Uchaguzi 2020 Kumkata Paul Makonda kwenye Kura za Maoni CCM, siyo maamuzi yenye akili

Acheni siasa zenu za kishabiki na kipuuzi, jimbo lipo kwa Ndugulile miaka 10 sasa na halijapotea, sasa mnaanza kuleta ukanda na usukuma wenu humu! Kafieni mbali
 
Umenena vyema kwa upande wako, sio kosa kwake kumuambia Mhe. Rais matamanio yake pia. Kazi ya Ukuu wa Mkoa kafanya vizuri, bila shaka hata kazi ya ubunge atamsaidia zaidi na zaidi.

Wewe ni mpiga zumari wa Makonda na unaruhusiwa kuwa hivo. Lakini unaposema kazi za ukuu wa mkoa kazifanya vizuri, unafungua milango ya kuulizwa ni kazi zipi hizo.

a) watoto walioachwa na baba zao?
b) wanawake wanaopigwa na waume zao?
c) miradi ya wizara na halmashauri kusemwa na yeye?
d) kuzuia shisha na matamasha?
e) kuleta furniture za majumbani kwa jina la samani za mashule?

Ambacho hukujua muda wote huo ni kuwa Makonda ni populist na mpenda kuonekana. Na alifanya mambo yanayoweza kumfanya akaandikwa kwenye magazeti au vyombo vya habari TU!! Alitafuta kuwa maarufu!! Alionesha kuwa Rais TU ndio lolote na wengine si lolote!! Alitoa matamko yanayohusu Dar es Salaam utadhani yeye ni Rais wa nchi. Tuna bahati wakuu wa mikoa mingi hawakuiga tabia zake kama walivoshauriwa. Tungesikia mambo ya ajabu sana kama wangeamua kuiga!!

Maamuzi ya wapiga kura wa CCM yaheshimiwe. Kwa CCM jambo hili ni kipimo. Wasipoheshimu haki ya mshindi Ndugulile, hawawezi kamwe kuwa na serikali inayoheshimu haki za mwananchi yeyote. Heshima na haki huanzia nyumbani!!!!
 
Mtulia kumbuka wewe ndie ulisababisha mauaji ya Binti mrembo Acwilina, wewe ndie ulisababisha wenzako kufungwa na kulipa mamilioni ya shs! mshahara wa dhambi ni mauti na laana ile itakuandama ktk maisha yako yote.
 
Ujumbe umefika kwa Magufuli ni kuwa aliowatumbua wengi wanapendwa na wananchi, Ndungulile na Makamba ni mfano.

Gambo na Bashite wote si wasafi lakini wameamua kumbakiza Gambo.
Na nape alimtumbua, but kashinda kwa kishindo
 
Toa kabisa kwenye orodha Tundu Lisu na makanjanja wenzie!

Kitu kingine ambacho nafikiri akili yako imeshindwa kukitambua ni kwamba Tz Ina watu 60 mil... Humo tumo wengi Sana tunaofaa Mara Mia kwa hao uliowataja!

Magu ni mzee wa kuangalia nje ya box, hiyo ndio inamtofautisha Sana yeye na Marais wengine. Na hii hupelekea wengine kufikiria Kuwa hashauriki! Mungu azidi kumuongoza, kumlinda na kumbariki rais wetu mpendwa Dr. John Magufuli na nchi yetu yote!
 
Kukatwa sio tatizo sababu unapoingia uwanjani tegemea kushindwa au kushinda.Aje huku Sengerema tuvue samaki si walishasema tujiajiri.
 
Bwana mdogo mpiga debe wa Makonda, tulikuambia lakini ukashupaza shingo.
Mtoto akililia wembe mpe.
 
Kwenye maisha😂😂
 
Mimi ni muumini wa humanity,so kila mtu anayo haki ya kuishi,kuona Jamii ikiteswa,umizwa,fanyiwa uovu ni against humanity.
 
Tetea msukuma mwenzako, pinga maumivu ya wengine
 
Yaani wakipatikana vijana kama makonda kama 20hivi Tanzania itapaa juu sana kiuchumi
Hahaha,Makonda alipokuwa Mkuu wa Mkoa wa Daresalam aliamrisha watu waanze kunywa pombe saa 10 jioni,yaani Baa zianze kufunguliwa kuanzia saa 10 jioni kwa siku za kazi..

Daresalam Salam Ndi mji mkubwa wa Biashara Tanzania

Mji wenye Bandari inayotegemewa na Nchi jirani, watu kutoka nchi za jirani Kama vile Rwanda,Congo,Zambia nk,humiminika Dar kibiashara..

Kufungwa kwa Baa kumeifanya Dar kukosa sehemu za kukutania watu,kumeifanya Serikali kukosa Kodi,raia kukosa ajira,nk

Miji yote mikubwa ya Biashara kuanzia Dubai,New York, Copenhagen, London, Paris,Ni miji ambayo watu hawalali,iko busy 24hr..

Binafsi amri Ile ya kufungua Baa saan10 jioni nimeona kuwa Makonda hana uwelewa wa anachokifanya,alikurupuka
 
Labda mleta uzi huu asichoelewa ni kuwa kilichomtokea Makonda ni msaada mkubwa sana kwa Mhe. Rais. Watanzania wanajua kuwa sakata la majina na vyeti vya Makonda halikwisha na kwa kweli sasa ndio ulikuwa wakati mzuri wa kulifikisha mwisho kwani kugombea kwake na hata kama angeshinda suala hilo lingepelekwa tume na tume ikileta figisu lingefika mahakamani kupinga ushindi wake. Mhe Rais amepata fursa ya kutupa nyama chini ili kuachana na nzi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Huyo unaempigia debe sidhani kama anania ya kusaidia raia ...mkuu wa mkoa ana nafasi kubwa sana ya kutumikia raia wake kuliko mbunge ...huwezi acha ukuu wa mkoa ukachukue fom ya ubunge kama kweli unania ya kutumikia raia,,

Nkujuze tu

Mkuu wa mkoa ana mshahara mkubwa kuliko mbunge

Huo ni mshahara

Mbunge ana posho kubwa kuliko mkuu wa mkoa

Kikao unajua kabisa ni 240k per day kwa muda bunge litakavokuepo

Plus posho ya milion 8 pesa ya kujikimu je

Haya ukistaafu yan ile miaka 5 ikiisha una kama 240mil kama asante😁😁 hivi huoni kama anafata hilo swala??

Maana kutumikia raia kama unataka basi ukuu wa mkoa ndo unaweza kwa asilimia 100
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…