Kumbe kuoa ni kugumu hivi? Aisee mniombee niko hoi bin taabani

Kumbe kuoa ni kugumu hivi? Aisee mniombee niko hoi bin taabani

Tatizo Nini mkuu chakula au Kodi ?

Mimi nakushauri Kama tatizo ni PESA ya chakula useme au Kama tatizo ni mambo mengine useme ili tuone tunakusaidiaje Ila jifunze uvumilivu usimfukuze huyo Mwanamke endelea kujenga naye future huko Mbele Kuna mwanga.
 
Hivi nyie wana mliokaa kwenye ndoa zaidi ya miaka kumi mmefanyeje aisee? Yaani sio poa wakuu yaani niko hoi bin taabani ndiyo kwanza ndoa yangu ina wiki mbili tu aisee najihisi kuchoka na kukata tamaa wakuu.

Majukumu yamenizidi, nakosa uhuru wa kuamua mambo yangu eti lazima mshirikishane wote kwenye nyumba yaani hapa nipo hoi bin taabani fanyeni wana wajamii forum mninusuru mambo sio poa niko chupli chupli mambo yamekwama wakuu.

Ndiyo kwanza nina miaka 27 yaani naona mambo yamenielemea majukumu yanakuwa mengi sana na wakuu naombeni msaada wenu.
Tatizo lilianzia ulipotamani michango ya sherehe ya harusi badala ya kufikiria ikiwa umepevuka au la kumdu masuala ya ndoa.
Usijali,kumbuka videos za ukumbini na namna ulivyokuwa unawachukia waliogoma kukuchangia.
 
Ulitumwa na nani!?,umewahi kuishi mwezi mmoja au miwili mfululizo na uliyemuoa kabla hamjaoana!?, Au mlikuwa mnaviziana mpewe baraka za kijinga na jamii?,

Tatizo la ndoa linaanzia pale mnapopanga kuoana kwa kuiridhisha jamii na mbwembwe nyingi. Ila ukiishi na mtu bila masharti na mikakati mingi ya ndoa au msukumo kutoka kwa ndugu jamaa na marafiki mnaishi vizuri tu tena kwa muda usiojulikana.

Ila mkianza mipango ya ndoa ikawa mingi ndo tatizo linapoanzia. Miaka 27 ulikuwa unawahi nini!?.., kama unaishi kijijini ni sawa hata ukiwa na miaka 23 tu.

Ila kama ni msomi na upo town 27 unajitafutia matatizo. Muda sio mrefu utaanza kulaumu wazazi, ndugu na jamaa, baadae serikali mwisho kabisa utaanza kuilaumu CCM, nawaona humu kila lawama ni kwa CCM[emoji1787]
Kataa ndoa kijana alikulupuka sana
 
Ulitumwa na nani!?,umewahi kuishi mwezi mmoja au miwili mfululizo na uliyemuoa kabla hamjaoana!?, Au mlikuwa mnaviziana mpewe baraka za kijinga na jamii?,

Tatizo la ndoa linaanzia pale mnapopanga kuoana kwa kuiridhisha jamii na mbwembwe nyingi. Ila ukiishi na mtu bila masharti na mikakati mingi ya ndoa au msukumo kutoka kwa ndugu jamaa na marafiki mnaishi vizuri tu tena kwa muda usiojulikana.

Ila mkianza mipango ya ndoa ikawa mingi ndo tatizo linapoanzia. Miaka 27 ulikuwa unawahi nini!?.., kama unaishi kijijini ni sawa hata ukiwa na miaka 23 tu.

Ila kama ni msomi na upo town 27 unajitafutia matatizo. Muda sio mrefu utaanza kulaumu wazazi, ndugu na jamaa, baadae serikali mwisho kabisa utaanza kuilaumu CCM, nawaona humu kila lawama ni kwa CCM🤣
😂
 
Mkuu komaa tu. Kwa umri wako mimi ni mdogo wako ila nimekomaa mpaka sasa naenda mwezi wangu wa nne. Hakuna mwanzo rahisi, na miezi 6 ya mwanzo ndio migumu balaa ila kila miezi inapoenda utaanza kuona unafuu kwenye ndoa yako. Mungu akusimamie
 
Unajiona hutoshi tatizo bado huamini kama umeoa, Yani mentality ya usingle inakusumbua na kujiona Bado mdogo Kwa hayo majukumu yako mapya, wakati tayari wewe ni mtu mzima uliyekomaa kidevu kabisa...Wala usiwe na presha kubali tu nafsini mwako kuwa kule ushatoka Sasa hivi upo ukurasa mwingine wa maisha, jitayarishe kuwa baba na kichwa cha familia Mzee...kuwa makini kama umechoka mapema hivi wahuni watakusaidia kweli.
 
Back
Top Bottom