Kumiliki bastola ni mzigo; ni salama zaidi ukiwa huna

Kumiliki bastola ni mzigo; ni salama zaidi ukiwa huna

dmkali

JF-Expert Member
Joined
Nov 17, 2014
Posts
11,793
Reaction score
22,552
Kuna watu wengi sana huomba ushauri wa kumiliki bastola.

Wakiamini usalama wao utaongezeka wakiwa na bastola.

Kama kuna huo ulazima wa kumiliki silaha unaothibitika, nashauri mamlaka irahisishe mchakato wa kuwapatia silaha wale watu wanaothibitisha wako mazingira hatarishi ya uvamizi, utaratibu wa muda kuwapatia silaha upunguzwe angalau ndani ya mwezi mmoja au wiki moja mtu mwenye ulazima sana apewe kibali cha kumiliki silaha kutokana na udharula wa mazingira aliyopo! (Apewe hata kibali cha dharula/temporary)

Lakini nje ya hapo silaha ni HATARI NA NI MZIGO MKUBWA SANA kuwa nao!

Ukweli ni kwamba bastola haiongezi usalama wowote bali inaongeza hatari ya usalama wako.

Kumiliki silaha ni mzigo mkubwa sana tena sana!
  • Ukiwa na silaha lazima uzingatie mavazi
  • Ukiwa na silaha muda wote kuificha (Ilinde ikulinde)
  • Ukiwa na silaha muda wote kuilinda ili adui asikupokonye
  • Ukiwa na silaha ni rahisi kujishtukia kwamba huenda kuna majambazi wanajua unayo hivyo watakuja kuipora ili wakaitumie kufanya uhalifu (ili waichukue lazima wakuue kwanza)
  • Kumiliki silaha ukipoteza au kuisahau mahali unawajibishwa kwa kosa la kutokuitunza silaha (kosa kisheria)
  • Ukiwa na silaha ni rahisi kuitumia ili kuwatisha watu (kosa). Bastola inatakiwa ukiitoa unapiga unless kimbia hapo
  • Ukiwa na silaha hutakubali kuumizwa kwa chochote hata kama ni mapenzi
  • Kama unapenda michepuko ndo kabisa hufai kumiliki silaha
  • Ukiwa na silaha ukiamka usingizini badala ya kuwaza sala unawaza bastola IPO haipo
  • Hutakiwi kugombea usafiri ukiwa na silaha
  • Ukiwa na mwenza mshenzi akijua una silaha mkigombana anaificha ili upagawe vizuri
  • Malaria ikipanda kichwani kidogo tu unajimaliza
  • Wanaotumia dawa za ukimwi siwashauri kabisa wawe na silaha.
  • Kumiliki silaha ni zaidi ya kulinda hirizi ya mganga!
Kiufupi kumiliki silaha ni mzigo mzigo mzigo mkubwa sana sishauri hata mtu atamani kumiliki silaha!

Bora umiliki Rungu kuliko bastola!

Halafu Ukiwa huna silaha mwili huwa una nguvu zaidi kuliko ukiwa na silaha! (Walegevu hubeba silaha, walio shupavu hupata silaha katika uwanja wa vita)

Mfano!
Tundu lissu angekuwa na silaha siku ile uwezekano wa kufa ungekuwa mkubwa zaidi, maana angepata ujasiri wa kutoka kujibu mapigo jambo ambalo lingerahisisha yeye kupigwa zaidi (Na ingesomeka ni mapigano)
Kukosa kwake Silaha kulimpa akili ya kumtegemea Mungu zaidi na kujificha
.

Kumiliki silaha ni sawa na kibubu cha hela chumbani ambacho muda wote roho inakereketa kutamani kukipasua hata ukisikia muuza mayai anapita nje!

Ndiyo maana asilimia kubwa ya watu wanaomiliki silaha huishia kujimaliza wenyewe, wenza au watoto wao kwa jambo dogo tu.

Sababu kubwa ni kwamba silaha inapumbaza akili kwa kuifanya uiwaze muda wote.

Uzuri wa silaha ni jeshini ambako huko silaha ni kitendea kazi namba moja! Kama una silaha ni bora kuikabidhi jeshini vinginevyo ni suala la muda tu siku utajua haujui.
 
Ukimiliki pesa wanakuja wenye siraha wanakudunda..

Ili uweke balance miliki uchawi kabla hawajaja tu steringi unakuwa ushajua kuna majambazi..😂
Uchawi ndo kiboko hata ukisahau kufunga mlango wanaambizana! Huko Mafia kuna maduka mengi hayana milango wanaweka mapazia!

Ukikuta pazia ndo kufuli, kama utaamua kuchukua bidhaa weka hela kwenye kopo
 
Utakuwa mtoto wa juzi.
Silaha kama shotgun au pistol ina stature yake na ndio maana kupewa ni kazi, na ina maadili yake!
 
Huna haki ya kujerui au kutoa roho ya mtu; kwa nini umiliki silaha?
Ni self defense mkuu, inahitaji discipline tu ndio maana umiliki wake mchakato wake ni mrefu, unaanzia kuomba serikali ya mtaa, kata, OCD, kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya, mkoa then makao makuu CAR.

Ukipitia mchakato huu bila kutumia rushwa kuvuka step ukipewa fire army licence wala haikupi mawenge.

Kwanza si lazima kuomba kumiliki pistol, kuna watu majukumu yao ni muhimu kuwa na pistol muda wote, ila kama huna ulazima unamiliki tu short gun yako inakuwa inakaa nyumbani kwa ajili ya self defense ya yeyote atakayetaka kuja kukujaribu nyumbani kwako, na ukiliza mlio siku moja tu wakishaambiana nyumba ile kuna moto hakuna wa kuja kukujaribu hata siku moja.
 
Uliyosema ni ya kweli. Binafsi hata silaha za jadi Ile jamii yangu labda kutembea some,rungu ama panga kiunoni ama kakisu umekificha ndani ya nguo. Yaani muda wote unawaza ugomvi. Ama mtu akikuchokoza kidogo tu unamjibu kunya kuwa Sasa 🐕 wewe unasemaje. Ama sema swii Kama wewe ni mwanaume.
So kiukweli silaha sio kabisa.
 
Unapinga au unaunga mkono
Tunakupinga umeandika usichokijuwa, wengine tunasubiri tarehe moja mwezi wa saba hunting season ianze tukapige bunduki maporini tulete vitoweo.

Hapa naandika haya Ammunition box yangu ina risasi 500.

Ukinivamia kichwa kichwa nyumbani hizi haziendi kupiga nyati, zitaishia mwilini mwako/mwenu.
 
Tunakupinga umeandika usichokijuwa, wengine tunasubili tarehe moja mwezi wa saba hunting season ianze tukapige bunduki maporini tulete vitoweo.

Hapa naandika haya Ammunition box yangu ina risasi 500.

Ukinivamia kichwa kichwa nyumbani hizi haziendi kupiga nyati, zitaishia mwilini mwako/mwenu.
Uzi haujawagusa nyie wawindaji na majangili!
Tunazungumzia silaha binafsi za kujilinda ni mzigo!
 
Ukiwa mtu wa showoff silaha pistol itakuendesha sana ila kama upo vizuri kichwani kumiliki ni jambo la msingi na sio gharama kama watu wanavyoaminishwa zaidi ya gharama ya kuinunua na kuilipia kila mwaka kuficha pistol sio kazi ngumu kama ulivyosema ni discipline tu.
 
Uzi haujawagusa nyie wawindaji na majangili !
Tunazungumzia silaha binafsi za kujilinda ni mzigo!
Kwani hata hizi short gun zinazoachwa nyumbani ukiwa na akili mbovu si unaweza kumuuwa mkeo? tena hawa wanawake wa sasa waliojaliwa kuchonga mdomo?

Point kubwa hapa ni discipline tu ya mtu mwenyewe.

Wajinga kama huyu hawana sifa ya kumilikishwa fire army ni zero brain, tena hii ni silaha ya serikali siyo yake.
 
Ni self defense mkuu, inahitaji discipline tu ndio maana umiliki wake mchakato wake ni mrefu, unaanzia kuomba serikali ya mtaa, kata, OCD, kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya, mkoa then makao makuu CAR.

Ukipitia mchakato huu bila kutumia rushwa kuvuka step ukipewa fire army licence wala haikupi mawenge.

Kwanza si lazima kuomba kumiliki pistol, kuna watu majukumu yao ni muhimu kuwa na pistol muda wote, ila kama huna ulazima unamiliki tu short gun yako inakuwa inakaa nyumbani kwa ajili ya self defense ya yeyote atakayetaka kuja kukujaribu nyumbani kwako, na ukiliza mlio siku moja tu wakishaambiana nyumba ile kuna moto hakuna wa kuja kukujaribu hata siku moja.
Ni muda gani utatakiwa kujeruhi au kuua? Na sheria zinasemaje, kama utaua au kujeruhi katika kujilinda?
 
Back
Top Bottom