Kumbukumbu ya kuzama kwa MV Bukoba tarehe 21 May, 1996

Kumbukumbu ya kuzama kwa MV Bukoba tarehe 21 May, 1996

Hii ajali imenikumbusha usemi wa baadhi ya watu wanapogombana aliyechukia zaidi humwambia mwenzake HATA NIKIFA SITAKI UJE KUNIZIKA. Inabidi usemi huu ukome kwa sababu waweza zama baharini na wala mwili wako usionekane na huta zikwa kweli.Mungu awapumzishe kwa amani waliokufa kwa ajali hii.
Na katika hiyo ajali kuna bwana mmoja miaka kadhaa nyuma alikuwa kamwambia baba yake katika ugomvi wao kuwa "Mimi si mwanao tena. Hata nikifa usinizike". Mzee nae akamjibu "Haya. Na sitakuzika mwanangu". Matokeo yake yule bwana hakuzikwa kweli na baba yake kwa sababu alikuwa ni mmoja wa watu waliopoteza maisha katika ajali hiyo lakini mwili wake haukupatikana kabisa.
 
ILIKUWA Mei 21,1996 katika ziwa Victoria, meli ya MV Bukoba ilipata ajali baada ya kupinduka na kuzama na hivyo kupelekea zaidi ya watu 800 kupoteza maisha. Meli hiyo ilizama ikiwa imebakiza takribani kilomita 30 kutia nanga kwenye bandari ya Jiji la Mwanza ikitokea mkoani Kagera.Jumamosi ya tarehe 21/05/2016 itatimia miaka 20 tangu ajali hiyo itokee. Daima tutazidi kuwakumbuka ndugu, jamaa na marafiki waliopoteza maisha katika ajali hiyo.sema neno kwa waliohusika na ajali hii
 
Hii ajali iliturudisha nyuma sana wakazi Wa Kagera, wafanyabiashara wengi walokuwa wanaenda kununua bidhaa Mwanza wengi walikufa, na baba yangu chupuchupu naye angesafiri siku ile, na mama tiyari alishamsindikiza ila ghafla tulimuona jioni akirudi, afu mzee wangu ni mtu kaksi sana alipoulizwa kwa nn kahairisha safari hakusema zaidi ya kuingia chumbani kulala na kuwasha redio yake Panasonic, kesho yake tunaambiwa ajali
 
Katika kumbukumbu za mwaka huu, ni vizuri seriali ikaweka wazi kilichotokea badala ya kuwafumba watu n akuishia kusema Marehemu walazwe pema wakati kuna mengi ya kujifunza.

Si kwa vyombo vya majini bali kila chombo cha usafiri.

WAtu waliokufa ni wengi zaidi ya 800.

Meli ilioveload watu na mizigo kupita uwezo wake kwa hesabu isiyosemekana kana kwamba hapakuwa na wataalamu, wala chombo cha kusimamia compliance and usalama wa wateja.
Jambo hili linatokea kila sehemu hata katika mabus na daladala. Utakuta makondakta wamejaza abiria na mizigo ndani ya basi la abiria. WAsimamizi wako barabarani kuongea na wafanyakazi wa mabus pembeni na kuruhusu gari kuondoka bila kuzingatia usalama wa abiria. Ikitokea ajail iwatu wanakufa kwa kugongwa na mizigo ama kufunikwa na kushindwa kujiokoa. Matumizi ya malori ya midanani yakiwa yajeaza mizigo na abiria juu!. Pikipiki na ubebaji wa mishkakki. Bodaboda kuendeshwa bila kufuata taratibu kwa maana ya kuchomekea kulia kushoto, kati kati ili mradi anakwenda bila kujua athari zake kwa mwendeshaji na abiria wake huku wasalama wakiona kawaida.

MV Bukoba ilikuwa meli lya miaka mingi na kila wakati ilikuwa katika matengenezo including siku ya ajali. Matumizi ya vyombo vibovu katika usafirishaji ni tatizo. Hili ni pamoja na daladala, mabusi, ndege n.k. Serikali kuruhusu ununizi wa vitu vichovu bila kuwa na kiwango cha mwisho cha uchakavu. Kulipisha kodi kubwa kwa muagizaji wa chombo kibovu hakuwi mbadala wa usalama wa watumiaji wa chombo hicho. Matumizi ya magari mabaya, machovu, machkavu na yasiyofaa kwa kusarifisha abiria mijiini na vijinini ni kuvundika mauti. Utakuta gari limechunika maviti hayana mavazi, nondo zimejaa kutu, uchafu n aharufu iliyokithiriri, hadi mende, kunguni na kila aina ya ubaya lakini wasimamizi wa usafiri wanachojali awe amelipia njia na leseni, bila kuzingatia abiria wanaathirikaje. Ifike mahali chombo chochote cha kubebea watu kinapokuwa kimechakaa, hata kama engine inaonekana nzima , kipigwe marufuku kutumika. Auze scraper ama akifanyie ukarabati na uthibitishwe na wataalam kwamba liko katika kiwango sahihi kwa matumizi ya bidamu.

Serikali isioykubali kushauriwa na kukosolewa ni mzigo mzito. MV bukoba ilivyoanza kuzama, Genji aliwaona akasema anazo boat zake mbili zisaidiane moja ivute kwa mbele nyingine ibaki nyuma ya meli ili kwa pamoja ziisogeze meli kweli maji mafupi kwa sababu ilikuwa karibu na pwani. Wenye wammlaka wakakataa msaada na ushauri huo sijui kwa ego au hofu ya nini. Wakasema wataalmu wanakuja toka Dar Es Salaam watakuja shughulikia as if kwamba kama wangeliikuta meli imezogezwa kwenye kina kifupi cha maji wasingeonyehs umahili wao.

Bahati mbaya utaalamu ukabuma. Wakatoboa meli na hiyvo kuboresha kasi ya kuzama na hivyo kuliltea taifa na hsa wananchi hasara isiyosahaulika ya kupoteza ndugu na mali kiasi kischosemekeana.

Srikali ijifunze kufahamu kwamba uongozi ni dhamana. And ukpewa uongozi haina maaan wewe una uelewa wa mambo yote kuliko watu wote unaowangoza. Kiongozi mzuri ni yulte anatumia vipaji, uwezo na kila nyenzo walizonazo anaowangoza na kila maarifa yaliyopo ili kufikia malengo yaliyokubalika. MV Bukoba, laiti mamlka ingtetambua uzalendo wa Genji, na kupima wazo lake badala ya kuangalia nani anasema kama tunavyoona leo kwa wabunge wa ccm na bunge lao vile wanafanya, wananchi wasingepoteza maisha kwanye MV. Wataalam wangetoboa na kuwatoa watu bila kuwazamisha.

Ubishi, majivuno, ego, ubinafsi, dharau, na umbumbumbu wa wenye mamlaka na mitazamo mibovu inaligharimu taifa. Kina vipaji vingi, maarifa, uwezo, elimu, utaalam na nia njema za kutisha kama zingelipewa nafasi kwa usimamizi sahihi zikatumika katika kuboresha nchi yetu, bila shaka tungelikuwa mbali na kwa kasi ya ajabu.

Ninaomba kwa hili la Mwaka huu tusikumbukie MV kwa kuweka mashada baharini ila atuwe wakweli kuchukua mafunzo kwa ajili ya maisha yetu.
 
Hivi hii siku ya kumbukumbu ya ajali ya MV Bukoba kwa sasa imeachwa chini ya usimamizi wa Flaviana Matata Foundation au bado serikali inatimiza wajibu wake ipasavyo kwenye haya maadhimisho?
 
Leo ni siku ya kumbukumbu ya kukumbuka ajali ya MV BUKOBA iliyoua wananchi takriban 800. Baada ya ajali hiyo tuliahidiwa na SERIKALI YA AWAMU YA NNE kuwa italeta meli mpya kubwa na yenye ubora kwa ajili ya usafiri wa wananchi wa Kanda ya Ziwa. Mpaka leo hatujaona hiyo meli na bado tunajiuliza HIVI TULIDANGANYWA NA SERIKALI YA AWAMU YA NNE?. Tunamwomba Mhe.Magufuli atimize ahadi yake kama alivyoahidi wakati akitafuta nafasi ya kingia Ikulu.
 
Hivi hii siku ya kumbukumbu ya ajali ya MV Bukoba kwa sasa imeachwa chini ya usimamizi wa Flaviana Matata Foundation au bado serikali inatimiza wajibu wake ipasavyo kwenye haya maadhimisho?
Haya mambo buana achana nayo, Serikali imelala doro wamemuachia Matata.
 
Siku kama ya leo miaka mingi iliyopita naikumbuka licha ya kuwa nilikuwa nasoma secondary. Lakini ilikuwa siku ngumu sana, Nakumbuka sana kwa sababu ilikuwa nchi imetoka kwenye uchaguzi mkuu wa 1995 na Mkapa kuwa Rais, nayakumbuka maneno ya watu wakisema huyu Rais ameanza kwa balaa,

Wewe unaikumbukaje siku hii? Naamini kuna wengi hawaikumbuki kabisa humu,

Namuomba Mungu awalaze mahala pema aaamin wale wote waliotangulia kwenye ajali Ile
 
Naikumbuka hii ajali. Niliisikia katika kiredio chetu kibovu nikiwa nimelala katika kitanda cha chuma ndani ya kibanda chetu kibovu cha udongo na makuti mjini Tanga. Kwa uchungu nilikuwa nao na ufukara wa kutokuwa na sehemu sahihi ya kuweka kumbukumbu, niliishia kuiandika tarehe hii kwenye ukuta wa udongo kwa kuukwaruza kwa kijiti.
Rest In Peace watanzania wenzangu wote mliotangulia.
 
...hii meli ilizama basi tu sababu ya umasikini wetu,ilikuwa inazama taratibu km tungekuwa na vifaa vya uokoaji naamini wangepona watu wengi sana.Halafu mbaya zaidi akatokea "genius" akashauri itobolewe!, yani wenyewe ndio tukaharakisha upotevu wa uhai wa watu wetu?!
...so sad indeed!
R.I.P.
....tutawakumbuka daima.
Yule mmiliki wa vivuko vya kamanga wakati ule alipinga kabisa wazo la kutoboa meli, alitaka ivutwe mpaka maji mafupi, Lakini hao magenius wetu walifosi matokeo yakawa hayo tena
 
Hivi hii siku ya kumbukumbu ya ajali ya MV Bukoba kwa sasa imeachwa chini ya usimamizi wa Flaviana Matata Foundation au bado serikali inatimiza wajibu wake ipasavyo kwenye haya maadhimisho?

Flaviana anafanya hvo sababu mama yake na baadhi ya ndugu zake walipoteza maisha kwenye meli hyo
 
Mimi najipa pole sana kwa kuwapoteza ndugu zetu na pia pole kwa Taifa letu kwa ujumla sisi kupoteza ndugu jamaa na marafiki
 
Pana bint alikuwa akisoma mwanza sasa wazazi wake wakamsindikiza vizuri mpaka meli inaondoka bint yumo kesho wake wanapata khabari za kuzama meli ikawa heka heka kuanza kufutilia baada ya siku kama nne watu wamelia na kunyamaza bint akatokea.Kumbe mambo yao ya ujana alishukia bandari ya kemondo kwa kijana mwenzie basi baada ya kujadiliana sana atokeje ikabidi wapatikane watu wazima kumpeleka kwao.
 
Binti mmoja wa Rugambwa Secondary akiitwa Shose. Alikuwa ndiyo anamaliza Form 6. O level alisoma Kilosa Secondary.
 
Back
Top Bottom