Kuibuka sasa kwa kashfa ya LUGUMI ni mpango wa Mungu Watanzania wamjue waliomuamini na kumsifia

Kuibuka sasa kwa kashfa ya LUGUMI ni mpango wa Mungu Watanzania wamjue waliomuamini na kumsifia

Hivi wakisimamishwa bila uchunguzi wewe si utakuja hapa kuanza kusema kuwa wanaonewa? Hivi mmejisahau huwa mnasema serikali ina kurupuka? Leo hii mnataka watu wasimanishwe kazi hata niki kuuliza nani asimamishwe na kwasababu gani hujui!

Kwanini mnakuwa na vichwa vya panzi? Hivi ulimsikia mwenye kiti wa PAC jana?
Uchunguzi upi unaotakiwa kufanyika? kama taarifa yenye nyaraka muhimu hawataki kutoa je ni sawa? na huo uchunguzi utathibitishwa vipi huku kukiwa hakuna nyaraka kutoka kwa wahusika?
 
Bana eee nyie gere inawasumbua tu mlitaka hizo dili mpige nyie?!!Niulize hapa kati sisi wote nani dili la hela lingetokea akaacha afe maskini jibu ni hakuna.
umaskini wetu ndo unafanya tuchukie wenye pesa yaani maskin wa tanzania akiambiwa achague atolewe jicho ili tajiri afilisike yupo tayar ht sshv
 
Salary Slip katika ubora wake.
Haaa haaa naona unamwita Mzee Mwanakijiji huu si uwanja wake yuko kwaaajili ya kusifia visivyosifika.
Kupitia Mzee Mwanakijiji, ndiyo sasa naanza kuwaelewa wananchi wa Tanzania kwa nini ni watu wa pekee duniani. Yawezekana zile kelele zote kuanzia gazeti lake la mtandaoni la Cheche zilisababaishwa na chuki zake binafsi kwa aliyekuwa Chaguo la Mungu wa wakati huo. Kwa bahati bado tupo tuliopinga hilo uchaguzi wa mwaka 2005, tukapinga wa 2010 na sasa tunapinga chaguo la sasa katika misingi ile ile.

Hata hivyo kwa sasa imekula kwetu kwani kwa miaka mingine 10 tutachezeshwa muziki ule ule kupitia santuri zile zile na bendi ile ile...kilichobadilika ni sura ya mwimbaji, katoka wa pwani kaingia wa bara! Lugumi na HSC hazigusiki, kuzigusa ni sawa na wanachoita wenzetu kufungua pandora box, usalama ni kutozigusa kabisaa...labda mgusaji awe na mikono isiyo doa, kitu kisichowezekana ndani ya mfumo huu tulioujenga chini ya CCM.
 
Mnaotegemea jipya kwenye utawala huo endeleeni kusubiri sana huu utumbuaji wa majipu ni zaidi ya sanaa za maigizo.
 
Mungu ana makusudio kwa watu wake waliokuwa wameanza kulishwa matango pori kupitia vyombo vya habari kuwa amepatika malaika tena mtenda haki asiyestahili hata kukoselewa na ukimkusoa wewe si mzalendo bali una wivu tu na chuki dhidi yake.

Tumeaminishwa haangali sura,hana chama,anasimamia haki,hamuogopi mtu, n.k na zaidi tumuombe kwa mungu.

Hata hivyo,limeibuka jambo ambalo litawasaidi wengi kama si wote kujua ukweli halisi kuhusu mtu huyu na kama kweli anafanya mambo yanayostahili yeye kuombewa.

Mungu aliona asisubiri sana maana watu wake wanazidi kupotea.

NB: Kupitia mungu huyo huyo,vice versa is also true.

Tusubiri.
Sidhani kama Rais ana chakuprove kwako, hata akisema walugumi wote wafilisiwe mtakuja na lingine. Magu is the real deal
 
Leo Rais Magufuli anasifiwa kwa sababu ana uwezo na ana uthubutu wa kuingilia mhimili wa Bunge na kuweka shinikizo wabunge wahojiwe kwa rushwa. Kesho Rais huyo huyo anashindwa kusaidia mhimili huo huo upate taarifa za ufisadi.

Wapiga vigelegele hawakosi sababu.
Suala la Lugumi linahusisha Mhimili wake mwenyewe, tena moja kwa moja (the executive). Waziri wa mambo ya ndani, IGP, Katibu Mkuu, ni wateule wa Rais. Waziri husika - ambae anahusishwa na tuhuma kupitia kampuni yake ya infosys, ndio bosi wa IGP na Katibu Mkuu ambao tunawatupia lawama juu ya hili.

Mwisho wa siku, wa kulaumiwa ni Rais Magufuli. Katibu mkuu na IGP wapo chini ya Waziri Kitwanga, mshirika kibiashara wa Lugumi. Ni sahihi kupiga danadana na nyaraka husika kwa kufuatana na Kiapo chao cha kazi kwa aliyewateua - Rais!

Kitendo cha Rais kutotengua UWaziri wa Kitwangwa lazima kizuie watendaji wake (Katibu Mkuu na IGP) kutoa ushirikiano kwani ukimya wa Rais maana yake ni kwamba mamlaka ya uteuzi (Rais) hajaridhia. Wangekuwa wamethibitishwa uteuzi wao na Bunge tungekuwa mbali na hili. Lakini Katiba ya wananchi hamtaki, na Rais Magufuli alishadokeza kwamba katiba ya Chenge ndio sahihi.

Suluhisho la suala hili lazima lianze na Rais mwenyewe. Anze kwa kutengua uwaziri wa Kitwanga kwanza, then rest will return to equilibrium.

Tusiwalaumu IGP na Katibu Mkuu mambo ya ndani bali Rais Magufuli kwa ukimya wake ambao tafsiri huko polisi na wizarani lazima iwe "Bwana mkubwa hajaridhia". Vinginevyo mtakuwa "Majipu".
 
Leo Rais Magufuli anasifiwa kwa sababu ana uwezo na ana uthubutu wa kuingilia mhimili wa Bunge na kuweka shinikizo wabunge wahojiwe kwa rushwa. Kesho Rais huyo huyo anashindwa kusaidia mhimili huo huo upate taarifa za ufisadi.

Wapiga vigelegele hawakosi sababu.
Suala la Lugumi linahusisha Mhimili wake mwenyewe, tena moja kwa moja (the executive). Waziri wa mambo ya ndani, IGP, Katibu Mkuu, ni wateule wa Rais. Waziri husika - ambae anahusishwa na tuhuma kupitia kampuni yake ya infosys, ndio bosi wa IGP na Katibu Mkuu ambao tunawatupia lawama juu ya hili.

Mwisho wa siku, wa kulaumiwa ni Rais Magufuli. Katibu mkuu na IGP wapo chini ya Waziri Kitwanga, mshirika kibiashara wa Lugumi. Ni sahihi kupiga danadana na nyaraka husika kwa kufuatana na Kiapo chao cha kazi kwa aliyewateua - Rais!

Kitendo cha Rais kutotengua UWaziri wa Kitwangwa lazima kizuie watendaji wake (Katibu Mkuu na IGP) kutoa ushirikiano kwani ukimya wa Rais maana yake ni kwamba mamlaka ya uteuzi (Rais) hajaridhia. Wangekuwa wamethibitishwa uteuzi wao na Bunge tungekuwa mbali na hili. Lakini Katiba ya wananchi hamtaki, na Rais Magufuli alishadokeza kwamba katiba ya Chenge ndio sahihi.

Suluhisho la suala hili lazima lianze na Rais mwenyewe. Anze kwa kutengua uwaziri wa Kitwanga kwanza, then rest will return to equilibrium.

Tusiwalaumu IGP na Katibu Mkuu mambo ya ndani bali Rais Magufuli kwa ukimya wake ambao tafsiri huko polisi na wizarani lazima iwe "Bwana mkubwa hajaridhia". Vinginevyo mtakuwa "Majipu".
isky ufafanuzi huu utakutoa tongotongo
 
Nina uhakika wa 100 % Kwamba Rais Magufuli ata lishughulikia swala hilo. Sina wasi wasi nae hata kidogo. Huo mkataba utafutwa na kosa la IGP Magu ni dogo. Mwenye Kesi ya tenda za Lugumi ni IGP aliyepita/ Mkwe wa Lugumi. Tulipiga kelele mwaka jana, Iweje kirungu cha Polisi ki nunuliwe kwa milioni 5, Watu wakatuona wajinga. Wabunge wametoa muda wa kupewa mkataba, Muda umekwisha, Basi wata wasilisha riport yao sehemu husika. Na huko ndiko tuna subiri kuona maamuzi sahihi. Na ikishindikana hapo basi nina uhakika Rais atachukua hatua stahili. Time will tell !!!
 
Lugumi and HSC are untouchables. Tutapiga vigelegele na chereko kwa mengine, sio haya.

Inasemekana Chama cha Mapinduzi kimejengewa ukumbi mpya dodoma kwa mkono wa HSC, ukumbi uliompitisha mgombea urais wa ccm.

Inasemekana Ofisi ndogo ya Lumumba inafanyiwa ukarabati na mtu huyo huyo, Jengo ambalo litatumiwa na mwenyekiti ajae wa ccm taifa.

Inasemekana Mjenzi huyu ameingizia TRA hasara za matrilioni ya shilingi. Inasemekana pia ni beneficiary wa mradi wa Kinyerezi II, mradi ambao ulitumika kama jukwaa la mbwembwe na vijembe vya kila aina kwa upinzani.

Kigogo pale Lumumba inasemekana hivi sasa anajengewa hekalu na Lugumi pale Masaki.

Kazi ya kamati ya PAC inaondolewa huko na kuhamishiwa kamati ya ulinzi na usalama. Kazi za kamati hii huwa hazihusishi media/public Bali hufanywa kwa siri kwa "maslahi ya taifa.

Mtuhumiwa yupo mafichoni nje ya nchi anasikilizia. Maji yakizidi kimo, italazimisha ahusishwe na tuhuma ambazo akina Ridhiwani na mafisadi wenzake hawataonekana hata kwa darubini ya NASA.

Hiyo ndio Tanzania mpya chini ya awamu ya tano (CCM).

ndo Tanzania ilipofikia, kitu kikifichuliwa kinapelekwa usirini huko kikashughulikiwe,mbna wanaenda against na rais wao. suala LA mkataba liwe siri why?
hili suala haliko kiusalama wa taifa hata nukta. wameamua kulindana, na ndugai anabariki tu...
 
Nina uhakika wa 100 % Kwamba Rais Magufuli ata lishughulikia swala hilo. Sina wasi wasi nae hata kidogo. Huo mkataba utafutwa na kosa la IGP Magu ni dogo. Mwenye Kesi ya tenda za Lugumi ni IGP aliyepita/ Mkwe wa Lugumi. Tulipiga kelele mwaka jana, Iweje kirungu cha Polisi ki nunuliwe kwa milioni 5, Watu wakatuona wajinga. Wabunge wametoa muda wa kupewa mkataba, Muda umekwisha, Basi wata wasilisha riport yao sehemu husika. Na huko ndiko tuna subiri kuona maamuzi sahihi. Na ikishindikana hapo basi nina uhakika Rais atachukua hatua stahili. Time will tell !!!
Jigsaw, nakupa tahadhari kidogo tu...mtumbua majipu yabidi kwanza awe na uhakika kwamba yeye si jipu! Je unaweza kukata tawi ulokalia ukabaki salama? Hicho ndicho kitendawili kinachomkabili Magufuli kwani alikuwa sehemu ya serikali iliyopita.
 
Jigsaw, nakupa tahadhari kidogo tu...mtumbua majipu yabidi kwanza awe na uhakika kwamba yeye si jipu! Je unaweza kukata tawi ulokalia ukabaki salama? Hicho ndicho kitendawili kinachomkabili Magufuli kwani alikuwa sehemu ya serikali iliyopita.
Alafu huu mkataba wa Lugumi haukuridhiwa na Baraza la Mawaziri Magu akiwemo?
 
Lugumi and HSC are untouchables. Tutapiga vigelegele na chereko kwa mengine, sio haya.

Inasemekana Chama cha Mapinduzi kimejengewa ukumbi mpya dodoma kwa mkono wa HSC, ukumbi uliompitisha mgombea urais wa ccm.

Inasemekana Ofisi ndogo ya Lumumba inafanyiwa ukarabati na mtu huyo huyo, Jengo ambalo litatumiwa na mwenyekiti ajae wa ccm taifa.

Inasemekana Mjenzi huyu ameingizia TRA hasara za matrilioni ya shilingi. Inasemekana pia ni beneficiary wa mradi wa Kinyerezi II, mradi ambao ulitumika kama jukwaa la mbwembwe na vijembe vya kila aina kwa upinzani.

Kigogo pale Lumumba inasemekana hivi sasa anajengewa hekalu na Lugumi pale Masaki.

Kazi ya kamati ya PAC inaondolewa huko na kuhamishiwa kamati ya ulinzi na usalama. Kazi za kamati hii huwa hazihusishi media/public Bali hufanywa kwa siri kwa "maslahi ya taifa.

Mtuhumiwa yupo mafichoni nje ya nchi anasikilizia. Maji yakizidi kimo, italazimisha ahusishwe na tuhuma ambazo akina Ridhiwani na mafisadi wenzake hawataonekana hata kwa darubini ya NASA.

Hiyo ndio Tanzania mpya chini ya awamu ya tano (CCM).

mkuu Mchambuzi inaonekana unaijua vizuri hili picha, please funguka mkuu kwa faida ya great thinker na Jamii Forum kwa ujumla
 
Mungu ana makusudio kwa watu wake waliokuwa wameanza kulishwa matango pori kupitia vyombo vya habari kuwa amepatikana malaika tena mtenda haki asiyestahili hata kukoselewa na ukimkusoa wewe si mzalendo bali una wivu tu na chuki dhidi yake.

Tumeaminishwa haangali sura,hana chama, anasimamia haki,hamuogopi mtu, n.k na zaidi tumuombe kwa mungu.

Hata hivyo,limeibuka jambo ambalo litawasaidia wengi kama si wote kujua ukweli halisi kuhusu mtu huyu na kama kweli anafanya mambo yanayostahili yeye kuombewa.

Mungu aliona asisubiri sana maana watu wake wanazidi kupotea-the earlier the better.

NB: Kupitia mungu huyo huyo,vice versa is also true.

Tusubiri.
Mungu wa kweli anasema zitiini mamlaka. labda kama unakusudia mungu wa ukawa. tumechoka na upuuzi wenu, ni muda sasa watu wafanye kazi
 
nilipokuja Dar kwa mara ya kwanza niliandamwa na majipu ambayo wenyeji waliniambia kuwa ni kutokana na mabadiliko ya hali ya hewa ambayo mwili haukuizoea
majipu hayo nilikuwa nasaidiwa na kaka yangu kuyatumbua. kuna moja lilikaa sehemu mbaya, nikamwambia bro aliache nitalitumbua mwenyewe. nililibinya kulitumbua lakini ukweli ni kwamba licha ya kufanikiwa kupunguza usaa, sikuweza kuondoa kiini chake, hivyo kulazimika kumrudia bro ili aendelee kunitumbua.
......nililazimika kukaa mkao wa aibu ili litumbuliwe vizuri. aiseeeee! kaka kiini alikitoa.
 
Sakata la LIGUMI limeibuliwa na kamati ya bunge kwa hiyo nadhani tusubiri taratibu zake zifuate mkondo husika lakini Rais kutoa maamuzi ni kuingilia muhimili mwingine,,,naweza kusahihishwa kama siko sahihi
 
Aisee wewe ndio umetowa mpya yaani unataka yeye asiwajibishwe kwa makosa yale yale aliyoyafanya basi akili na kuomba asamehewe wananchi watamuelewa lakini unajifanya mtakatifu wakati wewe mwenyewe mchafu hata bandari ya bagamoyo alisaini yeye mkataba kwa niaba ya serikali mbona amenyamaza huyo ni wale wale tuu

UKWELI ni kwamba hakuna mtu ambaye angeingia madarakani na kufanya kama anavyofanya. Wengi wanaolalamika ni wale waliokuwa wakifaidika na mfumo uliopita.
Kwa mtu wa kawaida kabisa hawezi tilia shaka utendaji wa Rais.
Hata kama aliharibu watanzania hawata angalia hilo wataangalia utendaji wake wa sasa.
Msimvunje moyo JPM, tumuache aendelee kutumbua majipu.
 
Back
Top Bottom