Kujenga na kumiliki nyumba ya kuishi ni muhimu kwa watu wa kipato cha chini?

Kujenga na kumiliki nyumba ya kuishi ni muhimu kwa watu wa kipato cha chini?

Kama unajua ni hulka ya binadamu...itafika wapi ndo ujue upo stable?
Unapopata ela na wazo la ujenzi wewe fanya
Ukiweza kujenga nyumba ya kuishi bila mkopo huku ukiendelea kuwa na kipato cha kukutosheleza mahitaji yako muhimu na ukiwa na akiba.
 
Mimi nimechangua kujenga kwanza kabla ya kuanzisha biasha au kimiliki gari
Nkimaliza kama nipo hai Basi nitafungua biashara
Nyumba natumia kama ngazi tu ya kuyafikia malengo mengine hata nikianguka bas niwe na sehem ya kuishi.
 
Mimi nimechangua kujenga kwanza kabla ya kuanzisha biasha au kimiliki gari
Nkimaliza kama nipo hai Basi nitafungua biashara
Nyumba naktumia kama ngazi tu ya kuyafikia malengo mengine hata nikianguka bas niwe na sehem ya kuishi.
Biashara utakayoanzisha baada ya kujenge nyumba mara nyingi ni ya kuganga njaa tu si kwa ajili ya mafanikio makubwa.
 
Biashara ni kipaji na ni hobby pia.

Mimi binafsi nikifanya biashara,siwezi pata kiu ya soda halafu mezani kuna buku naiangalia.

Unawezaona ni kwa namna gani biashara sio fani yangu.

Kingine inabidi tushukuru wafanyakazi wa aina hiyo,maana wanawapisha wasio wafanyakazi nao waishi kupitia biashara, vinginevyo itakuwa ni urafi na roho za ubinafsi.
Umeongea vizuri sana, kuna dhana potofu sana kwamba kila mtu anaweza biashara, wakati si kweli kabisa. Miaka ya nyuma niliwahi kuwa na mchepuko nikaufungulia biashara, tena kwa kukopa pesa mahala, lipa kodi ya fremu miezi mitatu, nunua mzigo wote, leseni etc... Nikapotea kikazi kama miezi mitatu hivi, aisee kurudi fremu nyeupe!! Nikakuta sanduku zima kajaza nguo na vikoro Koro vipya. Nikafuatilia kwa jirani zake story walizonipa nikachoka, nikamwambia funga fremu hiyo. Baada ya mwezi binamu yangu from village alipoona pamefungwa akaniomba na yeye ajaribu hiyo hiyo biashara kwenye hiyo fremu. Basi nikampa nusu mtaji na kulipa kodi mwezi mmoja, aisee alikomaa after three months fremu imejaa kupita ilivyokuwa mwanzo, na aliendelea mpaka akawa na maduka mawili.
 
Bro tukutane ukiwa na 50 years ukiwa na hela nyingi alafu huna nyumba
Hata nikifika 50 sina hela siwezi kuogopa nianze kujibana kisa nijenge. Tofauti yangu na wewe ni moja, wewe kila senti ukipata unawaza ununue tofali ujenge kozi kadhaa mimi nawaza hela hio nitaizalisha vipi zaidi na zaidi.
 
Biashara kabla ya ujenzi unatakiwa uwe makini sana, biashara ina sayansi yake. Nashauri jenga kwanza huku unafikiria hiyo sayansi ya biashara. Kumbuka katika mahitaji makuu ya binadamu, nyumba ipo ila biashara haipo, tafakari.
Chakula [emoji3591]Malazi/nyumba [emoji3591] Mavazi
 
Duniani tunapita tu, sasa kwa nini nijenge njiani?🙂🙂🙂🙂, Mimi masuala ya kujenga nyumba, mfano ya milioni 70, halafu niipangishe kwa laki 3 au laki 4 nipate hizo kodi.. kwanza inategemea na niliko ijenga (hata nikiishi mwenyewe baado).. hesabu zake ni baada ya miaka 15 au 17 ndo narudisha milioni 70 yangu niliyo jengea, hapo sijaweka hela niliyo nunulia kiwanja, repair, kodi ya ardhi na kodi ya majengo ya serikali na asilimia zingine.

Sasa hela hiyo si bora nika fanyie biashara ndani ya muda huo wa kusubiri kodi izalishe faida na mafaida.. au hela nilio weka irudi mara buku.. Milioni 70 ntakayo wekeza kwenye biashara ni lazima italeta faida kubwa mara idadi itakayo jizungusha.. potelea mbali mawazo ya kupata hasara..(biashara haidanganyi ukiwa serious na una imani) kwan ukijenga likaja tetemeko au bomoa bomoa na hulipwi fidia kama wale wa kimara ile inakuaga ni faida ?
Ukiwa unafanya biashara unaishi kwenye nyumba ya nani?

Au huwa unakaa pangoni kama Gaidi
 
Hata nikifika 50 sina hela siwezi kuogopa nianze kujibana kisa nijenge. Tofauti yangu na wewe ni moja, wewe kila senti ukipata unawaza ununue tofali ujenge kozi kadhaa mimi nawaza hela hio nitaizalisha vipi zaidi na zaidi.
Sasa hivi unaishi kwenye nyumba ya nani?
 
Hiyo pesa ya mshahara na mikopo unayotumia kujenga miaka 5 au 7 saba nyumba ya vyumba 4 si bora ungeiingiza kwenye biashara miaka 5 upate pesa za kutosha kukuwezesha kujenga ndani ya mwaka 1 au 2 na umalize kabisa huku ukiendelea kujipatia kipato kwenye uwekezaji wa pembeni ?
Biashara sio kila mtu anaweza kufanya
 
Hapa Tanzania watu wengi huchukulia kujenga na kumili nyumba ni hatua kubwa ya mafanikio katika miasha. Wafanyakazi wengi hukopa na kuishi na madeni ya viwanja na nyumba maisha yao yote ili tu wasikae katika nyumba za kupanga.

Pia wafanyakazi wengi wako tayari wasiwe na chanzo kingine chochote cha kipato kwa kuelekeza pesa yao yote wanayoipata katika ujenzi wa nyumba badala ya uwekezaji unaoleta fedha ili tu waishi katika nyumba zao wenyewe.

Katika muktadha wa utaalamu wa kifedha ni sahihi hasa kwa vijana kuelekeza nguvu na pesa zote katika ujenzi badala ya kuwekeza pesa katika biashara ambazo zitazalisha pesa zaidi na baadaye ndipo suala la ujenzi wa nyumba lifikiriwe baada ya kuwa na uhakika wa mtiririko mzuri wa kipato cha uhakika?
Kuna swala pia la kutambua nyakati majira na fursa. Kwa mfano, wakati mimi naanza kupata pata pesa angalau, viwanja vilikuwa vinapatikana kuanzia mbezi makonde , mbezi jogoo kuelekea tegeta , kwa bei chini ya tzs 3,000,000.
Wakati huo mimi niliamini katka kufanya biashara na kupata pesa ambayo kwayo jambo la 'ununuzi wa kiwanja na ujenzi wa nyumba lingerahisika. Kwa bahati mbaya, kabla malengo hayajatimia biashara zikayumba na mpaka leo zina survive, na 'sijaweza 'kupata kiwanja maeneo hayo, maana sasa bei haishikiki.
Kwa hiyo maamuzi mengine ni vizuri yakafanyika katika mu da muafaka ili kuepusha majuto ya baa dae , maana mambo na /maisha kwa ujumla yanaweza kubadilika usivyotarajia..
 
Aisee inabd ujenge kwanza ,mambo ya biashara yatafuata ,labda kama huna familia ,muhimu ni kujenga nyumba unayoimudu kwanza ,watoto na mke wapate pa kukaa

Kwanza kama umeoa na uko na mwanamke anayejielewa hawezi kushauri ukope hela ufanyage tu biashara na huna hata kiwanja mmepanga tu.
 
Biashara sio kila mtu anaweza kufanya
Wape/ wakopeshe/ingia ubia na wanaoweza kufanya biashara waongeze mtaji na faida kubwa ugaiwe na wewe usiyeweza biashara.
 
Umeongea vizuri sana, kuna dhana potofu sana kwamba kila mtu anaweza biashara, wakati si kweli kabisa. Miaka ya nyuma niliwahi kuwa na mchepuko nikaufungulia biashara, tena kwa kukopa pesa mahala, lipa kodi ya fremu miezi mitatu, nunua mzigo wote, leseni etc... Nikapotea kikazi kama miezi mitatu hivi, aisee kurudi fremu nyeupe!! Nikakuta sanduku zima kajaza nguo na vikoro Koro vipya. Nikafuatilia kwa jirani zake story walizonipa nikachoka, nikamwambia funga fremu hiyo. Baada ya mwezi binamu yangu from village alipoona pamefungwa akaniomba na yeye ajaribu hiyo hiyo biashara kwenye hiyo fremu. Basi nikampa nusu mtaji na kulipa kodi mwezi mmoja, aisee alikomaa after three months fremu imejaa kupita ilivyokuwa mwanzo, na aliendelea mpaka akawa na maduka mawili.
Kanunue hisa,ingia ubia na wanaojua biashara au jenga fremu za kupangisha.
 
Na mimi nashangaa, wakati una save pesa ambayo ungelipa kodi.....
Wafanyakazi wengi wanajenga nyumba za kuishi kwa mikopo yenye riba kubwa. Hakuna pesa wanayo save kwa sababu nyumba inakuwa haizalishi huku wakirejesha mkopo wenye riba.
 
Back
Top Bottom