Kujenga na kumiliki nyumba ya kuishi ni muhimu kwa watu wa kipato cha chini?

Kujenga na kumiliki nyumba ya kuishi ni muhimu kwa watu wa kipato cha chini?

Bro tukutane ukiwa na 50 years ukiwa na hela nyingi alafu huna nyumba
Shida iko wapi mzee?
Wahindi wanazeeka wamepanga Kariakoo na Upanga lakini akitaka kukuhamisha kwenye nyumba yako anakupa fedha na anakuhamisha anamiliki nyumba yako uliyojenga kwa miaka 7 kwa siku moja

Tafuta pesa mkuu achana na ngonjera za kuitwa mwenye nyumba wakati unapumulia mashine kwa umasikini.
 
Kama unaweza kupanga nyumba ya kutosha familia na ikasitirika ni bora kuanza na hiashara.
Kama unauwezo wa kupanga chumba kimoja au viwili na una fakimila ya watu 6 ni bora kujibana kujenga maana utaainika sana.

Shida unakuta umepanga chumba na seble familia kubwa mpaka kufikia watoto kulala seblem kwenye makochi...
 
Benki au taasisi za umma zingekuwa zina nyumba nyingi na za aina tofauti za kupanga kwa bei nafuu, kusingekuwa sana na mihemko ya kujenga nyumba kwa kila mtu.
Tatizo watu binafsi wanapangisha bila kuzingatia haki na sheria za kupangisha. matokeo yake ni kunyanyasa wapangaji na mara nyingi kuwadhalilisha mbele ya familia zao. Hiyo ndiyo inayofanya watu wengi wajitahidi wajenge nyumba ingawa wataishi maisha ya tabu.
Nyumba nzuri unayoweza kaa na familia yenye watoto 3 ni ngapi kwa mwezi?
The same time unadaiwa ada 2.5m kwa mwaka
Bado nauli
Chakula etc
Hapo ndo ujibane kujenga
 
Shida iko wapi mzee?
Wahindi wanazeeka wamepanga kariakoo na upanga lakini akitaka kukuhamisha kwenye nyumba yako anakupa fedha na anakuhamisha anamiliki nyumba yako uliyojenga kwa miaka 7 kwa siku moja

Tafuta pesa mkuu achana na ngonjera za kuitwa mwenye nyumba wakati unapumulia mashine kwa umasikini.
Hii mentality ya kiumaskini sijui imetoka wapi..watu ni waoga mnoo.katika hii thread watu walio changia positive hawazid wanne.wengi wanaogopa biashara!
 
Sina muda wa kujiuliza kwa mtu anayelialia, vifaa vikipanda tafuta hela zaidi maisha hayasimami…. ujenge usijenge kulialia haikusaidii.
Mtu amabe hushindwa kifikiria kabla ya kutenda ni MBUMBUMBUU

Fikiri kabla ya kutenda kid
 
Tengenezeni Future ya watoto wenu wakuu,acheni kukimbilia kuzika pesa..acheni ubinafsi..matokeo yake watoto wanakuja kuanza upya as if hakuwa na wazazi..
Kabisa, ilo Ni tatizo kwa familia nyingi Sana uku mtaani
 
Kama ujenzi wa sasa upo juu huo wa miaka ijayo utakuaje cuzzo,?

Miaka ya nyuma baba zetu walijejenga mfuko wa cement ukiwa elfu nne, 4000, sasa hivi supaset huku nilipo ni 16000/16500, hiyo miaka ijayo utanunuaje huo mfuko wa cement?

Kama umepata nafasi ya kujenga jenga sasa achana na story za watoto wanaotegemea nyumba za urithi watakupoteza
Off course,
Pamoja na bei za vifaa kuwa juu bado tunajenga lkn pia inawezekana sana bei za vifaa ikapunguzwa ikawa na unafuu kiasi flan watu wakamudu ujenzi ulio bora
 
Unajenga taratibu ndani ya miaka kadhaa nyumba ya 30mln inaisha .

Watumishi Wana salary na Wana uhakika wa mwisho wa mwezi.
Kwanini usifanye biashara kidogo kodogo ndani ya hiyo miaka kadhaa ukapata fedha za uhakika wa kujenga nyumba ya ndoto yako kwa faida na bila stress na bado biashara ikiendelea?
 
Mimi naona kuwa na nyumba ni muhimu sana kama huna kipato cha uhakika. Ila kama una uwekezaji wenye uhakika sidhani kama kuna haja ya kukimbilia kujenga
Yote 9&10 Kuna jamaa yupo ndani yaani seregerea now kwa case ya uhujumu uchumi wa 7b Ila Hana nyumba mtoto wake Hana sehemu ya kukaa alizoea kuishi Kila hotel hapa mjini je na huyu yupo kundi Gani lako???
 
Biashara ni kipaji na ni hobby pia.

Mimi binafsi nikifanya biashara,siwezi pata kiu ya soda halafu mezani kuna buku naiangalia.

Unawezaona ni kwa namna gani biashara sio fani yangu.

Kingine inabidi tushukuru wafanyakazi wa aina hiyo,maana wanawapisha wasio wafanyakazi nao waishi kupitia biashara, vinginevyo itakuwa ni urafi na roho za ubinafsi.
Mkuu,
Biashara unajifunza, ni kama mwajiriwa anayekwenda ofisini kwa mara ya kwanza anajifunza kwa wengine aliowakuta na baadae anaweza kuwa mtendaji mzuri zaidi yao hata kuwa boss wao.

Kama ilivyo kwa kazi nyingine biashara pia unajifunza. Ukimwona mtu anauza vifaa vya ujenzi amejifunza, muuza nguo amejifunza, hoteli amejifunza nawewe jifunze (kama unahitaji)

Tunafahamu hatuwezi kufanya bishara wote tunachofanya hapa jukwaani ni kuelimishana na kupeana moyo na uzoefu kwa wale "wanaotaka" kufanya biashara lakini wanakosa pa kuanzia na wanatamani kupata uzoefu kwa wengine.
That's it!
 
Asiye na kipato cha uhakika si ndio anatakiwa awekeze kwenye biashara ili apate zaidi sasa akitumia mtaji alionao kujenga anwezaje kuwekeza na kuwa na kipato cha uhakika?
Kwa maana nyingine umesema tajiri aendelee kuwa tajiri na masikini abaki na umasikini wake.

Mimi nadhani hapao ni vice versa
Asiye na kipato cha uhakika aelekeze nguvu na akili zake zote kuwekeza na kujijenga kiuchumi na aliye na uwekezaji wa uhakika hakuna shida akiamua kujenga nyumba ya kuishi.

Kwangu mimi shida si kuwekeza shida ni "Elimu ya uwekezaji"
kundi kubwa la watu hasa wa kipato cha chini na cha kati wanakosa elimu na ujuzi wa uwekezaji hii inapelekea kufeli mara kwa mara kwenye biashara na wengine wanawaangalia hao(waliofeli) kama mifano.

Kwenye kila biashara ambayo mmoja analalamika ilimwangusha na kumpa hasara kuna mwingine biashara hiyo hiyo imemtajirisha na anifanya mpaka leo kwenye hiyo nchi na sera hizo hizo anazolaumu mwingine.
Bado unadhani shida ni sera au sheria nk
Shida ni kutokuwa na taarifa sahihi na za kutosha za biashara/uwekezaji unaotaka kufanya.
Watu wengi wanatanguliza fedha kwenye biashara kabla ya kuwekeza "muda" na kutafuta ujuzi/uzoefu.
Hapo kwenye elimu ya uwekezaji ndio umenena haswaa. Sasa hapo unaposema mtu asiwekeze kwaajilI ya pesa kodi atakuwa analipa nini? Hela haupati mara moja, ukipata leo jenga subiri ukipata nyingine ndio uwekeze....mimi nadhani mtu akishakuwa na kwake ana uwezo wa kujilipua kivyovyote maana anajua mambo yakienda kombo atakaa hata miaka miwili ajipange upya ila sisi tunaoishi kwa hisani ya baba mwenye nyumba tupo very calculating maana unajua nikibugi hapa natupiwa virago nje. Yaani ukipata hela unaogopa hata kuitumia hata kama sio muda wa kulipa kodi ...uunafikiria hivi ikifika muda wa kulipa sina itakuwaje? Yaani muda wote unawaza kodi kodI kodi
 
Yote 9&10 Kuna jamaa yupo ndani yaani seregerea now kwa case ya uhujumu uchumi wa 7b Ila Hana nyumba mtoto wake Hana sehemu ya kukaa alizoea kuishi Kila hotel hapa mjini je na huyu yupo kundi Gani lako???
Huyo nae alibugi..anakaaje hotelini na yuko na familia
 
Hapo kwenye elimu ya uwekezaji ndio umenena haswaa. Sasa hapo unaposema mtu asiwekeze kwaajilI ya pesa kodi atakuwa analipa nini? Hela haupati mara moja, ukipata leo jenga subiri ukipata nyingine ndio uwekeze....mimi nadhani mtu akishakuwa na kwake ana uwezo wa kujilipua kivyovyote maana anajua mambo yakienda kombo atakaa hata miaka miwili ajipange upya ila sisi tunaoishi kwa hisani ya baba mwenye nyumba tupo very calculating maana unajua nikibugi hapa natupiwa virago nje. Yaani ukipata hela unaogopa hata kuitumia hata kama sio muda wa kulipa kodi ...uunafikiria hivi ikifika muda wa kulipa sina itakuwaje? Yaani muda wote unawaza kodi kodI kodi
Hizi ni fikra tu tulizo aminishwa vizazi na vizazi mkuu..Na kubadilika ni ngumu..
Mahitaji ya mwanadamu kamwe hayaishi mpaka tunaingia kaburini..Uwe na kwako,usiwe na kwako..Ishu ni je,tunawezaje kuyatimiza..
Mfano wa Mahitaji haya yapo tu..
Kula..
Afya...
Kuvaa..
Kuhudumia watoto mpaka wakue..
Utilities,(maji,umeme nk)
Kuna shughuli za kijamii wakati mwingine huwezi kuziepuka inayoambatana na gharama (misiba,sherehe,michango mbalimbali..)




Sent from my SM-A405FN using JamiiForums mobile app
 
Off course,
Pamoja na bei za vifaa kuwa juu bado tunajenga lkn pia inawezekana sana bei za vifaa ikapunguzwa ikawa na unafuu kiasi flan watu wakamudu ujenzi ulio bora

Kule juu nimekwambia bei ipande isipande no excuse ni kujenga tu, umejifanya kukaza fuvu kisha unakuja kukiri hapa…. unateseka mno.

Bei ipinguzwe na nani?
 
Haiwezekani kila mtu akanunua Eicher kwa sababu kila mtu anaangalia uwezo wake wa kukabiliana na changamoto za fursa kadhaa ndio maana lazima tofauti iwepo.

Binafsi ukinambia biashara nazotaka ni hizo za real estates, Ukandarasi,financial na kuuza madawa ya binadamu/ mifugo na kilimo na mwisho kilimo/ufugaji wenyewe.
sio biashara mbaya,ila mtaji na malengo ya muda mrefu vizazi na vizazi yanakuwa yamezingatiwa.

tunapozunguzia hawa wafanyakaz wenye vipato dhaifu,wanataka biashara yenye return ya muda mfupi,sababu mitaji dhaifu.

hapo ndio ujenzi wa slope au chumba na sebule vyenye matoleo huzaliwa.
 
Hapo kwenye elimu ya uwekezaji ndio umenena haswaa. Sasa hapo unaposema mtu asiwekeze kwaajilI ya pesa kodi atakuwa analipa nini? Hela haupati mara moja, ukipata leo jenga subiri ukipata nyingine ndio uwekeze....mimi nadhani mtu akishakuwa na kwake ana uwezo wa kujilipua kivyovyote maana anajua mambo yakienda kombo atakaa hata miaka miwili ajipange upya ila sisi tunaoishi kwa hisani ya baba mwenye nyumba tupo very calculating maana unajua nikibugi hapa natupiwa virago nje. Yaani ukipata hela unaogopa hata kuitumia hata kama sio muda wa kulipa kodi ...uunafikiria hivi ikifika muda wa kulipa sina itakuwaje? Yaani muda wote unawaza kodi kodI kodi
"Very calculating"
Nimependa sana huo msemo wako mama watoto, iko hivi..
Biashara zina changamoto ni kweli, unachopaswa kufanya ni kujifunza kuzizoea na kucheza nazo wakati wote na kujifunza namna bora ya kuzitatua.
Kama kuwa na nyumba yangu kutanifanya nirelax hiyo kwangu sio relief ni shida nyingine sihitaji kurelax kwasasa, huo muda utafika ila sio sasa.
Why relaxing at this age?

Inawezekana tunatofautiana kidogo lakini nikiona kuna gape fulani kwenye biashara yangu na naweza kupata pesa hata kama nalipa kodi kesho nitachukua hiyo pesa na nitawekeza, mwenye nyumba tutaongea tu si ni binadamu? halafu ukishakuwa MWAMINIFU kwenye maisha si rahisi kukwama. Naweza nikamkopa fulani nikamlipa fulani wakati nasubiri chazo fulani kitoe pesa nirudishe kwa mtu A. Lakini siwezi kukubali pesa inipite hivi hivi na nina WATU

Concept ya biashara ni pana sana.. yani ukiwa mfanyabiashara hata maisha yako binafsi unavyoongea, unavyowasiliana na watu, Mipango yako, matumizi yako, familia yako vinatakiwa viwe kibishara.

1.Jenga mahusiano mazuri na watu (marafiki wa faida) achana na kuambatana na watu wanaokata tamaa haraka.
2.Kuwa mwaminifu
3.Fanya utafiti kila mara.
4.Soma/ Jisomee ( Ongeza maarifa ya kitu unachofanya /kusudia kufanya kila upatapo fursa)
5.USIOGOPE.
 
Back
Top Bottom