Kuliko Bilion 34 kujenga soko Kariakoo bora soko lihamishwe

Kuliko Bilion 34 kujenga soko Kariakoo bora soko lihamishwe

Umeongea vizuri kuhusu Sustainable Cities, ila nimejaribu ku google kama kuna mamlaka yoyote inayoshughulikia mambo hayo hakuna. Kwenye miji iliyoendelea kila mji una mamlaka ya kushughulikia na green cities (City Park Authorities). Uki google Mamlaka kama hizo Tanzania utakutana na Hamidu city park[emoji23].View attachment 1999030


Tutafika Insh'Allah..ukweli tuna hiyo changamoto wala hatuwezi kukata. Hii Hamidu city ni ipi? 😀😀😀
 
Inaonekana watu wa mipango miji wamelala na viongozi wetu akili zimeganda. Nimeona leo kwamba soko la k'koo litajengwa upya kwa Billion 34, leo siyo mwaka 1970 jamani kwanini pesa zote zitumike kujenga soko tena eneo lenye tatizo la msongamano wa watu badala ya kulihamisha soko pembezoni mwa mji? Au wazanzibari wao kila kitu wanataka kiwe karibu na feri ili wakitoka Zanzibar wasipate usumbufu[emoji23]? Maana naskia tena kuna mradi mwingine wa soko la jangwani[emoji26][emoji26].
Hilo unalolisema angeliweza kulifanya Jiwe tu!
 
Una chuki na wamachinga eh!!?

Nchi ni yetu sote, nenda Hong Kong kawaulize wanapumlia wapi halafu uliza maendeleo yao then njoo na porojo zako.
Kama issue ni kuwaweka wamachinga mahali pazuri basi tuhamishe kiwanda cha urafiki na hata ile millenia business park, tujenge kariakoo kubwa ya kutisha ya ghorofa hata nne majengo makubwa kwa ajili ya wamachinga. Na tuweke miundo mbinu ya usafiri wa umma, kuingia na kutoka.

Hata mwekezaji mchina ameshajenga fremu hapo kiwandani, amewapangisha wamachinga
 
Kama issue ni kuwaweka wamachinga mahali pazuri basi tuhamishe kiwanda cha urafiki na hata ile millenia business park, tujenge kariakoo kubwa ya kutisha ya ghorofa hata nne majengo makubwa kwa ajili ya wamachinga. Na tuweke miundo mbinu ya usafiri wa umma, kuingia na kutoka.

Hata mwekezaji mchina ameshajenga fremu hapo kiwandani, amewapangisha wamachinga
Mh!! Mbona Urafiki hatunacho tena¡?!
 
Inaonekana watu wa mipango miji wamelala na viongozi wetu akili zimeganda. Nimeona leo kwamba soko la k'koo litajengwa upya kwa Billion 34, leo siyo mwaka 1970 jamani kwanini pesa zote zitumike kujenga soko tena eneo lenye tatizo la msongamano wa watu badala ya kulihamisha soko pembezoni mwa mji? Au wazanzibari wao kila kitu wanataka kiwe karibu na feri ili wakitoka Zanzibar wasipate usumbufu[emoji23]? Maana naskia tena kuna mradi mwingine wa soko la jangwani[emoji26][emoji26].

Mimi nazani tuachane na hili soko la kariakoo tena serikali ingetumia opportunity hii kujenga mradi wa kuwezesha kariakoo kupumua kwa kubomoa lile soko na kupanda miti eneo lile na kutengeneza city park yenye bustani na benchi za watu kupumzika. Itungwe sheria iundwe mamlaka ya City park Authority ya kusimamia mambo haya kwenye miji yetu ipendeze. Tuache fikra kwamba kila eneo lazima lijengwe mji ule hauna hata sehemu ya kupumzika, mtalii akienda k'koo leo hii hakuna hata sehemu ya kupumzika labda ale chips sehemu ambayo imejaa joto la moshi wa jiko la mkaa na hewa ya mafuta ya kukaanga.

Kwanini bado serikali inakaa na kuwaza kujenga jenga sehemu yenye msongamano hata parking za magari hakuna badala ya kujenga miradi ya kuboresha changamoto za mji kama kujenga jengo la parking pale kwenye soko japo mimi ningetamani pasijengwe chochote ipandwe miti tu pale mji upumue.

Leo tunataka kufanya makosa yaleyale ya kujenga mwendokasi jangwani kwa kujenga soko jingine pale la wamachinga badala ya kujenga daraja flyover la kutoka magomeni kwenda faya au interchange ya kutoka magomeni kwenda faya kwenda salender kwenda karume na kupanda miti mirefu ya misitu jangwani ili kusaidia joto la mji kupungua.

Ukizingatia eneo la jangwani ndiyo aneo peke kwenye mji wa dar es salaam lenye unapana wa kutosha ndani ya jiji lenye kutosha kujenga 4 tier interchange ambazo kwa Africa ziko mbili tuu, moja iko Ghana na nyingine iko South Africa.

Yani pale inasukwa interchange moja matata sana kono moja linaenda faya kono jingine linaenda magomeni, kono jingine linasambaa hadi salender , kono jingine linasambaa hadi mitaa ya ilala karume, kono jingine linakatiza hadi kinondoni studio au nyuma yake pale.

Hela tunazo invest kwenye mavitu yasiyo na kichwa (madege, ma dreamliner) tunaweza tukatoa kitu cha maana sana pale jangwani chenye kupunguza changamoto nyingi sana za mji na kutujengea heshima kubwa sana kama jiji.
View attachment 1999008

Vyote vinawezekana na ni vitu muhimu.

Soko jipya Kariakoo na miundombinu rafiki ni vizuri ijegwe. Na pia mapendekeze yako mengine yote yanaweza kufanywa kwa pamoja.
 
Mama ametoka kwenye mkutano na akapiga kelele ili pesa ya kukabiliana na madhara yatokanayo na mabadiliko ya tabia nchi itoke. Kwa picha ya Hong Kong ilivyozungukwa na msitu na miji mingine kwa waliotembelea nchi zilizoendelea, mama angefanya uamuzi wa kujenga mji mpya wenye sifa zote za kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi au bonde la Muhimbili/Jangwani lingepandwa miti ili wakazi wa Dar wapate Oxygen kwa miaka ijayo la sivyo joto litaua raia.
 
Kwa sababu kuna daraja tayari, kwa nini hiyo hela wasi plan kujenga soko kubwa Kigamboni? kuna space na mji ndiyo unajengaka kwa sasa.
 
Mimi nazani tuachane na hili soko la kariakoo tena serikali ingetumia opportunity hii kujenga mradi wa kuwezesha kariakoo kupumua kwa kubomoa lile soko na kupanda miti eneo lile na kutengeneza city park yenye bustani na benchi za watu kupumzika. Itungwe sheria iundwe mamlaka ya City park Authority ya kusimamia mambo haya kwenye miji yetu ipendeze. Tuache fikra kwamba kila eneo lazima lijengwe mji ule hauna hata sehemu ya kupumzika, mtalii akienda k'koo leo hii hakuna hata sehemu ya kupumzika labda ale chips sehemu ambayo imejaa joto la moshi wa jiko la mkaa na hewa ya mafuta ya kukaanga.
point.

Kariakoo hakuna hata sehemu ya kusema utapumzika walau unywe soda ambapo pana miti na hewa safi. kila sehemu majasho matupu.
 
Kwa sababu kuna daraja tayari, kwa nini hiyo hela wasi plan kujenga soko kubwa Kigamboni? kuna space na mji ndiyo unajengaka kwa sasa.
Yani tena siyo kigamboni tu, vitongoji vyote vilivyo pembezoni mwa jiji vingejengewa masoko makubwa kama hayo ili kuondoa msongamano katikati ya jiji hao wamachinga wasambazwe huko pembezoni mwa jiji.
 
Una chuki na wamachinga eh!!?

Nchi ni yetu sote, nenda Hong Kong kawaulize wanapumlia wapi halafu uliza maendeleo yao then njoo na porojo zako.
Ni kweli kabisa Tanzania hatujafikia hali ya kukataa wamachinga wasifanye biashara barabarani
 
point.

Kariakoo hakuna hata sehemu ya kusema utapumzika walau unywe soda ambapo pana miti na hewa safi. kila sehemu majasho matupu.
Shida kweli, na hiyo mijasho kwa asilimia kubwa ni ma pumzi ya watu wengine maana kila mtu anatoa carbon dioxide Na hakuna miti ya ku absorb co2 na ku release Oxygen.
 
Ukizingatia eneo la jangwani ndiyo aneo peke kwenye mji wa dar es salaam lenye unapana wa kutosha ndani ya jiji lenye kutosha kujenga 4 tier interchange ambazo kwa Africa ziko mbili tuu, moja iko Ghana na nyingine iko South Africa

Yani pale inasukwa interchange moja matata sana kono moja linaenda faya kono jingine linaenda magomeni, kono jingine linasambaa hadi salender , kono jingine linasambaa hadi mitaa ya ilala karume, kono jingine linakatiza hadi kinondoni studio au nyuma yake pale.

Hela tunazo invest kwenye mavitu yasiyo na kichwa (madege, ma dreamliner) tunaweza tukatoa kitu cha maana sana pale jangwani chenye kupunguza changamoto nyingi sana za mji na kutujengea heshima kubwa sana kama jiji.

View attachment 1999009
Ya ubungo bilioni 200 ,hii itakuwa trilioni 4 tunaweza
 
Mkuu umetisha,enzi za mwalimu mzee kawawa alitaka kule gymkhana watu walime mahindi,wazee wa nchii jii bana
 
Mama bado akili imelala sana bado yuko na kichwa kizito sana katika kufanya maamuzi, sio kila dodoso analowekewa mezani anaitikia tu?

Na hili linajidhihilisha serikali ya awamu ya sita (6) ni dhaifu sana, yaani analetewa pendekezo eti soko kubwa lijengwe jangwani, tunapiga makofi na kushangilia? tumerogwa siyo bure.

Jangwani hii ambayo mvua ya saa moja ikinyeesha panajaa maji lukuki, kwa maoni yangu ni vyema Mh. Mama Samia Suluhu Hassan akapatengeneza ili kumaliza tatizo la mafuriko kwanza na sio kukurupuka na kwenda kuwekeza hayo mabilioni huko.

Sitaki kuamini kama bado hajajifunza kwa kilichotokea kwenye makao ya mabasi ya mwendo kasi, mabasi mengi ya mwendokasi kila mara huaribika sababu ya mafuriko ya mara kwa mara.

Hivyo hilo soko ni vyema akapendekeza lijengwe sehemu nyingi eidha apeleke bunju ama mbagala huko.
 
Ya ubungo bilioni 200 ,hii itakuwa trilioni 4 tunaweza
Ubungo billioni 200 tulipigwa. South Africa walijenga 4 tier interchange kwa $84million, Ghana wamejenga 4tier interchange kwa $94million sis vidaraja viwili billioni mbili[emoji23]. Pale jangwani tukijenga ya kwetu kwenda faya, Magomeni, salender, karume, kinondoni studio haizidi $250 million. Ndege moja ya Dreamliner tumenunua $248 millioni tumeagiza nyingine moja $248 + $248 =$496 millioni tunabeba mizigo guangzhou sasa hv mchina mwenyewe anashangaa Dreamliner pekee la mizigo airport ni la Africa [emoji23].

Labda nikuulize wewe hapo unajiskiaje binafsi kuwa na madege mawili ya $496million au kuwa na madaraja ya yanayoungana kwenda faya, magomeni, salender, karume hadi kinondoni studio ipi itakusaidia wewe binafsi?
FB_IMG_1636097307809.jpg
interchange ya south Africa $84 million
_119331067_pokuaseinterchange2016'inaugurationof-fourtierpokuaseinterchangeinghana'.jpg
interchange ya Ghana $94 million
 
Back
Top Bottom