Robert Heriel Mtibeli
JF-Expert Member
- Mar 24, 2018
- 28,297
- 68,017
KULA KWA JASHO NI KUHANGAIKA KUTAFUTA RIZIKI SIO LAZIMA UTOE JASHO LA MWILI AU UFANYE KAZI ZA NGUVU YA MWILI
Anaandika, Robert Heriel
Mtibeli.
Kuna kasumba ambayo inatesa baadhi ya vijana wa kiume ndani ya jamii huku wakinukuu maandiko ya kwenye Biblia Kuwa "Mwanaume atakula kwa jasho"
Wengi hujikuta wakifanya kazi za nguvu na kutoa jasho bila akili kwa kisingizio cha kula kwa jasho. Alafu mwisho wa siku matokeo huwa madogo au hakuna kabisa
Elewa, kula kwa jasho haimaanishi kuwa ili upate riziki lazima jasho la mwili likutoke. Sio lazima.
Kinachozungumziwa hapo ni kuwa mwanaume lazima uhangaike na kutafuta riziki.
Kabla ya laana hiyo mwanadamu hakuwa anahangaika kupata riziki. Kazi yake ilikuwa kufanya kazi na uhakika wa kupata úlikuwepo.
Lakini baada ya laana
Inamlazimu kutumia jitihada ili kupata riziki aliyowekewa.
Kuihangaisha akili yako pia ni sehemu ya kuvuja jasho.
Ndio maana siku hizi kazi nyingi sio za kuvuja jasho la mwili lakini lazima uhangaike.
Hata zile zilizokuwa zinatoa watu jasho la mwili siku hizi zinarahisishwa, mfano Kilimo, siku hizi kuna zana nyingi za kilimo kama Matrekta, vifaa vya kuvuna, kupukuchua n.k.
Kuhangaisha akili ndio jasho lililoongelewa hapo.
Kwa sababu zifuatazo
1. Binadamu ndiye kiumbe mwenye akili na utashi kuliko viumbe wengine duniani.
Mungu asingeweza kumwambia binadamu atumie nguvu za mwili ilhali nguvu hizo hana.
Watu wote walioelewa andiko hilo kwa namna ya nguvu mwili walijikuta wakiwa maskini na vibarua kwa wale wenye Akili.
2. Tunda lililoliwa lilikuwa la ujuzi wa mema na mabaya.
Na adhabu ililenga ujuzi wa maarifa
Yaani pasipo maarifa huwezi kuishi maisha mazuri.
Kwa leo taikon acha apumzike.
Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Leo, Dar es salaam
Anaandika, Robert Heriel
Mtibeli.
Kuna kasumba ambayo inatesa baadhi ya vijana wa kiume ndani ya jamii huku wakinukuu maandiko ya kwenye Biblia Kuwa "Mwanaume atakula kwa jasho"
Wengi hujikuta wakifanya kazi za nguvu na kutoa jasho bila akili kwa kisingizio cha kula kwa jasho. Alafu mwisho wa siku matokeo huwa madogo au hakuna kabisa
Elewa, kula kwa jasho haimaanishi kuwa ili upate riziki lazima jasho la mwili likutoke. Sio lazima.
Kinachozungumziwa hapo ni kuwa mwanaume lazima uhangaike na kutafuta riziki.
Kabla ya laana hiyo mwanadamu hakuwa anahangaika kupata riziki. Kazi yake ilikuwa kufanya kazi na uhakika wa kupata úlikuwepo.
Lakini baada ya laana
Inamlazimu kutumia jitihada ili kupata riziki aliyowekewa.
Kuihangaisha akili yako pia ni sehemu ya kuvuja jasho.
Ndio maana siku hizi kazi nyingi sio za kuvuja jasho la mwili lakini lazima uhangaike.
Hata zile zilizokuwa zinatoa watu jasho la mwili siku hizi zinarahisishwa, mfano Kilimo, siku hizi kuna zana nyingi za kilimo kama Matrekta, vifaa vya kuvuna, kupukuchua n.k.
Kuhangaisha akili ndio jasho lililoongelewa hapo.
Kwa sababu zifuatazo
1. Binadamu ndiye kiumbe mwenye akili na utashi kuliko viumbe wengine duniani.
Mungu asingeweza kumwambia binadamu atumie nguvu za mwili ilhali nguvu hizo hana.
Watu wote walioelewa andiko hilo kwa namna ya nguvu mwili walijikuta wakiwa maskini na vibarua kwa wale wenye Akili.
2. Tunda lililoliwa lilikuwa la ujuzi wa mema na mabaya.
Na adhabu ililenga ujuzi wa maarifa
Yaani pasipo maarifa huwezi kuishi maisha mazuri.
Kwa leo taikon acha apumzike.
Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Leo, Dar es salaam