Kumbe Tanzania ilikopa fedha World Bank kuendeleza bandari, DP World anakuja kutumia fedha hizo kufanya kazi ambayo Tanzania imeikopea fedha WB-SOMA

Kumbe Tanzania ilikopa fedha World Bank kuendeleza bandari, DP World anakuja kutumia fedha hizo kufanya kazi ambayo Tanzania imeikopea fedha WB-SOMA

Hii ni kutoka report ya Worl Bank .................................BY MARIA SARUNGI

Muhimu kuhusu DPW na mradi wa Benki ya Dunia

Pesa za mkopo wa @WorldBankAfrica zimetumika (na kukamilika)
👉🏽 kupanua na kuimarisha Gati 1-7 na kujenga gati mpya Gerezani
👉🏽kupanua mlango wa bandari hadi Gati 11
👉🏽kuboresha na kuunganisha na reli
👉🏽 Kupanua na kuimarisha Gati 8-11
👉🏽Kuna RORO terminal ilijengwa na kukamilishwa

Sasa tuangalie wanachodai DP World kufanya kwa mujibu wa IGA
Cha kwanza kikubwa eti kujenga, kuendesha na kusimamia RoRo terminal na Gati 1-4 na gati 5-7
🙄
Yaani pesa zote zimewekezwa za walipa kodi kupitia mradi wa sasa wa WB alafu wao wanakuja kuendesha na kusimamia? Wanawekeza nini??

Ndiyo maana mkataba haujawekwa thamani ya uwekezaji wao 😄 kumbe wanadandia mradi unaoelekea kukamilika waje wajisifu!

YAANI KIUFUPI WANAKUJA KUTEKELEZA MRADI WA PESA ZA MKOPO WA WORLD BANK

Nyieeeeeeeeee!
Mnaotetea mkataba huu mnajua kuwa mnatumika kutetea ulaji wa genge ndogo!?
Ila #TutaelewanaTu
Halafu tulipe. Mungu anakuona saa100
 
Hayo yote ya nini jambo muhimu ni ufanisi ili serikali iongeze mapato kupitia bandari........na hilo Dp world ndo imekuja kutekeleza basi, hata kama mkataba ni wa miaka 100 as long serikali ina pata faida na inahudumia wananchi wake vizuri na kufanya maendelo hamna shida tuache fitina za kijinga.
Kuna guarantee gani kuwa DP world wataweza kuongeza mapato!!?
 
Serikali kulipa madeni yake shida, kutoa huduma shida za jamii inajikwamua. Ikawekeze tena bandarini wakati kuna mtu yupo tayari. Ambae kwanza anaweka hela yake, analipia kodi ya eneo bandari, anagawana mapato yake na TPA, na anaongeza volumes za mizigo TRA ipate kodi zaidi kwenye forodha.

Na akisharudisha hela yake na kutupa uzoefu maeneo yenyewe aliyopewa anawarudishia TPA; unataka nini tena kama ndio serikali.

Issue hapo ni kuingia mikataba mizuri ya utekelezaji; lakini IGA aina shida yoyote.

Akisharudisha hela yake anawarudishia TPA?
Hiyo kitu iko wapi kwenye conditions na terms?
 
Serikali kulipa madeni yake shida, kutoa huduma shida za jamii inajikwamua. Ikawekeze tena bandarini wakati kuna mtu yupo tayari. Ambae kwanza anaweka hela yake, analipia kodi ya eneo bandari, anagawana mapato yake na TPA, na anaongeza volumes za mizigo TRA ipate kodi zaidi kwenye forodha.

Na akisharudisha hela yake na kutupa uzoefu maeneo yenyewe aliyopewa anawarudishia TPA; unataka nini tena kama ndio serikali.

Issue hapo ni kuingia mikataba mizuri ya utekelezaji; lakini IGA aina shida yoyote.

Akisharudisha hela yake anawarudishia TPA?
Hiyo kitu iko wapi kwenye conditions na terms?
 
Sasa ulifikiri bandari yote ile imejengwa na nani< Waliaza Waarabu,wakaja Eajerumani, Wakaja Waingereza, Ikaja serikali ya Tanzania, wote wameijenga mpaka walivyofikia.



Unafikiri mkataba uliopo ni wa kujenga bandari? Huo kwa sasa hapa Dar hakuna, wa Dar ni wa kuendesha tu shughuli za makontena bandarini. Tena siyo bandari yote.

Bagamoyo, Tanga ndiyo mikataba yake ya brand new Bandari na uendeshaji.

Hawa labda mizigo ikizidi waingie mkataba mwengine wa kujenga, na hata wakijenga usifikiri kwa pesa zao, inakuwa ni grant tu. Maana yake kitachotumika kitarudishwa bila riba. Na huku kazi zinaendelea.

Ni kama ukodishe nyumba halafu wewe mpangaji uitengeneza na kuiboresha halafu mnakatiana kwenye kodi.

Hivi unafikiri DP World wana kazi ipi pale? Wao wanakodisha tu bandari wanailipia kodi. Na wao wanatukodisha huduma zao. Basi. Hakuna zaidi.
 
Mkataba wa IGA ni wa miaka mingapi?
Huu uliopo ni miezi 12 au chini ya hapo. Iwe tayari kuna mkataba wa HGA ambao huo sasa ndiyo utaainisha kila mradi utakuwa wa muda gani.

Soma kifungu cha 5:4
 
Huu uliopo ni miezi 12 au chini ya hapo. Iwe tayari kuna mkataba wa HGA ambao huo sasa ndiyo uytainisha kila mradi utakuwa wa muda gani.
Hiyo miezi 12 ni kwa mujibu wa mkataba au ni matamanio yako tu? Kifungu cha UKOMO kwenye huo mkatana kimesema ni miezi 12? Au we ymesoma mkataba wako na baba mwenyenyumba wako?
 
Kwani mkataba wa Dp world na Tpa tayari? Mbona mnaendekeza Cheap Politics hivi?

Dp world vifaa vyao sio vya kitoto eti waje watumie Existing infrastructure, Hizo Crane na miundombinu mingine capability yake wanayo wao tu ama ni kampuni chache zenye uwezo huo.

Kusema kwamba Dp world wanatutegemea sisi eti mkopo wetu wa World Bank uwawezeshe wao ni chai ya mchana.
Wewe uko nchi gani ndugu?
 
Let us agree to disagree, usinilazimishe niamini unacho amini, hoja yangu ni kwa DP world itaongeza ufanisi na mapato serikalini yataongezeka.......sisi wabongo tumeshindwa kuendesha bandari kwa mda mrefu
Kama kiongozi wa chini kashindwa Ina maana mkubwa wake kashindwa na mkubwa wa wote kwenye utendaji kwa njia hii ni Rais
 
Huo ndo ukweli na tatizo ni lipi waseme bayana siyo kuwa too general na kupotosha umma. Kama mtu hana capacity ya kuchambua hili bora kukaa kimya.

Tulishashindwa miaka kibao mpaka KAGAME alitucheka tukamjibu kwa kuwatimua Raia wa nchi yake.
Kagame aliwacheka raia au alimcheka Rais ili tujue tatizo liko wapi
 
Hiyo miezi 12 ni kwa mujibu wa mkataba au ni matamanio yako tu? Kifungu cha UKOMO kwenye huo mkatana kimesema ni miezi 12? Au we ymesoma mkataba wako na baba mwenyenyumba wako?
Kasome kifungu cha 5:4
 
Hayo yote ya nini jambo muhimu ni ufanisi ili serikali iongeze mapato kupitia bandari........na hilo Dp world ndo imekuja kutekeleza basi, hata kama mkataba ni wa miaka 100 as long serikali ina pata faida na inahudumia wananchi wake vizuri na kufanya maendelo hamna shida tuache fitina za kijinga.
Utakuta unaandika haya hata sehemu ya kulala hauna.
 
Hayo yote ya nini jambo muhimu ni ufanisi ili serikali iongeze mapato kupitia bandari........na hilo Dp world ndo imekuja kutekeleza basi, hata kama mkataba ni wa miaka 100 as long serikali ina pata faida na inahudumia wananchi wake vizuri na kufanya maendelo hamna shida tuache fitina za kijinga.
Upuuzi umeongea
 
Acha ujinga wewe, yaani watoke kwao kote huko ati waje kusaidia serikali yako ipate mapato? Mapato yaongezeke Kwa kiasi Gani na wao watakuwa wamechukuwa ngapi?
Hivi na hao TICS walitokea wapi? Kuja kuwekeza bandari? Mgekua mnayaweka wazi maana sisi wengine ma mbumbumbu
 
Akisharudisha hela yake anawarudishia TPA?
Hiyo kitu iko wapi kwenye conditions na terms?
Imesemwa mara kadhaa mkataba utaisha project activities/agreements. zitakapoisha.

Ila ana option ya kuomba kuongezewa muda, akikubaliwa huo sasa ni mkataba wa management tu, tofauti na mikataba ya mwanzo. Na si lazima TPA imwongezee muda.
 
Kasome kifungu cha 5:4
Pia kasome kile kifungu kinachosema mkataba ni hadi shughuli za kibandari zitakapokoma, sasa siju ni lini shughuli za kibandari ziliwahi kukoma hapa duniani. Na hairuhusiwi kujitoa kwenye mkataba, hata tukipigana nao vita, mkataba hauvunjiki, hata wakakiuka masharti ya mkataba, hauvunjiki.
 
Hii ni kutoka report ya Worl Bank .................................BY MARIA SARUNGI

Muhimu kuhusu DPW na mradi wa Benki ya Dunia

Pesa za mkopo wa @WorldBankAfrica zimetumika (na kukamilika)
👉🏽 kupanua na kuimarisha Gati 1-7 na kujenga gati mpya Gerezani
👉🏽kupanua mlango wa bandari hadi Gati 11
👉🏽kuboresha na kuunganisha na reli
👉🏽 Kupanua na kuimarisha Gati 8-11
👉🏽Kuna RORO terminal ilijengwa na kukamilishwa

Sasa tuangalie wanachodai DP World kufanya kwa mujibu wa IGA
Cha kwanza kikubwa eti kujenga, kuendesha na kusimamia RoRo terminal na Gati 1-4 na gati 5-7
🙄
Yaani pesa zote zimewekezwa za walipa kodi kupitia mradi wa sasa wa WB alafu wao wanakuja kuendesha na kusimamia? Wanawekeza nini??

Ndiyo maana mkataba haujawekwa thamani ya uwekezaji wao 😄 kumbe wanadandia mradi unaoelekea kukamilika waje wajisifu!

YAANI KIUFUPI WANAKUJA KUTEKELEZA MRADI WA PESA ZA MKOPO WA WORLD BANK

Nyieeeeeeeeee!
Mnaotetea mkataba huu mnajua kuwa mnatumika kutetea ulaji wa genge ndogo!?
Ila #TutaelewanaTu
kwa hiyo kwa lugha nyengine, ni kwamba tulikopa pesa world bank kuendeleza bandari ya DP WORLD? ila kulipa tutalipa sisi wananchi. is that what you mean?
 
Back
Top Bottom