Kumiliki bastola ni mzigo; ni salama zaidi ukiwa huna

Asilimia 90% watu wanaomiliki bastola huwa hawaitumii kama ilivyokusudiwa ...wengi wao huishia kujimaliza au kumaliza wengine kwasababu zisizo za kijambaz
Haswaa...

Nikubaliane na mtu aliesema kwamba unapokua na silaha, ni rahisi zaidi kudhurika kuliko ukiwa huna.

Miaka ya nyuma kidogo kuna ndugu yangu alikua bar usiku anapiga vyombo. Ghafla wakaingia wazee wa kazi wakaamrisha kila mtu alale chini! Ndugu yangu kwa kujua ana cha moto, na tayari ana chupa kadhaa kichwani, akakaidi ile amri na kutaka kuchomoa silaha yake. Jamaa walimmaliza pale pale halafu haoo wakaondoka zao.

Pia nakumbuka wakati niko shule ya msingi, kuna siku rafiki yetu mmoja alikuja na bastola shuleni! Akawa anatuonyesha akasema ni ya baba yake hua anaificha hapo nyumbani.

So ni kweli kuna watu wanaweza wakahitaji kua nazo, ila kwa matukio yanayoendelea nadhani majority ya watu haziwafai.
 
Kabisa
 
Kuna mtu huko wamegombania mipaka katoka na bastola kaua! Nazani sasa mnanielewa huu uzi
 
 
Mimi ninachoogopa zaidi ni mahali pa kuificha ili watoto wasiione. Ukiwa na watoto wa kiume, umri wa miaka 10 - 12 hivi, aisee labda uwe unatembea nayo. Mimi nikiwa na umri huo hakuna kitu chochote kile hapo nyumbani ambacho nilikua sijui kilipo hata kifichwe vipi😀
 
Kuna self nzuri ambayo unaweza kuwa unahifadhia
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…