Kumwambia mwanamke 'FANYA MAARIFA'

Kumwambia mwanamke 'FANYA MAARIFA'

Inategemea kua hio shida ni of what nature.... Kuna ile kama inahusiana na chakula ndani, anaona tu aibu kusema nenda angalau kwa wazazi kaombe unga kidogo tumekwama... anaona bora akwambie kua "fanya maarifa"..... Kawaida ya mwanamke ambae ni mwerevu (walau that is what I think) ni kutambua kua sio kila siku mume wake ataweza provide - na kwamba hata kama anaweza inaweza tokea in rare cases akakwama. Daima kulinda heshima ndani ya ndoa yenu inatakiwa kua na akili ya ziada mkichwa na maarifa pia....

Hivo basi daima hata kama woote wanafanya kazi na woote wana provide, ni lazima aweke akiba pembeni popote pale ndani ya nyumba ambayo inakua ni kinga ya kutatua tatizo pale ambapo litajitokeza na woote wasiwe na pesa (yaani mume na yeye mwenyewe mke); Hio akiba sio wanaume woote hujua kua inakuwepo.... Inapotokea kua kuna siku mlikwama kabisa mara nyingi akina mama huchukua hio akiba kuokoa jahazi kwa kumshirikisha mumeo na kumwambia "mume wangu nimeazima kwenye kikundi chetu kile cha upaku" sababu ya kusema hivi sio kwamba humuamini mumeo.... No! Ila tu ni ile haitakiwi hajenge kichwani mwake kuna akiba ndani for next time akikwama he wont try harder..... Hivo baas mara nyingi wanaume husema hivo sababu wanakua weshawahi pita in jams na mke aliokoa jahazi.... Siamini kua hua wanasema hivo kwa maana kwamba nenda kwa mpango wa kando ukatafute pesa.


Boss it has been Long.... Usiku mwema.

Ashadii hapa umemaliza kila kitu kabisa. Tatizo la the Boss anafikiria mpango wa kando lol. Afu wa mama huwa tunakuwa concern na kesho itakuwaje. Baadhi ya wababa akijua una haka ka akiba mbona atakubananisha umpe akalambe maji ya gold apunguze stress afu hyo kesho itajijua huko huko.
 
mimi sidhani mme akitamka fanya maarifa mke wangu anamaanisha awe na hicho mnaita kibuzi. kumbuka akiri ni nywele kila mmoja anazake, mwanamme anaweza kuwaza hadi mwisho bila kupata jawabu la kutatua matatizo katika familia yake na kwakuwa mke wake ndiyo msaidizi wake wa karibu ndiyo huhitimisha kwa kuomba msaada kwa mkewe namna watakavyo tatua matatizo yao. Kwa mke mvivu wa kufikiri na kufanya kazi atawaza kuwa na hicho kiitwacho kibuzi bali kwa yule mkakamavu, mjanja atafikiria pakutokea, yawezekana mmewe aliwaza kukaanga, kufunga na kuuza karanga rakini akaona aibu lakini kwa mke makini hilo si tatizo.
 
Mwanamme anafikiri,anatafuta,anahenya,anateseka ili familia yake ipate kuishi (namzungumzia mtu wa aina hiyo)..Inafikia nyakati kila anachkifanya kinagonga mwamba,mambo si kama yalivyokuwa awali.....Kwa kiswahili cha kisiasa inabidi kufunga mkanda..tuingie kwenye dharula ya muda.

Mambo yasiyo ya kawaida katika familia kama kunywa chai,kununua nguo mpya,kutumia mafuta mengi kwenye mboga,viungo visivyo vya lazima kama pilipili hoho vyote vinasitishwa..Mwendo unakuwa ni wa kula ili kuishi.Na ni nani waziri wa jiko na mambo ya dharula ? - Ni mwanamke..ndipo mwanaume anatoa wito..fanya maarifa - yaani tumia kila kilichopo kwa akili.

:A S-confused1:EDUCATION IS HOW CONFIDENT YOU ARE IN MAKING DECISION
 
Inategemea kua hio shida ni of what nature.... Kuna ile kama inahusiana na chakula ndani, anaona tu aibu kusema nenda angalau kwa wazazi kaombe unga kidogo tumekwama... anaona bora akwambie kua "fanya maarifa"..... Kawaida ya mwanamke ambae ni mwerevu (walau that is what I think) ni kutambua kua sio kila siku mume wake ataweza provide - na kwamba hata kama anaweza inaweza tokea in rare cases akakwama. Daima kulinda heshima ndani ya ndoa yenu inatakiwa kua na akili ya ziada mkichwa na maarifa pia....

Hivo basi daima hata kama woote wanafanya kazi na woote wana provide, ni lazima aweke akiba pembeni popote pale ndani ya nyumba ambayo inakua ni kinga ya kutatua tatizo pale ambapo litajitokeza na woote wasiwe na pesa (yaani mume na yeye mwenyewe mke); Hio akiba sio wanaume woote hujua kua inakuwepo.... Inapotokea kua kuna siku mlikwama kabisa mara nyingi akina mama huchukua hio akiba kuokoa jahazi kwa kumshirikisha mumeo na kumwambia "mume wangu nimeazima kwenye kikundi chetu kile cha upaku" sababu ya kusema hivi sio kwamba humuamini mumeo.... No! Ila tu ni ile haitakiwi hajenge kichwani mwake kuna akiba ndani for next time akikwama he wont try harder..... Hivo baas mara nyingi wanaume husema hivo sababu wanakua weshawahi pita in jams na mke aliokoa jahazi.... Siamini kua hua wanasema hivo kwa maana kwamba nenda kwa mpango wa kando ukatafute pesa.


Boss it has been Long.... Usiku mwema.

Well said Mami!!! Mume wako ana kifaa trust me!!!
 
Ila tukubaliane, huo wasiwasi wa TB kuhusu ku-take advantage hautakosekana kama mwanaume atahitaji kila mara mkewe 'afanye maarifa'. Ndo wakina marioo hao, yeye anauza sura kila siku hoping mkewe atamuweka mjini kwa maarifa. Ikila kwake usishangae, manake ile sense ya masculinity inapotea machoni kwa mkewe. Na mke anaanza kuona wale wawezeshaji ndo wako masculine (mangi included)

You said it right Mami!
 
Unavyomwambia mwanamke afanye maarifa wakati wewe yamekushinda
unamaanisha nini hapo? si atoke akatafute ili nae alete home?
sasa akileta unamuona ni mhuni wakati hata yeye ana kipato chake

ndo mana mm nasema nyie wanaume mnatufanya sie tuwe kwenye
mifumo yenu , mnatuweka katika nafasi ya mwisho sana wakati sie
ni walezi wakubwa wa familia kuliko nyie.
HATUTAKI KUKANDAMIZWA
 
Unavyomwambia mwanamke afanye maarifa wakati wewe yamekushinda
unamaanisha nini hapo? si atoke akatafute ili nae alete home?
sasa akileta unamuona ni mhuni wakati hata yeye ana kipato chake

ndo mana mm nasema nyie wanaume mnatufanya sie tuwe kwenye
mifumo yenu , mnatuweka katika nafasi ya mwisho sana wakati sie
ni walezi wakubwa wa familia kuliko nyie.
HATUTAKI KUKANDAMIZWA
ladyfurahia naomba nikupe changamoto hapo. Siamini kuwq mwanaume anayeijali familia atasema "fanya maarifa " kila siku.

Inatokea mara moja moja hana pesa, mtu hawezi kuwa, nacho kila siku. Na inawezekana katika yale matumizi anayotoa kila siku hutumii, yote, unajisevia kidogo. Angalau basi mambo yakiwa magumu, umpe tafu.

Hapa hatuongelei nani mlezi bora wa familia, bali mtoaji katika familia. Huyo mtoaji kuna, siku nae anakosa, hapo akisema fanya maarifq ndo wewe ujaribu au kuchukua savings zako, au kukopa nk..

Wanawake wanaolinda familia zao sidhani kama watapata shida kwa hilo, as long as it doesn't happen frequently!
 
Last edited by a moderator:
hapo nimekuelewa mkuu asante kwa kuniweka sawia
ladyfurahia naomba nikupe changamoto hapo. Siamini kuwq mwanaume anayeijali familia atasema "fanya maarifa " kila siku.

Inatokea mara moja moja hana pesa, mtu hawezi kuwa, nacho kila siku. Na inawezekana katika yale matumizi anayotoa kila siku hutumii, yote, unajisevia kidogo. Angalau basi mambo yakiwa magumu, umpe tafu.

Hapa hatuongelei nani mlezi bora wa familia, bali mtoaji katika familia. Huyo mtoaji kuna, siku nae anakosa, hapo akisema fanya maarifq ndo wewe ujaribu au kuchukua savings zako, au kukopa nk..

Wanawake wanaolinda familia zao sidhani kama watapata shida kwa hilo, as long as it doesn't happen frequently!
 
maarifa ni mengi kwa mwanamke
hasa village girls
utaomba unga kwa jirani
utakuwa na bustani ya viazi
utakuwa na bustani ya mboga mboga
utakusanya kuni uuze

so many

Na pia wamama wanajua kutunza akiba zao so pengine anaweza kua na hela bila baba kujua
 
Tatizo linakuja pale mwanaume anapoona kumbe inawezekana eeeh. Basi utafanya maarifa kila siku. Hawa waume wa Kibongo balaaa.
 
Kuna baadhi ya familia ....mwanaume akishindwa baadhi ya majukumu yake hasa ya kipato ni kawaida kusikia mume akimwambia mkewe 'fanya maarifa' au ufanye maarifa basi'.......

Hivi hili hasa linaamaanisha nini?

Maarifa gani ambayo mwanaume akishindwa, mwanamke ndo ataweza?

Halafu unakuta mwanamke 'anafanya kweli maarifa' na maisha yanakwenda...

Sasa 'haya maarifa' ya wanawake ni yapi?

Kwanza tungewauliza nyie wanaume, au ungeuliza wanaume wenzako naamini wanayo majibu ya busara . Halafu wanaume wa siku hizi wana makusudi nyingi sana
 
Tatizo linakuja pale mwanaume anapoona kumbe inawezekana eeeh. Basi utafanya maarifa kila siku. Hawa waume wa Kibongo balaaa.

hahaa haaa hili dongo limetugusa wengi..
 
Kwanza tungewauliza nyie wanaume, au ungeuliza wanaume wenzako naamini wanayo majibu ya busara . Halafu wanaume wa siku hizi wana makusudi nyingi sana


we huwezi maarifa kabisa?
 
Back
Top Bottom