Elections 2015 Kulinda kura: Wakili Peter Kibatala afungua kesi Mahakama Kuu

Elections 2015 Kulinda kura: Wakili Peter Kibatala afungua kesi Mahakama Kuu

Ni muafaka hili kufanyika ili kuondoa upotoshaji usio na msingi.
Kama kifungu cha 104(1) hakijitoshelezi kwa mahitaji ya sasa basi Sheria yenyewe ipelekwe Bungeni ili ibadilishwe na kama muda hautoshi, Tume ikae na Vyama vya Siasa na kutafuta muafaka wa kutumia Busara zaidi kuliko vitisho ili kutekeleza tafsiri ya Sheria isiyo sahihi..
 
ccm Maji ya shingo sasa Kila mbinu hoi mpaka Lubuva anajuta kuwa mwenyekiti Wa tume mhhhh hali ngumu mwaka huu.
 
mwaka huu mkoa kwa mkoa,wilaya kwa wilay, jimbo kwa jimbo,kata kwa kata,tarafa kwa tarafa,kijiji kwa kijiji,nyumba kwa nyumba, kituo kwa kituo,tume kwa tume.....Mpaka #MABADILIKO YATIMIE....bampa kwa bampa.....MPAKA MAGAMBA YAOMBE POOO....mtu kabakiza siku 9 ofisini alafu analeta mbwembwe......safi lissu kibatala mallya safari
 
Mimi hua namkubaligi sana lissu kumbe kuna majembe mengine zaidi yake viva ukawa viva lowassaaaa
 
Ukiwa na mtoto sijui anajiita UKAWA ni bora ukabadilishana na Lowassa akakupa kuku unywe mchuzi.Ili awe anamdekia barabara na kulinda kura.Yaani mtu asifanye kazi akakae kituoni anamlindia KULA Fred Lowassa.AKILI AU TOPE???!!Huyu Kibatala yupo kazini nadhani analipwa na FISADI LOWASSA.

Katika watu ambao hawajitambui niww sasa upige kura arafu ukalale hayo matokeo utamtangazia nani. Panua ubongo ww
 
Mkuu wala liberal approach haihitajiki kwani kifungu kipo wazi kabisa kuwa kukaa mita mia mbili toka sehemu ya kupigia kura sio kosa. Ila haisemi mkiwa hapo muwe kwa ajili ya kulinda kura. Kwa hiyo watu wakae mita hizo mia mbili ila polisi wakija wasiseme tupo hapa tunalinda kura hata kama mioyoni mwao lengo ni kulinda kura.

Usichokijua ni kuwa sheria ya Uchaguzi inasema siku ya kupiga kura hakutakuwa na mikusanyiko ya kisiasa.Mikusanyiko yote ya kisiasa mwisho wake ni siku ya mwisho wa kampeni ambayo ni tarehe 24 octoba 2015.Ukikusanya watu wako siku hiyo ya uchaguzi wawe wana UKAWA au CCM wakajikusanya mahali ni kosa kisheria.

Pili kwa mujibu wa sheria zinazohusu mikusanyiko ni lazima kutoa taarifa polisi kuwa kutakuwa na mkusanyiko mahali fulani na kwa lengo gani. Hivyo kama kurtakuwa na watu wenye lengo la kukusanyika popote inabidi wawasilishe maombi yao polisi wakijieleza wao ni akina nani ili wapewe ulinzi wa polisi

Tatu kuna sheria ya ardhi.Unaposema utakusanyika hapo kwenye mita 200 hilo eneo ni mali ya baba yako au mama yako? Huyo mwenye miliki ya hiyo ardhi karidhia? Hivyo kama kuna watu watakaotaka kukusanyika ni lazima wapeleke kibali cha mwenye eneo kuwa karidhia eneo lake litumike kwa mikusanyiko.Na kwamba mikusanyiko hiyo haitakuwa kero wala bugudha kwa wakazi wa eneo husika,majirani n.k Maana kama watu watajiamulia kukusanyika hiyo mita mia 200 bila mwenye eneo lake kuridhia ina maana ni uvamizi wa ardhi ya mtu bila ridhaa yake.Na huo ni uvunjifu wa amani kwenye eneo la watu.Hivyo Mahakama lazima iangalie maslahi ya wenye maeneo maeneo yao yasije vamiwa SIKU YA KUPIGA KURA NA KUKALIWA KWA MABAVU na hao wanaojiita walinda kura.

Polisi kwa kuliona hilo kuwa kutakuwa na uvunjaji sheria kwa watu kuvamia maeneo ya watu na kujikusanya wakasema kila mtu aende kwake asubirie kwake.Sababu vituo vya kupigia kura haviko mbali na makazi ya watu.Kwa nini watu wakae kwenye viwanja vya watu? Mahakama iliangalie hilo

Kwangu sikubali mtu akusanyike WALA KUWEKA MAKALIO YAKE KWENYE ENEO LANGU NITAITA DEFENDER NA GARTI LA WASHA WASHA HARAKA WAJE NA MABOMU NA VIRUNGU WAONDOE WAVAMIZI KWENYE ENEO LANGU.

Hawa akina KIBATALA wanataka kuleta vurugu na ugomvi kati ya wenye maeneo na hao watu anaotaka wakusanyike hizo mita mia mbili sababu sio kwao ni kwa watu.

Eti bila haya lowasa na mbowe wanatoa amri mkimaliza kura kaeni mita 200.Hilo eneo wanaloamrisha watu wakae ni la baba yake au mama yake lowasa au mbowe.Sheria ya ardhi iheshimiwe majaji msimamie hilo kwa maslahi ya wenye maeneo yao.Mkiwakubalia mnawaweka wenye maeneo matatizoni.
 
Sisiem mwaka huu kila wanachopanga hakiwezekani, yani hadi biti la jk limeshindikana lol...
Tarehe 25 kura kwa lowasa na UKAWA, tupige kura na kusubiri matokeo tafadhali
 
Hichi ndio kilipaswa kifanyike sio kuambiana tu kwa maneno huku Jamii forum tulinde kura ..nice move kwa ukawa
 
DAFTARI LA WAPIGA KURA WAMELISAHAU?
maana mpaka majumba yamepewa hadhi ya kupiga kura!
""KURA NI MALI KAMA MALI YOYOTE ILE INASTAHILI KULINDWA""
 
Ninapoishi (nyumbani) ni mita chini ya mia moja kutoka kituo cha kupiga kura. Sijui itanibidi nihame na familia baada ya kupiga kura au itakuwa vipi? Wanajukwaa ninaomba ushauri.
Asanteni sana.
 
Asante sana Advocate Kibatala haiwezekani nchi ikaendeshwa kama duka la mtu binafsi... Mtu anakurupuka tu kutoka Msoga huko na maagizo yanayokwenda kinyume cha sharia. Ngoja mahakama iwashikishe adabu.
 
Mimi Nitakuwa Wa Kwanza Kuwapeleka Ma Ccm The Hague! Wakamsalimie Fatouh Bensouda.
 
Tayari wakili jembe na nguli Peter Kibatala akiambatana na wanasheria nguli wa Ukawa Prof Safari, Mallya na Tundu Lissu asubuhi ya leo amefungua kesi mahakama kuu kuishitaki NEC kwa ukiukwaji wa sheria juu ya wananchi kukaa mita mia mbili na kulinda kura. Kesi imefunguliwa under certificate of urgency nadhani kama sijakosea kwa kiswahili ni 'hati ya dharura' ili isikilizwe na tafsiri itoke kabla ya uchaguzi.Tayari jalada lishapelekwa kwa pilato na wanasheria nguli wa Ukawa wamejipanga kwa hoja za nguvu na ushahidi wa kutosha.
Pia jopo la wanasheria nguli wa Ukawa wameiomba mahakama kuu ya Tanzania kutoa tafsiri ya kisheria juu ya matamshi ya rais wa nchi kuwa alitumia mamlaka gani kuvaa kazi za tume.

Polisi wanakuambia, mkusanyiko wowote ule unatakiwa kuwa na kibali.

Hivyo, kabla hamjabaki kwenye hayo maeneo mtakayobaki, hakikisheni mmepata vibali vya polisi ili kwa mujibu wa sharia., ila watu wakibaki bila kibali cha polisi, huo ni uvunjifu wa amani.

SIdhani kama ni hekima kuwaambia watu wabaki vituoni. Fikiria
1. Ukawa mmewaambia watu wenu wabaki
2. CCM watuambie watu tubaki
3. ACT wawaambie watu wao wabaki
4-8 na vyama vingine wawaambie watu wao wabaki

Je, nini kitatokea kwenye hayo makundi yatakayobaki kama sio uvunjifu wa amani? hivi mnafikiri amani ikivunjika na wewe utakatiwa ticket ya ndege kwenda nje au ni hao viongozi wanaowahamasisha tu ambao tayari wengi wao wanavisa za kwenda nje ya nchi tayari? akili za kuambiwa, changanyeni na za kwenu.

A QUOTE FROM JAMII FORUMS MEMBER CALLED UTAMADUNI
 
Nchi gani ulinzi unafanywa na mob.Mahakama isipotezewe muda.Polisi wafanye kazi zao.
 
Mkuu wala liberal approach haihitajiki kwani kifungu kipo wazi kabisa kuwa kukaa mita mia mbili toka sehemu ya kupigia kura sio kosa. Ila haisemi mkiwa hapo muwe kwa ajili ya kulinda kura. Kwa hiyo watu wakae mita hizo mia mbili ila polisi wakija wasiseme tupo hapa tunalinda kura hata kama mioyoni mwao lengo ni kulinda kura.
nimesikia leo wanasema kusubiria matokeo ni kuweka mkusanyiko usio na kibari!
 
Back
Top Bottom