Kumiliki nyumba au ardhi haviwezi kukupa utajiri bali vinalaza hela, fuatana nami ujifunze experience yangu ya umiliki wa hizi mali

Utawaponza...

Binafsi natak nimiliki Ardhi kadri itakavyowezekana..

Dsm tyr nina plot mbili, Mlandizi Mbili, Arusha nipo mbioni.. Kahama, Shinyanga moja moja..

Ardhi ina raha yake sana ukimiliki... ni heshima.
 
Sitaki nishikiwe na mtu Hela yangu. Nataka niwe nayo mwenyewe, niizungushe navyojua mimi. Kila nikiihitaji niweze kuitumia kwa wakati.
💯
Ni watu tu wanachukulia poa mitandao ya simu lakini unaweza kutunza mamilioni ya hela kwenye Mobile Money sio kwenda kusumbuana na bank kila kukicha mara ufike uambiwe mtandao upo chini mara foleni mara wakupangie kiasi cha kuchukua kana kwamba unaomba
 
Utawaponza...

Binafsi natak nimiliki Ardhi kadri itakavyowezekana..

Dsm tyr nina plot mbili, Mlandizi Mbili, Arusha nipo mbioni.. Kahama, Shinyanga moja moja..

Ardhi ina raha yake sana ukimiliki... ni heshima.
Ni jambo zuri boss ina heshima yake ni nzuri sana kwa mtu mwenye utulivu/subra nikama kupanda mti uje kula matunda huko mbeleni
Kuna watu wenye kichaa cha hela kama sisi huwa tunataka hela za moto huwa tunapata sana shida kusubiri
 
Kwa Trump, it was more of a 'preparation meets opportunity' kind of thing.

Kulikuwa na Real estate booming bussiness kipindi hicho na yeye alikuwa na capital ya kuwekeza

watu wanashindwa kuelewa kuwa business model ya real estates inategemea zaidi mwenendo wa uchumi wa nchi husika

Ndo maana sasa hivi watu wamegundua "Robert kiyasoki" na kitabu chake cha rich dad poor dad ukifata alichosema mle kuanzia chapter two imekula kwako sababu kile kitabu alifocus kwenye bussiness model za 70's to 90's na sio sasa ndo maana hata yeye kafilisika mara mbili..

Real estate ni bussiness nzuri sana ila lazima iwe ni awamu ya pili ya biashara yako tafuta biashara mama kwanza biashara ya real estate inaathiriwa sana na mwenendo wa uchumi wa nchi.. marekani miaka kadhaa nyuma watu walikuwa wanalia wengine wakasanda majengo, ofcourse kwa Afrika na uchumi wetu wa kujikimu mtu hataisanda nyumba ila mazingira ya eneo ndio yatakupangia bei ya kupangisha.. ndo maana kwa Bongo jenga uza ndio bussiness model ambayo watu wanafanya kuliko kupangisha so biashara yako ya kwanza isiwe real estate maana kupata faida kwake itabidi usubiri sana anza na biashara ingine kisha ukishasimama unaingia kwenye real estate ambapo unakuwa na malengo mawili moja kwa kupangisha pili as a collateral
 
Kabisa kaka... Ndyo mambo ambayo siyapendi hata kidogo.. Eti hela yangu mwenyewe naanza kupangiwa utaratibu wa kuipata,.. Mara kusubiri, mara hivi mara vilee
 
Hapo ndio utajua binadamu tunatofautiana pakubwa sana.
Wengine hivyo vitu vinetufanya tuone kuwa tulichelewa kuvipata.

Kwangu ardhi sintaacha kununua, nyumba sintaacha kujenga.
 
💯
 
Hapo ndio utajua binadamu tunatofautiana pakubwa sana.
Wengine hivyo vitu vinetufanya tuone kuwa tulichelewa kuvipata.

Kwangu ardhi sintaacha kununua, nyumba sintaacha kujenga.
💯
Binafsi mm ni wale watu wenye kichaa cha hela hela ya moto kabla haijapoa ndiyo maana napata tabu kusubiri ninyi mnaweza ndugu zangu na mnatoboa
 
Funzo nzuri sana hili. Thanks Mkuu. Mimi ndiyo maana hata vikundi vya vikoba huwa sichezi. Pesa napenda niwe nayo mkononi mwenyewe, niipangilie na kuizungusha mwenyewe.
Kama mimI, sijui ni ubinafsi au ni nini, lakini sijawahi kucheza hiyo michezo, wala kuwa kwenye vikundi coz najiona nakua mtumwa
Mimi mzigo nikitaka ku save naweka UTT, au nanunua asset kama ardhi n.k
 
Kuna mzee alinunua kiwanja 600,000 huko Daslamu nasikia alikiuza 370m+ sijui nilitaka kusema nini🐼
Ataje na time range kati ya mwaka alionunua hiko kiwanja mpaka mwaka anakuja kuuza
 
Utawaponza...

Binafsi natak nimiliki Ardhi kadri itakavyowezekana..

Dsm tyr nina plot mbili, Mlandizi Mbili, Arusha nipo mbioni.. Kahama, Shinyanga moja moja..

Ardhi ina raha yake sana ukimiliki... ni heshima.
Mkuu zingatia sana plot zako ziwe zina documents muhimu, Hati ya wizarani ndo kila kitu,
Hizi mambo kuandikishana kwa mwenyekiti zinatia mashaka sana, mimi nikiwa sina hati ya wizarani naona bado sijamiliki
 
Kwenye biashara ya majengo jambo muhimu zaidi ni kufahamu uchumi wa sehemu husika, hii itakusaidia kujua unatakiwa ujenge jengo lenye thamani gani

Hata jenga uza usipozingatia location inakula kwako. Mfano unaenda chamazi, kibulugwa, kongowe, kimbiji, mwasonga, mapinga ama chanika unajenga nyumba ya mil 200, ukitaka kuiuza ama kuipangisha itakupa stress

Kuna jamaa anafanya kazi posta alikuwa kapanga sinza, akaona kodi iko juu akanunua kiwanja mapinga na kujenga nyumba ya maana kwa ajili ya makazi. Akajikuta bill ya mafuta ni kubwa kuliko kodi aliyokuwa analipa sinza, hivyo akaamua kurudi sinza. Ile nyumba alikosa mpangaji hata wa laki 2 mwisho akaamua kumpa mtu aishi bure ili ailinde.
 
Well said Mkuu
Najiuliza hiyo biashara ambayo unazungusha unapata faida ambayo ni mara mbili ya mtaji sipati jibu.

Kila biashara na tija na changamoto zake:
Ardhi!
Tija ya Ardhi inategemea na factor kuu tatu, location kwa maana market value ya eneo (Kata), location kwa maana ya mtaa ardhi ilipo na locality kwa maana sehemu gani ya mtaa (je ni beach plot! corner plot! au kinagusa barabara kuu maarufu). Ukifanya maamuzi sahihi kuhusu hili umetoboa. Kibiashara, villa ya vyumba 4 iliyopo Beach Masaki/Oysterbay ina thanani kubwa mara 50 zaidi kuliko kipato cha nyumba ya aina hiyo iliyopo bunju/kimara. ujanja upo katika kununua kiwanja na siyo kujenga. Hivyo hata ujenge jengo zuri kiasi gani kama ulikosea kununua kiwanja imekula kwako. Ndio maana Ubungo plaza, Dege Beach NSSF na Kijichi NSSF projects zimekuwa feilure kubwa kibiashara. Changamoto ya ya investment kwenye ardhi ni initial investment cost ni kubwa na return ni 10 -20 yrs. tija yake ni kuwa baada ya 10-20 ambapo mwenye nyumba huwa anaonekana kula super normal profit with minimum risk and management cost.

Biashara nyinginezo!
Biashara za kuzungusha zina faida na hasara katika muda mfupi. Uzuri wa biashara ya kuzungusha unaweza kuanza na na mtaji mdogo baadaye ukapanda na kuwa mkubwa ndani ya miaka michache (initial investment cost siyo lazima iwe kubwa). Changamoto zake ni pamoja na risk inakuwa kubwa kwa kadiri unavyofanya biashara yenye super normal profit, competition inaibuka na kuua profit kila unapopata mafanikio hivyo mafanikio always ni ya muda mfupi. Hivyo suala la kupata na kukosa vina uzito unaofanana. Ili ufanikiwe kwenye biashara ni sharti kufanya maamuzi sahihi katika wakati sahihi na utekeleze mipango kwa usahihi. Kwenye maamuzi na mipango ndipo panaposababisha faida au hasara, na ndipo panapofanya baadhi wafanikiwe na wengine washindwe. Biashara pekee ambazo zina faida kubwa sawa au zaidi ya mtaji uliowekeza ni illigal business mifano kutoa rushwa ili upewe sehemu nono ya mgodi ambapo inabidi uwadhurumu wananchi na serikali, dawa za kulevya n.k

Hivyo inaweza isiwe sahihi kusema kwa ujumla kuwa biashara ya kuzungusha ni rahisi au inalipa zaidi kuliko kuwekeza kwenye ardhi. Maamuzi na mipango ndio siri ya kutoboa! hivyo tufanye utafiti kabla ya maamuzi ili tufanikiwe.

Mungu atusaidie
 
Well said mkuu
 
Ni kweli kabisa Mkuu. Mfano ni Dodoma, sasa hivi viwanja vya mjini kati havikamatiki. Hata fremu za biashara ni bei mbaya sana. Uchaguzi wa sehemu ya kuwekeza kwenye masuala ya ardhi ni muhimu sana.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…