Uchunguzi upi unaotakiwa kufanyika? kama taarifa yenye nyaraka muhimu hawataki kutoa je ni sawa? na huo uchunguzi utathibitishwa vipi huku kukiwa hakuna nyaraka kutoka kwa wahusika?Hivi wakisimamishwa bila uchunguzi wewe si utakuja hapa kuanza kusema kuwa wanaonewa? Hivi mmejisahau huwa mnasema serikali ina kurupuka? Leo hii mnataka watu wasimanishwe kazi hata niki kuuliza nani asimamishwe na kwasababu gani hujui!
Kwanini mnakuwa na vichwa vya panzi? Hivi ulimsikia mwenye kiti wa PAC jana?
Salary Slip katika ubora wake.
Kupitia Mzee Mwanakijiji, ndiyo sasa naanza kuwaelewa wananchi wa Tanzania kwa nini ni watu wa pekee duniani. Yawezekana zile kelele zote kuanzia gazeti lake la mtandaoni la Cheche zilisababaishwa na chuki zake binafsi kwa aliyekuwa Chaguo la Mungu wa wakati huo. Kwa bahati bado tupo tuliopinga hilo uchaguzi wa mwaka 2005, tukapinga wa 2010 na sasa tunapinga chaguo la sasa katika misingi ile ile.Haaa haaa naona unamwita Mzee Mwanakijiji huu si uwanja wake yuko kwaaajili ya kusifia visivyosifika.
Ni sawa na kusubiri mafuriko jangwani.Mnaotegemea jipya kwenye utawala huo endeleeni kusubiri sana huu utumbuaji wa majipu ni zaidi ya sanaa za maigizo.
Sidhani kama Rais ana chakuprove kwako, hata akisema walugumi wote wafilisiwe mtakuja na lingine. Magu is the real dealMungu ana makusudio kwa watu wake waliokuwa wameanza kulishwa matango pori kupitia vyombo vya habari kuwa amepatika malaika tena mtenda haki asiyestahili hata kukoselewa na ukimkusoa wewe si mzalendo bali una wivu tu na chuki dhidi yake.
Tumeaminishwa haangali sura,hana chama,anasimamia haki,hamuogopi mtu, n.k na zaidi tumuombe kwa mungu.
Hata hivyo,limeibuka jambo ambalo litawasaidi wengi kama si wote kujua ukweli halisi kuhusu mtu huyu na kama kweli anafanya mambo yanayostahili yeye kuombewa.
Mungu aliona asisubiri sana maana watu wake wanazidi kupotea.
NB: Kupitia mungu huyo huyo,vice versa is also true.
Tusubiri.
Sjui kwanini mimi nakesha kusubiri Escrow.Tusubiri na ya UDA na DART
Jinsi ile ile EPA ilivyosukwa kuibakiza CCM madarakani, vivyo hivyo ESCROW ilisukwa miaka kumi baadaye kuibakiza CCM madarakani.Sjui kwanini mimi nakesha kusubiri Escrow.
isky ufafanuzi huu utakutoa tongotongoLeo Rais Magufuli anasifiwa kwa sababu ana uwezo na ana uthubutu wa kuingilia mhimili wa Bunge na kuweka shinikizo wabunge wahojiwe kwa rushwa. Kesho Rais huyo huyo anashindwa kusaidia mhimili huo huo upate taarifa za ufisadi.
Wapiga vigelegele hawakosi sababu.
Suala la Lugumi linahusisha Mhimili wake mwenyewe, tena moja kwa moja (the executive). Waziri wa mambo ya ndani, IGP, Katibu Mkuu, ni wateule wa Rais. Waziri husika - ambae anahusishwa na tuhuma kupitia kampuni yake ya infosys, ndio bosi wa IGP na Katibu Mkuu ambao tunawatupia lawama juu ya hili.
Mwisho wa siku, wa kulaumiwa ni Rais Magufuli. Katibu mkuu na IGP wapo chini ya Waziri Kitwanga, mshirika kibiashara wa Lugumi. Ni sahihi kupiga danadana na nyaraka husika kwa kufuatana na Kiapo chao cha kazi kwa aliyewateua - Rais!
Kitendo cha Rais kutotengua UWaziri wa Kitwangwa lazima kizuie watendaji wake (Katibu Mkuu na IGP) kutoa ushirikiano kwani ukimya wa Rais maana yake ni kwamba mamlaka ya uteuzi (Rais) hajaridhia. Wangekuwa wamethibitishwa uteuzi wao na Bunge tungekuwa mbali na hili. Lakini Katiba ya wananchi hamtaki, na Rais Magufuli alishadokeza kwamba katiba ya Chenge ndio sahihi.
Suluhisho la suala hili lazima lianze na Rais mwenyewe. Anze kwa kutengua uwaziri wa Kitwanga kwanza, then rest will return to equilibrium.
Tusiwalaumu IGP na Katibu Mkuu mambo ya ndani bali Rais Magufuli kwa ukimya wake ambao tafsiri huko polisi na wizarani lazima iwe "Bwana mkubwa hajaridhia". Vinginevyo mtakuwa "Majipu".
Lugumi and HSC are untouchables. Tutapiga vigelegele na chereko kwa mengine, sio haya.
Inasemekana Chama cha Mapinduzi kimejengewa ukumbi mpya dodoma kwa mkono wa HSC, ukumbi uliompitisha mgombea urais wa ccm.
Inasemekana Ofisi ndogo ya Lumumba inafanyiwa ukarabati na mtu huyo huyo, Jengo ambalo litatumiwa na mwenyekiti ajae wa ccm taifa.
Inasemekana Mjenzi huyu ameingizia TRA hasara za matrilioni ya shilingi. Inasemekana pia ni beneficiary wa mradi wa Kinyerezi II, mradi ambao ulitumika kama jukwaa la mbwembwe na vijembe vya kila aina kwa upinzani.
Kigogo pale Lumumba inasemekana hivi sasa anajengewa hekalu na Lugumi pale Masaki.
Kazi ya kamati ya PAC inaondolewa huko na kuhamishiwa kamati ya ulinzi na usalama. Kazi za kamati hii huwa hazihusishi media/public Bali hufanywa kwa siri kwa "maslahi ya taifa.
Mtuhumiwa yupo mafichoni nje ya nchi anasikilizia. Maji yakizidi kimo, italazimisha ahusishwe na tuhuma ambazo akina Ridhiwani na mafisadi wenzake hawataonekana hata kwa darubini ya NASA.
Hiyo ndio Tanzania mpya chini ya awamu ya tano (CCM).
Jigsaw, nakupa tahadhari kidogo tu...mtumbua majipu yabidi kwanza awe na uhakika kwamba yeye si jipu! Je unaweza kukata tawi ulokalia ukabaki salama? Hicho ndicho kitendawili kinachomkabili Magufuli kwani alikuwa sehemu ya serikali iliyopita.Nina uhakika wa 100 % Kwamba Rais Magufuli ata lishughulikia swala hilo. Sina wasi wasi nae hata kidogo. Huo mkataba utafutwa na kosa la IGP Magu ni dogo. Mwenye Kesi ya tenda za Lugumi ni IGP aliyepita/ Mkwe wa Lugumi. Tulipiga kelele mwaka jana, Iweje kirungu cha Polisi ki nunuliwe kwa milioni 5, Watu wakatuona wajinga. Wabunge wametoa muda wa kupewa mkataba, Muda umekwisha, Basi wata wasilisha riport yao sehemu husika. Na huko ndiko tuna subiri kuona maamuzi sahihi. Na ikishindikana hapo basi nina uhakika Rais atachukua hatua stahili. Time will tell !!!
Alafu huu mkataba wa Lugumi haukuridhiwa na Baraza la Mawaziri Magu akiwemo?Jigsaw, nakupa tahadhari kidogo tu...mtumbua majipu yabidi kwanza awe na uhakika kwamba yeye si jipu! Je unaweza kukata tawi ulokalia ukabaki salama? Hicho ndicho kitendawili kinachomkabili Magufuli kwani alikuwa sehemu ya serikali iliyopita.
Lugumi and HSC are untouchables. Tutapiga vigelegele na chereko kwa mengine, sio haya.
Inasemekana Chama cha Mapinduzi kimejengewa ukumbi mpya dodoma kwa mkono wa HSC, ukumbi uliompitisha mgombea urais wa ccm.
Inasemekana Ofisi ndogo ya Lumumba inafanyiwa ukarabati na mtu huyo huyo, Jengo ambalo litatumiwa na mwenyekiti ajae wa ccm taifa.
Inasemekana Mjenzi huyu ameingizia TRA hasara za matrilioni ya shilingi. Inasemekana pia ni beneficiary wa mradi wa Kinyerezi II, mradi ambao ulitumika kama jukwaa la mbwembwe na vijembe vya kila aina kwa upinzani.
Kigogo pale Lumumba inasemekana hivi sasa anajengewa hekalu na Lugumi pale Masaki.
Kazi ya kamati ya PAC inaondolewa huko na kuhamishiwa kamati ya ulinzi na usalama. Kazi za kamati hii huwa hazihusishi media/public Bali hufanywa kwa siri kwa "maslahi ya taifa.
Mtuhumiwa yupo mafichoni nje ya nchi anasikilizia. Maji yakizidi kimo, italazimisha ahusishwe na tuhuma ambazo akina Ridhiwani na mafisadi wenzake hawataonekana hata kwa darubini ya NASA.
Hiyo ndio Tanzania mpya chini ya awamu ya tano (CCM).
Mungu wa kweli anasema zitiini mamlaka. labda kama unakusudia mungu wa ukawa. tumechoka na upuuzi wenu, ni muda sasa watu wafanye kaziMungu ana makusudio kwa watu wake waliokuwa wameanza kulishwa matango pori kupitia vyombo vya habari kuwa amepatikana malaika tena mtenda haki asiyestahili hata kukoselewa na ukimkusoa wewe si mzalendo bali una wivu tu na chuki dhidi yake.
Tumeaminishwa haangali sura,hana chama, anasimamia haki,hamuogopi mtu, n.k na zaidi tumuombe kwa mungu.
Hata hivyo,limeibuka jambo ambalo litawasaidia wengi kama si wote kujua ukweli halisi kuhusu mtu huyu na kama kweli anafanya mambo yanayostahili yeye kuombewa.
Mungu aliona asisubiri sana maana watu wake wanazidi kupotea-the earlier the better.
NB: Kupitia mungu huyo huyo,vice versa is also true.
Tusubiri.
Aisee wewe ndio umetowa mpya yaani unataka yeye asiwajibishwe kwa makosa yale yale aliyoyafanya basi akili na kuomba asamehewe wananchi watamuelewa lakini unajifanya mtakatifu wakati wewe mwenyewe mchafu hata bandari ya bagamoyo alisaini yeye mkataba kwa niaba ya serikali mbona amenyamaza huyo ni wale wale tuu