Kuhusu Muungano, Makamo wa Kwanza wa Zanzibar, Adai ni Zanzibar Pekee iliyopoteza Sovereignty, Je Yuko Sahihi?

Kuhusu Muungano, Makamo wa Kwanza wa Zanzibar, Adai ni Zanzibar Pekee iliyopoteza Sovereignty, Je Yuko Sahihi?

Kwanza rekebisha. Jee in makamo was kwanza au wa Pili.
Kwenye mada.
Mtoa mada wewe ni mkereketwa ulie na chuki zilizojificha dhidi ya Zanzibar.

Kujificha nyuma ya kiini macho cha Tanzania wakati unajua fika by practice na reality kilichoondoka ni neno Tanganyika tu.

Hakuna Muungano huu. Wizara za Tanganyika kwa mambo ya Tanganyika zinaitwa za Tanzania.

Kibaya zaidi kumezaliwa matatizo kibao ya Muungano Leo zinaitwa kero. Lkna shida ni mfumo na muundo.
Linapokuja suala LA haki za Zanzibar, wasomi wote wa Bara na wachambuzi wanakuwa wanafiki.

Nini kimejificha nyuma ya chuki hii?
Ndio maana tuna wazanzibari katika bunge la Tanganyika? Ndio maana tuna mawaziri wazanzibari katika wizara za Tanganyika? Mnafik ni wewe. Na uliyejaa chuki dhidi ya kile unachokiita Tanganyika ni wewe. Ni haki gani ambayo mzanzibari ananyimwa katika serikali ya Tanganyika? Wakati huo huo kuna haki kibao mtanganyika hanazo huko Zanzibar lakini bado unalia na kumuita mtanganyika mbaguzi na mwenye chuki dhidi yenu! Hivi mnatuita machogo kwa sababu mnatupenda sana?

Wewe ni mnafik mkubwa uliyejaa chuki. Ubaya ni kuwa kuna watanganyika wana entertain chuki na unafik wenu kiasi kwamba hamtaki kuambiwa ukweli.

Amandla....
 
Makamu wa Rais yuko sahihi. Zanzibar ilikoma kuwa soverign state. Ikapoteza baadhi ya vyombo muhimu (fedha, majeshi na uraia) kwa Tanganyika. Wakapewa kuwa autonomous state (mambo ambayo nchi nyingine huita provinces - SA, au states huko USA. Zina magavana, mabunge, na hata mahakama zao. Zanzibar iliingizwa kwenye mambo 9 ya muungano ili Tanganyika iyadhibiti. Ndicho anachomaanisha Makamu wa Rais.

Kubadilisha jina la nchi na kuiita Jamhuri ya Muungano wa Tanzania haikuwa ni kuzaliwa kwa taifa jipya - ilikuwa ni kuichukua Zanzibar!! Burma ilitwa Myanmar, Swaziland imeitwa Eswatini na hata Afghanistan imeitwa Imarati ya Kiislamu ya Afghanistan.

Je, Tanganyika ilipoteza nini katika muungano??
 
Huu Muungano una kasoro nyingi za kimuundo ndio maana unakuwa na changamoto nyingi sana. Kibaya zaidi ni kuwa imekosekana nia ya dhati katika kutatua changamoto hizo ndio maana imebaki kuwa kama ndoa ya wanandoa waliochokana lakini wanaogopa talaka.
 
Ukifikiri kwa mawazo huru bila kukariri;

1. Zanzibar haina uwezo wa kuamua lolote kama Tanzania haikubali (Tanzania ni kubwa kuliko Tanganyika au Zanzibar na ni Tanganyika ukiongeza mambo ya Muungano kihalisia).
2. Serikali ya Tanzania inashughulikia mambo yote yaliyokuwa ya Tanganyika pamoja na yale yaliyokubaliwa kwenye muungano.
Tanzania ukitoa mambo ya Muungano unapata Tanganyika.
 
Lini Zanzibar walipoteza?? Wao bado wanasomeka Zanzibar!
Ili kuwa dola kamili/ state, panatakiwa pawepo watu, Serikali, ardhi, na sovereignty/uhuru wa ndani na nje.

Zanzibar ina watu, Serikali, na ardhi ila haina uhuru wa kitaifa na kimataifa, kwa sababu kitaifa mfanya maamuzi mkuu ni Serikali na Bunge la JMT, wakati kimataifa Tanzania ndiyo yenye utambulisho. Pia ulinzi na Usalama ni jukumu la Tanzania.

Kwa hiyo Zanzibar siyo huru wala siyo dola kamili
 
Asante sana, anayezungumza ni Makamo wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Mhe
Othman Masoud Othman Sharrif sio Makamo wa Pili. Naombeni sana mnisamehe kuwachanganya hawa Makamo wawili, hivyo vyeo vya Zanzibar ambayo havitambuliki ndani ya katiba ya JMT, vinatuchanganya sana sisi waumini wa supremacy ya Katiba. Kama katiba yetu ya JMT haiwatambui Makamo hawa, who M I nisiwachanganye ?.
Mixing is highly regreted. Mode please do the needful.
P
Camalad paskali ndiyo maana tunataka muungano uvunjike why usitambue viongozi wetu wa kitaifa Zanzibar?.

Au hujui pasipo SUK nchi inachafuka?.
Wewe hauwatambui ila Rais wako anawatambua ndiyo maana week hii makamu wa pili wa rais wa Zanzibar alikuwa mkoani Tanga kwa ziara ya kichama na serikali akiweka jiwe la msingi kwenye miradi ya maendeleo pia kuimarisha chama.
 
... binafsi naona Znz wana nufaika mnoo na muungano huu, wenzetu wamefanikiwa kulinda haki za raia wao mfano umiliki waa ardhi, pamoja na haki zengine.. wa znz wengi sanaa wana plots huku bara na hakuna waku wauliza ...binafsi mie huwa sielewi kabisaa
Hilo liko wazi na halina mjadala, kwanza wana kauli yao eti ardhi ni ndogo, wakiruhusu wageni ardhi itajaa haraka although wageni wanaruhusiwa kununua apartment zilizo tayari ila si kununua ardhi.

Sheria za visiwani zinambana sana raia kutoka Tanganyika kuliko anayetoka ughaibuni, tena akiwa raia asiye na uwezo kimapato.

Huwa nasema wanaopiga kelele muungano uvunjike ni watu hohehae ila, wenye akili hawawezi ruhusu hilo, sababu mojawapo ni ule uwekezaji walioufanya Tanganyika, yaani Wapemba na waunguja wengi sana wamewekeza bara so, nani ataruhusu arudi kwao Pemba kuacha assets kibao kule chuchubani au mvuti?.
 
Wazanzibari wengi wanajuta kumfukuza Sultan na kuungana na Tanganyika. Tena wanaona yale mapinduzi ni kama yalipangwa na watu ambao si Wazanzibari. Sultan wa Oman angekuwa bado anatawala Zanzibar ingekuwa kama Muscat siku hizi. Utajiri wote wa mafuta ya Oman, Wazanzibari wameukosa. Wamebaki na umasikini na kuburuzwa na serikali ya JMT.
 
Wanabodi
Wale wenye access na Plus TV, watch now kipindi cha Uso kwa Uso, Makamo wa Kwanza wa Zanzibar, Mhe. Othman Masoud Othman asema uongo wa wazi wa mchana kweupe kuhusu muungano wetu.

Masoud Masoud anadanganya uongo kuwa eti tulipoungana, ile 1964, ni nchi moja tuu ya Zanzibar, ndio pekee iliyopoteza sovereignity yake na kuikabidhi kwa serikali ya Tanganyika, lakini Tanganyika haikupoteza sovereignity yake, kitu ambacho sii kweli.

Ukweli ni kuwa, tulipoungana nchi zote mbili, Jamhuri ya Tanganyika na Jamhuri ya Watu wa Zanzibar, nchi zote mbili zilipoteza sovereignity zake, kwa Zanzibar kupoteza sovereignity yake na Tanganyika pia ikapoteza sovereignity yake, tukaunda nchi moja mpya ya Tanzania. Nchi ya Zanzibar haipo na nchi ya Tanganyika pia haipo, kilichopo ni nchi moja mpya ya JMT, ambayo ina sehemu mbili, Tanzania Bara iliyokuwa Tanganyika na Tanzania Visiwani, au Tanzania Zanzibar iliyokuwa Jamhuri ya Watu wa Zanzibar.

Mimi sitatizwi na uongo wowote wa kawaida ambao hauna madhara, lakini uongo mkubwa kama huu, kuhusu muungano wetu adhimu, la kutoka kwa mtu mwenye cheo kikubwa kama hiki, ni uongo wenye madhara makubwa sana kwa mustakabali mwema wa muungano wetu ambao una ill motives behind. Jee lengo la uongo huu ni nini?.

Wakati wa Bunge la Katiba, niliwahi kutoa angalizo hili kuhusu mtu huyu
na kweli Dr. Shein alimshughulikia.

Muungano wetu ni muungano wa nchi mbili zenye hadhi sawa sawa, hakuna mkubwa wala mdogo, ndani ya muungano Tanganyika na Zanzibar ziko sawa sawa na zote mbili zilipoteza sovereignity zake na kuikabidhi kwa serikali ya JMT.

Muungano wetu ni aina ya muungano very unique duniani, kimataifa muungano wetu ni union wa nchi mbili zimeungana na kuunda nchi moja ya Tanzania. Hivyo Tanzania kimataifa ni nchi moja ya JMT, ni taifa moja, ni dola moja yenye rais mmoja, rais wa JMT ambaye ni Samia. Pia tuna Amiri Jeshi Mkuu mmoja tuu. Kimataifa Zanzibar sio nchi, Zanzibar ni sehemu ya JMT yenye utawala wake wa ndani.

Muungano wetu ndani ya muungano, muungano wetu ni muungano wa nchi mbili, yaani federation, hivyo ndani ya muungano, Zanzibar ni nchi, yenye rais wake, serikali yake, ina katiba yake, ambayo mabadiliko yaliyofanywa 2010 kuunda SUK, hayatambuliwi na katiba ya JMT. Kwa vile ndani ya muungano Zanzibar ina mamlaka yake huru bila kuingiliwa na serikali ya JMT, la katiba hiyo ni kwa ajili ya mambo yake ya ndani, japo katiba hiyo iko kinyume cha katiba ya JMT, lakini kwa vile ni ya ndani ya Zanzibar,

Sasa mtu huyu ndio yuko ndani ya nyumba, yuko jikoni kabisa, asipothibitiwa, amini usiamini, amini nawaambieni akija tokea kufika kule juu kileleni, very soon, tutagawana fito!.

Paskali
Correction

Asante sana, anayezungumza ni Makamo wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Mhe
Othman Masoud Othman Sharrif sio Makamo wa Pili. Naombeni sana mnisamehe kuwachanganya hawa Makamo wawili, hivyo vyeo vya Zanzibar ambayo havitambuliki ndani ya katiba ya JMT, vinatuchanganya sana sisi waumini wa supremacy ya Katiba. Kama katiba yetu ya JMT haiwatambui Makamo hawa, who M I nisiwachanganye ?.
Mixing is highly regreted. Mode please do the needful.
P
Wewe unaijua Zanzibar kuliko Masoud Othman ?? Be serious man .... Wasukuma na Zanzibar wapi na wapi !!

Masoud Othman kaongea ukweli ambao ninyi wengi wenu mmedanganywa na wengine hawataki kuusikia.
 
Wanabodi
Wale wenye access na Plus TV, watch now kipindi cha Uso kwa Uso, Makamo wa Kwanza wa Zanzibar, Mhe. Othman Masoud Othman asema uongo wa wazi wa mchana kweupe kuhusu muungano wetu.

Masoud Masoud anadanganya uongo kuwa eti tulipoungana, ile 1964, ni nchi moja tuu ya Zanzibar, ndio pekee iliyopoteza sovereignity yake na kuikabidhi kwa serikali ya Tanganyika, lakini Tanganyika haikupoteza sovereignity yake, kitu ambacho sii kweli.

Ukweli ni kuwa, tulipoungana nchi zote mbili, Jamhuri ya Tanganyika na Jamhuri ya Watu wa Zanzibar, nchi zote mbili zilipoteza sovereignity zake, kwa Zanzibar kupoteza sovereignity yake na Tanganyika pia ikapoteza sovereignity yake, tukaunda nchi moja mpya ya Tanzania. Nchi ya Zanzibar haipo na nchi ya Tanganyika pia haipo, kilichopo ni nchi moja mpya ya JMT, ambayo ina sehemu mbili, Tanzania Bara iliyokuwa Tanganyika na Tanzania Visiwani, au Tanzania Zanzibar iliyokuwa Jamhuri ya Watu wa Zanzibar.

Mimi sitatizwi na uongo wowote wa kawaida ambao hauna madhara, lakini uongo mkubwa kama huu, kuhusu muungano wetu adhimu, la kutoka kwa mtu mwenye cheo kikubwa kama hiki, ni uongo wenye madhara makubwa sana kwa mustakabali mwema wa muungano wetu ambao una ill motives behind. Jee lengo la uongo huu ni nini?.

Wakati wa Bunge la Katiba, niliwahi kutoa angalizo hili kuhusu mtu huyu
na kweli Dr. Shein alimshughulikia.

Muungano wetu ni muungano wa nchi mbili zenye hadhi sawa sawa, hakuna mkubwa wala mdogo, ndani ya muungano Tanganyika na Zanzibar ziko sawa sawa na zote mbili zilipoteza sovereignity zake na kuikabidhi kwa serikali ya JMT.

Muungano wetu ni aina ya muungano very unique duniani, kimataifa muungano wetu ni union wa nchi mbili zimeungana na kuunda nchi moja ya Tanzania. Hivyo Tanzania kimataifa ni nchi moja ya JMT, ni taifa moja, ni dola moja yenye rais mmoja, rais wa JMT ambaye ni Samia. Pia tuna Amiri Jeshi Mkuu mmoja tuu. Kimataifa Zanzibar sio nchi, Zanzibar ni sehemu ya JMT yenye utawala wake wa ndani.

Muungano wetu ndani ya muungano, muungano wetu ni muungano wa nchi mbili, yaani federation, hivyo ndani ya muungano, Zanzibar ni nchi, yenye rais wake, serikali yake, ina katiba yake, ambayo mabadiliko yaliyofanywa 2010 kuunda SUK, hayatambuliwi na katiba ya JMT. Kwa vile ndani ya muungano Zanzibar ina mamlaka yake huru bila kuingiliwa na serikali ya JMT, la katiba hiyo ni kwa ajili ya mambo yake ya ndani, japo katiba hiyo iko kinyume cha katiba ya JMT, lakini kwa vile ni ya ndani ya Zanzibar,

Sasa mtu huyu ndio yuko ndani ya nyumba, yuko jikoni kabisa, asipothibitiwa, amini usiamini, amini nawaambieni akija tokea kufika kule juu kileleni, very soon, tutagawana fito!.

Paskali
Correction

Asante sana, anayezungumza ni Makamo wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Mhe
Othman Masoud Othman Sharrif sio Makamo wa Pili. Naombeni sana mnisamehe kuwachanganya hawa Makamo wawili, hivyo vyeo vya Zanzibar ambayo havitambuliki ndani ya katiba ya JMT, vinatuchanganya sana sisi waumini wa supremacy ya Katiba. Kama katiba yetu ya JMT haiwatambui Makamo hawa, who M I nisiwachanganye ?.
Mixing is highly regreted. Mode please do the needful.
P
Kwa nini vibali vya maendeleo ya zanzibar vinatoka Tanganyika., mfano mduchu juzi kuhusu babara ya wete mkoani, kwann nje hakuna balozi yoyote kutoka zanzibar? Othman alimaanisha yote hayo
 
Ukifikiri kwa mawazo huru bila kukariri;

1. Zanzibar haina uwezo wa kuamua lolote kama Tanzania haikubali (Tanzania ni kubwa kuliko Tanganyika au Zanzibar na ni Tanganyika ukiongeza mambo ya Muungano kihalisia).
2. Serikali ya Tanzania inashughulikia mambo yote yaliyokuwa ya Tanganyika pamoja na yale yaliyokubaliwa kwenye muungano.
Tanzania ukitoa mambo ya Muungano unapata Tanganyika.
Waziri wa Ujenzi wa hiyo unayoiita Tanganyika ni Mpemba. Wabunge kutoka Zanzibar wana uwezo wa kuchangia jambo lolote katika Bunge la Tanganyika. Niambie kuna mawaziri wangapi watanganyika katika SMZ? Au katika BMZ? Wazanzibari hawafiki milioni tatu lakini kwenye hilo bunge la Tanganyika yenye zaidi ya watu milioni 58 wanapewa haki sawa na watanganyika bila kubaguliwa!

Amandla...
 
Kwa nini vibali vya maendeleo ya zanzibar vinatoka Tanganyika., mfano mduchu juzi kuhusu babara ya wete mkoani, kwann nje hakuna balozi yoyote kutoka zanzibar? Othman alimaanisha yote hayo
Umewahi sikia mahali kuna ubalozi wa Scotland, Wales, Northern Ireland, Catalonia, California, Texas, Kerala n.k.? Tangu lini umesikia barabara za Zanzibar zimeingia kwenye bajeti ya Tanganyika? Kama mnataka kuwa na balozi zenu vunjeni Muungano. Badala ya kuzunguka mbuyu mwambieni Rais wa JMT kuwa hamtaki Muungano, sio kujificha kwenye kile mnachoita kero. Pitisheni muswaada kwenye Baraza lenu la kusema kuwa hamtaki Muungano. Chama chake cha ACT Wazalendo kiweke kwenye ilani yake kuwa hakitaki Muungano. Shida kwani iko wapi? Fanyeni hivyo halafu muuone watanganyika wangapi watawabembeleza. Na mnaweza kukuta ndugu zenu wenyewe watawageuka.

Amandla...
 
Ukifikiri kwa mawazo huru bila kukariri;

1. Zanzibar haina uwezo wa kuamua lolote kama Tanzania haikubali (Tanzania ni kubwa kuliko Tanganyika au Zanzibar na ni Tanganyika ukiongeza mambo ya Muungano kihalisia).
2. Serikali ya Tanzania inashughulikia mambo yote yaliyokuwa ya Tanganyika pamoja na yale yaliyokubaliwa kwenye muungano.
Tanzania ukitoa mambo ya Muungano unapata Tanganyika.
Mkuu kipengele cha kwanza sio sahihi hata kidogo... Znz ina jiamulia mambo yake yote ambayo sio ya muungano na mengine kadhaa mfano mdogo swala la ardhi wameamua kuwa sideline wa tanganyika, znz walijiamukia kuwa na serikali ya maridhiano, znz walijiamulia kuwa na vitambulisho vya mkaazi ambavyo ww mbara huwezi pewa ng'oooo lkn huku bara vya NIDA ndivyo ivyo ivyo tuna gawana nawo
 
Back
Top Bottom