Pre GE2025 Kuhusu nafasi ya Urais ndani ya CCM: Kinana amedanganya, na kwa vyovyote hana dhamira njema

Pre GE2025 Kuhusu nafasi ya Urais ndani ya CCM: Kinana amedanganya, na kwa vyovyote hana dhamira njema

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Ndo Sa100 pia apitie mchujo, hakuna anaeungana na Magu katika wizi wa uchaguzi.

Hilo liko wazi binafsi nilipinga uchaguzi huo.

Magu tulimuunga mkono Kwa Uzalendo na uthubutu na uchapakazi.

Lazima wanachama waruhusiwe kuchukua fomu na mchujo ufanyike.
Apitoe mchujo au usanii?
 
Mama Samia Suluhu Hasan, huwa anapita humu. Bila shaka atazingatia ushauri wako bora kabisa, huku akiwapuuza chawa wanaotaka aminye demokrasia ndani ya chama. Na kama mimi kumshauri pia kwa kulinda heshima yake na kulinda uislamu wake ningemshauri aache kugombea 2025 alichopewa na Mungu bila kukitaabikia kinamtosha. Isipokuwa akina Lucas Mwashambwa.
 
Apitoe mchujo au usanii?
Usanii, sawa kabisa, kama tu usanii wa Uchaguzi wa kura ya Urais ilhali inajulikana akitangazwa hakuna Rufaa popote.

Huo usanii ufanyike.

HOFU ya nini ilhali anajua atapita?
 
Umeongea vyema sana mkuu, kuna kipindi waziri mkuu wa Uingereza mama Susan May aliitisha uchaguzi wa mapema kutafuta kuungwa mkono zaidi, na hata waziri mkuu wa Japan Shinzo Abe aliwahi fanya..........sasa unajiuliza hawa viongozi wa wadanganyika wanahofia nini kuingia kwenye mchakato wa kutafuta kuungwa mkono? ngozi nyeusi tuna matatizo ya kiasili, si bure....

Na ukumbuke bi hadija hakuwahi kupitishwa na mchakato wa uchaguzi ndani ya chama chake kuwania nafasi ya urais.​
 
Kinana amesema uwongo kuwa eti CCM imekuwa na utaratibu wa kutoruhusu kuwepo na ushindani ndani ya CCM wa kumpata mgombea wa chama kwenye kiti cha Urais pale ambapo Rais aliyepo madarakani hajamaliza vipindi viwili vya Urais wake. Amesema hayo akimlenga Rais wa Sasa.

Uwongo wa Kinana upo katika ukweli ufuatao:

1. Huko nyuna hakujawahi kuwa na Rais wa kiolpindi cha dharula. Hivyo hakujawahi kuwa na desturi ya kumpitisha Rais wa Dharula bila ya kura za wajumbe wa vikao vikuu vitatu vya CCM. Kifo cha Rais Magufuli ndiyo ilikuwa dharula ya kwanza kwa Taifa.

2. Rais wa sasa hakuwahi kupigiwa kura na wajumbe wa Kamati Kuu, Halmashauri Kuu na Mkutano Mkuu kuwa mgombea wa CCM kwenye kiti cha Urais. Utamaduni anaousema ni kwa Rais aliyepo madarkani ambaye kipindi chake cha kwanza cha Urais alichaguliwa na vikao vilivyotajwa kuwa mgombea wa Urais kupitia CCM. Lakini siyo kwa mtu ambaye hajawahi kupigiwa kura hata moja na wajumbe wa vikao hivyo kwa nafasi ya Urais.

3. Rais wa sasa ni Rais wa dharula. Katiba, kwa kuzingatia ukweli kuwa nchi isiingie kwenye mkanganyiko pale inapotokea dharula ya kifo cha Rais akiwa madarkani, ndiyo inayotamka ni nani awe Rais wa dharula katika kipindi hicho cha dharula. Huyu anakuwa Rais wa dharula mpaka wakati ule ambapo chama kitampata mtu ambaye vikao vya chama vitamchagua mtu ambaye wanataka awe ngombea wa Urais kupitia chama chao. Kulazimisha Rais wa dharula, ambaye hakuna uhakika kama chama kinaridhika awe mgombea wao kwa nafasi ya Urais, ni kukiuka misingi mikuu ya demokrasia.

Kwenye nchi zenye watu wenye akili timamu, ambako viongozi nao wana akili timamu, siku zote viongozi hutafuta uhakika wa kutaka kujua kama watu wanaotaka wawaongoze wanataka waongozwe na viongozi husika. Watawala wanapojua kuwa wananchi wao wanawataka wawaongoze, inawapa nguvu viongozi katika utendaji wao wa kazi kwa sababu wanatambua kuwa nyuma yao kuna umma mkubwa wa watu unaowataka wao viongozi wawe mbele yao katika utendaji wao wa kuyaongoza mataifa yao. Huku kwetu, sijui ni ujinga, upunguani au ushetani, watawala wanaogopa wananchi kuwadhihirishia viongozi kama wanawataka wawe viongozi wao au la. Ndiyo maana akina Kinana wanatamka wazi kuwa ndani ya CCM hakutakuwa na nafasi kwa wanaCCM kuthibitisha kama wanataka aliyekuwa Rais wa dharula, sasa awe Rais wa kuchaguliwa au apumzike na kupewa heshima yake ya kuiongoza nchi katika kipindi cha dharula.
Hongera kwa andiko elimishi na la ukweli mtupu. Kwa andiko hili umenipa matumaini kwamba bado kuna wa -Tanzania wenye busara!!!!!
 
Nikikuteua wewe kuwa manager, na mwingine kama msaidizi wako, haimaanishi huyo msaidizi wako anafaa kuwa meneji bali ana uwezo wa kuziba pengo endapo katika hali ya dharula wewe huwezi kufanya mambo fulani au akatimiza majukumu yako wewe kama meneja kwa muda fulani tu kwa sababu wewe hupo.

Kimantiki ni kwamba wale waliomchagua Magufuli walikubali Magufuli kuwa Rais na Samia kuwa msaidizi wake, hawakumchagua Magufuli na Samia, wote kwa pamoja kuwa Marais. Msaidizi ni mtu anayepokea maagizo au maelekezo na siye anayefanya maamuzi ya mwisho.
Kwenye karatasi ya kura alikuwepo JPM na Samia sio kwamba alikuwepo JPM pekee so kusema alichaguliwa JPM sio samia inakuwa sio sawa.

Pili huwezi sema umemteua makamu eti kuziba pengo kwa muda tu ilihali katiba ipo wazi ukisafiri, ukiugua, au kufariki basi Makamu ndio anakua Rais!! Huwezi risk kiasi hiko.

Nachoweza kusema, next time mtakua makini kwenye kuchagua wagombea wenza na hili ni mpaka chadema walimuweka yule Said Issa kama makamu mwenyekiti. At some point Lissu alikua abroad na Mbowe alikua jela, yule jamaa akawa mwenyekiti kwa almost mwezi mzima na ilihali hamna anachoweza!!
 
Fukuto gani, si walimchagua kuwa mwenyekiti wao kwa kura zote za ndio, sasa nani wa kumchallenge Mwenyekiti? Ana uwezo wa kufukuza kamati kuu nzima na hamna pa kumpeleka. Ndugai huyo hapo alipojaribu kumpinga alipata nini? Na leo keshasahaulika kabisa.
Na huo ndio ukweli mchungu !
🙏🙏
 
Hapo Namba 2 si sawa. Magufuli na Samia walipitia mchakato mmoja hadi Magufuli akawa Rais. Kura alizopata Magufuli kwenye Urais kwenye ile karatasi alikuwepo pia Samia. Kuna watu walimchagua Magufuli kwa sababu tu ya uwepo wa Samia. Si sawa kusema eti hakupigiwa kura.

Samia hakupigiwa kura hata 1 kwaajili ya kuwa Rais. Kila aloyempigia kura Magufuli, alipiga kura ya Magufuli kuwa Rais na Samia kuwa Makamu wa Rais. Nikisema kuwa wewe unafaa kuwa meneja wangu, na Mwashambwa kuwa makamu wako, haimaanishi Mwashambwa anafaa kuwa meneja, ila ina maana ninaona kuwa anafaa kufanya kazi kwa maelekezo yako. Au katika hali ya dharula ana uwezo wa kuishikilia hiyo nafasi wakati natafuta replacement yako.
 
Acha Ujinga, Magu ilikuwa Awamu yake ya pili,alipitia mchujo na kushinda.

Sa100 hajawahi pigiwa kura popote kabla, jambo Hilo ni LAZIMA lifanyike nw!!
Jamaa yenu si aliprint fomu moja tu? Hatutaki arudie mtu Kama yule na Mungu asaidie
 
Hoja namba mbili izingatiwe ,japo wao katiba inaruhusu kupingana ila hifanya mazoea

Kimsingi ni patashika apumzika kwa amani ,kakayangu BERNARD membe
 
Usipotoshe.

Mchakato ndani ya vyama kila mwanachama anachukua fomu mwenyewe hachukui na mgombea mwenza.

Akishapitishwa na chama anatakiwa sasa achague mgombea mwenza kuendana na matakwa ya tume ya uchaguzi ya Taifa na ndio kilichofanyika.

Kilichombeba Magufuli ni historia yake ya kiutendaji kama waziri katika wizara mbali mbali.

Rekodi ya Magufuli pekee ilitosha kumbeba bila kujali nani alikua mgombea mwenza.

Kama alivyowahi kusema mwenyewe kuwa yeye alipenda Mwinyi awe mgombea mwenza ila Chama kwa sababu zao wenyewe wakampendekeza Samia.

Hivyo swala la Samia kumbeba Magufuli hapo liondoe bali itambulike kuwa Magufuli ndie alimbeba Samia.

Hata akikataa ila ukweli ndio huo.
Hivi kweli Samia ambebe Magufuli! Hata mtandaoni tu Samia watu hawamkubali Ukiingia mtandaoni X utaona kabisa people are not ready kwa huyu Mama!
 
Kinana amesema uwongo kuwa eti CCM imekuwa na utaratibu wa kutoruhusu kuwepo na ushindani ndani ya CCM wa kumpata mgombea wa chama kwenye kiti cha Urais pale ambapo Rais aliyepo madarakani hajamaliza vipindi viwili vya Urais wake. Amesema hayo akimlenga Rais wa Sasa.

Uwongo wa Kinana upo katika ukweli ufuatao:

1. Huko nyuma hakujawahi kuwa na Rais wa kipindi cha dharula. Hivyo hakujawahi kuwa na desturi ya kumpitisha Rais wa Dharula bila ya kura za wajumbe wa vikao vikuu vitatu vya CCM. Kifo cha Rais Magufuli ndiyo ilikuwa dharula ya kwanza kwa Taifa.

2. Rais wa sasa hakuwahi kupigiwa kura na wajumbe wa Kamati Kuu, Halmashauri Kuu na Mkutano Mkuu kuwa mgombea wa CCM kwenye kiti cha Urais. Utamaduni anaousema ni kwa Rais aliyepo madarkani ambaye kipindi chake cha kwanza cha Urais alichaguliwa na vikao vilivyotajwa kuwa mgombea wa Urais kupitia CCM. Lakini siyo kwa mtu ambaye hajawahi kupigiwa kura hata moja na wajumbe wa vikao hivyo kwa nafasi ya Urais.

3. Rais wa sasa ni Rais wa dharula. Katiba, kwa kuzingatia ukweli kuwa nchi isiingie kwenye mkanganyiko pale inapotokea dharula ya kifo cha Rais akiwa madarkani, ndiyo inayotamka ni nani awe Rais wa dharula katika kipindi hicho cha dharula. Huyu anakuwa Rais wa dharula mpaka wakati ule ambapo chama kitampata mtu ambaye vikao vya chama vitamchagua mtu ambaye wanataka awe ngombea wa Urais kupitia chama chao. Kulazimisha Rais wa dharula, ambaye hakuna uhakika kama chama kinaridhika awe mgombea wao kwa nafasi ya Urais, ni kukiuka misingi mikuu ya demokrasia.

Kwenye nchi zenye watu wenye akili timamu, ambako viongozi nao wana akili timamu, siku zote viongozi hutafuta uhakika wa kutaka kujua kama watu wanaotaka wawaongoze wanataka waongozwe na viongozi husika. Watawala wanapojua kuwa wananchi wao wanawataka wawaongoze, inawapa nguvu viongozi katika utendaji wao wa kazi kwa sababu wanatambua kuwa nyuma yao kuna umma mkubwa wa watu unaowataka wao viongozi wawe mbele yao katika utendaji wao wa kuyaongoza mataifa yao. Huku kwetu, sijui ni ujinga, upunguani au ushetani, watawala wanaogopa wananchi kuwadhihirishia viongozi kama wanawataka wawe viongozi wao au la. Ndiyo maana akina Kinana wanatamka wazi kuwa ndani ya CCM hakutakuwa na nafasi kwa wanaCCM kuthibitisha kama wanataka aliyekuwa Rais wa dharula, sasa awe Rais wa kuchaguliwa au apumzike na kupewa heshima yake ya kuiongoza nchi katika kipindi cha dharula.
Hauna akili.
 
Kinana amesema uwongo kuwa eti CCM imekuwa na utaratibu wa kutoruhusu kuwepo na ushindani ndani ya CCM wa kumpata mgombea wa chama kwenye kiti cha Urais pale ambapo Rais aliyepo madarakani hajamaliza vipindi viwili vya Urais wake. Amesema hayo akimlenga Rais wa Sasa.

Uwongo wa Kinana upo katika ukweli ufuatao:

1. Huko nyuma hakujawahi kuwa na Rais wa kipindi cha dharula. Hivyo hakujawahi kuwa na desturi ya kumpitisha Rais wa Dharula bila ya kura za wajumbe wa vikao vikuu vitatu vya CCM. Kifo cha Rais Magufuli ndiyo ilikuwa dharula ya kwanza kwa Taifa.

2. Rais wa sasa hakuwahi kupigiwa kura na wajumbe wa Kamati Kuu, Halmashauri Kuu na Mkutano Mkuu kuwa mgombea wa CCM kwenye kiti cha Urais. Utamaduni anaousema ni kwa Rais aliyepo madarkani ambaye kipindi chake cha kwanza cha Urais alichaguliwa na vikao vilivyotajwa kuwa mgombea wa Urais kupitia CCM. Lakini siyo kwa mtu ambaye hajawahi kupigiwa kura hata moja na wajumbe wa vikao hivyo kwa nafasi ya Urais.

3. Rais wa sasa ni Rais wa dharula. Katiba, kwa kuzingatia ukweli kuwa nchi isiingie kwenye mkanganyiko pale inapotokea dharula ya kifo cha Rais akiwa madarkani, ndiyo inayotamka ni nani awe Rais wa dharula katika kipindi hicho cha dharula. Huyu anakuwa Rais wa dharula mpaka wakati ule ambapo chama kitampata mtu ambaye vikao vya chama vitamchagua mtu ambaye wanataka awe ngombea wa Urais kupitia chama chao. Kulazimisha Rais wa dharula, ambaye hakuna uhakika kama chama kinaridhika awe mgombea wao kwa nafasi ya Urais, ni kukiuka misingi mikuu ya demokrasia.

Kwenye nchi zenye watu wenye akili timamu, ambako viongozi nao wana akili timamu, siku zote viongozi hutafuta uhakika wa kutaka kujua kama watu wanaotaka wawaongoze wanataka waongozwe na viongozi husika. Watawala wanapojua kuwa wananchi wao wanawataka wawaongoze, inawapa nguvu viongozi katika utendaji wao wa kazi kwa sababu wanatambua kuwa nyuma yao kuna umma mkubwa wa watu unaowataka wao viongozi wawe mbele yao katika utendaji wao wa kuyaongoza mataifa yao. Huku kwetu, sijui ni ujinga, upunguani au ushetani, watawala wanaogopa wananchi kuwadhihirishia viongozi kama wanawataka wawe viongozi wao au la. Ndiyo maana akina Kinana wanatamka wazi kuwa ndani ya CCM hakutakuwa na nafasi kwa wanaCCM kuthibitisha kama wanataka aliyekuwa Rais wa dharula, sasa awe Rais wa kuchaguliwa au apumzike na kupewa heshima yake ya kuiongoza nchi katika kipindi cha dharula.
Rais ni Samia na formality zitafuatwa kama kawaida.

Na Kwa kutumia huo utaratibu inaweza kumpa Samia miaka 15 ya kuwa Rais unless yeye atumie busara maana anaweza sema awamu hii ni ya dharura hivyo haiko rasmi.

Je mko tayari? Usiempenda kaja.
 
Rais ni Samia na formality zitafuatwa kama kawaida.

Na Kwa kutumia huo utaratibu inaweza kumpa Samia miaka 15 ya kuwa Rais unless yeye atumie busara maana anaweza sema awamu hii ni ya dharura hivyo haiko rasmi.

Je mko tayari? Usiempenda kaja.

Siyo suala la mtu kukubali au kukataa bali ni suala la katiba.

Katiba iliishatamka kuwa ikitokea Makamu wa Rais amekuwa Rais kutokana na dharula iliyotokea, ataruhusiwa kugombea nafasi ya Urais, na akichaguliwa kuwa Rais, hataruhusiwa kushikilia zaidi ya vipindi viwili, ile ya Urais wa dharula, nayo ikihesabiwa kama kipindi kimoja. Hivyo Samia katiba inamruhusu kugombea nafasi ya Urais, na akichaguliwa, hicho ndicho kipindi chake cha mwisho.
 
Back
Top Bottom