Uchaguzi 2020 Kulikuwa na ulazima gani kununua ndege za kibiashara kwa cash kuliko kununua matrekta na kuyagawa kila kijiji ili kulitupa jembe la mkono?

Wewe ungekuwa sawa ungejua umuhimu wa kuingiza pato kupitia Atcl na watalii kwa pamoja.
 
Ushamba na ulimbukeni ni mzigo kwa taifa letu
 
ikiwa yesu pamoja na utukufu wake bado alipigwa vita na kudharauliwa magufuli ni nani asipigwe vita?

taifa kumiliki ndege linapata hadhi na thamani kubwa kimataifa bt nyie mazuzu mlozoea kupinga kila kitu lazima mpinge tu
 
Ndege alinunua ili apande yeye na wanaccm wenzake.
 

"amemaliza upande mmoja
SAMAHANI HAPO NIMEJADILI KIUCHUMI"

Macro / micro ?
 
Nakupongeza kwa mada hii.
 
Hakuna kiji kisicho na wakulima, vinginevyo utuambie wanaishi kwa nyama au samski tu na kwamba hawaishi kwa nafaka na mboga.
 
Wakishalima watasafilishaje mazao yao?
Au mnataka walime kisha viozee ndani na wapate hasara kisha mseme hapakuwa na mikakati?
Serikali kwa awamu zote wamejitahidi upande wa barabara, ni wakati muafaka kabisa kuwekeza kwenye kilimo kwa dhati kabisa. Takribani robo tatu ya wananchi wanategemea kilimo na ukiwekeza hapo utabadilisha uchumi wa wengi.
 
Mkinipa kura tuu.. Naongeza nyingine tano
 
Kwel ujinga na ushamba ni mzigo mzto
 
Kijiji gani kina heka zisizozidi 10?
Tuanzie hapa kwanza
Wewe unaongelea tractor la kijiji??? Ardhi ni ya wana vijiji, yaani kwa kiswahili chepesi ni ya individuals na ardhi zao zipo scattered, hapa una eka 2, pale eka 4 na kuendelea,
Sasa economically sio efficient kuwa na patches of land ya kupima here and there , ndio maana nakwambia ni juu yangu Mimi na wewe tujiunge kwa njia moja au nyingine tulime kwa pamoja tractor likija linapiga eka 10 na zaidi.

Sasa vikundi vidogo vidogo ni rahisi ku manage.

Tatizo la tractor la kijiji watu wasio kuwa na uchungu nalo ni shida kuli manage ktk matumizi ya kila siku na ktk repair.

Kama hulijui hilo utakuwa unaishi sayari nyingine.

Hata china wameisha toka huko unakofikiria wewe.
 
Serikali kwa awamu zote wamejitahidi upande wa barabara, ni wakati muafaka kabisa kuwekeza kwenye kilimo kwa dhati kabisa. Takribani robo tatu ya wananchi wanategemea kilimo na ukiwekeza hapo utabadilisha uchumi wa wengi.
Tatizo nyie mko mjini mnaona mabarabara mnadhani yamefika vijijini, kuna shemu ya km 50 bado watu wanasafili kwa tsh 8000 kitu ambacho wangelipa kwenye rami 3000, hivo huyo mtu anaumia na gharama
Sasa kusafirisha mazao bei itakuwa kiasi gani?.
 
Tatizo nyie mko mjini mnaona mabarabara mnadhani yamefika vijijini, kuna shemu ya km 50 bado watu wanasafili kwa tsh 8000 kitu ambacho wangelipa kwenye rami 3000, hivo huyo mtu anaumia na gharama
Sasa kusafirisha mazao bei itakuwa kiasi gani?.
Mkuu huko sahihi kabisa, lakini uwekezaji kwenye miundombinu ya kilimo haukwepeki na hakuna kisingizio chochote kitakachokubalika kuhalalisha jambo hilo. Awamu hii kuna mambo tumeyafanya ambayo hayakuwa na umuhimu wowote huku tukitelekeza sekta ya kilimo. Hili jambo halihitaji kusubiri hizo barabara, hayo mambo yanaweza fanywa kwa pamoja kidogo kidogo
 
Wazo zuri
i wish miaka 5 ijayo viongozi waboreshe upatikanaji wa hizi zana ili wanakijiji waache kulima na mkono.,

Zipatikane japo kwa kukodisha kwa bei ndogo ama free kwa zamu na utaratibu fulani utakaowekwa
 
Wakishalima watasafilishaje mazao yao?
Au mnataka walime kisha viozee ndani na wapate hasara kisha mseme hapakuwa na mikakati?
Nmekuelewa vzuri sana tatizo sio matrekta Wala nn, tatzo ni masoko tu yanahitajika. Watu wanalima sana na mazao yao wanayauza bei rahisi mno na mengine kuoza kbs kabla ya kuyauza. Matrekta mengi tu huko vijijini hekari moja anakulimia kwa elfu arobain tu. Watafuteni masoko uone watu watakavyoipasua hii ardhi ya Tanzania
 
Wewe unawaza kua Trekta la Kijiji basi kila mtu ana amri nalo, sivyo hivyo, ondoka kwenye mawazo hayo.

Trekta anakabidhiwa mtu atakaekua "Custodian", atakaewajibika kwa lolote. Ardhi ni ya wanakijiji lakin wengine hawalimi sababu gharama za kulima ni kubwa. Likiwepo hilo trekta ambalo wanakijiji watagharamia Gharama Pekee za kuliendesha basi Wengi watashawishika kulima
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…