Kukopa Trillion 4 ndani ya wiki 1 huku Mradi wa Bwawa la Nyerere umekwama kwa kukosa pesa si busara

Kukopa Trillion 4 ndani ya wiki 1 huku Mradi wa Bwawa la Nyerere umekwama kwa kukosa pesa si busara

Hizo trillion 4 zinaenda wapi wakati hata pesa za miradi muhimu kabisa hakuna?!

Ni kwanini tusikope fedha kukamilisha miradi strategic ambayo tumeshaianza?
Mkuu Nani kakudanganya kuwa mradi wa bwawa la Umeme umesimama? Mimi Niko eneo la mradi kwa miezi nane Sasa, mradi uko unaendelea na waajiriwa tuna lipwa mishahara Kama kawaida.

Anayeeneza kukwama kwa mradi wa bwawa la Umeme taarifa anazitoa wapi!!?
 
Mbona unajichanganya?
Lalamiko lako ni nini?
Fedha za ujenzi hakuna?
Au, maji hajajazwa kwenye bwawa?
Au, crane la tani 26 halijafika?
Au, bwawa limechelewa kukamilika?
Pesa zinapewa vipaumbele kwingine, halafu mradi unapokwama vinaletwa visingizo vingi, Crane ni moja wapo, maana mradi hauwezi kukamilika leo halafu tusubiri mwaka mzima ili lijae.., lilitakiwa liwe limeshaanza kujazwa, kutokujazwa kama ilivyopangwa ndio kukwama huko
 
.
Walisema jiwe anakopa sana, bora yeye tuliona miradi mikubwa kadhaa.
.
Hehee...hawa wa sasa wanakopa kama wendawazimu, kila kukicha ni kutembeza bakuli. Miradi mipya mikubwa hakuna na hata iliyopo inasusua.
Inaumiza mno!!!
 
Mkuu Nani kakudanganya kuwa mradi wa bwawa la Umeme umesimama? Mimi Niko eneo la mradi kwa miezi nane Sasa, mradi uko unaendelea na waajiriwa tuna lipwa mishahara Kama kawaida.

Anayeeneza kukwama kwa mradi wa bwawa la Umeme taarifa anazitoa wapi!!?
Sio taarifa natoa wapi, hilo bwawa lilitakiwa liamze kujazwa toka November 2021, tukaambiwa hatuna crane, hadi leo Nov 2022, halijaanza kujazwa, kwanini?!
 
hawana pesa za makusanyo wanaogopa aibu ya nchi kukwama, na kuna mtu anaenda kuwa mstaafu soon, kwa hio anajiandalia pesa za ubilionaire, chukua chako mapema, walishamtonya mwisho wake 2025 acha ajichotee kwa kisingizio cha kukopa. Maisha ni zawadi kupata kombolela enjoy your life Mama la Mama its ur time usjiechekwa bure.
 
IMG-20220105-WA0033.jpg
 
Aliposema tu unakopa huku unalipa huku kama kwenye vicoba vya akina mama nikajua kazi tunayo
 
Lile bwawa ni hasara sana, Mabadiliko ya tabia ya nchi ni duniani kote, mvua zimepungua, Vyanzo vya maji vinakauka kila siku, Umeme wa gesi ni wa uhakika kuliko huo wa maji, maana mvua zisiponyesha umeme hakuna, hakuna haja ya kupeleka pesa kwenye bwawa ilihali Mabadiliko ya mazingira yanabadilika
 
Lile bwawa ni hasara sana, Mabadiliko ya tabia ya nchi ni duniani kote, mvua zimepungua, Vyanzo vya maji vinakauka kila siku, Umeme wa gesi ni wa uhakika kuliko huo wa maji, maana mvua zisiponyesha umeme hakuna, hakuna haja ya kupeleka pesa kwenye bwawa ilihali Mabadiliko ya mazingira yanabadilika
Mabadiliko ya tabia nchi inamaanisha ukame na mafuriko, jielimishe kwanza ndio uropoke. Na ikitokea mvua zikanyesha, hayo maji hutaki yafue umeme?
 
Back
Top Bottom