Kumbe kuoa ni kugumu hivi? Aisee mniombee niko hoi bin taabani

Kumbe kuoa ni kugumu hivi? Aisee mniombee niko hoi bin taabani

Hivi nyie wana mliokaa kwenye ndoa zaidi ya miaka kumi mmefanyeje aisee? Yaani sio poa wakuu yaani niko hoi bin taabani ndiyo kwanza ndoa yangu ina wiki mbili tu aisee najihisi kuchoka na kukata tamaa wakuu.

Majukumu yamenizidi, nakosa uhuru wa kuamua mambo yangu eti lazima mshirikishane wote kwenye nyumba yaani hapa nipo hoi bin taabani fanyeni wana wajamii forum mninusuru mambo sio poa niko chupli chupli mambo yamekwama wakuu.

Ndiyo kwanza nina miaka 27 yaani naona mambo yamenielemea majukumu yanakuwa mengi sana na wakuu naombeni msaada wenu.
Hujasema bado.
NDOA NI KWAAJILI YA WANAWAKE NA WANAUME WAJINGA.
#KATAANDOA
 
Hivi nyie wana mliokaa kwenye ndoa zaidi ya miaka kumi mmefanyeje aisee? Yaani sio poa wakuu yaani niko hoi bin taabani ndiyo kwanza ndoa yangu ina wiki mbili tu aisee najihisi kuchoka na kukata tamaa wakuu.

Majukumu yamenizidi, nakosa uhuru wa kuamua mambo yangu eti lazima mshirikishane wote kwenye nyumba yaani hapa nipo hoi bin taabani fanyeni wana wajamii forum mninusuru mambo sio poa niko chupli chupli mambo yamekwama wakuu.

Ndiyo kwanza nina miaka 27 yaani naona mambo yamenielemea majukumu yanakuwa mengi sana na wakuu naombeni msaada wenu.
Wana Jf tukusaidie vip mkuu,tukuoe ama?!
 
Kuhusu uchumi, jenga urafiki na mwenzio, mshirikishe kwa namna unapata kipato chako ili awe na soni kwa matumizi yaso na lazima na pia awe na huruma na kumudu kukusaidia baadhi ya mahitaji.

Kuhusu kumshirikisha kila Jambo my dear huwezi kukwepa, lazma yale ya muhimu umwambie , la sivyo jiandae kwa fita muraaa.... kununiwa, kulipiziwa kisasi, vikao visivyoisha....

Zaidi nikupongeze kwa kuoa mapema, ukitulia na kumuheshimu mkeo na kumpenda, na kumthamini utakua na ndoa bora, mengine yanahitaji uvumilivu, jitahidini mte geneze chemistry itawabeba katika vingi, Kuna mda mapenzi yanaisha ,ila ile bond inawafanya mnasonga....
 
Ndio shida ya kuoa baada ya kuanza kubalehe tu.
Wenzako huwa wanamaliza balehe kwanza.
Mapenzi (ndoa) haina mwenyewe.
Dr. Mwaka huyo na Haji Manara.
Kama haujaingia kwenye ndoa unaweza fikiri kama ulivyoandika.
Ndoa hizi, unaweza kuishi na mwenzako vizuri na kwa upendo ila mkifikisha miaka ya uzeeni mnatengana.
Tuombeane heri ndugu. Mapenzi hayana mwenyewe.
Hapo ulipo, unaweza kuwa na jamaa mnapendana na ukawaona wengine ni wajinga tu ila............. Mwisho unashituka ushakuwa single mom
 
Mkuu sisi tulisha waambia KATAA NDOA SAVE KIBUNDA,

na ukishindwa kuishi mwenyewe vuta mama ishi nae UCHUMBA SUGU AU OA MWANAMKE MWENYE HELA KAMA WAO WANAVYO TAKA MWANAUME MWENYE HELA

Umepuuza yote hayo ukaenda kuoa kwa tamaa zako huku ukijua utakua una ichapa kila siku, mambo yamekuendea vibaya unakuja hapa kusumbua watu,

kua kwanza alafu uje tukushauri cha kufanya maana bado wewe ni mtoto
 
Kizazi hiki kinazidi kupoteza WANAUME.

Je hukujua kuwa kuoa ni kwa wanaume wanaojiweza kimwili na kiakili? Kuoa sio jambo analostahili kila binadamu aliyezaliwa na uume. Ingekupendeza ungeendelea kubaki kwenye chama cha wakataa ndoa (incapable males) na sio kuingia sehemu usiyoistahili.

Utoke upesi huko ulikojiingiza kabla ya kuyaharibu maisha ya huyo binti uliyemuoa. Hivi na nyinyi wasichana, watu immature namna hii mnawaaminije kuingia nao kwenye ndoa? Oooh sorry nimesahau kuwa jamii yeyote haikosi watu wenye vipaji vya upumbavu. BTW wapumbavu kutoka jinsia mbili tofauti mmekutana hivyo endeleeni na upumbavu wenu.
 
Back
Top Bottom