Kumuelewa vyema Hayati Mwalimu Julius Nyerere upeo uwe mkubwa

Kumuelewa vyema Hayati Mwalimu Julius Nyerere upeo uwe mkubwa

Phillipo Bukililo

JF-Expert Member
Joined
Dec 29, 2015
Posts
18,487
Reaction score
13,611
Julius Kambarage Nyerere nilimuona mara nyingi akihutubia pale ikulu Dar miaka ile ya 1980 mwanzoni. Alijaliwa ushawishi katika hoja zake. Siku moja alihutubia kwa muda mrefu kidogo halafu ndege ikawa inakatiza juu angani, akasema Mungu ameileta ile ndege ili mimi nimalize kuhutubia!, wote tukaangua vicheko.
Akijiamini sana katika uwezo wake wa kujenga hoja na wa kumsikiliza mtoa hoja na kuja na majibu yenye mantiki ya kina.

Mwalimu Nyerere aliipenda mno Tanzania na alijaliwa pia uwezo wa maono aliouchanga na kazi ya kuongoza nchi nchanga kama yetu. Yapo maneno ya mwisho aliyosema pale uwanja wa ndege mwaka 1999 akiwa njiani kwenda London kutibiwa saratani na huko mauti yakamkuta, alisema kuwa hata akifa ataendelea kuiombea nchi hii!.

Mwalimu Nyerere alisema Uhuru wetu hautakuwa na maana kama majirani zetu wa kusini wanaendelea kuteseka. Haikuwa ajabu tukawa mstari wa mbele katika kupigania haki za kisiasa na kiuchumi za mataifa mengi ya kusini mwa afrika. Nazikumbuka ofisi za FRELIMO zilizokuwa pale mtaa wa Ohio zinatazamana na ubalozi wa Misri na pembeni kuna ubalozi wa Msumbiji.

Miaka ile mahali pale palikuwa na watu wanaingia na kutoka muda mwingi wa siku za kazi, na nje kulikuwa na ulinzi wa askari wa FFU. Palikuwa ndio ofisi zenye kutambulisha mapambano ya kidugu ya kuikomboa sehemu kubwa ya kusini mwa afrika.

Wapo wabunge wenye kuongea maneno ya kejeli wanapouongelea mchango wa Tanzania wa ukombozi wa kusini mwa afrika, wanasema ni hulka yake binafsi ya kupenda sifa iliyotupeleka huko na kujikuta tukitumia pesa nyingi ambazo zingeweza kutumika katika kuleta maendeleo ya Tanzania.

Kwamba Nyerere alipenda zaidi sifa za kimataifa na akaona ni kawaida tu kupeleka maaskari huko kusini mwa afrika, ni maneno yanayotoka vinywani mwa wabunge wanaowakilisha nchi hii haswa wanapokosa majibu ya maswali mengi wanayoulizwa na wapiga kura wao huko majimboni.

Hii Njaa iliyoipiga Malawi na kusababisha matatizo na umaskini wa ghafla kwa kiasi kikubwa msaada umetoka kwetu Tanzania. Na hawa Wamalawi ni Wanyasa ambao baadhi yao walifikia hatua ya kuwa sehemu ya serikali ya awamu ya kwanza.

Hii mipaka iliyowekwa na wakoloni ipo kwa maslahi yao kwanza na sio maslahi ya afrika. Waliichora wakiwa na malengo yao ya kufaidika na utajiri wa chini ya ardhi kuliko kuangalia itaathiri vipi ustawi wa jamii zinazotenganishwa na mipaka yenyewe.

Mwenda yupo Tanzania, yupo Malawi na yupo Zambia. Tambwe yupo Tabora na yupo DRC. Niyonzima yupo Ngara na yupo Rwanda. Hivyo kuamua kuwasaidia kijeshi yale mataifa ya kusini mwa afrika hakuna tofauti yoyote ile na kuamua kupeleka maelfu ya magunia ya mahindi kwa watu wale wale.

Nyerere aliiona afrika hii ya leo ikiwa katika vita nzito ya kujitambulisha kama sehemu tajiri na yenye kitu cha maana cha kuchangia, miaka ile akiwa pale Magogoni Ikulu. Kuliko wanasiasa wa kisasa wanavyoiona afrika na kushindwa kutambua maana ya uwepo wa ndugu halisi wanaotenganishwa na mipaka iliyowekwa kimaslahi tena miaka 139 iliyopita kule Ujerumani.

Endelea kulala mahali pema peponi Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere, maono yako yataendelea kuishi daima kwa wale wenye kupenda kufikiria kwa kina.
 
Sometimes it needs to be smart or intelligent enough to understand the smart or the intelligent person.

Hata Galileo hakuelewaka kwa watawala wa kirumi wakati ule kuhusu nadharia zake kwa dunia ndio inalizunguka jua na sio jua ndio inalizunguka dunia kwasababu alikuwa ni intelligent mno kuelewaka wakati ule mpaka ilipokuja kuthibitika kisayansi alikuwa sahihi.
 
Alikiri mwenyewe kwamba kwa KATIBA hii ukipata Rais wa Tanzania asiye na maono, asiye na hofu ya Mungu basi itakuwa ni hatari, lakini cha ajabu yeye akaondoka madarakani na kutuachia zigo hili watanzania ambalo kweli bado linatutesa.

Rais gani aamue kubadili katiba? kila mmoja anaingia na kutoka na kujitua zigo la lawama na suala la Muugano wetu huu ndiyo linaongeza ugumu wenyewe. Baba bora ni yule anayefikiri kama hatakuwepo Duniani kesho yake je mfumo gani familia yake watautumia ili waishi maisha bora, na mfumo huo ni lazima uanze kufanya kazi kabla hajaaga Dunia.

Kwa mengine - yes aliipenda Tanzania sana.
 
Julius Kambarage Nyerere nilimuona mara nyingi akihutubia pale ikulu Dar miaka ile ya 1980 mwanzoni. Alijaliwa ushawishi katika hoja zake. Siku moja alihutubia kwa muda mrefu kidogo halafu ndege ikawa inakatiza juu angani, akasema Mungu ameileta ile ndege ili mimi nimalize kuhutubia!, wote tukaangua vicheko.
Akijiamini sana katika uwezo wake wa kujenga hoja na wa kumsikiliza mtoa hoja na kuja na majibu yenye mantiki ya kina.

Mwalimu Nyerere aliipenda mno Tanzania na alijaliwa pia uwezo wa maono aliouchanga na kazi ya kuongoza nchi nchanga kama yetu. Yapo maneno ya mwisho aliyosema pale uwanja wa ndege mwaka 1999 akiwa njiani kwenda London kutibiwa saratani na huko mauti yakamkuta, alisema kuwa hata akifa ataendelea kuiombea nchi hii!.

Mwalimu Nyerere alisema Uhuru wetu hautakuwa na maana kama majirani zetu wa kusini wanaendelea kuteseka. Haikuwa ajabu tukawa mstari wa mbele katika kupigania haki za kisiasa na kiuchumi za mataifa mengi ya kusini mwa afrika. Nazikumbuka ofisi za FRELIMO zilizokuwa pale mtaa wa Ohio zinatazamana na ubalozi wa Misri na pembeni kuna ubalozi wa Msumbiji.

Miaka ile mahali pale palikuwa na watu wanaingia na kutoka muda mwingi wa siku za kazi, na nje kulikuwa na ulinzi wa askari wa FFU. Palikuwa ndio ofisi zenye kutambulisha mapambano ya kidugu ya kuikomboa sehemu kubwa ya kusini mwa afrika.

Wapo wabunge wenye kuongea maneno ya kejeli wanapouongelea mchango wa Tanzania wa ukombozi wa kusini mwa afrika, wanasema ni hulka yake binafsi ya kupenda sifa iliyotupeleka huko na kujikuta tukitumia pesa nyingi ambazo zingeweza kutumika katika kuleta maendeleo ya Tanzania.

Kwamba Nyerere alipenda zaidi sifa za kimataifa na akaona ni kawaida tu kupeleka maaskari huko kusini mwa afrika, ni maneno yanayotoka vinywani mwa wabunge wanaowakilisha nchi hii haswa wanapokosa majibu ya maswali mengi wanayoulizwa na wapiga kura wao huko majimboni.

Hii Njaa iliyoipiga Malawi na kusababisha matatizo na umaskini wa ghafla kwa kiasi kikubwa msaada umetoka kwetu Tanzania. Na hawa Wamalawi ni Wanyasa ambao baadhi yao walifikia hatua ya kuwa sehemu ya serikali ya awamu ya kwanza.

Hii mipaka iliyowekwa na wakoloni ipo kwa maslahi yao kwanza na sio maslahi ya afrika. Waliichora wakiwa na malengo yao ya kufaidika na utajiri wa chini ya ardhi kuliko kuangalia itaathiri vipi ustawi wa jamii zinazotenganishwa na mipaka yenyewe.

Mwenda yupo Tanzania, yupo Malawi na yupo Zambia. Tambwe yupo Tabora na yupo DRC. Niyonzima yupo Ngara na yupo Rwanda. Hivyo kuamua kuwasaidia kijeshi yale mataifa ya kusini mwa afrika hakuna tofauti yoyote ile na kuamua kupeleka maelfu ya magunia ya mahindi kwa watu wale wale.

Nyerere aliiona afrika hii ya leo ikiwa katika vita nzito ya kujitambulisha kama sehemu tajiri na yenye kitu cha maana cha kuchangia, miaka ile akiwa pale Magogoni Ikulu. Kuliko wanasiasa wa kisasa wanavyoiona afrika na kushindwa kutambua maana ya uwepo wa ndugu halisi wanaotenganishwa na mipaka iliyowekwa kimaslahi tena miaka 139 iliyopita kule Ujerumani.

Endelea kulala mahali pema peponi Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere, maono yako yataendelea kuishi daima kwa wale wenye kupenda kufikiria kwa kina.
Nyerere alijitaidi sana ila huwa nawaza, alikuwa hawezi kufanya vizuri zaidi ya hapo!?
Naona kuna vingi alicha haviko sawa
 
Na moja ya jambo kubwa linaloidumaza Africa na watu wake ni UBINAFSI. Waasisi wetu wengi waliukwepa sana, ndio uliowasaidia kuijenga Africa pamoja na kwamba hatukua tumeelimika vya kutosha. Leo viongozi wamejaa UBINAFSI na uroho uliopitiliza,unakuta mtu mmoja ana hodhi ardhi akali 1000 zimekaa bila kutumika,majumba kila mikoa,pesa zimefichwa nje ya nchi. Huku raia kila siku maisha yanazidi kupanda kila leo,hakuna mpango bora wa kuwasaidia kujikwamua kiuchumi,zaidi ya kuonyeshwa kwenye makaratasi eti uchumi umepanda.

Bado tunasafari ndefu mbele,Tu watumwa(hatuko huru) zaidi ya mwanzo.
 
Julius Kambarage Nyerere nilimuona mara nyingi akihutubia pale ikulu Dar miaka ile ya 1980 mwanzoni. Alijaliwa ushawishi katika hoja zake. Siku moja alihutubia kwa muda mrefu kidogo halafu ndege ikawa inakatiza juu angani, akasema Mungu ameileta ile ndege ili mimi nimalize kuhutubia!, wote tukaangua vicheko.
Akijiamini sana katika uwezo wake wa kujenga hoja na wa kumsikiliza mtoa hoja na kuja na majibu yenye mantiki ya kina.
Mwalimu Nyerere hajawahi kuhutubia taifa akitokea Ikulu!, alikuwa anaenda uwanja wa Taifa au mahali fulani ila sio kutokea Ikulu.
Endelea kulala mahali pema peponi Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere, maono yako yataendelea kuishi daima kwa wale wenye kupenda kufikiria kwa kina.
Naunga mkono hoja
P
 
Nyerere alijitaidi sana ila huwa nawaza, alikuwa hawezi kufanya vizuri zaidi ya hapo!?
Naona kuna vingi alicha haviko sawa
Hakuwa na msaada kama marais waliomfuatia. Alikuwa na kazi ya kujenga msingi wa nyumba hawa wengine kazi yao ni kupaka rangi na kubadilisha mabati na vioo kurekebisha mabomba ya vyooni yasivuje.

Hakuwa na hazina ya wasomi waliokuja baadae, alitumia nguvu kubwa kuhakikisha hawa kina Mfugale na mainjinia wengine wanasoma bure ili waje kuilipia elimu yao kwa ufanisi wa kazi.
 
Hakuwa na msaada kama marais waliomfuatia. Alikuwa na kazi ya kujenga msingi wa nyumba hawa wengine kazi yao ni kupaka rangi na kubadilisha mabati na vioo kurekebisha mabomba ya vyooni yasivuje.

Hakuwa na hazina ya wasomi waliokuja baadae, alitumia nguvu kubwa kuhakikisha hawa kina Mfugale na mainjinia wengine wanasoma bure ili waje kuilipia elimu yao kwa ufanisi wa kazi.
Ukweli Nyerere alifeli siasa zake na uchumi hata alipoondoka hakukuwa na msingi imara aliouacha tofauti kabisa na wenzake kina Mao, Lenin au Fidel japo alionekana kuwa na nia njema
 
Mwalimu Nyerere hajawahi kuhutubia taifa akitokea Ikulu!, alikuwa anaenda uwanja wa Taifa au mahali fulani ila sio kutokea Ikulu.

Naunga mkono hoja
P
Mkuu Nyerere ni moja ya watu wa kulaumiwa kabisa kama sio yeye pengine tungekuwa na shirikisho la umoja wa Africa kama nkwame nkruma na Gadafi walivyopendekeza badala yake yeye akata block kwanza kwa maana jumuiya za kikanda,
Kama unachochote cha kusema hapo mkuu Pascal naomba mchango wako
 
Alikiri mwenyewe kwamba kwa KATIBA hii ukipata Rais wa Tanzania asiye na maono, asiye na hofu ya Mungu basi itakuwa ni hatari, lakini cha ajabu yeye akaondoka madarakani na kutuachia zigo hili watanzania ambalo kweli bado linatutesa.

Rais gani aamue kubadili katiba? kila mmoja anaingia na kutoka na kujitua zigo la lawama na suala la Muugano wetu huu ndiyo linaongeza ugumu wenyewe. Baba bora ni yule anayefikiri kama hatakuwepo Duniani kesho yake je mfumo gani familia yake watautumia ili waishi maisha bora, na mfumo huo ni lazima uanze kufanya kazi kabla hajaaga Dunia.

Kwa mengine - yes aliipenda Tanzania sana.
Nakataaa nyerere ni mzandiki na mbaguzi aside na huruma! Mkatilina muuaji
 
Mkuu Nyerere ni moja ya watu wa kulaumiwa kabisa kama sio yeye pengine tungekuwa na shirikisho la umoja wa Africa kama nkwame kruma na Gadafi wakivyopendekeza badala yake yeye akata block kwanza kwa maana jumuiya za kikanda,
Kama unachochote cha kusema hapo mkuu Pascal naomba mchango wako
Kabisa! Anapaswa kulaumiwa na kumpiga vita yeye ndio chanzo cha katiba hii mbovu! Hapaswi kuwa shujaa wa hili Taifa
 
Julius Kambarage Nyerere nilimuona mara nyingi akihutubia pale ikulu Dar miaka ile ya 1980 mwanzoni. Alijaliwa ushawishi katika hoja zake. Siku moja alihutubia kwa muda mrefu kidogo halafu ndege ikawa inakatiza juu angani, akasema Mungu ameileta ile ndege ili mimi nimalize kuhutubia!, wote tukaangua vicheko.
Akijiamini sana katika uwezo wake wa kujenga hoja na wa kumsikiliza mtoa hoja na kuja na majibu yenye mantiki ya kina.

Mwalimu Nyerere aliipenda mno Tanzania na alijaliwa pia uwezo wa maono aliouchanga na kazi ya kuongoza nchi nchanga kama yetu. Yapo maneno ya mwisho aliyosema pale uwanja wa ndege mwaka 1999 akiwa njiani kwenda London kutibiwa saratani na huko mauti yakamkuta, alisema kuwa hata akifa ataendelea kuiombea nchi hii!.

Mwalimu Nyerere alisema Uhuru wetu hautakuwa na maana kama majirani zetu wa kusini wanaendelea kuteseka. Haikuwa ajabu tukawa mstari wa mbele katika kupigania haki za kisiasa na kiuchumi za mataifa mengi ya kusini mwa afrika. Nazikumbuka ofisi za FRELIMO zilizokuwa pale mtaa wa Ohio zinatazamana na ubalozi wa Misri na pembeni kuna ubalozi wa Msumbiji.

Miaka ile mahali pale palikuwa na watu wanaingia na kutoka muda mwingi wa siku za kazi, na nje kulikuwa na ulinzi wa askari wa FFU. Palikuwa ndio ofisi zenye kutambulisha mapambano ya kidugu ya kuikomboa sehemu kubwa ya kusini mwa afrika.

Wapo wabunge wenye kuongea maneno ya kejeli wanapouongelea mchango wa Tanzania wa ukombozi wa kusini mwa afrika, wanasema ni hulka yake binafsi ya kupenda sifa iliyotupeleka huko na kujikuta tukitumia pesa nyingi ambazo zingeweza kutumika katika kuleta maendeleo ya Tanzania.

Kwamba Nyerere alipenda zaidi sifa za kimataifa na akaona ni kawaida tu kupeleka maaskari huko kusini mwa afrika, ni maneno yanayotoka vinywani mwa wabunge wanaowakilisha nchi hii haswa wanapokosa majibu ya maswali mengi wanayoulizwa na wapiga kura wao huko majimboni.

Hii Njaa iliyoipiga Malawi na kusababisha matatizo na umaskini wa ghafla kwa kiasi kikubwa msaada umetoka kwetu Tanzania. Na hawa Wamalawi ni Wanyasa ambao baadhi yao walifikia hatua ya kuwa sehemu ya serikali ya awamu ya kwanza.

Hii mipaka iliyowekwa na wakoloni ipo kwa maslahi yao kwanza na sio maslahi ya afrika. Waliichora wakiwa na malengo yao ya kufaidika na utajiri wa chini ya ardhi kuliko kuangalia itaathiri vipi ustawi wa jamii zinazotenganishwa na mipaka yenyewe.

Mwenda yupo Tanzania, yupo Malawi na yupo Zambia. Tambwe yupo Tabora na yupo DRC. Niyonzima yupo Ngara na yupo Rwanda. Hivyo kuamua kuwasaidia kijeshi yale mataifa ya kusini mwa afrika hakuna tofauti yoyote ile na kuamua kupeleka maelfu ya magunia ya mahindi kwa watu wale wale.

Nyerere aliiona afrika hii ya leo ikiwa katika vita nzito ya kujitambulisha kama sehemu tajiri na yenye kitu cha maana cha kuchangia, miaka ile akiwa pale Magogoni Ikulu. Kuliko wanasiasa wa kisasa wanavyoiona afrika na kushindwa kutambua maana ya uwepo wa ndugu halisi wanaotenganishwa na mipaka iliyowekwa kimaslahi tena miaka 139 iliyopita kule Ujerumani.

Endelea kulala mahali pema peponi Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere, maono yako yataendelea kuishi daima kwa wale wenye kupenda kufikiria kwa kina.
Chanzo na mizizi ya umasikini na matatixo ya Tz mpaka leo kwa 80% yali asisiwa na Nyerere, mpaka leo hatuja recover economic depression ya vita ya kagera ya miaka ya 1978/9 madhara ha hiyo vita yalikua makubwa kuliko mafanikio na Nyerere ndo alikua architecture wa hiyo vita, kwa sabb zake binafsi eti kumkomboa rafiki yake Obote, kabla ya Uhuru na siasa za ujamaa Tz alikua bora kuliko Kenya na Zimbabwe, Nyerere kavuruga kila kitu kwa kutafuta umaarufu wake binafsi.
 
Ibaki kusema tusifukue makaburi, bali tusafishe mashamba, tuyalime na tuwapatie vijana kwa mujibu wa Bashe.
 
Back
Top Bottom