Kujiendeleza kwa kusoma MD mwakani

Kujiendeleza kwa kusoma MD mwakani

Tunaangalia ubora sio kujipendelea. Hao wanafunzi wa Sudan ulitegemea waseme sio chuo bor na wakati wameponea hapo kama wakimbizi. Na hao sio references . Dogo nenda Makerere utarudi unaweza kujieleza na Kimombo vizuri.
 
Mkuu GPA za nacte hizo wanahesabu mwaka wa mwisho tu yani NTA LEVEL 6, kwahiyo matokeo ya mwaka wa kwanza na pili hayana nafasi kwenye kutafuta GPA hivyo ukipata "A" flat mwaka wa mwisho ndio inakua GPA ya 5. ila pia katika mfumo wa ajabu basi ni huu wa nacte yani awajumlishi matokeo ndo maana GPA nying za nacte ni fake tu.
Kumbe hili suala ni kweli? Niliwahi kuambiwa nikajua uongo, sasa ndo GPA gani hii? Wizii mtupuu.
Khaaaah
 
Hivi hii ni kwelii?

Maana nilishangaa mshikaji mmoja karibia kila CAT anapiga zake GPA ya 2.0 havuki hapo wala hashuki hapo.

Cha kushangaza paper la mwisho mwaka wa tatu kakunja GPA ya 4.7
Khaaaah [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] ndo nimechekaa sana.
 
Wewe omba ndugu yangu hapo MUHAS unapata na mkopo juu, Usisikilize sana hao watu wanaokuogopesha kuwa Muhas ni pagumu hakuna ugumu wowote ule mimi kuna jamaa yangu tumemaliza nae O level alipata Div Four ya 26 kipindi cha Kikwete ile wanafunzi walivyofeli sana hadi wakafanya kutoa matokeo mara ya pili bado akabaki na iyo Four ya 26 akaenda zake Certificate akapiga na Diploma akaomba hapo MUHAS akapata na mkopo walimpa alivyofika hapo akawa ndio class leader kwenye masuala ya taaluma mwisho ameacha historia hapo MUHAS alitoka na Gpa kali hadi wakampa offer abaki hapo Muhimbili hospital ila alipata fursa fulani yupo Botswana huko saivi Hospitali nyeti ya vigogo wa serikali anakula maisha tu safari za nje ni kugusa anakuwa hadi kwenye safari ya mkubwa wa nchi na kwa mwezi ananiambia anakunja Si chini ya 25M
Wee ni muongo sanaa khaaah, [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Achana na hii takataka sio vyuo vyote vilipenda kushiriki, tuletee ile ranking ya Kimataifa kila mwaka inatoka na mwaka huu ilitoka mwezi wa 8 ndio ujue. Tangu lini University of Cape Town ulishawahi kupitwa Afrika.
Hawezi kuja na majibu huyu hhiyo data haipo africa mzee
 
Hii ndio Uni ranking, Top 200 University 2023. Hii wadau wingi wa elimu na DVCA waliongea namna watakavyofanya kuboresha.
View attachment 2805590
Hii ndo ipo sawa mzee huyo analeta kuongea asichojua dogo aombe Makerere hapo,japo kwa makerere sasa hivi wameanzisha qualification lazima uwe na experience ya miaka miwili kazini toka umalize diploma ndo wanakuchukua kuna ambao wamekosa hapo kwa hiki kigezo
 
Itokee bahati wengi wa Diploma wasiombe hapo atapata, kwa sababu miaka hii naona equivalent hawaombi wengi sana kama miaka ya 2015 hadi 2018. Namshauri aombe ila na vyuo vingine pia.
Wengi wa diploma wanaomba sana kwa sasa asikudanganye mtu,competition kubwa sana kwa sasa hiyo GPA zipo kibao
 
Sawa mkuu ndio na mwambia GPA za 5 zipo nyingi sana na nafasi ni chache, form four Physics, Chemistry and Biology angekuwa na B and above angalau.
Ila mwache aombe tu anaweza pata
 
Habarini, nina swali nimemaliza clinical medicine mwaka huu nina GPA ya Tano. Nataka kujiendeleza MD bahati mbaya nafasi za MD Serikalini kumejaa na private siwezi kumudu ada, nauliza mwakani nikiapply naweza kupata chuo kama MUHAS na kuhusu mkopo kuna uwezekano wa kupata?

O level nina dv 2 ya 21 phy D, chem C , bios C na maths D .
Ulipataje gpa ya 5 kwa hayo matokeo ya o level??kweli mambo hubadilika
 
Kumbe hili suala ni kweli? Niliwahi kuambiwa nikajua uongo, sasa ndo GPA gani hii? Wizii mtupuu.
Khaaaah
Nacte kuna upuuzi mwingi sana kule sijui kuna shida gani. nacte ukipata chini ya gpa ya 4 basi umetaka mwenyewe, kule gpa za 5 za kumwaga mkuu.
 
Nacte kuna upuuzi mwingi sana kule sijui kuna shida gani. nacte ukipata chini ya gpa ya 4 basi umetaka mwenyewe, kule gpa za 5 za kumwaga mkuu.
Nacte hawahusiki ni chuo tu kikiamua kukaza. Chuo ndio kina peleka matokeo nacte.
 
Back
Top Bottom