Kumbukumbu ya kuzama kwa MV Bukoba tarehe 21 May, 1996

Kumbukumbu ya kuzama kwa MV Bukoba tarehe 21 May, 1996

Hivi majuzi niliipanda MV VICTORIA, meli pekee ya abiria iliyosalia kwa safari za Mwanza - Bukoba, aisee ni majanga! Meli hiyo ikiendelea kufanya safari zake bila kufanyiwa ukarabati wa hali ya juu, watanzania tujiandae kupokea msiba mkubwa kuzidi ule wa MV BUKOBA! Eee.. Mungu baba igutushe serikali na ikaikarabati meli hii, nayo ikaepusha janga la kupoteza roho za watanzania wengine wengi zaidi, kwani meli hii ni kubwa na inabeba abiria wengi zaidi ya ile MV BUKOBA!

Mkuu wa mkoa wa Kagera aliisimamisha safari zake takribani miezi miwili sasa imepita.
 
Hii ajali imenikumbusha usemi wa baadhi ya watu wanapogombana aliyechukia zaidi humwambia mwenzake HATA NIKIFA SITAKI UJE KUNIZIKA. Inabidi usemi huu ukome kwa sababu waweza zama baharini na wala mwili wako usionekane na huta zikwa kweli.Mungu awapumzishe kwa amani waliokufa kwa ajali hii.
 
Nakumbuka nilikuwa ndo tunamaliza mock ya form four kuna dogo form one anatuambia kuna meli imezama, watu wakaanza kumtukana atoe definition ya boat. Hiyo itakuwa boat sio meli. Nilipiga simu home kuomba nauli maza analia. It was terrible....
 
...hii meli ilizama basi tu sababu ya umasikini wetu,ilikuwa inazama taratibu km tungekuwa na vifaa vya uokoaji naamini wangepona watu wengi sana.Halafu mbaya zaidi akatokea "genius" akashauri itobolewe!, yani wenyewe ndio tukaharakisha upotevu wa uhai wa watu wetu?!
...so sad indeed!
R.I.P.
....tutawakumbuka daima.
 
Hii ni kumbukumbu nzito sana. Wakati huo 1996, nilikuwa nasoma darasa la saba Nyamagana primary school na nilikuwa nasoma darasa moja na Haji Rume, Mtoto wa captain wa meli hiyo. Alikuja mwalimu mkuu, Mr. Paskal na kwa sauti akaita...Haji, Kuja hapa Baba!!....na kumpa taarifa ya ajali. Darasa lilitahamaki kwa taarifa hizo na wakati huo kama mnajua Nyamagana primary school iko pembeni ya kilima. Wanafunzi wengi tulienda kilimani angalau kuweza kuangalia ziwani kama tunaweza iona meli hiyo kwa mbali.

Kwa muda wa week nzima maeneo ya nyamagana yalizizima na shule ilikuwa haisomeki tena....Kibaya zaidi, kulitokea report ya misiba mingi mtaani nilioishi....

Wapumzike kwa amani..
Umenikumbusha Mwalimu Paschal. Bado yupo Nyamagana?
 
Back
Top Bottom