na kuikabidhi kwa Jamhuri ya Tanganyika, lakini Tanganyika haikupoteza sovereignity yake, bali Tanganyika ilibadili tuu jina kutoka Tanganyika kugeuka Tanzania with its sovereignity, kitu ambacho sii kweli!.

Kiukweli kabisa Tanzania bado tunahitaji sana civic éducation kuhusu huu muungano wetu, hata kwa baadhi ya Viongozi wetu, hawaujui vizuri huu muungano wetu hivyo wanapotosha bure watu wao na umma kwa ujumla.

Msingi mkuu wa muungano wetu ni dhima, kuwa sisi Watanzania ni ndugu moja, sisi ni wamoja, hivyo muungano ni kurudisha tuu asili yetu iliyotenganishwa na wakoloni. Dhima hiyo ndio ikatumiwa na Nyerere na Karume kuasisi huu muungano uliopo hadi leo. Hivyo anapoibuka kiongozi yeyote kutaka kuipotosha hii Dhima, Wazalendo tuliopo tunaoujua ukweli huu hatuwezi kunyamaza !.

Ukweli ni kuwa, tulipoungana ile 1964, nchi zote mbili, Jamhuri ya Tanganyika na Jamhuri ya Watu wa Zanzibar, nchi zote mbili zilipoteza sovereignity zake, kwa Zanzibar kupoteza sovereignity yake na kuikabidhi kwa Tanzania, la Tanganyika pia sio tuu ikapoteza sovereignity yake, bali hadi jina lake la Tanganyika na kuikabidhi kwa Tanzania. Tukaunda taifa moja jipya la Tanzania lenye nchi mbili ndani yake na zote hazina sovereignity zake. Nchi iliyokuwa Jamhuri ya Watu wa Zanzibar ikawa haipo tena na nchi ya Jamhuri ya Tanganyika pia ikawa haipo, kilichopo ni nchi moja mpya ya JMT, ambayo ina sehemu mbili, Tanzania Bara iliyokuwa Tanganyika na Tanzania Visiwani, au Tanzania Zanzibar iliyokuwa Jamhuri ya Watu wa Zanzibar.

Mimi sitatizwi na uongo wowote wa kawaida ambao hauna madhara, lakini uongo mkubwa kama huu, kuhusu muungano wetu adhimu, na kutoka kwa mtu mwenye cheo kikubwa kama hiki, aliyekuwa mwanasheria Mkuu wa Zanzibar, huu ni uongo wenye madhara makubwa kwa mustakabali mwema wa muungano wetu. Uongo kama huu una kitu kinachoitwa "ill motives" kwenye "the reasons or motivés behind" Jee lengo la uongo huu ni nini?.

Wakati wa Bunge la Katiba, niliwahi kutoa angalizo hili kuhusu mtu huyu
na kweli Dr. Shein alimshughulikia.

Muungano wetu ni muungano wa nchi mbili zenye hadhi sawa sawa, hakuna mkubwa wala mdogo, ndani ya muungano Tanganyika na Zanzibar ziko sawa sawa na zote mbili zilipoteza sovereignity zake na kuikabidhi kwa serikali ya JMT.

Muungano wetu ni aina ya muungano very unique duniani, kimataifa muungano wetu ni union wa nchi mbili zimeungana na kuunda nchi moja ya Tanzania. Hivyo Tanzania kimataifa ni nchi moja ya JMT, ni taifa moja, ni dola moja yenye rais mmoja, rais wa JMT ambaye ni Samia. Pia tuna Amiri Jeshi Mkuu mmoja tuu. Kimataifa Zanzibar sio nchi, Zanzibar ni sehemu ya JMT yenye utawala wake wa ndani.

Muungano wetu ndani ya muungano, muungano wetu ni muungano wa nchi mbili, yaani federation, hivyo ndani ya muungano, Zanzibar ni nchi, yenye rais wake, serikali yake, ina katiba yake, ambayo mabadiliko yaliyofanywa 2010 kuunda SUK, hayatambuliwi na katiba ya JMT. Kwa vile ndani ya muungano Zanzibar ina mamlaka yake huru bila kuingiliwa na serikali ya JMT, la katiba hiyo ni kwa ajili ya mambo yake ya ndani, japo katiba hiyo iko kinyume cha katiba ya JMT, lakini kwa vile ni ya ndani ya Zanzibar,

Kwa upande wa GNU au SUK,
ni serikali ya coalition. Kwenye coalition zote kuna the majority na a minority. A minority ndani ya coalition anatekeleza sera za à majority. Hivyo Viongozi wa ACT ndani ya serikali ya SUK ya Zanzibar, wanatekeza sera CCM.

Hivyo Viongozi wote wa ACT Wazalendo waliomo ndani ya Serikali ya Umoja wa Kitaifa ya Zanzibar wanapaswa kuhubiri na kutekeleza sera za CCM, hivyo hata wanapoalikwa popote kwenye public, watatanguliza maslahi ya Zanzibar kwa mujibu wa sera za chama tawala.

Sasa mtu huyu ndio yuko ndani ya nyumba, yuko jikoni kabisa, asipothibitiwa, amini usiamini, amini nawaambieni akija tokea kufika kule juu kileleni, very soon, tutagawana fito!.

Paskali
Huyu OMO ulianza kumkosoa toka kitambo.
 
Hili ni wazo lake kuwa walipotenza ni wazanznibar na wala sio Tanganyika. Okay suluhu ni nini? Suluhu ni kuwapa serikali yao huru. Na iwapo kuna faida yoyote ya ushirikiano uwe defined kama ule EAC. Na naona bora iwe hivyo tushirikiane tu kwenye EAC period. Na wao kwa mamia kwa maelfu Warudi kwao Zanzibar. Kwani wabara hawana cha kupeteza kwani walibaguliwa na hawakuruhusiwa kuhodhi ardhi Zanzibar.
 
Wanaoutaka muungano na kuubembeleza zaidi sio wazanzibari ni Watanganyika maana ndio wanaonufaika nao wamekuwa wakiinyonya zanzibar miaka nenda miaka rudi sasa ccm wa zanzibar hawawezi inua mdomo kusema chochote., Ofisi za TRA zimejazana Zanzibar zinakusanya kodi kutoka kwa wazanzibari zikiwanufaisha watanganyika kulipana mishahara, posho na chakula chao cha kila siku.
Zanzibar inachangia 1% ya makusanyo yote ya TRA. Nenda kaangalie facts and figures pale Wizara ya Fedha afu uje hapa tubishane kwenye hili la kodi
 
Kama nchi 2 huru zimeungana kwanini mamlaka ya kuteuwa mabalozi kuwakilisha tanzania wanatoka bara pekee? Wazanzibar wamekuwa wakiukataa muungano miaka yote lakini ni kwa sababu zanzibar imepokwa soverenity yake toka enzi za mchonga meno., kwanini Karume aliuwawa?? lete majibu
Imepokwa sovereigninty ? Vipi kuhusu kutokuwepo kwa serikali ya Tanganyika ilhali kuna Rais wa Zanzibar na serikali ya SMZ kiujumla wake ?
Zanzibar ina makamu wawili wa rais ambao ni wake, jaji mkuu wake, mwanasheria mkuu wake, DPP wake, mamlaka zake za udhibiti uchumi mfano ZURA, ZIPA, Tume yake ya Ushindani wa kibiashara na kdhalika.

Unaweza kunitajia mwanasheria mkuu wa Tanganyika ni nani? Jaji mkuu wa Tanganyika ni nani ? Makamu wa rais wa Tanganyika ni nani ? DPP wa Tanganyika je ?
Na kama hivi vitu vyote Tanganyika haina, je ni nani aliyepokwa sovereignity kati ya Tanganyika na Zanzibar ?
 
Hlo jibu lake lipo wazi kwa kila mwnye akili timamu,nchi ambayo hata kiongozi wake hatambulik kmataifa c usanii huo?????
Kwa mujibu wa muungano huu, Zanzibar ni sehemu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ndio maana hatambuliki kimataifa.

Hebu nijibu hili swali, hivi Scotland ni nchi ?
 
Back
Top Bottom