Kujenga na kumiliki nyumba ya kuishi ni muhimu kwa watu wa kipato cha chini?

Nyumba yako umeikatia Bima .?..Basi tushuke kidogo..Ina Title Deed?
Kama la.. basi jua unajifariji

Sent from my SM-A405FN using JamiiForums mobile app

Sijaelewa maswali yako yamelenga kwenye nini, mfano Yes nyumba haina bima so what? Unadhani hapa nchini kuna nyumba ngapi zenye bima? Karibia nyumba zote hazina bima lkn hiyo haizuii watu kujenga
 
Kama huna kipaji cha biashara, kopa, jenga nyumba. Unaweza ukazika pesa kwenye biashara ikaoza na kuwa mbolea, ila ukizika kwenye nyumba, mbegu itaota na kutoa matunda. Ila kama una kipaji cha biashara, kopa, wekeza, utajenga nyumba nyingi zaidi. Kujenga ni muhimu!!! Hivi kwa mwaka mwenye nyumba anakupiga ngapi?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kujenga ni jambo la maana sana, ila siyo kwa mkopo wala kwa ajili ya kuweka kama dhamana kwenye mkopo baadae, nyumba yako ya kuishi ibaki hivyo
 
Anaweza akakopa pia na kuanzisha biashara na kisha biashara ikafa na kupoteza pesa zote alizokopa huku akiendelea kulipa huo mkopo na akiteseka kwa kuishi kwa nusu mshahara. Hata wewe ulikopa 12m ukaziweka kwenye biashara na zikapotea zote huku ukiendelea kuishi kwa nusu mshahara.
 
Kujenga ni jambo la msingi sana ila mtu ajenge kwa mujibu wa uchumi wake unavyomruhusu.
Biashara ni sawa pia ila chance ya kuzeekea kwenye nyumba za watu ni kubwa usipokuwa makini. Wafanyabiashara wengi wanacontradict mtaji na faida.
 
Maisha hayana formula. Mnao ona nyumba ni kikwazo cha maisha ya biashara itakuwa si wazoefu wa biashara. Ukiwa na nyumba mfanyabiashara ndio dhamana yako. Waulize wafanyabiashara wasio na asset nyumba wanavyozodolewa na mabank. Nimejenga na nafanya biashara najua umuhimu wa vyote.

Sent from my TECNO BA2 using JamiiForums mobile app
 
Nilifuga mbwa nyumba ya kupanga ,niliishia kulalamikiwa na wapangaji wenzangu kuwa analeta viroboto na nikaambiwa na mwenye nyumba nitoe mbwa wangu au nihame ...niliamua kumpatia jamaangu akamfuge morogoro huko

Hakuna raha kama kuamka kwenye nyumba yako ,ukiwa na familia yako
 
Human BASIC NEEDS maisha ni nyumba mzee hata iwe yamabati
 
Bro tukutane ukiwa na 50 years ukiwa na hela nyingi alafu huna nyumba
utakua kituko mbele ya jamii mwisho wa siku umekufa watu ndo wanajua kutamba kote mjini kumbe huna hata kibanda cha kulala

familia yako inarudi kijijini kwakushindwa kulipa kodi...

huniambiaa chochote kujenga muhimu bana

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…