Kulikuwa na umuhimu gani kwa viwanja vya Uhuru na Mkapa kujengwa sehemu moja?

Kulikuwa na umuhimu gani kwa viwanja vya Uhuru na Mkapa kujengwa sehemu moja?

Kwa maoni yangu, naona pale ulipo uwanja wa taifa panafikika kirahisi zaidi kutokea pande zote za jiji. Angja watu wanvyopata tabu kwenda Azam complex chamazi. Ni nafuu zaidi hapo ulipo!

Lakini pia, viwanja viwili kuwepo eneo moja bado haipunguzi idadi. Bado vinahesabika ni viwili, na sioni chochote kinachopungua hapo. Labda mleta mada uniambie umeona mapungufu yapi baada ya hivyo viwanja kujengwa sehemu moja!
 
mkuu Infantry Soldier amini nakwambia watu wanasanda kwenye kucheki mpira Chamanzi Azam complex wanakwambia pako kushoto ntaangalia tu kwenye tv.hata Azam f.c kuna mechi zao wanazipeleka kwa Mkapa angalau watu watakwenda wengi kuliko Chamanzi.

Hapo kwa Mkapa ni katikati watu wa Kino,Temeke,Ilala ni rahisi kufika na watu wa huko ndo wenye mpira wao sasa.
 
Ilitakiwa ule wa uhuru urekebishwe kuwa standard ya kimataifa kwenye pitch na majukaa halafu wa mkapa ungejengwa sehemu nyingine.

Nchi ingekuwa na viwanja vingi ili angalau tuwaze kuandaa afcon.
Uandae afcon kwa wachezaji gani?
 
mkuu Infantry Soldier amini nakwambia watu wanasanda kwenye kucheki mpira Chamanzi Azam complex wanakwambia pako kushoto ntaangalia tu kwenye tv.hata Azam f.c kuna mechi zao wanazipeleka kwa Mkapa angalau watu watakwenda wengi kuliko Chamanzi.

Hapo kwa Mkapa ni katikati watu wa Kino,Temeke,Ilala ni rahisi kufika na watu wa huko ndo wenye mpira wao sasa.
Mechi ambazo Azam anapeleka kwa Mkapa ni akicheza na Simba au Yanga tu kwa sababu ya sitting capacity ya Chamazi kuwa ndogo ukilinganisha na mashabiki wa timu hizo mbili kubwa.
 
Mechi ambazo Azam anapeleka kwa Mkapa ni akicheza na Simba au Yanga tu kwa sababu ya sitting capacity ya Chamazi kuwa ndogo ukilinganisha na mashabiki wa timu hizo mbili kubwa.
Mkuu, mbona husemi kuna tatizo gani viwanja kua hapo vilipo?

Why are we trying to fix what's not broken?
 
Mechi ambazo Azam anapeleka kwa Mkapa ni akicheza na Simba au Yanga tu kwa sababu ya sitting capacity ya Chamazi kuwa ndogo ukilinganisha na mashabiki wa timu hizo mbili kubwa.
Ukiangalia mechi iliyopita Azam na Simba mashabiki waliokuwepo uwanjani wangetosha vizuri Azam complex.

Azam wangeipeleka Chamanzi iyo mechi watazamaji wangeingia wachache zaidi kwasababu Chamanzi kuwa mbali na maeneo ya wanapotoka wenye mpira wao.
 
Ukiangalia mechi iliyopita Azam na Simba mashabiki waliokuwepo uwanjani wangetosha vizuri Azam complex.

Azam wangeipeleka Chamanzi iyo mechi watazamaji wangeingia wachache zaidi kwasababu Chamanzi kuwa mbali na maeneo ya wanapotoka wenye mpira wao.
Mkuu, suala la low turnout is not predictable ukizingatia Simba ni timu kubwa hivyo Azam alijua fika wangejaa ndio maana wakaenda kwa Mkapa
 
Habari za muda huu ndugu zangu wa jamiiforums.

Eti wataalam wa mipango miji, kulikuwa na umuhimu gani kwa kiwanja cha soccer cha Uhuru pamoja na ule wa Benjamin William Mkapa kujengwa sehemu moja?

View attachment 2419759

Eneo ulipojengwa uwanja wa Mkapa lilikuwa eneo la wazi na ndio sehemu ambayo chuo cha ufundi stadi cha VETA kilikuwa kinatumia katika kufunza madereva wachanga.

Nilisoma shule ya msingi Kibasila mwaka 1999 hivyo ninapajua sana eneo lile. Kabla ya ule uwanja wa Mkapa kujengwa kulikuwa na geti dogo la kuingilia shule ya secondary ya JKT Jitegemee (Jiteute) miaka hiyo pamoja na mnara wa ndege vita ya jeshi iliyoanguka wakati wa kuwapokea rasmi mashujaa wa vita ya Kagera. Hivyo lile eneo ninalijua vema tu.

Kwanini uwanja wa Mkapa haukupelekwa Boko au Bunju kama walivyofanya hospitali ya Muhimbili kujenga branch Mloganzila na ukizingatia kipindi kile maeneo ya njia ya Bagamoyo hayakuwa expensive kama ilivyo sasa?

MSAADA: Kwa wataalama wa mipango miji kulikuwa na umuhimu wowote wa kuwa na viwanja viwili vya soka eneo moja?

USISAHAU: ENDELEA KUWA MZALENDO IPENDE TANZANIA. USICHAFUE TASWIRA NJEMA YA TAIFA LAKO. USTAWI WA NCHI YETU UNAANZA NA WEWE. TIMIZA WAJIBU WAKO IPASAVYO.
Mkuu unaikumbuka picha ya uwanja wa Uhuru ulivyokuwa?

Je mmiliki wa uwanja wa Mkapa na Uhuru ni mmoja?

Je muda gani ulipita tangia wa Mkapa kujengwa na wa Uhuru kufanyiwa marekebisho?

Mi nadhan wa Mkapa namna ulivyojengwa kisasa ulilenga michezo na wa Uhuru ukaonekana kama wa magwaride na kumbu kumbu za kihistoria kabla maamuzi mengine ya kuuboresha hayajafanyika.
 
Back
Top Bottom