Kumbe Abushiri wa Tanga aliyepigana na wajerumani na kunyongwa hakuwa na maana yoyote

Kumbe Abushiri wa Tanga aliyepigana na wajerumani na kunyongwa hakuwa na maana yoyote

Kitabu gani mkuu? Na Hio website wala haisemi wamekua treated vizuri tu, bali inaelezea vitu ambavyo vina Make sense.

Mfano kwenye Mashamba walipewa eneo la kujikimu, siku kadhaa analima shamba la master na siku kadhaa analima shamba lake na anaweza akauza mazao yake kupata hela ya matumizi yake. Still ni mfumo wa kinyonyaji ila Binadamu anaweza vumilia.

Tofauti na chumvi ambazo zinaongeawa as if hao Watumwa walikua ni ma robot.
Utumwa ulikuwa ukatili
 
Wadiz,
Ukifika Mkwawa Museum Kalenga utakuta historia ya urafiki kati ya Abushiri na Mtwa Mkwawa.

Utakuta bunduki ambayo Abushiri alimpa Mkwawa na ndiyo bunduki iliyomsaidia Mkwawa kuanza kutengeneza bunduki nyingine yeye mwenyewe.

Hii ndiyo bunduki Mkwawa aliitumia katika vita vya Wahehe na Wajerumani.
Mkwawa na Abushiri walifanya biashara pamoja.

Abushiri ndiye aliyemsilimisha Mtwa Mkwawa akawa Muislam na Mkwawa akachagua jina la Abdallah.

Abushiri hakuishia hapo alimfundisha Mkwawa kusoma na kuandikwa kwa hati za Kiarabu hadi akajua.

Barua za Mkwawa zipo hapo Mkwawa Museum.

Baada ya kusilimu Mkwawa akawa hampi mtu uongozi katika himaya yake hadi kwanza amekuwa Muislam.

View attachment 2645380
View attachment 2645381
Barua alizokuwa akiandika Mtwa Abdallah Mkwawa
Inategemea unaitazamaje historia ya Abushiri na umeisoma kutoka vyanzo gani?

Je ni kweli Abushiri alikuwa anafanya biashara ya utumwa?
Je kuna ushahidi wowote kuwa Abushiri alifanya biashara hii na Mkwawa?

Ngome ya Mkwawa ilishambuliwa kwa kupigwa mizinga kutoka upande wa Tosamaganga na leo hapo limejengwa kanisa kubwa na maarufu.

Hakuna uwezekano kuwa hii ni kumbukumbu kwa kuanguka kwa Mtwa Abdallah Mkwawa?

Kuwa wanahistoria wanaotafsiri hili kama moja ya kusafisha njia ya kuingiza ukoloni kwani wamishionari walifuatiwa nyuma na wakoloni.

Lakini kuna wanahistoria wanatazama athari ya kusilimu kwa Mkwawa na matokeoa yake.

Je Uislam ulienea baada ya kifo cha Mkwawa au ulishindwa kukua?

Manispaa ya Iringa ina misikiti 25 yote inasaliwa Sala ya Ijumaa na mkoa mzima una misikiti 80.

Baadhi ya wanahistoria wanajiuliza nini ilikuwa athar ya kusilimu kwa Chief Mkwawa?

Ingekuwaje kama Mkwawa angekufa mpagani?

Laiti Abushiri angekuwa ''dubwana la hovyo'' (ovyo) asingeweza kuwa na usuhuba na Mtwa Mkwawa kiasi cha kumtia katika Uislam na kumfunza kusoma na kuandika.

Wazalendo hawa wawili wote wameacha historia kubwa ya vita vyao na Wajerumani.



Umeshawah kujiuliza Kwa nn hao wazalendo wako hawakupigana na mwarabu Bali walipigana na mjeruman ,.... ?? Hao jamaa walihusika kwenye biashara ya utumwa Kwa kumuuzia mateka mwarabu , walikuwa wanavamia himaya zingine Kwa nguvu , pindi wanaposhinda waliwachukua mateka na kuwauza Kwa waarabu ... Tatizo lilikuja mjeruman hakutaka hzo mambo , yeye alitaka resources wao wakaona wanapoteza umiliki wakaamua kuingia front , walichofanywa wanajua wenyewe ......
 
Umeshawah kujiuliza Kwa nn hao wazalendo wako hawakupigana na mwarabu Bali walipigana na mjeruman ,.... ?? Hao jamaa walihusika kwenye biashara ya utumwa Kwa kumuuzia mateka mwarabu , walikuwa wanavamia himaya zingine Kwa nguvu , pindi wanaposhinda waliwachukua mateka na kuwauza Kwa waarabu ... Tatizo lilikuja mjeruman hakutaka hzo mambo , yeye alitaka resources wao wakaona wanapoteza umiliki wakaamua kuingia front , walichofanywa wanajua wenyewe ......
Kabla ya Kuja Mjerumani alikuja Mreno, Mreno alinunua Watumwa ila pia walipigana na makabila ya Tanzania kwa nini?

Issue hapa ni kuingilia utawala wa watu.

Mwarabu hakutawala, aliwaacha watawala wa kiswahili kama walivyo, alishirikiana nao kibiashara na kila mtu alifaidika. Vitabu vingi nilivyosoma Kuanzia kilwa hadi Zanzibar ulikua ni kama muunganiko tu wa kibiashara kuanzia pwani, uchagani hadi Uganda huko.

Wareno na wajerumani wao hawakutaka kushirikiana na watawala waliowakuta, waliwaua, Walichukua mali bila kulipa na sehemu zote wanazoteka mali ni zao wenyeji hawapati kitu. Kwao concept Ya Biashara haikuepo ndio maana walipigana na watawala waliowakuta.
 
Shuleni tulifundishwa habari ya Abushiri wa Tanga kupigana na wakoloni wa kijerumani. Alitajwa kama shujaa mpigania uhuru kumbe hamna lolote. Kumbe jamaa alikuwa anamiliki mashamba makubwa na watumwa. Kifupi alikuwa anapigania nafasi ya kuendelea kukandamiza wengine. Hakuwa na maana kabisa.
View attachment 2644629
NGOJA WAJE....
 
Baba...
Nifahamishe ''issues'' unazotaka kuzijua.

Ikiwa najua vitabu nitakuelekeza na pia naweza hata mimi nikakueleza baadhi ya mambo katika hizo ''issues.''

Halikadhalika kuna elimu kubwa sana mitandaoni unaweza kufanya ''search.''
Historia ya Tanzania/Tanganyika/Zanzibar ila kabla ya mwaka 1900
 
Zous,
Huyu uliyemtaja jina lake ni Abdulraufu Songea Mbano lakini wanahistoria wamefuta jina la ''Abdulraufu'' wanamwita Songea Mbano.

Kaburi lake lipo peke yake Mahenge Songea kwenye makumbusho ya Vita Vya Maji Maji pembeni ya kaburi la halaiki ambalo majemadari wenzake wa vita hivyo wamezikwa.

Kuna historia ya kusikitisha sana ya kunyongwa kwao.

Majemadari hawa walikuwa Waislam na hukumu ya kuuliwa kwao ilipopitishwa na Wajerumani alikuja mmeshionari kutoka Peramiho akawaambia kuwa ikiwa watakubali kubatizwa hawatanyongwa.

Hii ilikuwa ghilba waliwabatiza na kuwapa majina ya Kikristo kisha wakawanyonga.
Orodha ya majina yao ipo hapo Mahenge kwenye mnara wa kumbukumbu.

Katika hawa majemadari kuna mwanamke pekee aliyenyongwa huyu wanamwita kwa jina moja ''Mkomanile'' lakini jina lake la Khadija Mkomanile.

Wanahistoria wamefuta jina lake la Khadija.

View attachment 2645371
Majemadari walionyongwa wa kwanza kulia waliosimama n Abdulraufu Songea Mbano
View attachment 2645373
Nduna Abdulraufu Songea Mbano


Shukran mkuu kwa kuniongezea jambo.kuna maneno yaliandikwa kwenye Hilo kaburi la majemedari.nimeyasahau ila yalikua yanahamasisha xnaa uzalendo
 
Hata wale wa kusini waliopigana vita vya Maji maji walikuwa wanataka kuendelea na biashara ya utumwa sio ?



Ukweli ni kwamba Abushiri na ukanda wa pwani walishakuwa na ustaarabu kitambo na waligomea wakoloni wa Kutoka German kwa wakati huo hata wadigo walishawagomea German wakakimbilia huko Lushoto kwa wasambaa kuanzisha makanisa.
 
Shukran mkuu kwa kuniongezea jambo.kuna maneno yaliandikwa kwenye Hilo kaburi la majemedari.nimeyasahau ila yalikua yanahamasisha xnaa uzalendo
Zous,

Mnara wenye majina ya wazalendo walionyongwa na Wajerumani katika Vita Vya Maji Maji:

1685895705999.png


''Kwa mara ya kwanza nilitembelea makumbusho hayo mwishoni mwaka 2007.

Baada ya kusaini kitabu cha wageni na kulipa ada ya kituo muhudumu wa kituo hicho alitupa karatasi yenye orodha ya majina ya wale wote walionyongwa na kuzikwa hapo.

orodha hiyo na hasa ukiwa Mwislam jambo moja litakustuwa. Robo tatu ya walionyongwa na kuzikwa hapo ni Waislaam.

Linaanza jina lake la Kiiislam, kisha kwenye mabano kuna jina la Kikristo na mwishoni linaishia jina la kiasili, mfano Abdulrahman [Dominic] Mputa Gama.

Muhudumu akatueleza kuwa hawa mashujaa wa vita vya Maji Maji kabla ya kunyongwa alikuwako padri ambae aliwabatiza na kuwapa majina ya Kikristo na baadae kunyongwa, wengi walibatizwa kwa hadaa kuwa wakibatizwa wataachiwa huru, wote katika hao walionyongwa walikuwa ni Waislam.

Uzuri ni kwamba katika orodha hiyo kulikuwa na jina na sahihi ya yule padri aliyewabatiza, na kwa mkono wake [huyo padri] aliiyaandika hayo majina.

Karatasi yenyewe ilihifadhiwa vizuri kwenye fremu ngumu ya kioo.

Tuliomba kwa nguvu zote kupatiwa hiyo karatasi ya majina hata kwa kununua lakini haikuwezekana pamoja na kuwaona wakubwa wa kituo hicho.

Niliporudi kwa mara ya pili mwezi July 2009 nilipata mstuko.

Karatasi iliyohifadhiwa kwenye fremu ngumu ya kioo, iliyokuwa na majina ya Kiislaam ya mashujaa wa vita vya Maji Maji, haikuwapo,na badala yake imewekwa karatasi nyingine ombayo ndani ya karatasi hiyo majina ya Kiislaam ya mashujaa hao wa vita vya Maji Maji yameondolewa na kuachwa majina ya ubatizo na yale ya kiasili tu, jina la padri, sahihi yake na wadhifa wake katika Kanisa Katoliki pia vimeondolewa na karatasi yenyewe haikuwa kwenye fremu ya kioo na ilikuwa katika fotokopi tu.''

Huo hapo chini ni mnara wa wazalendo walionyongwa Kilwa kabla ya Vita Vya Maji Maji lakini mnara umeandikwa kwa makosa kuwa walinyongwa katika vita hivyo:

1685896376550.png
 
Hizi historia zingefutwa tu hazina maana yeyote katika maisha. Tuanzie enzi za Nyerere na Uhuru mpaka udikteta wa kina Magufuli
 
sababu ni muislamu ndie habari zake zimepinduliwa angekuwa Romani angepewa sifa nyingi za uongo
 
Hakika Mkuu, naamini Chifu Mangungo angekuwa amepiga shule angekuwa Mtawala mzuri kuliko tulionao miaka ya hivi karibuni

Umewahi kukisoma Kitabu kinaitwa Black Shadow?

Kilifutwa baada ya Watawala kuto kukipenda vile kimewazungumzia
Mkuu hiki kitabu naweza PATA nakala durufu(photocopy) yake kama unacho?
 
Mkuu hiki kitabu naweza PATA nakala durufu(photocopy) yake kama unacho?
Hiki kitabu kilizuiwa kutumika na Serikali, bahati nzuri ninacho kwenye library yangu ya Kijijini huko.

Nina ratiba ya kwenda huko mwezi huu mwishoni, nikikumbuka nita scan nikutumie soft copy Mkuu
 
Back
Top Bottom