Kumuenzi Baba wa Taifa: CCM, Serikali, Viongozi na Watanzania kwa Ujumla. Je, tunamuenzi kwa Mawazo, Maneno na kwa Vitendo? Tunamuishi?

Kwakweli wakulima na wafanyakazi kwasasa jambo lao ni kupiga kura na mara moja moja kupokea takrima kutoka kwa wenye chama.

Ndio maana baadhi ya viongozi wa CCM hawaoni haya kusema "CCM ina wenyewe" na wenyewe ndio wao!

Mwalimu amefariki, hata kumpa heshima siku ya kumbukumbu yake watu wanaona ni shida, kila mwaka inaunganishwa na shughuli za kuzima mwenge na maadhimisho ya siku ya vijana.

Watawezaje kumuishi mwalimu??
 
Mkuu ile sadaka yako ya fomu kwa CCM mpaka leo hii ina kuuma! Ila naamini unge pata nafasi usinge andika haya hapa.

Katika uhai wake Mwalimu alichukia malaya malaya wa kisiasa jitahidi mkuu ujiepushe na kundi la malaya wa kisiasa.
 
Walamba asali hawawezi kumuenzi Nyerere hata siku moja ndo maana hata siku yake wanaichakachua na kuipachika majina lukuki, mara siku ya kilele cha mwenge, mara siku ya vijana, maana hawana huo ujasiri wa kumuenzi, nafsi zinawasuta kwa uharamia wanaowafanyia watanzania kinyume na falsafa ya mwalimu.​
 
CCM ya sasa ni tofauti na ya zamani;
Viongozi wanajijengea kuwa 'miungu watu'
Rushwa imekuwa sehemu ya kazi kwao!
Wamekosa hata ujasiri wa kumtaja Mwalimu Nyerere kwani NAFSI zinawasuta!
 
Kuyaishi mawazo ya mwalimu Nyerere kunahitaji kujitoa mhanga.
Maana kuna mahali maneno yanakata huku na huku.
Viongozi wengi wanachukua yale yanayopuliza ila yanayouma wanayakwepa kidogo.

Mfano suala la udini, ukabila na ukanda, kwenye hii nchi viongozi wengi wameshindwa kulisimamia na hata kulikemea. Na kwa sasa ndio linazidi kukita mizizi
 
Paskali bana, miaka hii kweli bado unasisitiza watu waishi kwa falsafa za Nyerere?! Kizazi kilichoamini falsafa za Nyerere kilishapita na waliobaki wako ukingoni. Zungumzia ajira ili watu wajikwamue na sio hizo falsafa za karne iliyopita.
 
Paskali bana, miaka hii kweli bado unasisitiza watu waishi kwa falsafa za Nyerere?! Kizazi kilichoamini falsafa za Nyerere kilishapita na waliobaki wako ukingoni. Zungumzia ajira ili watu wajikwamue na sio hizo falsafa za karne iliyopita.
Falsafa za Nyerere zitakufa kwa mafisadi na walamba asali tu siyo kwa watu wanaoamini katika kujenga misingi ya utu, uadilifu, umoja, kujitegemea, maendeleo ya wananchi kiujumla, uwajibikaji........huwezi kutegemea ajira za vijana kutoka kwenye uongozi unaoamini katika kulamba asali na kula kwa urefu wa kamba, na hapo ndo falsafa za Nyerere zinapotamalaki.
 
Welldone Adv.Mayala, moja ya mada yako Safi kabisa, yes President Nyerere (rip)ni ICON wetu na tujivunie, binafsi nimesaidiwa mno na Botswana army (nilipata matatizo karibu na barracks yao)baada ya mazungumzo mazuri ikiwa ni pamoja na mimi to drop name...Nyerere!!
 
Zidumu fikra za mwenyekitu. Huna kitu wewe ni zezeta tu kwa akili hizi ambazo CCM wanatufundisha.
Hamna kiongozi hata mmoja anatamani awaache watoto wake kama Mwalimu alivyoacha wanawe.

CCM ya leo hapendwi mtu lapendwa pochi
 

Ni kweli, lakini falsafa za karne iliyopita kwenye kizazi hiki boss? Au mmeishiwa na hoja ndio mnakuja na hizi story za zama damu?
 

Katika kumuishi Baba wa Taifa, viongozi wetu kubalini kukosolewa, Mwalimu alikosoa kupitia Tujisahihishe, Uongozi Wetu na Hatma ya Tanzania, na kitabu cha Nyufa.
Dr. Bashiru ametumia haki yake na uhuru wake freedom of expression kufanya ukosoaji, asibezwe, asitukanwe, asidhihakiwe, asiadhibiwe, bali aheshimiwe na nashauri apelekwe ubalozini kama Polepole!.
P
 
Hii ilikuwa makala utangulizi, makala mwendelezo ni hii Tumuenzi Vipi Baba wa Taifa?, Kwa Mawazo na Maneno tu, Au Kwa Matendo? Wito Kwa Viongozi Wetu, Muenzini Mwalimu kwa Kumuishi na Sio kwa Blah Blah! nimeisha muomba mode aziunganishe.
P
 
Tumuenzi Mwalimu Nyerere kwa matendo na kumuishi na sio kwa maneno tuu!.
Happy Nyerere Day!.
P
 
Kumuenzi Nyerere ni kuhakikisha tunaishi kwa Amani na mshikamano.
Ila pia ni kufuta ujinga zake zote
1. Kufuta mbio za mwenge
2. Kufuta ujamaa ambao Nyerere aliusoma na hakuuelewa.
3. Kufuta Kiswahili kuwa lugha ya kufundishia Ili kuifungua nchi
4. Kufuta udini kwenye ajira za serikali ambao yeye ndio muasisi
5. Kufuta katiba yake ya hovyo inayodidimiza raia
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…