Ivonya-Ngia
JF-Expert Member
- Jul 16, 2009
- 703
- 383
Swali hili ni kufuatia hali halisi iliyopo CCM, kama watu kama Kingunge Ngombale Mwiru na Juma Mwapachu, wameamua kuachana na CCM, Jee Nyerere angebaki?!.
Pasco
sidhani kama nyerere alikuwa na mapungufu ya kifikra kama hao watu wawili uliowataja hapo na instead nyerere angerekebisha tu hiyo hali ndani ya chama na maisha yangeendelea. ushujaa siyo kukimbia tatizo bali ni kulikabili na kulitatua kwani unaweza ukajikuta unatoka katika afadhali na kwenda katika potelea mbali.
Wanabodi,
Leo tunaadhimisha miaka 16 tangu kifo cha Baba wa Taifa, Mwalimu, Julius Kambarage Nyerere, swali langu ni kama Mwalimu Nyerere angekuwa hai hadi leo, jee angeendelea kuwepo CCM?!.
Niliwahi kupandisha uzi humu, kuelezea kama Mwalimu Nyerere angekuwa hai hadi leo, angemuunga nani mkono, mode wakaufuta huo uzi, japo mimi kama mwana jf, siruhusiwi kuingilia mamlaka ya mode kuifunga thread yoyote, ila pia tufike mahali, mwanajf yoyote ambaye ni thread starter, awe na the right to information kuwa thread yako imefutwa na kuelezwa sababu za ni kwa nini imefutwa!.
Swali hili ni kufuatia hali halisi iliyopo CCM, kama watu kama Kingunge Ngombale Mwiru na Juma Mwapachu, wameamua kuachana na CCM, Jee Nyerere angebaki?!.
Pasco
Kingunge amejidhalilisha sana, aina yake ndiyo wale Mwalimu alikuwa anawaambia wasiwe wajinga kama Lowassa.Kingunge halinganishwi na Mwalimu Nyerere. Tayari Kingunge alishanasa kwenye mtego wa mafisadi. Hata hivyo, jambo moja nalijua kuwa hakika, Edo asingethubutu kugombea urais kama mwl angelikuwepo
Mnaweweseka sana.Aliishaikataa ccm tangu akiwa hai. Naamini anaikataa hata huko aliko
Ni mwaka wa 16 tangu alipotutoka Baba wa Taifa letu Mwl. Julius Kambarage Nyerere 14/10/1999. Je ni nani atamrithi Mwl. Nyerere baada ya uchaguzi?MIAKA 16 BILA MWALIMU NANI ATAMRITHI?
· Mwalimu alichukia rushwa na kuikemea wazi wazi nani atamrithi Mwalimu?
· Mwalimu alikuwa anapenda sana kufanya kazi, alishiriki kilimo na hata ujenzi nani atamrithi Mwalimu?
· Mwalimu alichukia mafisadi na kuwapinga wazi wazi nani atamrithi Mwalimu?
· Mwalimu alikuwa kiongozi msafi nani atamrithi Mwalimu?
· Mwalimu hakuwahi kujilimbikizia mali za umma nani atamrithi Mwalimu?
· Mwalimu alikemea udini, ukabila na ukanda nani atamrithi Mwalimu?
Ikulu haimfai huyo mzeeHATUFAI
Mtu yoyote,anayeonekana anapenda sana kwenda ikulu,hata yupo tayari kununua kura kufika ikulu ni wa kukwepa kama ukomaa:Mwl 1922-1999
Aliishaikataa ccm tangu akiwa hai. Naamini anaikataa hata huko aliko[
Si kweli, ninachokumbuka ni kwamba alikataa viongozi wabovu, wasio na maadili. Na pia alikataa matendo ya ovyo yanayokwenda nje ya misingi ya uongozi, chama ni kama gari ambayo unaweza kubadili mfumo wa kutumia mafuta ukatumia gesi mzee
Aliishaikataa ccm tangu akiwa hai. Naamini anaikataa hata huko aliko
Si kweli, ninachokumbuka ni kwamba alikataa viongozi wabovu, wasio na maadili. Na pia alikataa matendo ya ovyo yanayokwenda nje ya misingi ya uongozi, chama ni kama gari ambayo unaweza kubadili mfumo wa kutumia mafuta ukatumia gesi mzee
Magufuli nyerere hamjui au Nyerere hamjui magufuli???