Kumbe Abushiri wa Tanga aliyepigana na wajerumani na kunyongwa hakuwa na maana yoyote

Utumwa ulikuwa ukatili
 
Umeshawah kujiuliza Kwa nn hao wazalendo wako hawakupigana na mwarabu Bali walipigana na mjeruman ,.... ?? Hao jamaa walihusika kwenye biashara ya utumwa Kwa kumuuzia mateka mwarabu , walikuwa wanavamia himaya zingine Kwa nguvu , pindi wanaposhinda waliwachukua mateka na kuwauza Kwa waarabu ... Tatizo lilikuja mjeruman hakutaka hzo mambo , yeye alitaka resources wao wakaona wanapoteza umiliki wakaamua kuingia front , walichofanywa wanajua wenyewe ......
 
Kabla ya Kuja Mjerumani alikuja Mreno, Mreno alinunua Watumwa ila pia walipigana na makabila ya Tanzania kwa nini?

Issue hapa ni kuingilia utawala wa watu.

Mwarabu hakutawala, aliwaacha watawala wa kiswahili kama walivyo, alishirikiana nao kibiashara na kila mtu alifaidika. Vitabu vingi nilivyosoma Kuanzia kilwa hadi Zanzibar ulikua ni kama muunganiko tu wa kibiashara kuanzia pwani, uchagani hadi Uganda huko.

Wareno na wajerumani wao hawakutaka kushirikiana na watawala waliowakuta, waliwaua, Walichukua mali bila kulipa na sehemu zote wanazoteka mali ni zao wenyeji hawapati kitu. Kwao concept Ya Biashara haikuepo ndio maana walipigana na watawala waliowakuta.
 
NGOJA WAJE....
 
Baba...
Nifahamishe ''issues'' unazotaka kuzijua.

Ikiwa najua vitabu nitakuelekeza na pia naweza hata mimi nikakueleza baadhi ya mambo katika hizo ''issues.''

Halikadhalika kuna elimu kubwa sana mitandaoni unaweza kufanya ''search.''
Historia ya Tanzania/Tanganyika/Zanzibar ila kabla ya mwaka 1900
 

Shukran mkuu kwa kuniongezea jambo.kuna maneno yaliandikwa kwenye Hilo kaburi la majemedari.nimeyasahau ila yalikua yanahamasisha xnaa uzalendo
 
Hata wale wa kusini waliopigana vita vya Maji maji walikuwa wanataka kuendelea na biashara ya utumwa sio ?



Ukweli ni kwamba Abushiri na ukanda wa pwani walishakuwa na ustaarabu kitambo na waligomea wakoloni wa Kutoka German kwa wakati huo hata wadigo walishawagomea German wakakimbilia huko Lushoto kwa wasambaa kuanzisha makanisa.
 
Shukran mkuu kwa kuniongezea jambo.kuna maneno yaliandikwa kwenye Hilo kaburi la majemedari.nimeyasahau ila yalikua yanahamasisha xnaa uzalendo
Zous,

Mnara wenye majina ya wazalendo walionyongwa na Wajerumani katika Vita Vya Maji Maji:



''Kwa mara ya kwanza nilitembelea makumbusho hayo mwishoni mwaka 2007.

Baada ya kusaini kitabu cha wageni na kulipa ada ya kituo muhudumu wa kituo hicho alitupa karatasi yenye orodha ya majina ya wale wote walionyongwa na kuzikwa hapo.

orodha hiyo na hasa ukiwa Mwislam jambo moja litakustuwa. Robo tatu ya walionyongwa na kuzikwa hapo ni Waislaam.

Linaanza jina lake la Kiiislam, kisha kwenye mabano kuna jina la Kikristo na mwishoni linaishia jina la kiasili, mfano Abdulrahman [Dominic] Mputa Gama.

Muhudumu akatueleza kuwa hawa mashujaa wa vita vya Maji Maji kabla ya kunyongwa alikuwako padri ambae aliwabatiza na kuwapa majina ya Kikristo na baadae kunyongwa, wengi walibatizwa kwa hadaa kuwa wakibatizwa wataachiwa huru, wote katika hao walionyongwa walikuwa ni Waislam.

Uzuri ni kwamba katika orodha hiyo kulikuwa na jina na sahihi ya yule padri aliyewabatiza, na kwa mkono wake [huyo padri] aliiyaandika hayo majina.

Karatasi yenyewe ilihifadhiwa vizuri kwenye fremu ngumu ya kioo.

Tuliomba kwa nguvu zote kupatiwa hiyo karatasi ya majina hata kwa kununua lakini haikuwezekana pamoja na kuwaona wakubwa wa kituo hicho.

Niliporudi kwa mara ya pili mwezi July 2009 nilipata mstuko.

Karatasi iliyohifadhiwa kwenye fremu ngumu ya kioo, iliyokuwa na majina ya Kiislaam ya mashujaa wa vita vya Maji Maji, haikuwapo,na badala yake imewekwa karatasi nyingine ombayo ndani ya karatasi hiyo majina ya Kiislaam ya mashujaa hao wa vita vya Maji Maji yameondolewa na kuachwa majina ya ubatizo na yale ya kiasili tu, jina la padri, sahihi yake na wadhifa wake katika Kanisa Katoliki pia vimeondolewa na karatasi yenyewe haikuwa kwenye fremu ya kioo na ilikuwa katika fotokopi tu.''

Huo hapo chini ni mnara wa wazalendo walionyongwa Kilwa kabla ya Vita Vya Maji Maji lakini mnara umeandikwa kwa makosa kuwa walinyongwa katika vita hivyo:

 
Hizi historia zingefutwa tu hazina maana yeyote katika maisha. Tuanzie enzi za Nyerere na Uhuru mpaka udikteta wa kina Magufuli
 
sababu ni muislamu ndie habari zake zimepinduliwa angekuwa Romani angepewa sifa nyingi za uongo
 
Hakika Mkuu, naamini Chifu Mangungo angekuwa amepiga shule angekuwa Mtawala mzuri kuliko tulionao miaka ya hivi karibuni

Umewahi kukisoma Kitabu kinaitwa Black Shadow?

Kilifutwa baada ya Watawala kuto kukipenda vile kimewazungumzia
Mkuu hiki kitabu naweza PATA nakala durufu(photocopy) yake kama unacho?
 
Mkuu hiki kitabu naweza PATA nakala durufu(photocopy) yake kama unacho?
Hiki kitabu kilizuiwa kutumika na Serikali, bahati nzuri ninacho kwenye library yangu ya Kijijini huko.

Nina ratiba ya kwenda huko mwezi huu mwishoni, nikikumbuka nita scan nikutumie soft copy Mkuu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…