Pre GE2025 Kuhusu nafasi ya Urais ndani ya CCM: Kinana amedanganya, na kwa vyovyote hana dhamira njema

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Ngoja tuone !
Ila inafikirisha sana !
Pia Kinana ametumia neno “ sio dhambi “ kama atapitishwa !
Hiyo ina maana lipo fukuto Chamani au labda ni mawazo yake tu !
Ngoja tuone !!
 
Hapo Namba 2 si sawa. Magufuli na Samia walipitia mchakato mmoja hadi Magufuli akawa Rais. Kura alizopata Magufuli kwenye Urais kwenye ile karatasi alikuwepo pia Samia. Kuna watu walimchagua Magufuli kwa sababu tu ya uwepo wa Samia. Si sawa kusema eti hakupigiwa kura.
 
Rais wa sasa ni Rais wa dharula. Katiba, kwa kuzingatia ukweli kuwa nchi isiingie kwenye mkanganyiko pale inapotokea dharula ya kifo cha Rais akiwa madarkani,
Ni mgombea mwenza hata 2020 aligombea kwa tiketi moja na JPM na walikua wote kwenye ballot paper. So sio Rais wa dharura bali Makamu wa Rais ambaye alipigiwa kura na wananchi.

Sasa kama aliaminiwa awe number mbili, yule top akifariki kivipi asiaminiwe? Kama wao walimchagua kwa huruma za muungano au gender balance its up to them ila katiba lazima iheshimiwe.

Ni hivi, Samia ndio mgombea wa Ccm 2025 kwa sababu ya precedence ya 2020 na 2010, kama JPM anger uhuru Membe achukue fomu hata leo wangepata confidence ya kupambana dhidi ya samia.

Sasa kama vile wao walivyokataza asichukue mtu fomu 2020 basi ndio wembe ule ule atautumia samia kufukuza wote wenye kutaka fomu ya Urais.
 
Hiyo ina maana lipo fukuto Chamani
Fukuto gani, si walimchagua kuwa mwenyekiti wao kwa kura zote za ndio, sasa nani wa kumchallenge Mwenyekiti? Ana uwezo wa kufukuza kamati kuu nzima na hamna pa kumpeleka. Ndugai huyo hapo alipojaribu kumpinga alipata nini? Na leo keshasahaulika kabisa.
 
Usipotoshe.

Mchakato ndani ya vyama kila mwanachama anachukua fomu mwenyewe hachukui na mgombea mwenza.

Akishapitishwa na chama anatakiwa sasa achague mgombea mwenza kuendana na matakwa ya tume ya uchaguzi ya Taifa na ndio kilichofanyika.

Kilichombeba Magufuli ni historia yake ya kiutendaji kama waziri katika wizara mbali mbali.

Rekodi ya Magufuli pekee ilitosha kumbeba bila kujali nani alikua mgombea mwenza.

Kama alivyowahi kusema mwenyewe kuwa yeye alipenda Mwinyi awe mgombea mwenza ila Chama kwa sababu zao wenyewe wakampendekeza Samia.

Hivyo swala la Samia kumbeba Magufuli hapo liondoe bali itambulike kuwa Magufuli ndie alimbeba Samia.

Hata akikataa ila ukweli ndio huo.
 
Acha Ujinga, Magu ilikuwa Awamu yake ya pili,alipitia mchujo na kushinda.

Sa100 hajawahi pigiwa kura popote kabla, jambo Hilo ni LAZIMA lifanyike nw!!
 
Ndio ameishatuchagulia rais hivyo 2025,kwa katiba iliyopo hta CCM wakaweka njiwe bado litapita kwa kura nyingi zaidi ya asilimia 80%,
Sio litapita, sema watatangazwa kwa kura zaidi ya 80%. Kuna tofauti ya kupata na kutangazwa.
 
Acha Ujinga, Magu ilikuwa Awamu yake ya pili,alipitia mchujo na kushinda.

Sa100 hajawahi pigiwa kura popote kabla, jambo Hilo ni LAZIMA lifanyike nw!!
Hata zikipigwa kura ni kiini macho tu, atatangazwa kwa idadi ya kura azitakazo. Dhalimu magu ndio aliharibu heshima ya uchaguzi ndani ya chama chake na nchi hii.
 
Hata zikipigwa kura ni kiini macho tu, atatangazwa kwa idadi ya kura azitakazo. Dhalimu magu ndio aliharibu heshima ya uchaguzi ndani ya chama chake na nchi hii.
Ndo Sa100 pia apitie mchujo, hakuna anaeungana na Magu katika wizi wa uchaguzi.

Hilo liko wazi binafsi nilipinga uchaguzi huo.

Magu tulimuunga mkono Kwa Uzalendo na uthubutu na uchapakazi.

Lazima wanachama waruhusiwe kuchukua fomu na mchujo ufanyike.
 
Nikikuteua wewe kuwa manager, na mwingine kama msaidizi wako, haimaanishi huyo msaidizi wako anafaa kuwa meneji bali ana uwezo wa kuziba pengo endapo katika hali ya dharula wewe huwezi kufanya mambo fulani au akatimiza majukumu yako wewe kama meneja kwa muda fulani tu kwa sababu wewe hupo.

Kimantiki ni kwamba wale waliomchagua Magufuli walikubali Magufuli kuwa Rais na Samia kuwa msaidizi wake, hawakumchagua Magufuli na Samia, wote kwa pamoja kuwa Marais. Msaidizi ni mtu anayepokea maagizo au maelekezo na siye anayefanya maamuzi ya mwisho.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…