Kumkaribisha Haji Manara Jangwani Ni Kosa Kubwa Sana!

Kumkaribisha Haji Manara Jangwani Ni Kosa Kubwa Sana!

Aliewaitaga nyani hakukosea kabisa,mpira sio maneno wala sio uhamasishaji,bado mna akili za kijamaa na kishoshalist kuamini propaganda inaweza kufanya kazi!!
Mpira ni uwekezaji,na management nzuri,duniani kote uko mpira ulipopiga hatua kuna uwekezaji mkubwa umefanyika kuanzia kwenye wataalamu wa benchi la ufundi,wachezaji wazuri,vifaa vya mazoezi,vifaa tiba,lishe,na program tofauti za kiufundi.

Suala la makelele halina tofauti na waliopigana vita ya majimaji,kuamini kwenye propaganda kuwa wanaweza kuwashinda watu wanaotumia zana zenye teknolojia ya kisasa mwisho wa siku watu wakafa kwa kuamini ujinga,au walioamini propaganda za babu wa loliondo mwisho wa siku wakatumia kikombe kisicho na utaalamu na uthibitisho wa kisayansi wakafa!!

Watu wa Yanga kwa sababu ya ulofa wao, GSM amepoka madaraka kinyemela na sasa wanaongoza timu kwa manufaa ya kibiashara ya jina lao,bila kujali utamaduni wa timu hio,kama kweli yanga wanaitaji mafanikio waache kuwekeza kwenye propaganda wawekeze kwenye utaalamu zaidi.
Umepanic mkuu,hivi ndivyo wananchi tulivyompitia manara na sasa hivi tunamvizia babra
 

Attachments

  • 240641877_941327323090701_8596545863605743341_n.mp4
    706.8 KB
Umepanic mkuu,hivi ndivyo wananchi tulivyompitia manara na sasa hivi tunamvizia babra
Akili za watanzania bwana!! Nipaniki kwa lipi? Kwangu mimi mpira ni burudani nikiwa nauangalizia uwanjani,bar,au nyumbani na familia,mimi sio mshabiki wa insta au kwenye radio za FM,mimi nafurahi tu kuona simba ilivyobadilika na kuendeshwa kisasa kwa juhudi za MO,napenda timu zote zingekuwa hivi,na CCM ingeboresha viwanja kuweza kuvutia angalau hata watu wenye kariba yetu waweze kuja viwanjani kuangalia burudani uko mikoani nafikili unaweza kunielewa.
 
Usimtusi mtu kwa sababu ana amini kitu tofauti na wewe.

Nikukumbushe tu kuwa Yondani pia alikuwa ni Reject.
Sijamtusi mtu, nimecaption alichosema, alipoulizwa kuhusu kuhamia yanga alisema over his dead body, sasa ameshahamia yanga
 
Wanajanvi.

Sina shaka na uwezo wa Haji kwenye matumizi ya kimkakati ya Kimasoko. Ila kwa kutumia jicho la tatu ninaona kama ni kosa kubwa sana kumkaribisha huyu Mwamba pale Jangwani kwa sababu ya historia yake kwenye eneo la nidhamu na weledi.

Ni kweli kuwa ametokea kwenye familia yenye vina saba na Yanga SC lakini kwa bahati mbaya amekwisha chafuka akiwa Simba SC kwa tabia zake za kinidhamu ambazo kila mwanasoka amepata kuzishuhudia.

Sijatambua ni nini klabu kama klabu imepanga kunufaika na huyu mwamba ikiwa klabu iko kwenye safari ya kuwa klabu yenye kuendeshwa kwa ueledi mkubwa.

wengi tunafurahi leo kwa kuwa inaonekana kama tumewashinda wapinzani katika hili, (Ni kweli kwasababu alikuwa mtu muhimu sana kiuhamasishaji katika klabu yao) lakini sioni jambo chanya la kiutofauti sana ambalo atalileta Jangwani zaidi ya maneno ya Taarab ambayo tulikwisha amua kujitenga nayo tangu tulipo mfukuza Jerry Muro.
Kijana tulia...
 
Akili za watanzania bwana!! Nipaniki kwa lipi? Kwangu mimi mpira ni burudani nikiwa nauangalizia uwanjani,bar,au nyumbani na familia,mimi sio mshabiki wa insta au kwenye radio za FM,mimi nafurahi tu kuona simba ilivyobadilika na kuendeshwa kisasa kwa juhudi za MO,napenda timu zote zingekuwa hivi,na CCM ingeboresha viwanja kuweza kuvutia angalau hata watu wenye kariba yetu waweze kuja viwanjani kuangalia burudani uko mikoani nafikili unaweza kunielewa.
Kisasa kivipi,ebu niambie mo uendeshaji wake una tofauti gani na manji alivyokua Yanga,imagine leo hii mo aondoke simba,mtaanzaje anzaje kuiendesha timu,bro huwajui wahindi wewe
 
kuna kingine basi zaidi ya taarab za kuwafurahisha mashabiki mzee!? ,jiandaeni na hilo kila siku mtakuwa kwenye media kukanusha kauli zake za kipuuzi .
 
Hivi unadhani Simba ni mtu? Yaani uwe na tatizo na CEO na Chairman halafu useme sina tatizo na Simba. Wakati hawa ndio madereva wa Simba
Tunaropoka tu kumponda ila raia wengi wameajiriwa na wapo kazini sababu ya kiwango cha mshahara na si mapenzi na kazi yake.
 
Siku Yanga akifungwa na Simba ndio, Haji Manara atapoitwa msaliti huko [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Haji ni mtata baada ya miaka kadhaa hata hapo Yanga atawavuruga tu,historia yake inajieleza wazi hajapata kufanya kazi mahala na akatoka salama.
Kwani aliwahi kuwa na kazi pale simba? Maana yeye anadai alikuwa ni kibarua tu,hakuwa na mkataba wowote.

Muacheni jamaa ajitafutie maisha yake, hata angesema akae tu bila kazi Ili kuonyesha mapenzi yake Simba wewe usingeweza kunisaidia chochote zaidi ya kelele tu humu mitandaoni.
 
Unafiki na uchumia tumbo
Uchimia tumbo?😂 Aiseeeh kwahiyo Haji alitakiwa kukaa bila ajira Ili kuonyesha kuwa ana mapenzi na Simba? Okay asipochumia tumbo lake wewe ungempa masaada gani zaidi ya kuandika tu huku jF?

Shida ni kwamba mlitaka mwana aadhirike Ili mpate kumzomea.
 
Mtu mwenye akili timamu anawaza hivyo. Ndio maana huwa nasema tatizo la Yanga ni uongozi wao kutotumia akili
Mbaya zaidi manara mwenyewe alishawahi wasema hivyo hivyo now wame prove alichokisema ni ukweli
 
Sitashangaa akirudi simba ila kwa sasa tuchukue kwake kile tunachoweza kuchukua
Amenyea Kambi hawezi kurudi Simba SC.

kwani kitengo chake cha kuaminisha watu Simba SC kama Real Madrid ni kupoteza muda ambao ungetumika kujiweka sawa walau kuifikia Ahly

Simba SC inaangaliza zaidi kwenda mbele.
 
.
FB_IMG_1630232080690.jpg
 
Back
Top Bottom