Kulikoni, mpakani na Rwanda sisi ni shamba la bibi?

Kulikoni, mpakani na Rwanda sisi ni shamba la bibi?

brazaj

JF-Expert Member
Joined
Jul 26, 2016
Posts
31,698
Reaction score
41,733
Zitambue tofauti hizi mpakani mwa Tanzania na Rwanda katika boda ya Rusumo:

1. Miundo mbinu upande wa Rwanda ni bora zaidi. Barabara, taa za barabarani, security cameras, majengo, fencing, furnitures nk upande wa Rwanda ni kama Ulaya.

2. Upande wa Rwanda taratibu zote katika kila idara yaani forodha, afya, polisi, immigration, usalama nk ni wazi na hakuna rushwa.

3. Waliopo kwenye eneo la serikali mpakani upande wa Rwanda ni wale tu wanaohusika kwa shughuli rasmi za hapo. Yaani wafanyakazi, mawakala wa forodha, mawakala wa bima za magari, wasafiri wavukao nk.

4. Hakuna anayeweza kuvuka kuingia Rwanda pasipo sababu wala idhini ya idara zote husika za huko yaani immigration, usalama na polisi.

5. Upande wa Rwanda wafanyakazi maisha ni kula kwa viwango vya mishahara yao.

6. Kuhusiana na Tanzania itoshe kusema huku ndiko kwenye ulaji wa urefu wa zile kamba zetu. Yaone magari ya wafanyakazi huku. Ama Kwa hakika wanalamba asali kweli kweli.

7. Eneo la serikali huku limesheni hadi wasiohusika. Kuvuka kuja Tanzania ni bwerere ambapo kama hata wapiga debe kutoka Rwanda wanajifanyia shughuli zao Tanzania kwa raha zao tumebakiza nini?

Yapo mengi ya kushangaza ila itoshe kusema kwa hakika sisi ni shamba la bibi.

Tuendelee kulea hali hizi hadi lini?
 
Zitambue tofauti hizi mpakani mwa Tanzania na Rwanda katika boda ya Rusumo:

1. Miundo mbinu upande wa Rwanda ni bora zaidi. Barabara, taa za barabarani, security cameras, majengo, fencing, furnitures nk upande wa Rwanda ni kama Ulaya.

2. Upande wa Rwanda taratibu zote katika kila idara yaani forodha, afya, polisi, immigration, usalama nk ni wazi na hakuna rushwa.

3. Waliopo kwenye eneo la serikali mpakani upande wa Rwanda ni wale tu wanaohusika kwa shughuli rasmi za hapo. Yaani wafanyakazi, mawakala wa forodha, mawakala wa bima za magari, wasafiri wavukao nk.

4. Hakuna anayeweza kuvuka kuingia Rwanda pasipo sababu wala idhini ya idara zote husika za huko yaani immigration, usalama na polisi.

5. Upande wa Rwanda wafanyakazi maisha ni kula kwa viwango vya mishahara yao.

6. Kuhusiana na Tanzania itoshe kusema huku ndiko kwenye ulaji wa urefu wa zile kamba zetu. Yaone magari ya wafanyakazi huku. Ama Kwa hakika wanalamba asali kweli kweli.

7. Eneo la serikali huku limesheni hadi wasiohusika. Kuvuka kuja Tanzania ni bwerere ambapo kama hata wapiga debe kutoka Rwanda wanajifanyia shughuli zao Tanzania kwa raha zao tumebakiza nini?

Yapo mengi ya kushangaza ila itoshe kusema kwa hakika sisi ni shamba la bibi.

Tuendelee kulea hali hizi hadi lini?
Rwanda ni kama Mkoa wa Tabora na wanaiba madini ya Kongo huwezi lingasha na linchi likuubwa kama Tz hata hivyo hakuna cha maana walichituzidi kuanzia barabara hadi majengo marefu. Acha kudanganya 😠😠
 
Du hii kali mno, mpaka wa Rwanda 🇷🇼 na Tanzania 🇹🇿 ni mpaka kweli upande wa Rwanda 🇷🇼 ila Tanzania mmmmm, huu mpaka sijawahi kufika, ila wa tunduma/nakonde unaweza kucheza bao upande wa Tanzania na kuagiza uletewe hindi la kuchoma kutoka nakonde na ukaletewa within 10mins!,tembea uone
 
Rwanda ni kama Mkoa wa Tabora na waiba mafini ya Kongo huwezi lingasha na linchi likuubwa kama Tz hata hivyo hakuna cha maana walichituzidi kuanzia barabara hadi majengo marefu. Acha kudanganya 😠😠
No ni sawa kabisa na wilaya ya kahama!
 
Ndio alinganishe na nchi inayoanzia mtwara hadi Karega, Ruvuma hadi Rombo, Dar- Kigoma
PK Aliwahi kumtambia Jakaya kuwa anaweza kuendesha TZ kwa bandari ya Dar Jakaya akamjibu lami aliyojenga ukiiweka rwanda hata sebule na choo zote haienei. Alipoendelea na kiromoromo alikipata nini? Operesheni kimbunga! Alikoma!
 
Rwanda ni kama Mkoa wa Tabora na waiba mafini ya Kongo huwezi lingasha na linchi likuubwa kama Tz hata hivyo hakuna cha maana walichituzidi kuanzia barabara hadi majengo marefu. Acha kudanganya 😠😠

Mada umeielewa lakini mkuu? Mada haihusu Tanzania wala Rwanda bali mpakani mwa Tanzania na Rwanda. Rejea kujiridhisha.
 
PK Aliwahi kumtambia Jakaya kuwa anaweza kuendesha TZ kwa bandari ya Dar Jakaya akamjibu lami aliyojenga ukiiweka rwanda hata sebule na choo zote haienei. Alipoendelea na kiromoromo alikipata nini? Operesheni kimbunga! Alikoma!
Halafu anatokea Dogo mmoja kaishia Kigali tu analeta uzi, muulize ni mkoa/mji gani mwingine anaujua nje ya Kigali anaanza kugoogle 🤣🤣🤣🤣🤣🤣
 
PK Aliwahi kumtambia Jakaya kuwa anaweza kuendesha TZ kwa bandari ya Dar Jakaya akamjibu lami aliyojenga ukiiweka rwanda hata sebule na choo zote haienei. Alipoendelea na kiromoromo alikipata nini? Operesheni kimbunga! Alikoma!
Maneno tu ya mitandaoni na chumvi nyingi! Mbona tulikuwepo na hatukuyaona.
Kwan opereshen ya kufukuza wahamiaj bongo ina athiri nn kagame
 
Huu ni mpaka??

Katika mada yote rasmi ni mpakani hapo.

"Zitambue tofauti hizi mpakani mwa Tanzania na Rwanda katika boda ya Rusumo:

1. Miundo mbinu upande wa Rwanda ni bora zaidi. Barabara, taa za barabarani, security cameras, majengo, fencing, furnitures nk upande wa Rwanda ni kama Ulaya."


Kwani wewe unasoma kutokea kwenye mada ipi?

Ninakazia: rejea kusoma uko nje ya mada.
 
Katika mada yote rasmi mpakani hapo.

"Zitambue tofauti hizi mpakani mwa Tanzania na Rwanda katika boda ya Rusumo:

1. Miundo mbinu upande wa Rwanda ni bora zaidi. Barabara, taa za barabarani, security cameras, majengo, fencing, furnitures nk upande wa Rwanda ni kama Ulaya."


Kwani wewe unasoma kutokea kwenye mada ipi?

Ninakazia: rejea kusoma uko nje ya mada.
Ungejikita kwenye heading yako ila umeshindwa ku-focus na mada ukaingiza mambo mengine ndio maana watu hawajadili mpaka wanajadili development as a whole
 
Ungejikita kwenye.heading yako ila umeshindwa ku-focus na mada ukaingiza mambo mengine ndio maana watu hawajadili mpaka wanajadili development as a whole

Ninaandika nilichokiona mpakani. Heading Iko wazi:

"Kulikoni, mpakani na Rwanda sisi ni shamba la bibi?"​


Kushindwa kwako kuelewa hakukufanyi utafute visingizio.

Uliyeshindwa ku-focus ni wewe.
 
Back
Top Bottom