Kumekucha: DPP Mganga na DCI Boaz watua Ukara huko Ukerewe kuchunguza mauaji ya kisiasa

Wanakula posho za bure. Vurugu zinaazishwa na Tume ya uchaguzi.
 
Mkuu unapata wapi ujasiri wa kumwita mtu "takataka"?
unaweza kuumba hata kucha ya binadamu achilia mbali viungo vingine ?

Kama umediriki kumwita takataka ukipata upenyo wa kumdhuru huyu mtu utashindwa ?

Jaribu kuwa na utu hata kinafiki.
Tatizo lipo kwenye mstari huo wa mwisho hapo " unafiki kwangu mwiko"

Kuna mtu anaeleza mtizamo wake na kuna mtu anakurupuka tu na kumwaga sumu bila kujua madhara ya sumu anayomwaga... Huyu anastahili kushughulikiwa Mara moja kuepusha sumu kusambaa.

Hata Mungu alivyoona Kaumu Lutti wanakithirisha kuingiliana waume kwa waume na wake hawawataki aliamua kuondoa walio wema na kuteketeza wale waovu.

SISI NI WAWAKILISHI WA MUNGU
 
Kwahiyo mnamamlaka ya kuita watu wengine takataka ??

No wonder mnaua binadamu wenzenu ili mbaki madarakani
 
Futa tarime
 
Mkuu ikiwa kampeni zinafanyika Tanzania Basi tambua ni lazima serikali iwaingilie. Amani ya nchi lazima ilindwe hakuna ambaye anaweza kufanya vile anataka bila kufuata kanuni na sheria za nchi
Yaaa lazima serikal iwaingilie.
 
Huku ndio mlikoifikisha nchi?
Kwa faida gani?
Na nani anae faidika kwa haya myatendayo?

Ni wapinzani wangapi wameuawa lakini hakuna jitihada zozote zilizoonekana kufuatilia hilo?
Ni wapinzani wangapi wameshambuliwa lakini wenye dhamana yakuchunguza wamekuwa wakitoa majibu mepesi hata bila ya uchunguzi kwamba waathirika kwa namna moja ama nyingine wanahusika?
Ni mara ngapi vyombo vya dola vimesaidia wahalifu dhidi ya upinzani?

Lakini leo hii wameuawa wana ccm DCI, na DPP wameingia mtaani haraka sana kutafuta wauaji.
Je wana ccm ndio wenye haki katika nchi hii kiasi kwamba wapewe upendeleo wa wazi katika kila jambo?
Walio uawa ni binadamu na ni waTZ, lakini kwa mfumo huu utawalaumu watu wasipokuwa na simanzi pale baadhi ya watu wanapopata matatizo ikiwemo mauaji kama haya?

Kitendo cha DCI na DPP kukimbilia haraka kwenye eneo la tukio, hali yakuwa ipo wazi kabisa kuwa ni mihemko ya kisiasa kusipelekee kuwatisha ama kutowatendea haki wakazi wa maeneo husika kwa sababu tu za kisiasa.
 
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]Ile Nchi hii ingekuwa ni daladala hakika ningeshuka
 
Nyambaf! Ben saanane, tundu lissu, Alfonse mawazo, azory mbona hawachunguzi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…