Pre GE2025 Kuhusu nafasi ya Urais ndani ya CCM: Kinana amedanganya, na kwa vyovyote hana dhamira njema

Pre GE2025 Kuhusu nafasi ya Urais ndani ya CCM: Kinana amedanganya, na kwa vyovyote hana dhamira njema

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Siyo suala la mtu kukubali au kukataa bali ni suala la katiba.

Katiba iliishatamka kuwa ikitokea Makamu wa Rais amekuwa Rais kutokana na dharula iliyotokea, ataruhusiwa kugombea nafasi ya Urais, na akichaguliwa kuwa Rais, hataruhusiwa kushikilia zaidi ya vipindi viwili, ile ya Urais wa dharula, nayo ikihesabiwa kama kipindi kimoja. Hivyo Samia katiba inamruhusu kugombea nafasi ya Urais, na akichaguliwa, hicho ndicho kipindi chake cha mwisho.
Formality zitafuatwa,kwani wewe shida Yako ni nini? Mbona Kinana amesema Hawaoni shida Samia Kugombea mara ya pili au Kuna sehemu Katiba inasema successor wa kifo hatKmakiwi Kugombea?

Kama ni formality subiria mda zitafuatwa kama ilivyokuwa wakati wanamchagua kuwa Mwenyekiti wa Chama.
 
Formality zitafuatwa,kwani wewe shida Yako ni nini? Mbona Kinana amesema Hawaoni shida Samia Kugombea mara ya pili au Kuna sehemu Katiba inasema successor wa kifo hatKmakiwi Kugombea?

Kama ni formality subiria mda zitafuatwa kama ilivyokuwa wakati wanamchagua kuwa Mwenyekiti wa Chama.

Kama kuna mtu atasema Rais Samia haruhusiwi au hatakiwi kugombea au kuendelea kuwa Rais, basi labda huyo mtu ni punguani. Jambo la muhimu apite kwenye njia iliyonyoka na safi.

Hapa watu wanalaani kauli ya kinafiki ya Kinana ya kusema eti fomu ya mgombea wa CCM kwa nafasi ya Urais itachapishwa moja, yaani maana yake ni kuwa hakuna mwanaCCM atakayeruhusiwa kuchukua fomu ya kugombea nafasi ya Urais kupitia CCM. Kwanza hilo likitokea litamtia doa Rais Samia ambaye angependa kufanya tofauti na madikteta waliotangulia kwenye upande wa demokrasia. Kama Rais Samia atakubali hilo, hata zile R zake 4 zitaonekana ni unafiki.

Ndani ya CCM, hata kama wakichapisha fomu 100, siamini kama wapo watakaomshinda mwenyekiti wao katika uteuzi wa nafasi ya mgombea wa nafasi ya Urais kupitia CCM.

Rais Samia, binafsi naamini, kuna majitu maovu, kwa dhamira zao mbaya, wanapenda kumpitisha kwenye njia chafu ili waonekane kuwa wao ndio walimwezesha kuwa Rais, na akiwa Rais waendelee kuwa na nafasi ya pekee kiasi cha kutoguswa hata wanapoendelea na uovu wao au ili waendelee kupata upendeleo.
 
Hapo Namba 2 si sawa. Magufuli na Samia walipitia mchakato mmoja hadi Magufuli akawa Rais. Kura alizopata Magufuli kwenye Urais kwenye ile karatasi alikuwepo pia Samia. Kuna watu walimchagua Magufuli kwa sababu tu ya uwepo wa Samia. Si sawa kusema eti hakupigiwa kura.
Hakupigiwa kura na wajumbe wa vikao vitatu vya juu vya CCM.

Mbona inaeleweka!??
Unashindwaje kuelewa hapo wewe Mzee Kijana !!??
 
Kwenye karatasi ya kura alikuwepo JPM na Samia sio kwamba alikuwepo JPM pekee so kusema alichaguliwa JPM sio samia inakuwa sio sawa.

Pili huwezi sema umemteua makamu eti kuziba pengo kwa muda tu ilihali katiba ipo wazi ukisafiri, ukiugua, au kufariki basi Makamu ndio anakua Rais!! Huwezi risk kiasi hiko.

Nachoweza kusema, next time mtakua makini kwenye kuchagua wagombea wenza na hili ni mpaka chadema walimuweka yule Said Issa kama makamu mwenyekiti. At some point Lissu alikua abroad na Mbowe alikua jela, yule jamaa akawa mwenyekiti kwa almost mwezi mzima na ilihali hamna anachoweza!!
Ndugu zitto junior hapa ndugu Bams anazungumzia mchakato ndani ya CCM.
Mh. Samia hakuwahi pitia mchakato ndani ya CCM.
 
Ndugu zitto junior hapa ndugu Bams anazungumzia mchakato ndani ya CCM.
Mh. Samia hakuwahi pitia mchakato ndani ya CCM.
Mchakato wa ndani si aligombea uenyekiti na hao hao wajumbe wakampa 100% ya kura kipi kitabadilika wamnyime urais ila wamuachie uenyekiti, is it even possible?

Udhaifu wa katiba ya chama sio kosa la Samia
 
Mchakato wa ndani si aligombea uenyekiti na hao hao wajumbe wakampa 100% ya kura kipi kitabadilika wamnyime urais ila wamuachie uenyekiti, is it even possible?

Udhaifu wa katiba ya chama sio kosa la Samia



Lakini je anayonafasi ya kuweza kufanya mabadiliko ktk kuboresha?
 
Mchakato wa ndani si aligombea uenyekiti na hao hao wajumbe wakampa 100% ya kura kipi kitabadilika wamnyime urais ila wamuachie uenyekiti, is it even possible?

Udhaifu wa katiba ya chama sio kosa la Samia
Yeye mwenyewe anazungumzia Reform. Kama kuna mambo yapo hovyo kwenye katiba yao, mazoea au kanuni, yeye ana mchango gani katika kuyarekebisha?

Hata mimi siamini kama kuna mwanaCCM wa kumshinda. Lakini kama una uhakika wa kushinda hata ukishindanishwa, una haja gani ya kupitia njia za panya kuufikia ushindi?
 
Yeye mwenyewe anazungumzia Reform. Kama kuna mambo yapo hovyo kwenye katiba yao, mazoea au kanuni, yeye ana mchango gani katika kuyarekebisha?

Hata mimi siamini kama kuna mwanaCCM wa kumshinda. Lakini kama una uhakika wa kushinda hata ukishindanishwa, una haja gani ya kupitia njia za panya kuufikia ushindi?
Mkuu hata akichukua fomu peke yake bado kuna kura za ndiyo na hapana, so sio kwamba hakuna mchakato ila hata huko US Biden hana mpinzani maana amesema anagombea tena.
 
Hapo Namba 2 si sawa. Magufuli na Samia walipitia mchakato mmoja hadi Magufuli akawa Rais. Kura alizopata Magufuli kwenye Urais kwenye ile karatasi alikuwepo pia Samia. Kuna watu walimchagua Magufuli kwa sababu tu ya uwepo wa Samia. Si sawa kusema eti hakupigiwa kura.
Hujamwelewa mwandishi,mwandishi kasema hakuna mchujo uliompitisha samia kwenye chekecheo la kugombea kuteuliwa na ccm,kwa sababu samia yeye aliteuliwa tu na jpm.
 
Ni mgombea mwenza hata 2020 aligombea kwa tiketi moja na JPM na walikua wote kwenye ballot paper. So sio Rais wa dharura bali Makamu wa Rais ambaye alipigiwa kura na wananchi.

Sasa kama aliaminiwa awe number mbili, yule top akifariki kivipi asiaminiwe? Kama wao walimchagua kwa huruma za muungano au gender balance its up to them ila katiba lazima iheshimiwe.

Ni hivi, Samia ndio mgombea wa Ccm 2025 kwa sababu ya precedence ya 2020 na 2010, kama JPM anger uhuru Membe achukue fomu hata leo wangepata confidence ya kupambana dhidi ya samia.

Sasa kama vile wao walivyokataza asichukue mtu fomu 2020 basi ndio wembe ule ule atautumia samia kufukuza wote wenye kutaka fomu ya Urais.
Watu wengi sana mna elimu,lkn kwa nn mnaonyesha ujinga mkubwa!?.
 
Watu wengi sana mna elimu,lkn kwa nn mnaonyesha ujinga mkubwa!?.
Ujinga ni upi? Hata USA Biden hashindanishwi na mtu maana ni incumbent.

Kwa mnaodai Samia hakuchaguliwa not true maana alikuwepo kwenye ballot.

Kwa hoja ya kwamba CCM haikumpitisha , aligombea uenyekiti na alipata kura zote za NDIO, sasa legitimacy ipi hiyo ya kisiasa na kisheria asiyokuwa nayo?

Kwa hili mnamuonea bure
 
Back
Top Bottom