KUMEKUCHA! JNHPP Kuanza kujazwa maji Disemba 15, 2022

KUMEKUCHA! JNHPP Kuanza kujazwa maji Disemba 15, 2022

Hadi sasa ujenzi wa mradi huo umefikia 77.15% ambapo hadi kufikia tarehe 15, 2022 ambayo ni siku ya kuanza kujaza maji bwawani, ujenzi unatazamiwa kufikia 80% huku uzalishaji wa umeme ukitarajiwa kuanza rasmi Aprili 2024.
hapa kuna ubabaishaji, au kuweka chumvi nyingi pasipokuwa na lazima.
Hiyo asili mia 77.15 imejengwa kwa muda gani? Hiyo iliyobakia kufikia asilimia 80 itamalizika kwenye siku kadhaa tu?
Ujenzi wa Bwawa la JNHPP ni wa teknolojia ya kisasa na uimara wake bwawa hilo litadumu kwa miaka 100 ijayo.
Mradi huu umeleta ajira nyingi sana kwa Watanzania. Mradi umeajiri watu 12,298 huku 11,190 sawa na 90.99% ni Watanzania na 1,108 sawa na asilimia 11.01% wakiwa ni raia wa kigeni.
Hizi ni porojo zilezile zilizozoeleka.
Hawa waTanzania waliajiriwa huko wamejengewa uwezo, ili kama pakitokea uhitaji wa dharura watausimamia wao bila ya kuwaita tena hao wanaojenga?
Tukitaka kujenga bwawa jingine dogo zaidi ya hili, hawa waTanzania wenzetu wataimudu kazi hiyo?
 
Kwani lile winch la Makamba lililokuwa bandarini tangia mwaka juzi lilishafika huko Rufiji kwenye hilo bwawa? Kuna aliyeliona likipelekwa huko kufunga hilo geti ili maji yaanze kujazwa?
 
Maji hayo hayo ilipaswa yajazwe mwaka Jana!

Lkn alipoingia mzee wa ten percent, kila kitu kimeharibika
Tatizo mnapenda sana kusikia maelezo ya wanasiasa...

Hebu tafakarini...

Mradi wa Rusumo ambao World Bank na African Dev Bank wali-approve pesa tangu 2014 umechukua takribani miaka 5 na bado hujawa operational.

Leo hii, JNHPP ambao ni mradi mkubwa maradufu compared na Rusumo, huku pia ukitegemea mikopo na tozo, halafu unaamini kabisa huo mradi ungekamilika mapema kuliko ule wa Rusumo ambao sio tu pesa ipo lakini pia ujenzi wake ulianza mapema kuliko JNHPP?!

Au tuchukulie hata ule mradi wa Ethiopia ambao hadi sasa installed capacity iliyofanyika ni ONLY 750MW... huu mradi umechukua miaka mingapi kumaliza just first phase?!

Tatizo mkiambiwa uhalisia wa mambo mnadhani tuna chuki na JPM, na kwenu nyinyi kumpenda JPM ni kukubali kila kilichokuwa kinasemwa na utawala wake hata kama ni uongo!!
 
Kama sikosei kuna wakati ilisemwa lingeanza kujazwa maji mwezi April mwaka huu unaoisha.

Usiwaamini wanasiasa kinachotamkwa midomoni sicho kilichopo kichwani.
It's politics, na hata hii ya sasa ni politics...

Politics is another version of saying yote hayo ni UONGO MTUPU!!

Anyway, nilipita kwenye chanzo kimoja nikakuta pamekauka balaa hadi nikaogopa!! Baada ya kudodosa, nikaambiwa maji yamezuiwa kuingia huko kwa ajili ya JNHPP.

Kama maelezo yale ni kweli, basi pia inawezekana safari hii "wakajaza" maji hapo JNHPP! Hata hivyo, itakuwa ni kujaza kwa political show na sio kwamba mradi unakaribia kukamilika!
 
Tatizo mnapenda sana kusikia maelezo ya wanasiasa...

Hebu tafakarini...

Mradi wa Rusumo ambao World Bank na African Dev Bank wali-approve pesa tangu 2014 umechukua takribani miaka 5 na bado hujawa operational.

Leo hii, JNHPP ambao ni mradi mkubwa maradufu compared na Rusumo, huku pia ukitegemea mikopo na tozo, halafu unaamini kabisa huo mradi ungekamilika mapema kuliko ule wa Rusumo ambao sio tu pesa ipo lakini pia ujenzi wake ulianza mapema kuliko JNHPP?!

Au tuchukulie hata ule mradi wa Ethiopia ambao hadi sasa installed capacity iliyofanyika ni ONLY 750MW... huu mradi umechukua miaka mingapi kumaliza just first phase?!

Tatizo mkiambiwa uhalisia wa mambo mnadhani tuna chuki na JPM, na kwenu nyinyi kumpenda JPM ni kukubali kila kilichokuwa kinasemwa na utawala wake hata kama ni uongo!!
Usituaminishe .Kila kitu ni usimamizi usiokuwa na mashaka .
 
Kama ulikuwa na shaka kuhusu ujenzi wa Bwawa la JNHPP kwamba litaanza lini kufanya kazi ya kuzalisha umeme, basi wakati wa kumaliza kabisa shaka zako umefikia tamati.

Serikali imesema kwamba kuanzia Disemba 15, 2022 itaanza kujaza maji kwenye bwawa hilon ambapo maji hayo yatajazwa hadi Aprili mwaka 2023 ili kufikia kiwango ambacho kinatosha kuzalisha umeme.

Hadi sasa ujenzi wa mradi huo umefikia 77.15% ambapo hadi kufikia tarehe 15, 2022 ambayo ni siku ya kuanza kujaza maji bwawani, ujenzi unatazamiwa kufikia 80% huku uzalishaji wa umeme ukitarajiwa kuanza rasmi Aprili 2024.

Ujenzi wa Bwawa la JNHPP ni wa teknolojia ya kisasa na uimara wake bwawa hilo litadumu kwa miaka 100 ijayo.
Mradi huu umeleta ajira nyingi sana kwa Watanzania. Mradi umeajiri watu 12,298 huku 11,190 sawa na 90.99% ni Watanzania na 1,108 sawa na asilimia 11.01% wakiwa ni raia wa kigeni.

Kubwa jingine kuhusu bwawa hili ni kwamba hata kuwe na ukame utakaodumu kwa miaka mitatu bwawa hili halito acha kuzalisha umeme kwani lina uwezo mkubwa sana wa kutunza maji.

Nimependa sana namna vile Mheshimiwa Rais Samia Suluhu alivyoweza kusimamia vizuri kabisa miradi iliyoachwa na mtangulizi wake. Mama anafanya kazi kubwa sana na kwa hili anapaswa kupewa pongezi za dhati kabisa. Hongera sana Rais Samia Suluhu.

Kama wanasema uzalishaji utaanza 2024 ongeza hapo miaka 3. Kama wanasema ujenzi umefikia 77%, gawanya kwa 2 upate ukweli wa mambo!
 
Ngoja tutunze maneno ya sifa hadi lianze kujazwa kweli. Tumeshadanganywa sana na hilo bwana

Kama umegundua kwenye bandiko kuu kuna april 2023 na april 2024 kama tarehe za kuanza kuzalisha umeme. Sijui kama ni type au makusudi!! Nami nasubiri!!
 
Anyway, nilipita kwenye chanzo kimoja nikakuta pamekauka balaa hadi nikaogopa!! Baada ya kudodosa, nikaambiwa maji yamezuiwa kuingia huko kwa ajili ya JNHPP.
Ni wapi huko bwashee? Ebu tuambie na sisi tujiridhishe! Kama maji yamezuiwa kuingia huko kwa ajili ya jnhpp wakati hata ujazaji maji jnhpp haujaanza maana yake ni kwamba hayo maji yanatiririka bure kwenda baharini. Makes no sense.
 
Ahsante mkuu! Kuna sehemu pia imeandikwa april 2023 uzalishaji unaanza! Huenda kuna makusudi ya kuweka tarahe hizi mbili.
Hizo tarehe tofauti tofauti ndio mfumo wa serikali yetu siku hizi,tusuburie tarehe nyingine hiyo April ifika.
Kama umejifunza chochote toka Mabehewa ya TRC Rais alisema tumeagiza Mtumba,Waziri kasema mapya,Msigwa kasema mapya,Kadogosa kasema mapya.
Mara ni Treni ya SGR,nara zina testiwa kwenye reli ya zamani.
Anacho kisema Waziri,msemaji na mkurugenzi huwezi kuwaamini,kila moja na lwake
 
Back
Top Bottom