Kuibuka kwa bodaboda wazee, kijana unajifunza nini?

Kuibuka kwa bodaboda wazee, kijana unajifunza nini?

Habari!

Binafsi ninapomwona bodaboda mtu mzima mwenye miaka 50-60 napata mshituko kidogo na kuanza kuiogopa kesho yangu.

Najiuliza maswali yafuatayo;

1. Kayumba ukumbwani mpaka kaamua kuingia kwenye kazi za vijana wanaoishi vijiweni kutwakutwa kwa utani na matusi?
2. Atafanya hiyo kazi mpaka lini, na siku akiacha ataenda kufanya kazi gani?
3. Je, Mimi nikiyumba uzeeni nitafanya kazi gani?

NJE YA MADA

Vijana tijifunze kuwekeza kwenye shughuli ambazo zitaleta matunda baadaye na si kuangalia leo tu.
Nikienda kutafuta bodaboda huwa napenda kuwasapot hawa wazee maana wana majukumu kuliko kiasi
 
Mhubiri 3:1-8 BHN

Kila kitu kina majira yake, kila jambo duniani lina wakati wake:

1 Timotheo 5:8 BHN

Lakini kama mtu hawatunzi watu wa jamaa yake, hasa wale wa nyumbani kwake, basi, mtu huyo ameikana imani, na ni mbaya zaidi kuliko mtu asiyeamini.


2 Wathesalonike 3:10 BHND

Tulipokuwa pamoja nanyi tulikuwa tukiwaambieni, “Mtu yeyote asiyependa kufanya kazi, asile chakula.”

Methali 14:23 BHN

Bidii katika kila kazi huleta faida, lakini maneno matupu huleta umaskini.

Methali 28:20 BHN

Mtu mwaminifu atapata baraka tele, lakini mwenye pupa ya kuwa tajiri hataepa adhabu.
 
Huwezi kumlinganisha bodaboda na mtumishi wa umma kwa namna yoyote ile labda mtumishi wa umma mlevi.
Mimi ninadhaminika, naweza kupata milioni zaidi ya kumi bila barua ya udhamini kutoka kwa mwenyekiti.
Mimi nikiugua hata miezi kadhaa nitaendelea kulamba mshahara na posho , natibiwa kwa bima n.k
Nyumba yangu sijawahi kumuona bodaboda mwenye nyumba kama yangu.
Acheni ujinga, bodaboda ni last option
Akili mgando hiyo.unapaswa uwaze nje ya box jombaa
 
Akili za mleta mada bwana.
Kuna bodaboda wajinga kama walivyo waajiriwa wengine wajinga wanaostaafu bila maandalizi yoyote.

Fikiria mtu anachukua boda ya mkataba, anafanya 12months mkataba unaisha, anachukua nyingine, ile yake anampa mtu analeta hesabu, baada ya miaka mitatu anakuwa na boda zake tatu anachukua hesabu za wiki/siku.

Kuna boda wapo very smart kichwani, wanaingiza vipato vikubwa kuliko hata waajiriwa.
Tusikariri.
 
Habari!

Binafsi ninapomwona bodaboda mtu mzima mwenye miaka 50-60 napata mshituko kidogo na kuanza kuiogopa kesho yangu.

Najiuliza maswali yafuatayo;

1. Kayumba ukumbwani mpaka kaamua kuingia kwenye kazi za vijana wanaoishi vijiweni kutwakutwa kwa utani na matusi?
2. Atafanya hiyo kazi mpaka lini, na siku akiacha ataenda kufanya kazi gani?
3. Je, Mimi nikiyumba uzeeni nitafanya kazi gani?

NJE YA MADA

Vijana tijifunze kuwekeza kwenye shughuli ambazo zitaleta matunda baadaye na si kuangalia leo tu.
Ninapopanda bodaboda anayoiendesha mtu mzima huwa na amani kweli nenda moi kaangalie jinsi vitoto vilivyovunjika miguu.
Bodaboda wengi ni rika la vijana wa sekondari au vyuoni.
 
Halafu akiumwa anafany nin, atafanya kazi , hizo hela atapata ,bodaboda anaweza kuamka asubuhi pikipiki imeibiwa , kazi haina security yoyote future ya kijana ambaye ni bodaboda ni kuja kuwa nani,mfano Mimi nalima na mkulima my future ni kwamba siku moja MUNGU akipenda nije kuwa mkulima mkubwa, unaweza shauri mwanao awe bodaboda
Acheni mawazo haya ya kizamani ya kuamini kuajiriwa tu au kulima.
Kuna dogo amepiga kazi ya boda kwa mkataba akapata zake 2 na bajaji 1. Pia akamiliki mgahawa na kuajiri watu huku mwenyewe akipiga bajaji ya mkataba kwa mtu mwingine.

Huyo utamlinganisha na mwajiriwa wa chini wa serikali? A mkulima wa kilimo kidogo duni cha jembe la mkono?

Sandali Ali mwenyewe huenda hamfikii kipato chake kwa siku/mwezi.
Huyo anakopesheka na anaweza kujilipia bima ya afya.

Barua ya dhamana ya mwenyekiti wa serikali za mtaa ina shida gani? Si mbadala tu wa barua ya mwajiri? Au inapunguza kiwango cha kukopeshwa?
Kuna watu wamekopa milioni zaidi ya hizo 10M kwa hiyo barua ya utambulisho.
Huwezi kumlinganisha bodaboda na mtumishi wa umma kwa namna yoyote ile labda mtumishi wa umma mlevi.
Mimi ninadhaminika, naweza kupata milioni zaidi ya kumi bila barua ya udhamini kutoka kwa mwenyekiti.
Mimi nikiugua hata miezi kadhaa nitaendelea kulamba mshahara na posho , natibiwa kwa bima n.k
Nyumba yangu sijawahi kumuona bodaboda mwenye nyumba kama yangu.
Acheni ujinga, bodaboda ni last option
 
Acheni mawazo haya ya kizamani ya kuamini kuajiriwa tu au kulima.
Kuna dogo amepiga kazi ya boda kwa mkataba akapata zake 2 na bajaji 1. Pia akamiliki mgahawa na kuajiri watu huku mwenyewe akipiga bajaji ya mkataba kwa mtu mwingine.

Huyo utamlinganisha na mwajiriwa wa chini wa serikali? A mkulima wa kilimo kidogo duni cha jembe la mkono?

Sandali Ali mwenyewe huenda hamfikii kipato chake kwa siku/mwezi.
Huyo anakopesheka na anaweza kujilipia bima ya afya.

Barua ya dhamana ya mwenyekiti wa serikali za mtaa ina shida gani? Si mbadala tu wa barua ya mwajiri? Au inapunguza kiwango cha kukopeshwa?
Kuna watu wamekopa milioni zaidi ya hizo 10M kwa hiyo barua ya utambulisho.
Kama ni rahisi hayo uliyoyaeleza hapa acha kufanya mambo yako kwani bajaji na pikipiki za mkataba ziko nyingi na ili upewe huulizwi hata elimu yako.
 
Kama ni rahisi hayo uliyoyaeleza hapa acha kufanya mambo yako kwani bajaji na pikipiki za mkataba ziko nyingi na ili upewe huulizwi hata elimu yako.
Hakuna kitu rahisi au kazi rahisi kwenye utafutaji.
Ajira pia ni mateso na manyanyaso kwa sehemu zingine.
Unaweza kuhamishwa sehemu uliyowekeza na kupelekwa sehemu ya ovyo.
Kuna wanaotoa ngono kwa boss wao.
Kuna wanao pigwa uhamisho mbali na filia zao au kupangiwa safari ili boss wao apate muda wa kuwachukulia wake zao n.k.
Kuna wanasingiziwa makosa na kujikuta jela n.k.
 
Back
Top Bottom