Kumbe sababu ya kifo cha Mkapa ni Cardiac Arrest. Asante sana mwanafamilia William Erio kumaliza sintofahamu hii

Ukweli wanao watanzania moyoni na akilini mwao ingawa wanafamilia wamejitahidi kutaka kutuaminisha walichokisema wao
 

Hujaelewa , alipelekwa hosp kwa case ya malaria , hyo cardiac arrest imetokea ghafla akiwa huko hospital
 
We acha tu Kaka...Mkapa alisema TAIFA LINA WAANDISHI KANJANJA.....na hwenda pia tuna madaktari KANJANJA Hawa wa humu MITANDAONI....

NImemuelewa ERIO;
CAUSE OF DEATH:CARDIAC ARREST SECONDARY TO SEVERE(COMPLICATED MALARIA).

Mengine ni POROJO ZA KINDWANYE
 
Tumechoka kudanganywa
Nkurunzinza walisema hivyohivyo na kuficha ukweli kuwa ni Upumuaji
Huyu mzee naye wanatuambia hivyohivyo wakati dalili ni Upumuaji

Malofa na Wapumbavu hatuwezi kujua tu. Tutasubili waendelee kutuhabarisha kuwa sio UPUMUAJI
 
Nawe pia haujaelewa. Ni malaria ndio imemuua. Ndio imesabisha cardiac arrest. Ni malaria ndio imesabisha kifo. Usitenganishe malaria yake na cardiac arrest. Kinachoitwa kifo/death ndio cardiac arrest hiyo kwa kitaalam.
Hujaelewa , alipelekwa hosp kwa case ya malaria , hyo cardiac arrest imetokea ghafla akiwa huko hospital
 
Umbea na uongo unasumbua sana binadamu (watanzania) hivi kweli unapoteza muda kutaka kujua chanzo cha kifo?wote tunajua kifo kinatafutaga sababu,tumuombee akimaliza mwendo salama tena ameishi umri wa kutosha kabisa wa kimungu sasa mwenzangu na Mimi hatujui tutakufaje tuko busy kujadili na kujifanya madaktari bingwa😕😕😕
 
Wewe akili ndio huna, alikua anaumwa Malaria na anaendelea vzr akifuatilia habari ktk Tv, alipokua amekaa kwenye kiti akajisikia ghafla vibaya Cardiac arrest, sasa ww ulitaka wampeleke Jakaya Kikwete Cardiac kwa tatizo la Malaria ?
Aaah Mkuu maneno makali sana hayo nikose akili tena. Ni suala la kuelewa nimeelewa sasa Mkubwa
 
Mkuu kifo cha mkapa ni covid 19 lakini kwa kuwa ilishatangazwa kuwa corona imekwisha Tanzania imekuwa vigumu kusema kafa kwa covid 19 na pia wameogopa wanafamilia kutengwa na jamii, tuendelee kuamini kile mmoja anakiamini moyoni mwake na hao wanafamilia acha waseme hayo kwani wapo watakaoamini kama alivyoamini Paskal mayala.
 
Mimi sikumtibu lakini. Kama wewe ulimtibu basi nakushukuru kwa taarifa.
 

Kulikua na Sababu Gani Sasa ya kuwa na Kauli tofauti tofauti?
Ndugu wanasema ni Mshtuko wa Moyo na kafia nyumbani...
Hiyo story ya Hospital imetoka wapi
 
Kama ni hivyo hata wanafamilia wasingesema kafa kwa nini wangesema kafariki tu, kujua kitu Tatizo siyo kupoteza mda, ina maana wanafamilia kusema kilichopoteza uhai ni umbea?
 
Wataalamu wa afya wanatumia vigezo 2 kueleza chanzo cha kifo chochote:- 1. Immediate cause na 2. Underlying cause, wakati mwingine huongeza intermediate cause na contributory cause,....nafikiri watanzania hatujajua tunachotaka kujua kati ya hayo na hivyo wanashindwa kutupatia jibu sahihi.
 
Kulikua na Sababu Gani Sasa ya kuwa na Kauli tofauti tofauti?
Ndugu wanasema ni Mshtuko wa Moyo na kafia nyumbani...
Hiyo story ya Hospital imetoka wapi
Familia wamejichanganya sana na wamemfanya kikwete aonekane muongo wakati kikwete alienda kumuona kweli na mkweli ni kikwete na Hosptal alipokuwa kikwete anapajua, wanafamilia wamejichanganya sana ni Aibu kubwa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…