Kumbukumbu ya kuzama kwa MV Bukoba tarehe 21 May, 1996

Kumbukumbu ya kuzama kwa MV Bukoba tarehe 21 May, 1996

Katika kumbukumbu za mwaka huu, ni vizuri seriali ikaweka wazi kilichotokea badala ya kuwafumba watu n akuishia kusema Marehemu walazwe pema wakati kuna mengi ya kujifunza.

Si kwa vyombo vya majini bali kila chombo cha usafiri.

WAtu waliokufa ni wengi zaidi ya 800.

Meli ilioveload watu na mizigo kupita uwezo wake kwa hesabu isiyosemekana kana kwamba hapakuwa na wataalamu, wala chombo cha kusimamia compliance and usalama wa wateja.
Jambo hili linatokea kila sehemu hata katika mabus na daladala. Utakuta makondakta wamejaza abiria na mizigo ndani ya basi la abiria. WAsimamizi wako barabarani kuongea na wafanyakazi wa mabus pembeni na kuruhusu gari kuondoka bila kuzingatia usalama wa abiria. Ikitokea ajail iwatu wanakufa kwa kugongwa na mizigo ama kufunikwa na kushindwa kujiokoa. Matumizi ya malori ya midanani yakiwa yajeaza mizigo na abiria juu!. Pikipiki na ubebaji wa mishkakki. Bodaboda kuendeshwa bila kufuata taratibu kwa maana ya kuchomekea kulia kushoto, kati kati ili mradi anakwenda bila kujua athari zake kwa mwendeshaji na abiria wake huku wasalama wakiona kawaida.

MV Bukoba ilikuwa meli lya miaka mingi na kila wakati ilikuwa katika matengenezo including siku ya ajali. Matumizi ya vyombo vibovu katika usafirishaji ni tatizo. Hili ni pamoja na daladala, mabusi, ndege n.k. Serikali kuruhusu ununizi wa vitu vichovu bila kuwa na kiwango cha mwisho cha uchakavu. Kulipisha kodi kubwa kwa muagizaji wa chombo kibovu hakuwi mbadala wa usalama wa watumiaji wa chombo hicho. Matumizi ya magari mabaya, machovu, machkavu na yasiyofaa kwa kusarifisha abiria mijiini na vijinini ni kuvundika mauti. Utakuta gari limechunika maviti hayana mavazi, nondo zimejaa kutu, uchafu n aharufu iliyokithiriri, hadi mende, kunguni na kila aina ya ubaya lakini wasimamizi wa usafiri wanachojali awe amelipia njia na leseni, bila kuzingatia abiria wanaathirikaje. Ifike mahali chombo chochote cha kubebea watu kinapokuwa kimechakaa, hata kama engine inaonekana nzima , kipigwe marufuku kutumika. Auze scraper ama akifanyie ukarabati na uthibitishwe na wataalam kwamba liko katika kiwango sahihi kwa matumizi ya bidamu.

Serikali isioykubali kushauriwa na kukosolewa ni mzigo mzito. MV bukoba ilivyoanza kuzama, Genji aliwaona akasema anazo boat zake mbili zisaidiane moja ivute kwa mbele nyingine ibaki nyuma ya meli ili kwa pamoja ziisogeze meli kweli maji mafupi kwa sababu ilikuwa karibu na pwani. Wenye wammlaka wakakataa msaada na ushauri huo sijui kwa ego au hofu ya nini. Wakasema wataalmu wanakuja toka Dar Es Salaam watakuja shughulikia as if kwamba kama wangeliikuta meli imezogezwa kwenye kina kifupi cha maji wasingeonyehs umahili wao.

Bahati mbaya utaalamu ukabuma. Wakatoboa meli na hiyvo kuboresha kasi ya kuzama na hivyo kuliltea taifa na hsa wananchi hasara isiyosahaulika ya kupoteza ndugu na mali kiasi kischosemekeana.

Srikali ijifunze kufahamu kwamba uongozi ni dhamana. And ukpewa uongozi haina maaan wewe una uelewa wa mambo yote kuliko watu wote unaowangoza. Kiongozi mzuri ni yulte anatumia vipaji, uwezo na kila nyenzo walizonazo anaowangoza na kila maarifa yaliyopo ili kufikia malengo yaliyokubalika. MV Bukoba, laiti mamlka ingtetambua uzalendo wa Genji, na kupima wazo lake badala ya kuangalia nani anasema kama tunavyoona leo kwa wabunge wa ccm na bunge lao vile wanafanya, wananchi wasingepoteza maisha kwanye MV. Wataalam wangetoboa na kuwatoa watu bila kuwazamisha.

Ubishi, majivuno, ego, ubinafsi, dharau, na umbumbumbu wa wenye mamlaka na mitazamo mibovu inaligharimu taifa. Kina vipaji vingi, maarifa, uwezo, elimu, utaalam na nia njema za kutisha kama zingelipewa nafasi kwa usimamizi sahihi zikatumika katika kuboresha nchi yetu, bila shaka tungelikuwa mbali na kwa kasi ya ajabu.

Ninaomba kwa hili la Mwaka huu tusikumbukie MV kwa kuweka mashada baharini ila atuwe wakweli kuchukua mafunzo kwa ajili ya maisha yetu.[Umenigusa
 
Mungu azilaze pema roho za marehemu na wale waliopoteza ndugu zao Mungu awatie faraja.
Tuliobaki tukumbuke kuwa, uzembe ndio chanzo kikubwa cha ajari nyingi, na meli hiyo ilizama kwa sababu za uzembe na pengine rushwa na magendo!
Pamoja na tukio hilo baya sana, bado uzembe umeendelea kuonekana, mfano kule Zanziba tumeshuhudia ajari za meli zilizoaababishwa na uzembe ulele! Mungu atuponye Watanzania!
 
Ajali ya MV bukoba haikutoa funzo kwa mamlaka husika japo ajali haina kinga lakini ya MV spice iliozama mkondo wa Nungwi ni somo kubwa sana lililoacha maumivu ya hali ya juu hadi sasa! Udhaifu wa uokozi na utoaji taarifa mapema ni vitu ambavyo vinge kopiwa toka mv bukoba lkn ndio hivyo tena yale yale
 
Maswali magumu sana..Serikali imefanya nini kuepusha ajari za namna hii? Je imeweka kitengo cha uokozi kama ikitokea Meli ikazama ziwani jinsi ya kuokoa watu? Je Bandari za Bukoba na Kemondo zimeimalishwa kuzuia watu wasiokuwa na ticket na wazamiaji kupanda Meli?..Je MV Victoria imefanyiwa lini matengenezo makubwa ili kuokoa roho za watu zisije angamia tena?..Usafiri wa Basi toka Bukoba kuja Mwanza ila changamoto ya Kivuko inajulikana? Kuna mhindi "inasemekana" alipiga simu Mwanza kwa wenzie na kutangaza mtu atayeokoa Maisha yake atapewa Nusu ya Mali zake ndo maana Wajanja wakakikimbilia kutoboa meli ili kumuokoa ili waweze kutajirika...Je serikali iliwachukulia hatua gani hao walitoa uamuzi wa kutoboa meli na kusababisha izame kabisa!??

Wapumzike kwa Amani watu wote walitangulia mbele ya haki!!!

Duh🙁 mwaka 96 cm za mkononi zilikuwepo mkuu? Au unamaanisha cm ya namna gn?
 
Inasemekana wamerekani ndo walioizamisha ndo maana hata taarifa za kuzama Tanzania ilipewa na Marekani. Baada ya tukio hilo ndipo Alkaeda walipolipua ubalozi wa Tanzania na Kenya ikiwa ni kisasi kwa kifo cha kamanda wao. Inasemekana hata kulipuliwa kwa majengo ya Twin Towers ni muendelezo wa hiyo movie

Marekani ni mshenzi sana, ajali zote zinazotokea ktk nchi yake huwa nafurahia mno maana kapoteza innocent people wengi mno, yaani natamani vile vigorofa viwili vilivobakia pale new york vipitiwe na vibaraka wao isis or Alqaida!!
 
Wapo wanaodai ilikua kafara ya mkapa ctaki kuamin juu ya hilo
na kumbuka nilimpoteza mjomba Wang Aliamin abubakary kachwamba...mungu amulaze mahali pema peponi.. ameen

Poleni sana mkuu, na pole kwa wote waliofiwa...hakuna atayebakia wote njia moja
 
...hii meli ilizama basi tu sababu ya umasikini wetu,ilikuwa inazama taratibu km tungekuwa na vifaa vya uokoaji naamini wangepona watu wengi sana.Halafu mbaya zaidi akatokea "genius" akashauri itobolewe!, yani wenyewe ndio tukaharakisha upotevu wa uhai wa watu wetu?!
...so sad indeed!
R.I.P.

....tutawakumbuka daima.

Sio kwa sababu ya umasikini jombaa... titanic na concordia pia ni kwa sababu ya umasikini?
 
naumia sn nchi yngu,yan tumesahau kbsaaa! juz ile gari kigamboni tumehenya kweli kuitoa,seuse madudu makubwa( meli) tutaeza kuokoa watu kwa wkt? tupotupo tu.
 
Haya mambo buana achana nayo, Serikali imelala doro wamemuachia Matata.
Nae Flaviana leo katangaza kuwa mwaka huu ndiyo mwisho kujishughulisha na kumbukumbu hiyo na kuomba wadau wengine wajitokeze kuchukua kijiti chake.
 
Duh🙁 mwaka 96 cm za mkononi zilikuwepo mkuu? Au unamaanisha cm ya namna gn?
Kwa mwaka huo 1996 simu za mkononi tayari zilikuwepo na huduma zake zilikuwa zinatolewa na kampuni ya Mobitel. Kipindi hicho ni watu wachache tena wenye uwezo ndiyo waliweza kumiliki simu hizo. Binafsi kwa mkoa wa Mwanza na kwa mara ya kwanza niliona mtu ninaemfahamu akimiliki simu ya mkononi mwishoni mwa 1996. Baadae na mimi nikadunduliza na kununua ya kwangu mwanzoni mwa mwaka 1998.

Kwa kuangalia hizo facts hapo juu utaona kwamba kuna uwezekano wa huyo jamaa kuwasiliana na ndugu zake kwa simu ya mkononi akiwa ndani ya meli wakati wa ajali hiyo May 1996.
 
Namkumbuka dada Zaynab Mussa, ilikuwa akirudi likizo kutoka Rugambwa ss tunapiga nae prac za kemia kibaha sec, ile anamaliza pepa anarudi toka Bukoba anazama na mv Bukoba!dah nililia sana coz nilikuwa nampenda sana
 
Nae Flaviana leo katangaza kuwa mwaka huu ndiyo mwisho kujishughulisha na kumbukumbu hiyo na kuomba wadau wengine wajitokeze kuchukua kijiti chake.
Nimeshangaa kweli baada ya kujua ni mtu na si wizara ndio inaratibu maazimisho haya
 
0
Kama sikosei kwa mwaka huo 1996 simu za mkononi tayari zilikuwepo na zilikuwa zinatolewa na kampuni ya Mobitel. Kipindi hicho ni watu wachache tena wenye uwezo ndiyo waliweza kununua na kumiliki simu hizo. Binafsi simu ya kwanza ya mkononi kwa hapa Tanzania niiona mwanzoni mwa 1997. Baadae na mimi nikadunduliza na kununua ya kwangu mwanzoni mwa mwaka 1998.

Kwa kuangalia hizo facts hapo juu utaona kwamba kuna uwezekano wa huyo jamaa kuwasiliana na ndugu zake kwa simu ya mkononi akiwa ndani ya meli mwaka huo 1996.



Mkuu nashkuru sana nilikuwa sijui hilo,
 
Nilikuwa kwenye kumbukumbu kwana walio nusurika na hiyo ajali walikuwa wanasimulia kwa uchungu sana na tena hii ajali ilipoteza watu wengi sana wa bukoba katika marafiki wangu watano wahaya unakuta wanne hii ajali iliwagusa kama siyo baba na mama kaka ndugu wa karibu
 
Tar 21.5.1996 watanzania na watu wengine hawataisahau ikiwa walipoteza wapendwa wao kwenye ajali ya meli ya MV bukoba, je tumejifunza nini? Kuna marekebisho yoyote yanafanywa au tahadhari kuchukuliwa yasitokee maafa kama haya kwenye vyombo vyetu vya usafiri au tunangoja maafa yatokee tena ndio tuanze kujipanga?
 
Back
Top Bottom